Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo aandika barua ya kujiuzulu

Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo aandika barua ya kujiuzulu


Taarifa zilizotufikia usiku huu ni kuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo, amejiuzulu nafasi yake hiyo.

Vyanzo vyetu vilivyo karibu na CCM vimethibitisha kuwa tayari Chongolo amewasilisha barua yake ya kujiuzulu kwa Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan.

Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama (NEC), ambavyo vinafanya vikao vyake vya kawaida jijini Dar es Salaam, Novemba 29, 2023, huenda vikampitisha Katibu Mkuu mpya wa CCM ambaye atachukua nafasi ya Chongolo.

Sababu za kujizulu kwa Chongolo tutawaletea baadae.


=====

UPDATES: 28 NOV 2023

======

JamiiForums imejihakikishia kuwa ni barua aliyoandika mwenyewe ila taarifa za kuwa amepata ajali si za kweli bali gari lake lilihusika na ajali mapema Machi/Aprili.
View attachment 2827882
Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) 01 Mei 2021 iliza nafasi ya Ukatibu Mkuu iliyoachwa tangu Machi 26, mwaka 2021, kwa kumteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo, kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho.

Nafasi hiyo iliachwa wazi baada ya aliyekuwa akiishikilia, Dk Bashiru Ally, kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi. Itakumbukwa kuwa wakati Dk Bashiru anateuliwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi, alikuwa Katibu Mkuu wa CCM, nafasi aliyoihudumu kwa kipindi cha miaka miwili na miezi minane.

Nyota ya Chongolo kupanda kisiasa ilianza kuonekana zaidi tangu Juni 27, 2016 wakati Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli, alipomteua Chongolo kuwa Mkuu wa Wilaya ya Longido.

Julai 28, 2018, Chongolo alihamishwa kutoka Wilaya ya Longido kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Dar Es Salaam
View attachment 2827887
Akiwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni alifanya mambo Mbalimbali.

1). Novemba 6, 2018 Chongolo aliiagiza Polisi Kata ya Kijitonyama kuwakamata wanaume wanaonunua machangudoa.

2). Septemba 22, 2019, aliunda kamati ya watu sita kuchunguza tukio la ajali ya moto uliotekeleza Hoteli ya Coco Beach.

3). Novemba 9, 2019, alitekeleza agizo la Rais John Magufuli, la kumrudishia nyumba bibi mwenye umri miaka 80, Amina Muhenga, aliyoidai zaidi ya miaka 30.

4). Januari 17, 2020, Chongolo alipiga marufuku wanafunzi walioanza kidato cha kwanza mwaka huo kurudishwa nyumbani kwa sababu ya kutokuwa na sare za shule.

5). Februari 25, 2020, alisema wilaya yake ilitenga Sh3.4 bilioni kwa ajili ya kuwakopesha wanawake, vijana na wenye ulemavu katika bajeti ya mwaka 2020/21.

6). Januari 10, 2021, alifanya operesheni maalum iliyofichua nyumba zinazohifadhi watu wenye ulemavu wanaotumika kuomba jijini Dar es Salaam.

7). Aprili 1, 2021, alitoa siku 21 kwa wataalamu wa Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka (Dawasa) kwenda kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji kwa wakazi wa Kata ya Mbezi Juu. Nk

Chongolo ni Katibu Mkuu wa kumi wa CCM tangu chama hicho kilipozaliwa Februari 5, 1977.

Kabla ya kuteuliwa kuwa mkuu wa wilaya, Chongolo amewahi kuwa Ofisa wa chama kwenye Idara ya Uenezi makao makuu wakati huo Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi akiwa Nape Nnauye.

Pia, amewahi kuwa Mhariri wa Redio Uhuru ambayo inamilikiwa na CCM.

Kwa nyakati tofauti, Chongolo pia amewahi kuwa Katibu wa Bodi ya Shirika la Magazeti ya Chama (Uhuru na Mzalendo).
View attachment 2827893

MHESHIMIWA DR. SAMIA SULUHU HASSAN MWENYEKITI WA CCM NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

YAH; KUJIUZULU.

Kichwa cha barua chahusika.

NOVEMBA 27, 2023

Mh. Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwanza nitumie fursa hii kukushukuru wewe binafsi na Chama Cha Mapinduzi kwa kuniamini, kunilea na kunivumilia wakati wote wa uongozi wangu.

Mh. Mwenyekiti, utakumbuka kuwa Aprili 30, 2021 niliteuliwa na Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kuwa Katibu Mkuu wa CCM. Uteuzi wangu ulitokana na mapendekezo yako, upendo wako na uongozi wako wenye mapenzi mema kwangu, kwa chama na taifa.

Mh. Mwenyekiti, siku chache zilizopita nimechafuliwa kupitia mitandao ya kijamii. Hali hiyo imenikumbusha wajibu wa kiongozi kuwajibika kwa maslahi ya Chama wakati wote unapotuhumiwa au kuhisiwa kufanya jambo lolote kinyume na kanuni, taratibu, miiko na tamaduni za Chama chetu.

Mh Mwenyekiti naomba uridhie ornbi langu kwako la kujiuzulu. Natambua kuwa uimara wa CCM unatokana na uongozi wako imara unaolenga kukuza na kustawisha hali ya maisha ya wananchi kijamii na kiuchumi.

Mh. Mwenyekiti sipo tayari kuona Chama Cha Mapinduzi kinachafuka kwa kuhusisha nafasi yangu ya Katibu Mkuu na uvumi wa matendo,tabia au mienendo ninayochafuliwa nayo.

Mh. Mwenyekiti kwa unyenyekevu mkubwa naomba uridhie ombi langu.

Mwisho, japokuwa si kwa umuhlmu, nakuombea kwa Mwenyezi Mungu akuepushe na akulinde dhidi ya hila, husda na watu wote wenye nla ovu dhldi yako, Chama, Serikali na Taifa kwa ujumla. Nakuahidi kuendelea kuwa mwana CCM mtilfu wakati wote.


Wako mtiifu, Chongolo Katibu Mkuu
Hahahahah maji na mafuta vinaanza kujitenga
 
Umefikiri vyema...

Hii hoja yako, likely, imeunusa ukweli wa maamuzi ya huyu KM wenu...

Nafikiri pia, baadhi ya viongozi wakuu wa CCM hawakubaliani Paul Makonda a.k.a DAB kupewa nafasi hiyo ndani ya chama kutokana na tatizo la uadilifu wa kimaadili alilonalo huyu uliyemwita "dogo" yaani Paul Makonda..

Mimi sitashangaa hata Makamu Mwenyekiti wenu Abdulhaman Kinana akitupa jezi pia..!!
Uko CCM ni nani mwenye maadili anaweza simama kumsema mwenzie kuwa hafai kabisa kuwa CCM au kuwa kiongozi kabisa! Nani msafi ndani ya CCM?😂😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom