Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani aandika barua ya Kujiuzulu. Lugola na Andengenye wakalia kuti kavu, Rais Magufuli asema hawafai

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani aandika barua ya Kujiuzulu. Lugola na Andengenye wakalia kuti kavu, Rais Magufuli asema hawafai

Alafu alikuwa waziri pekee aliyekuwa analala na ilani ya CCM, akienda chooni anayo. Na alishona mashati yenye mifuko ya bendera ya taifa. Kumbe anaenda kusaini mikataba ya ovyo....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakika Maneno ya mkulu yana thibitisha usemi wa "NYANI HAONI KUNDULE"
 
Najiuliza tu,

Je Ikulu iliwapa kibali cha kusafiri kwenda huko Romania kwa majadiliano? Walipokuwa Romania, hawakumpa mkuu feedback ya kinachoendelea huko ughaibuni, wao wakaamua kusaini mkataba juu kwa juu?

Kama Raisi anasema anayetakiwa kuingia mikataba ya kupokea pesa kwa niaba ya waTZ ni wizara ya fedha, inamaanisha mkataba uliosainiwa si halali.

Katibu mkuu na Kamishna wa Fire hawakuyajua hayo?
 
Kujiuzulu peke yake hakutoshi, ni vyema adhabu kali zikachukuliwa kwa sababu kufanya jambo linalohusu pesa za umma kwa mtu mwenye madaraka makubwa na pengine katika utendaji wake ametumbua wengi kwa vikosa vidogo ni lazima mtu kama huyu achukuliwe adhabu kali.

Wakati wa hayati Mwalimu Nyerere watu wa namna hii waliswekwa ndani kwa kipindi kisilichojulikana.
Kipindi hiki tunawaita mafisadi na kuwashitaki mahakamani.

Haiwezekani watumishi wengine wafanye makosa madogo madogo (ukilinganisha na hili la Shs Trilion moja baada ya kubadilishwa toka pesa za kigeni ) wasulubiwe mahakamani na kufukuzwa kazi lakini hawa vingunde waachwe warudi bara barani na kutamba kuwa wao ni watu maalumu.

Hawa wakirudi bungeni watasemaje?
 
Kwa jinsi umeandika kwa sauti ya juu lazima watakusikia.
 
hizi kazi za kuteuliwa Zina changamoto

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli tupu mkuu! Mfano Tobias Andengenye nimesoma naye ni mtu mwadilifu sana kiasi kwamba Schoolmates zake wote tulikuwa tunajivunia hatua aliyokuwa nayo kwa kusema anaistahili kwa sababu ya uadirifu wake. Lakini ghafla anazalilishwana Mteuzi na Mtenguaji.
 
Kama walidirki kufanya hivo Hawa Ni wahujum uchumi wanapaswa kukamatwa na kueleza watanzania kwa Nini waliamua kufanya hivo,Hali wakijua Ni kinyume cha maadili ya uongozi.
Hawa pia naona Ni mafisadi tu.
 
Hakika nchi hii inashangaza sana.Nilishangaa sana niliposikia Mh Kangi Lugola kateuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani,kwani Mh Kangi aliwahi kuwa na kesi ya Kudai na Kupokea Rushwa yeye na Mbunge mwenzake,kesi iliyokuwa Mahakama ya Kisutu.

Sikumbuki iliishaje lakini hii ni Tanzania hakuna kinachoshindikana ukiwa Mh.Haya leo yametimiwa Uzalendo wa Kangi Lugola upo wapi? Kangi alibadili mitindo ya mavazi yake,akivaa Mashati yenye Mifuko ya Bendera ya Tanzania,Kangi akitembea na Ilani ya Chama chake,hakika niliamini Kangi ni mzalendo wa Nchi Yake.
Screenshot_20200123-122102_Google.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamani mwenye ile picha inayoonyesha Kangi akinengua na mdada mmoja ambaye inasemekana ni askari wa kike atuwekee hapa jamani!
 
Ni kweli kabisa! Utadhani siku ya leo polisi wote wamevalishwa kofia nyeupe maana wametapakaa Barabarani, vituo havihesabiki.
 
Lugola pamoja na kumsifia Rais leo kafukuzwa hadharani.Ningekuwa Lugola ningeaga nakwenda kuko joa na nasepa mbele kwa mbele.

Ana bahati hajasekwa ndani kwa kuvunja sheria
 
Back
Top Bottom