Katiba Mpya: NEC ya CCM yatoa tamko kuwa serikali 2 ndio msimamo wa chama!

Katiba Mpya: NEC ya CCM yatoa tamko kuwa serikali 2 ndio msimamo wa chama!

Wananchi wanataka serikali mbili. Ila vibaraka wa wazungu wakiongozwa na dr slaa ndo wanataka kulazimisha serikali tatu
Wananchi wanataka uwepo wa serikali ya Tanganyika na ile ya Zanzibar zilizo sawa katika Muungano. Wazanzibari, wamechoshwa na "serikali ya Tanganyika" kujivika koti la serikali ya Muungano!
 
endeleeeni kujitoa fahamu tu.. subiri nguvu ya umma tu
Nguvu ya umma ni dawa gani hapa tanzania.
Nguvu ya umma imeshindwa hata zitto itaweza kwa watanzania wote,tuacheni na tanzania yetu nendeni kwenu kwa kagame.
 
Hizo serikali tatu koja wewe utaihudumia wewe,
kwanza leo hakuna NEC ya ccm huyu mburula sijui hiyo nec ya machame au kibosho.
NEC ya CCM ipo. Ndio hiyo ilikuwa inakutana juzi na jana. Zipo NCHI mbili tayari. Na kila NCHI ina serikali yake. Katiba ya sasa ya JMT ni kichekesho tu. Haina maana yoyote.
 
Nguvu ya umma ni dawa gani hapa tanzania.
Nguvu ya umma imeshindwa hata zitto itaweza kwa watanzania wote,tuacheni na tanzania yetu nendeni kwenu kwa kagame.

Dawa ya kutibu ukichaa na ujuha wa sio taka serikali ya tanganyika...

mtaisoma muda huu...
 
Uzi umejaa division 5 wa JF.. Wakiongozwa na Simiyu Yetu ..

:thumbdown::thumbdown::thumbdown::thumbdown:
 
Last edited by a moderator:
Serikali tatu ndiyo mdudu gani unatuletea hatutaki serikali za majaribio ulishawahi kuona wapi duniani muungano wa serikali tatu kama siyo mambo ya kihuni.

Ulisha wahi kuona wapi nchi2 zinaungana zinatokea serekali2 badala ya moja?.
 
Msimamo wa ccm ndo msimamo wa Watanzania

Msimamo wa CCM ni msimamo wa wafanyabiashara na wezi wa mali za umma. Kwani wanajua kurejea kwaserikali ya Tanganyika kutawanyima upopo wa kijifanya Waunguja wa Mzizima.
 
mimi kuna maswali najiuliza,ivi ihi nchi ni ya chama cha mapinduzi au ya watanzania? 2 je ajenda ya serikali [2] ni yawatanzania au ni ya chama cha mapinduzi? [3] watanzania walishirikishwa wapi wakati mh nyerere na mh karume walipo kubaliana kuunganisha nchi 2 yaani tanganyika na zanzibar?[4] kuna nini nyuma ya panzia kwa nini chama cha mapinduzi kina ngangania serikali 2? 4 kwanini chama cha mapinduzi kisiheshimu demokrasia ya kuwaacha watanzania wajiamulie mstakabali wa nchi yao juu ya muundo gani wanautaka kuliko kungangania serikali 2? [5] chama cha mapinduzi kitamtawala nani wakati kinampuuza mtawaliwa? mimi naona tunapo eletea kama busara haita tumika kwenye bunge la katiba tutarajie ngumi kupigwa bungeni, aona muungano wa vyama vya upinzani unakujatena na watanzania wakiipigia kura ya hapana rasimu ya katiba ya chama cha mapinduzi, maana wao watatumia wingi wao bungeni kulinda maslai yao kuliko maslai ya wenye nchi, mungu atusaidie watanzania juu ya jambo hili,
 
Kikao cha siku 2 cha NEC ya Chama cha Mapinduzi(CCM) kimemalizika na kutoa taarifa kupitia katibu wa Itikadi na uenezi wa chama hicho,bwana Nape Nnauye kuwa wamekubaliana kuendelea na msimamo wa kuunga mkono serikali 2.

Pia,bwana Nape ameongeza kuwa watafanyia kazi changamoto za muungano zinazolalamikiwa.

Katika hatua nyingine,Nape amesema hawatishiwa na hatua ya vyama vingine kwenda kwa wananchi kwani hata wao(CCM) wanaweza kwenda kwa wananchi na kuwaeleza jambo hilo.


CHANZO:ITV

MY TAKE:
Hatua hii ni sawa na kutangaza mgogoro mapema!
ccm wametengeneza dili nyingine ya kupiga hela. Kwa msimamo huu wa ccm suala la katiba halipo tena!
 
Kikao cha siku 2 cha NEC ya Chama cha Mapinduzi(CCM) kimemalizika na kutoa taarifa kupitia katibu wa Itikadi na uenezi wa chama hicho,bwana Nape Nnauye kuwa wamekubaliana kuendelea na msimamo wa kuunga mkono serikali 2. Pia,bwana Nape ameongeza kuwa watafanyia kazi changamoto za muungano zinazolalamikiwa. Katika hatua nyingine,Nape amesema hawatishiwa na hatua ya vyama vingine kwenda kwa wananchi kwani hata wao(CCM) wanaweza kwenda kwa wananchi na kuwaeleza jambo hilo. CHANZO:ITV MY TAKE: Hatua hii ni sawa na kutangaza mgogoro mapema!
daah? Sikutegemea kazenj kuburuza nchi kubwa kama Tanganyika na kuifanya koloni lake! Nahisi watanganyika tumelaaniwa!
 
Nguvu ya umma ni dawa gani hapa tanzania.
Nguvu ya umma imeshindwa hata zitto itaweza kwa watanzania wote,tuacheni na tanzania yetu nendeni kwenu kwa kagame.

Bw,simiyuYetu jaribu kutumia kichwa kufikiri,usjitoe akili kwa sababu ya kibaba cha siku moja,watu wa aina yako ni hatari sana katika jamii,sisi hapa Unguja wallah hatutakubali katu kuendelea kufunikwa na Serikali ya Muungano,tumeshindwa kwa miaka mingi kupata maendeleo ya Nchi yetu sababu ya upuuzi huu.
 
Kama ni serikali mbili za Tanzania Bara yenye uhuru kamili na Tanzania Visiwani yenye uhuru kamili hapo sawa lakini kuwa na serikali ya muungano yenye nchi moja yenye uhuru kamili huku nchi nyingine haieleweki...hapo sikubaliani nao.

Jambo la msingi hapa ili kumaliza kero zote za muungano ni Kuwa na serikali moja ya Jamhuri ya Muungano wa watu wa Tanzania ambapo Zanzibar itafutwa na Tanganyika haitarudi tena huku tukiwa na rais mmoja tu.
 
Unazmzungumzia Lisu gani? Huyu huyu aliyegaragazwa na Albert Msando, kijana mdogo kabisa hadi akaomba poo pale alipoomba watumie lugha ya kiswahili badala ya kiingereza?
Hayo ya Msando Topic ingine kabisa. Hili la Muungano na Katiba ya Zanzibar fuatilia tu hotuba zake kama Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria Bungeni.

CCM wanaoneana haya hadi kwenye mambo mazito na ya msingi kabisa kama Katiba ya JMT. Huu msimamo wa sasa wa NEC yao ni usanii tu.
 
Back
Top Bottom