Katika hotuba hizi mbili (Mbowe & Lissu) ni mwana - CHADEMA gani timamu hajawaelewa viongozi hawa kupata heshima ya kuzungumza na Rais Samia?

Mnachoniuzi nyie watu hamnaga msimamo kiongozi wenu akisema samia mbaya woote mnaanza kubadilika ngoja tuone mbona muda bado
 
Ni mtu mjinga tuu ndiye awazaye hivyo. Jee ndugu nawe ni mjinga?
Ujinga ni ukosefu wa elimu, mimi ni mjinga na nimekua mjinga mara nyingi, ila nadhani wewe ni mpumbavu. Pamoja na kupewa elimu bado unang'ang'ania ujinga wako.
 
Ndiyo maana mapinduzi hayaishi.Wanajitakia wenyewe.Kuna yule mbibi aliwahi kusema,tena bungeni kwamba CCM haitoondolewa kwa vipande vya makaratasi madarakani.Inafurahisha sana.
 
Ujinga ni ukosefu wa elimu, mimi ni mjinga na nimekua mjinga mara nyingi, ila nadhani wewe ni mpumbavu. Pamoja na kupewa elimu bado unang'ang'ania ujinga wako.
Hapo ndio mwisho wa fikra zako? Unakubali kuwa ni mjinga kutokana na swali langu, sasa kwa swali ulilokubali ndio kunanifanya kuwa mpumbavu au unatudhibitishia kuwa sio mjinga tu bali na mpumbavu?
Ok, hongera kwa vipaji hivyo
 
Bado najaribu kujiridhisha anachoongea Mbowe baada ya kufutiwa kesi, na mazungumzo yake na mama. Kwasasa sitaki kutoa mtazamo wangu nasubiri muda uamue, lakini nina mashaka fulani.
 
Mnachoniuzi nyie watu hamnaga msimamo kiongozi wenu akisema samia mbaya woote mnaanza kubadilika ngoja tuone mbona muda bado

Kwa taarifa yako kiongozi akisema tunachoamini tunakuwa naye, lakini akisema tusichoamini atajikuta akibaki mwenyewe. Subiri kwenye hili la Mbowe aende kinyume na tunachoaamini, ndio atajua hajui.
 
Mbowe ni mfanyabiashara smart. Anauza pale profit inapokuwa at maximum. Angalia ule wakati wa Dr. Slaa to Lowassa. Afu linganisha na muda huu.
 
Reactions: Tui
Bado najaribu kujiridhisha anachoongea Mbowe baada ya kufutiwa kesi, na mazungumzo yake na mama. Kwasasa sitaki kutoa mtazamo wangu nasubiri muda uamue, lakini nina mashaka fulani.
Nadhani utakuwa umesikia Shaka alichosema kuhusu kamati kuu na agizo lao kwa serikali about Polisi.
Kama ccm imeanza kuwakana polisi ujue kuna mazito chini ya kapeti
 
Nadhani utakuwa umesikia Shaka alichosema kuhusu kamati kuu na agizo lao kwa serikali about Polisi.
Kama ccm imeanza kuwakana polisi ujue kuna mazito chini ya kapeti

Hiki ndio ninataka kujiridhisha nacho kwa vitendo, mkuu umesahau kuwa ccm ni wepesi wa kutoa ahadi za uongo ili kuhadaa umma?
 
Mazingira ya kuendesha siasa za upinzani hapa Afrika hutegemeana na aina gani ya uongozi uliopo madarakani wenye dhamana ya kuongoza nchi. Ninasema hivyo kwa sababu viongozi wengi hapa barani Afrika, wale waliopo madarakani ama wale hata waliowahi kushika madaraka ya kuongoza serikali za nchi zao wana sifa zinazofanana sana kiutendaji.

Wanapoingia madarakani kwa mara ya kwanza wanakuwa karibu sana na wananchi na huku wakitoa ahadi lukuki kuwa watazingatia, kutii na kusimamia matakwa ya katiba. Na kwa msingi huu hujinadi kuwa watahakikisha kuwa wanatenda haki kwa watu wote kupitia haki zao zote zilizowekwa kikatiba.

Lakini wakinogewa na kulewa na madaraka hapo ndipo linapogeuka kuwa ni tatizo kubwa. Pale udhaifu na madudu yao ya kiuongozi yanapoanza kuwekwa hadharani, basi hapo ndipo madhila ta siasa zao huanza kuonekana, huku wahanga wakubwa wakiwa ni vyama makini na vyenye nguvu vya upinzani, wanaharakati, wanahabari na vyombo vya habari.

Si jambo baya kwa mhanga wa siasa chafu za chama tawala kufanya maridhiano na kiongozi wa nchi. Hii inatokana na ukweli kwa inahitajika "entry point" ili kurudisha mazingira rafiki ya chama cha upinzani kuendesha shughuli zake za kisiasa. Kuna mambo machache ambayo haiyumkini yanapelekea kuwepo kwa dhamira hii njema, ambayo kwa uchache ni;
1. Nchi ikiwa na katazo la Rais la wanasiasa wa vyama vya kufanya siasa za wazi ili wapate kunadi sera, kuimarisha vyama vyao na kuongeza idadi ya wanachama
2. Nchi ikiwa na viongozi na wanachama wengi wa vyama vya upinzani wakiwa mahabusu huku wakikabiliwa na kesi zinazotokana na kuendesha shughuli zao halali za kisiasa.
3. Nchi ikiwa inakabiliwa na wakimbizi wengi wa kisiasa wanaoishi nje ya nchi kwa hofu ya usalama wa maisha yao, kwa sababu zitokanazo na shughuli zao za kisiasa.
4. Nchi ikiwa na watu wengi waliouawa, kujeruhiwa, kupata ulemavu kisa eti kutokana na hisia ya wao kuwa ni wapinzani wa chama tawala.
5. Nchi ikiwa na watu waliopoteza ajira, kushushwa vyeo, kuhamishwa katika maeneo yao ya kazi kutokana na misimamo yao ya itikadi za kisiasa.
6. Nchi kuwa na watu ambao akaunti zao za fedha, biashara ama vitega uchumi kuhujumiwa kutokana na misimamo yao ya itikadi za kisiasa.

Haya ndiyo mambo ya msingi ambayo yamepelea FAM na TAL kuweza kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na Rais SSH. Viongozi wa chama makini ambacho kimepitia changamoto nyingi zitokanazo na rafu mbaya za kisiasa katika kipindi cha awamu ya tano ya uongozi wa kiimla wa JPM hawawezi kukwepa kufanya hivyo. Nafasi nzuri ikitokea ya kuponya majeraha basi milango huwa wazi ili kurahisisha zoezi hilo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…