Katika hili mimi nasimama na Mbowe, hakika jamaa kakomaa kisiasa na anaijua vizuri siasa

Mbowe iko akili....
 
Kwann umeficha identity Yako ya CCM?

Ungedeclare interest ungeeleweka vizuri zaidi.
Ni wapi mimi niliwahi kusema kuwa mimi ni mwana CCM?
Naomba ushahidi wenye fact kupitia kadi yangu ya chama au kauli yangu mwenyewe nikisema kuwa mimi ni mwana CCM.
Karibu utoe ushahidi wa hayo maombi yangu mkuu. Nakuruhusu.
 
Labda Mbowe ndie anaemtuma kupitia mlango wa nyuma ili alete amsha amsha katika maridhiano yao.
Kwahiyo unataka kumaanisha kuwa Mbowe ni muoga, hana ujasiri wa kuongea mwenyewe hadi amtumie mtu mungine?
No i don't think so!
 
Hao hao wajinga unaosema hapa ndio wanaomdanganya mpaka anaamini kuwa yeye sasa ni sikio lililozidi kichwa, kwamba anaamini kuwa yeye sasa yuko juu zaidi ya chama na viongozi wengine wa chama.
Ila ameshindwa kujifunza kupitia kwa kina zito na Dr Slaa ambao wajinga wengine walikuwa wanawaaminisha kuwa ni maraisi wa mioyo yao. Lkn mwisho wa siku wakajikuta wameondoka peke yao na familia zao.
 
Kama hivi ndivyo kwanini Lissu anahangaika kuwalaumu wenzake chamani? anawachorea ramani waonekane kama wepesi waliokubali kutongozeka mbele ya Samia..

Kama tatizo liko CCM, apeleke shutuma zake huko kwa 100% but not otherwise.
Jamaa anatafuta kujijenga kisiasa kupitia migongo ya wenzake. Hajui kwamba bila Mbowe wala Chadema yeye hawezi kufika popote.
 
Labda sikuliona vizuri hilo swala unalozungumzia hapa. Hebu nikumbushe lipo katika comment ya namba ngapi?
 
Labda sikuliona vizuri hilo swala unalozungumzia hapa. Hebu nikumbushe lipo katika comment ya namba ngapi?
Achana na post namba, mimi nakuuliza ni kipi kinafanya maridhiano huko Zanzibar hayajeshimiwi, lakini huku Bara yataheshimiwa? Rejea uhuni katika uchaguzi wa 2015 huko Zanzibar.
 
Hata ikitokea maridhiano yamevunjika Leo, Bado wananchi wataendelea kuiamini CDM Kwa misimamo ya Lissu, Heche na Wenje.

Siasa zetu zinachukua episode ingine.

Tusubiri.
Bora Heche na Wenje wanaonekana wamekomaa kisiasa kwa kuyamaliza mambo yao kupitia vikao halali vya chama. Tofauti na jamaa ambae mwisho wa siku sikio litaponza kichwa.
 
Achana na post namba, mimi nakuuliza ni kipi kinafanya maridhiano huko Zanzibar hayajeshimiwi, lakini huku Bara yataheshimiwa? Rejea uhuni katika uchaguzi wa 2015 huko Zanzibar.
Uhuni upi wakati maalim Seifu alikimbilia kujitangaza mshindi wa uchaguzi kinyume na katiba yao ambayo inataka mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ndio atangaze mshindi wa uchaguzi?
Je inamaana maalim yeye hakujua kama alichofanya kilienda kinyume na katiba yao?

Au ndio ile ya mshika makali kutaka kushindana na mshika mpini ili atapokatika vidole aonewe huruma kuwa kaonewa?
 

Mtu akikimbikia kujitangaza unafuta uchaguzi?
 
Bora Heche na Wenje wanaonekana wamekomaa kisiasa kwa kuyamaliza mambo yao kupitia vikao halali vya chama. Tofauti na jamaa ambae mwisho wa siku sikio litaponza kichwa.
Hata Lema akiwa nje ya nchi Naye amekuwa akihoji maridhiano na kusema huo ni msimamo wake binafsi.
Hata Msigwa pia ilikuwa hivyo ktk suala la Loriondo.

CDM IPO democracy, hivyo ni kawaida.
 
Makala ndefu hizi huchosha kusoma, lakini nimekusoma vya kutosha hadi ulipoanza kujitambulisha sababu zinazokufanya umshabikie Mbowe.

Kwanza nikusifu kwa uandishi mzuri, na umejieleza vyema toka mwanzo historia yako ilivyo kuhusu maswala ya siasa.

Kwa wakati huu ngoja nisiandike mengi sana, lakini inatosha kusema yafuatayo:
1. Umejiunga na vyama tele, lakini hujaeleza hasa sababu zako za kuyumbayumba kote huko. Hii ni dalili mbaya, na wengi watakuhukumu kwa msimamo wako huu wa sasa kutokana na yumbayumba yako hiyo

2. Umemsifu Mbowe kwa uhadari wake wa uongozi hadi hapo alipoingia yule jamaa 2015. Sasa swali kwako ni hilo hilo, unajuaje wakati huu na Samia Mbowe huyo huyo hakukengeuka kama alivyokwishaonekana kuwa huko nyuma, au kwa vile tu wakati huu ni Samia na siyo Ngoyayi?
Hapana, usinielewe vibaya, sina maana mbaya kwa Samia, lakini huyo huyo ndiye Mwenyekiti wa Chama ambacho katika uhai wa maisha yako yote hukueleza kuwa uliwahi kuwa mwanachama au mpenzi wa chama hicho. Hapa unahitaji kutoa maelezo juu yake. Huu ni upungufu mkubwa kwa upande wako
3. Hivi vyama vya siasa havianzishwi kwa sababu ya kutafuta maslahi ya viongozi wao. Katika maelezo yako mengi hujaeleza kwa nini wakati huu unaona Mbowe anacheza vizuri na uongozi wake wa chama kiasi cha kustahili sifa unazommiminia.
Hakuna mtu hata mmoja anayekata maridhiano, kama kuna maridhiano juu ya jambo lolote, lakini hiyo siyo sababu ya kubadili mwelekeo wa chama katika malengo yake.

Ngoja niishie hapa kwa sasa, isije ikawa gazeti jingine.
 
Makala yako imeanzia hapa kuwa mbovu, kwa sababu ulionyesha waziwazi rangi zako zilivyo. Umeshutumu na kutoa hukumu palepale.
 
Aiseee!
Nilikuwa sijakusoma hadi huku chini.

Ukianzia pale ulipoanza kumsema "mtu wa ugaibuni, hadi huku mwisho; mada yako umeinyonga kabisa. 'Objectivity'
ukaitupa jalalani moja kwa moja!

Pole yako.
 
..Lissu hapingi maridhiano.

..Lissu anatetea maridhiano yenye tija.

..Hoja za Lissu ndizo zitakazompa nguvu Mbowe anapojadiliana na CCM.
Very bright reply mkuu JokaKuu !
Hapa umemjibu mleta hoja na wengine wengi hasa wanaccm maana hii ndiyo hoja yao wanayochomeka baada ya kushindwa kumuelewa Lissu ambaye hajui Kuremba maneno bali fact.
Wasilojua ni kuwa viongozi wa Chadema wanaunga mkono kauli ya Lissu na ndio maana wanaunga mkono maandamano ya BAWACHA.
 
Lisu anatakiwa akae na viongozi wenzake wa chama awambie kile kinachohitajika kufanywa katika maridhiano hayo, badala ya kuanza kuzunguka nchi nzima kupinga wazi wazi kile kinachofanywa na chama katika maridhiano yao.
Utakuwa una kichwa kigumu kuelewa kama hoja zilizojibiwa na JokaKuu na wengine hujaelewa. Au waliokupa hii assignment hawajaridhika na juhudi zako! Analofanya Lissu ni mission ya chama
 
Sijui ni sababu zipi zinazowafanya baadhi ya watu kudhani kwamba maana ya maridhiano ni kuifungia CHADEMA sandukuni.
Maridhiano hayana maana ya kuifanya CHADEMA iwe CCM.

Maridhiano hayafuti mambo yanayosimamiwa na CHADEMA kama chama

Maridhiano hayawezi kuilazimisha CHADEMA kutosemea mambo ambayo haikubaliani nayo.

Na hayo maridhiano kama lengo lake ni kufifisha juhudi za CHADEMA kuiondoa madarakani CCM, hayo ni maridhiano yasiyokuwa na maana yoyote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…