Katika Dunia yenye takribani watu Bilioni 8 leo, zaidi ya watu Bilioni 110 wamewahi kuishi na kufa

Katika Dunia yenye takribani watu Bilioni 8 leo, zaidi ya watu Bilioni 110 wamewahi kuishi na kufa

Nimeuguza mtu mpaka kanifia mikononi.
Alikuwa anatapatapa huku anasema anaogopa sana, anasema eti kuna watu wako kwa mbali anawaona wanamsubiri.
inasemekana mtu mwenye makandokando mengi ndo anapataga shida na kuona vitu vya ajabu wakati wa kufa
ila wale mambo machache wanakufa kimyakimya , tena wengine wanaaga
bibi yangu alimwambia mzee wangu amgeuze, baada ya kumgeza kakimya kakapita, kumsemesha alishakata moto
 
Hii itukumbushe kuwa hii Dunia tunapita, na itusaidie kupunguza kama sio kuacha kabisa kiburi na kujipa umuhimu.

Waliowahi kuishi na kuondoka ni wengi zaidi ya waliopo leo, na kila mmoja kwa wakati wake alikuwa na umuhimu wake.

Hivyo nafasi ya wewe kuishi leo isikufanye ufikiri kuwa ni ya kipekee sana, utaondoka siku moja na watakuja wengine. Maisha yataendelea vizuri tu bila uwepo wako.

Hii nimekumbushwa na huyu kijana wangu mkubwa, nami nikaona niwakumbushe.

Ncha Kali.
Ujumbe kuntu kabisa.
 
Hujaona ile video inayotrend insta?
Mtu aliyehai anapigana na kufukuza kiumbe kisichoonekana ila mwisho wa siku roho inanyofolewa kimaajabu!
Kuogopa lazima.
Clip za insta ni vichekesho tu au maudhui kwa lengo fulani, katika hali halisi huwezi kupata camera.
 
inasemekana mtu mwenye makandokando mengi ndo anapataga shida na kuona vitu vya ajabu wakati wa kufa
ila wale mambo machache wanakufa kimyakimya , tena wengine wanaaga
bibi yangu alimwambia mzee wangu amgeuze, baada ya kumgeza kakimya kakapita, kumsemesha alishakata moto
Inatia sana huzuni.
Umenikumbusha kisa cha marehemu bibi yangu aliyefariki 2015.
Alifariki Jumatatu saa 2 asubuhi.
Jana yake Jumapili nilikesha Coco beach, piga sana pombe.
Inafika asubuhi saa 1, napigiwa simu bibi ananiita.
Kufika pale, kila mtu ananiambia bibi yako yuko hoi, anakuita.
Nafika chumbani na pombe pombe zangu bibi akaniambia nimpakate, nikampakata.
Akasema unanuka pombe na kwanini jana hujaenda kanisani.
Aliniambia maneno 3 tu.
Moja, acha pombe,
Pili, usiache kwenda kanisani na jambo la 3 ni siri yangu.
Baada ya pale akanipa funguo kisha akaniambia nakukabidhi huu funguo, tafuta mlango unaoingia funguo hii.
Baada ya pale nikaita watu huku nimempakata.
Akatabasamu, akafumba macho mwenyewe kisha akakata roho.
Aloooo.....sitasahau.
Bibi yangu alikuwa kipenzi changu sana sana sana.
 
Inatia sana huzuni.
Umenikumbusha kisa cha marehemu bibi yangu aliyefariki 2015.
Alifariki Jumatatu saa 2 asubuhi.
Jana yake Jumapili nilikesha Coco beach, piga sana pombe.
Inafika asubuhi saa 1, napigiwa simu bibi ananiita.
Kufika pale, kila mtu ananiambia bibi yako yuko hoi, anakuita.
Nafika chumbani na pombe pombe zangu bibi akaniambia nimpakate, nikampakata.
Akasema unanuka pombe na kwanini jana hujaenda kanisani.
Aliniambia maneno 3 tu.
Moja, acha pombe,
Pili, usiache kwenda kanisani na jambo la 3 ni siri yangu.
Baada ya pale akanipa funguo kisha akaniambia nakukabidhi huu funguo, tafuta mlango unaoingia funguo hii.
Baada ya pale nikaita watu huku nimempakata.
Akatabasamu, akafumba macho mwenyewe kisha akakata roho.
Aloooo.....sitasahau.
Bibi yangu alikuwa kipenzi changu sana sana sana.
Umeweza kuacha pombe mpwa?
 
Hii itukumbushe kuwa hii Dunia tunapita, na itusaidie kupunguza kama sio kuacha kabisa kiburi na kujipa umuhimu.

Waliowahi kuishi na kuondoka ni wengi zaidi ya waliopo leo, na kila mmoja kwa wakati wake alikuwa na umuhimu wake.

Hivyo nafasi ya wewe kuishi leo isikufanye ufikiri kuwa ni ya kipekee sana, utaondoka siku moja na watakuja wengine. Maisha yataendelea vizuri tu bila uwepo wako.

Hii nimekumbushwa na huyu kijana wangu mkubwa, nami nikaona niwakumbushe.

Ncha Kali.
Kwani ni lini ulishawahi kuwaza namna hiyo kwamba wewe ni 'so special' katika hii dunia?

Hauna umuhimu wowote katika jamii, katika nchi na katika dunia.

Upo duniani kwa ajili ya manufaa yako ya kuenjoy life period

Ndiyo maana ukifa hata sasa hivi, wataolia ni ndugu zako ambao wewe ulikuwa ni mlishi wao, lakini wengine ni kucheka, kucheza bao msibani na kuangalia saa za adhuhuri kuwahi makaburini wakakufukie wawahi mambo yao.

Hauna umuhimu wowote hata ukifa sasa hivi.
 
Back
Top Bottom