Katika dunia hii ya kidigitali kulilia mikutano ya hadhara ni ujuha wa kiwango cha ajabu

Katika dunia hii ya kidigitali kulilia mikutano ya hadhara ni ujuha wa kiwango cha ajabu

Utazeeka pia au kwa vile unakula bure hapo kwa dada yako unadhani utabaki hivyo. Mkuu kama ibada zinafanyika kwa mtandao, matibabu yabafabyika kwa mtandao, jana tumeona Kamati kuuya CHADEMA ikiongozwa na Gaidi inafanyika kwa njia ya mtandao- kulilila mikutano ya hadhara ni ujuha
Kifupi ww ndo juha usiyejua umuhimu wa mikutano ya hadhara...sema tu umeamua kutuelezea ulivyo juha ...

Sent from my DRA-LX5 using JamiiForums mobile app
 
Una stahiki na uhuru wako wa kusema unachowaza ila ukweli unabaki pale pale nendeni kidigitali- mikutano ya hadhara karne hii ni ujuha
Unafanya na wangapi!!?? Sasa naamini unaweza kutwanga nafaka na kutenganisha na makapi lakini kamwe hauwezi kumtemganisha mpumbavu na upumbavu wake. Unathibitisha hilo
 
Mtu kutaka haki yake si ujuha.

Nyerere alienda New York City mwaka 1959, akawa anahojiwa katika jopo la kipindi cha TV cha former first lady wa US, Mrs. Eleanor Roosevelt, mke wa Rais Frank Delano Roosevelt.

Katika mahojiano yale, Nyerere aliulizwa, watu wako hawako tayari, hawana elimunya kuendesha nchi, huoni kwamba Watanganyika kupata uhuru sasa ni mapema sana?

Nyerere akatoa mfano mmoja wa kifalsafa sana. Akasema, ukimkuta mtu ana koti lake, koti halimtoshi vizuri, utamwambia wewe nipe hili koti lako halikutoshi? Akasema muache mtu na koti lake, ni lake, kama linamtosha au halimtoshi ni suala jingine, yeye mwenyewe ataamua kwa uhuru wake alifanye nini koti lake.

Akasema tulikuwa nanuhuru kabla ya wakoloni, hata kama hatukuwa vizuri sana, lakini tulikuwa tunajiendesha wenyewe, tunataka kurudi kujiendesha wenyewe tuamue mambo yetu. Ni haki yetu.

Ukweli kwamba koti halimtoshi hauondoi ukweli kwamba koti ni lake, haukupi wewe haki ya kuamua afanye nini nankoti hilo.

Haki ya mikutano ya hadhara ni ya kikatiba, waachieni watu wawe nayo. Kama mitandao ina ufanisi zaidi, ukiwaingezea na hiyo haki ya mikutano on the ground utaharibu nini? Ni haki yao.

Msikilize Nyerere akidai uhuru wa Tanganyika anavyopangua hoja hii ya kusema "uhuru huu haukufai"


Mwalimu genius..
JokaKuu
 
Katika ulimwengu huu wa kidigitali kila kitu kinaweza kufanyika kwa urahisi, uhakika, na ufanisi mkubwa kwa kutumia teknolojia ambazo hazihitaji watu kukusanyika na kukutana mwili kwa mwili. Lakini hapa Tanzania naona kama ni tofauti. Hili limuejidhihirisha kwa jinsi watu walivyokamia mikutano ya hadhara wakiwemo wanajinasabu kwenda kidigitali.Hii ni aibu na ishara mbaya.
Nchi hii bado tupo nyuma sana kidijitali huo ndio ukweli ! Huwezi kuwafikia watu wengi kwa njia hiyo !!
 
Nchi hii bado tupo nyuma sana kidijitali huo ndio ukweli ! Huwezi kuwafikia watu wengi kwa njia hiyo !!
Mkuu hapa inawezekana- ukitumia bulky SMS unafikia watanzania karibu 50m
 
K
Mkuu tafuta takwimu
Around 70 percent of the surveyed population used a mobile phone daily in Tanzania as of 2021.22 Nov 2022
"70% of the surveyed population" tells us very little because we do not how big was the surveyed area and in which locale. Ukifanya survey Magomeni Mapipa, ya Dar, unaweza kupata hizo takwimu. Na hizo Takwimu hazisemi kati ya hao walilotumia simu, waliotomua 'Vitochi' ni wangapi na walilotumia 'Simujanja' ni wangapi.
Unaposema ulimwengu wa Dijitali, kimsingi, unazungumzia wale wenye Simujanja ambao wanaweza kujiunga na mitandao ya kijamii. Na kwa hakika, wenye Vitochi ni wengi sana kuliko wenye Smartphone. Kwa hiyo Mikutano ya hadhara ni muhimu.
 
K

"70% of the surveyed population" tells us very little because we do not how big was the surveyed area and in which locale. Ukifanya survey Magomeni Mapipa, ya Dar, unaweza kupata hizo takwimu. Na hizo Takwimu hazisemi kati ya hao walilotumia simu, waliotomua 'Vitochi' ni wangapi na walilotumia 'Simujanja' ni wangapi.
Unaposema ulimwengu wa Dijitali, kimsingi, unazungumzia wale wenye Simujanja ambao wanaweza kujiunga na mitandao ya kijamii. Na kwa hakika, wenye Vitochi ni wengi sana kuliko wenye Smartphone. Kwa hiyo Mikutano ya hadhara ni muhimu.
So mkuu CHADEMA waliposema wanaenda kidigitali nu utopia?
 
Back
Top Bottom