Katiba Mpya: NEC ya CCM yatoa tamko kuwa serikali 2 ndio msimamo wa chama!

Katiba Mpya: NEC ya CCM yatoa tamko kuwa serikali 2 ndio msimamo wa chama!

Kama wananchi hawataiona ccm kama ndio sababu ya wao kuwa maskini wa kutupwa, basi tusubiri hadi Yesu alete nabii wa kuwafunulia.Kwanini walianzisha mchakato ambao umetafuna fedha za wananchi maskini wa taifa hili?Iko siku watawajibika kwa wanayoyatenda.
 
Hayo ni maoni ya ccm sio maoni ya watanzania,

Watanzania 64% wametoa maoni yao mbele ya tume ya mzee wetu Warioba kuwa wao wanataka muungano wa serikali tatu.

Maoni ya umma wa wengi yaheshimiwe,
 
Kikao cha siku 2 cha NEC ya Chama cha Mapinduzi(CCM) kimemalizika na kutoa taarifa kupitia katibu wa Itikadi na uenezi wa chama hicho,bwana Nape Nnauye kuwa wamekubaliana kuendelea na msimamo wa kuunga mkono serikali 2.

Pia,bwana Nape ameongeza kuwa watafanyia kazi changamoto za muungano zinazolalamikiwa.

Katika hatua nyingine,Nape amesema hawatishiwa na hatua ya vyama vingine kwenda kwa wananchi kwani hata wao(CCM) wanaweza kwenda kwa wananchi na kuwaeleza jambo hilo.


CHANZO:ITV

MY TAKE:
Hatua hii ni sawa na kutangaza mgogoro mapema!
Sawa kabisa serikali mbili tu, anayetaka tatu ahame nchi. Cha msingi marekebisha katiba ya zanzibar na ya muungano kukidhi mapendekezo mengine chanya katika rasimu sio kubomoa badala ya jujenga. Kwanza Warioba kazi yake kashamaliza lakini anaendelea kuwafanyia kazi kina Jussa utadhani katumwa.
 
Kama ni serikali mbili za Tanzania Bara yenye uhuru kamili na Tanzania Visiwani yenye uhuru kamili hapo sawa lakini kuwa na serikali ya muungano yenye nchi moja yenye uhuru kamili huku nchi nyingine haieleweki...hapo sikubaliani nao.

Jambo la msingi hapa ili kumaliza kero zote za muungano ni Kuwa na serikali moja ya Jamhuri ya Muungano wa watu wa Tanzania ambapo Zanzibar itafutwa na Tanganyika haitarudi tena huku tukiwa na rais mmoja tu.


Wewe ni mmoja kati ya MAADUI wa Zanzibar.
 
Naona dalili za kupata katiba mpya sasa zimeeanza kuonekana mapema serikali mbili ndiyo mpango mzima ndiyo zimetufikisha hapa tulipo.
yes zimetufikisha hapa kwenye huu umasikini chini ya jemadari KJ
 
Kwa namns hii, hili BUNGE la KATIBA halina maana tena, maana kwa jinsi lilivyoudwa ki-CCM basi maamuzi ya NEC ndiyo yatakayopita. Inaniuma sana jinsi tulivyoingia gharama zisizo na msingi, tumeunda TUME ya kukusanya MAONI, na sasa tumeunda BUNGE la KATIBA, yote haya ni ufujaji wa pesa, kupoteza muda na dharau kubwa kwa wananchi.
 
Kweli ccm hamna aibu! Tumetumia muda mwingi kuelezea kwa nini tunataka serikali 3 leo mnatudharau? ngoja mtaona joto ya jiwe. Mlikuwa wapi wakati znz wanavunja katiba kwa kutangaza mipaka, wimbo n.k.
 
kama naona Muamsho vile wanajipanga?maoni ya wengi kuachwa ni dalili tosha ya mabavu,
 
Naamini wanaotaka serikali mbili watashindwa......time will tell.
 
mtu akikutukana kuwa una akili kama ya ccm, ujue ni tusi kubwa sana.

ngoja waipitishe bungeni halafu tuikatae kwenye kura za maoni. hivi hawa maccm hawakujufunza kenya? duh inaskitisha kweli?
 
Mimi sioni kama wamehamua vibaya, hata mimi hapa siyo mwanaccm lakini nataka serikali mbili yaani Serikali ya Zanzibar na Serikali ya TANGANYIKA basi

Kikao cha siku 2 cha NEC ya Chama cha Mapinduzi(CCM) kimemalizika na kutoa taarifa kupitia katibu wa Itikadi na uenezi wa chama hicho,bwana Nape Nnauye kuwa wamekubaliana kuendelea na msimamo wa kuunga mkono serikali 2.

Pia,bwana Nape ameongeza kuwa watafanyia kazi changamoto za muungano zinazolalamikiwa.

Katika hatua nyingine,Nape amesema hawatishiwa na hatua ya vyama vingine kwenda kwa wananchi kwani hata wao(CCM) wanaweza kwenda kwa wananchi na kuwaeleza jambo hilo.


CHANZO:ITV

MY TAKE:
Hatua hii ni sawa na kutangaza mgogoro mapema!
 
Nikijibiwa maswali haya 99 nitaacha kuidai Tanganyika, naanza na maswali matano.... 1. Waziri mkuu wa JMT huwa anaenda ZNZ na kushughulika na miradi ya maendeleo? 2. ZNZ kwenye maboresho ya katiba yao waliitambua ni nchi na mkuu ni Rais, Rais wa Tanganyika yu wapi? 3. Wabunge kutoka bara wapo ZNZ? 4. Mawaziri toka bara wanachaguliwa ZNZ? 5. M-ZNZ RUKSA KUMILIKI ARDHI BARA, JE MTZ BARA KWA NINI SIO RUKSA KUMILIKI ARDHI ZNZ? Kuna usawa hapo? Ukweli ni kwamba Nchi kama Marekani ni Muungano wa nchi nyingi tu lakini ni utaratibu tu... Ni bora niambiwe Tanganyika na ZNZ zina mawaziri wakuu na Rais ni 1 wa JMT kuliko Muungano wa nchi 2 zenye serikali 2
 
kulikuwa na haja gani ya kuunda tume ya kupita na kukusanya maoni kwa wanachi ikiwa maoni ya ccm ndio yanayofaa kuwa katiba ya tanzania?
 
Sawa kabisa serikali mbili tu, anayetaka tatu ahame nchi. Cha msingi marekebisha katiba ya zanzibar na ya muungano kukidhi mapendekezo mengine chanya katika rasimu sio kubomoa badala ya jujenga. Kwanza Warioba kazi yake kashamaliza lakini anaendelea kuwafanyia kazi kina Jussa utadhani katumwa.

Hii nchi si mali ya CCM bali ni mali ya watanzania wote na ndio wenye maamuzi.

Swala la katiba linaweza kupelekea ghasia na vurugu zitakazomuondoa JK madarakani.

Tumechoka kuendeshwa na hili genge la watu wachache kwa maslahi yao!
 
Back
Top Bottom