Katika jambo kubwa ninalojivunia, ni kutambua kuwa hakunaga UCHAWI

Katika jambo kubwa ninalojivunia, ni kutambua kuwa hakunaga UCHAWI

Niambie wapi nije supervision na vyombo vya habari unielezee vizuri ujibu na maswali yangu🤣
😂 Hapana, mtoto alikua anachezea cm, naona akaandika ivo, nimeelewa hakuna uchawi 🙌🏾🤣

Vyombo vya habari tena🏃🏾‍♀️🏃🏾‍♀️
 
Mkuu leo usiku nipo nawewe,, naamini kesho utakuja na uzi mpyaaaaa😎🤏🏾🤼‍♀️😌 wabishi kama nyie ndo tunawataka.
Naomba uwe na mimi Ms R , kama kweli upo serious.
 
Jambo kama wewe hujakutana nalo haimaanishi kwamba halipo.Siku ukikutana nalo ndio utajua.wale waliokutana nayo wanajua lipo.sasa ni ngumu kumuaminisha mtu kitu ambacho hajakishuhudia,Nawale waliokishuhudia uwaaminishe kua hakipo.
 
Kwa kweli nawashukuru wazazi wangu na Walezi wangu na babu wa babu zangu na bibi wa bibi zangu kwa kuwa hii ajenda haikuwa kabisa sehemu ya ukoo wetu si kwa baba si kwa mama.

Niliwahi kumuuliza babu yangu mmoja kuhusu je amewahi waona wachawi? Akiwa na miaka takribani 78 hivi na mimi nimeshamaliza Chuo kikuu udaktari alinijibu "hayo mambo mimi nayasikia tu stori kila mtu anasema naye kasikia, mimi sijayawahi hata yaona" RIP Babu yangu na Bibi yangu na wazazi wangu kwa ujumla, mlinifanya imara nitabaki kuwa imara daima.

Nawasihi wote tuepuke hizi fikra za Imani ya uchawi kwani ni adui wa maendeleo. Inawezekana kuendelea na kufanikiwa nje ya fikra hizi na nje ya kufanyiwa ushirikina shirikina.
Nachoona Madam ni unachanganya kati ya "Kiamini uchawi upo" na "Kuamini katika uchawi".....Katika hoja zako unaamini mtu kuamini uchawi upo basi eti anaamini katika uchawi kwamba hawezi fanikiwa bila uchawi nk sihivyo.

Mimi nadhani mapambano hayo unayolenga yalenge kwenye kupambana na fikra za kuamini katika uchawi ndio inaleta madhara katika jamii kama mauji ya albino nk na sio kupambana na watu kufuta imani kuwa uchawi upo hio imani inamzizi mzito wa imani ya kidini pia.

Mimi sijawai kuona tulip lolote la kichawi wala sina ushahidi wowote kushuhudia uchawi tangu nizaliwe ila naamini uchawi upo maana kitabu changu cha Dini ya kiislam kimesema upo, sasa kukataa kuwa haupo hii inakuwa ni sawa na kuoingana na maandiko ya kidini.

Pia nashangaa mtu anayesema anaamini MUNGU then anasema uchawi haupo hii inaonesha kuamini kwako Mungu kuna mashaka sana huna imani na wala huzingatii maandiko yake maana both Islamic and Christian writtings zime eleza uchawi upo.

Kwangu mtu anayeamini uchawi upo na haamini kwenye uchawi so perfect kuliko huyu ambae haamini kua uchawi upo.

Swali kwako Mdam:
Unaamini vipi dini yako na uamini uchawi.
 
Mheshimiwa,
Kuishi Tanzania na kuijua Tanzania hakumanishi Zambia haipo, maana yangu ni kwamba kutokupitia hali hiyo hakufanyi uchawi usiwepo.
Binafsi sishabikii uchawi wala ushirikina wa aina yeyote na wala haunipi hofu katika kufanya mambo yangu ila haimanishi haupo, maana hata kifo kipo lakini haimanishi niache kupambana kuishi vizuri.

Kuna elimu ya uchawi ngazi ya degree kabisa sio mambo ya kufikirika.

Elimu bora sio kuficha uchawi kwamba haupo ni kuhakikisha watu wanafanya mambo yao bila hofu ya uchawi na kutojiingiza huko kuharibu maendeleo na mambo chanya katika jamii.

Nimewasilisha.
Nimekusoma ila nami hoja yangu ni kuwa, imebaki kuwa dhana ambayo yule aiaminiye ana hasara. Hakuna kuendelea kupitia masharti ya dhana hiyo, halipo hilo. Wasome wapeane digrii ila mwisho wa siku wote hao wanafanya kazi halali na wasipofanya wanakufa masikini tu. Huku sasa kwetu, mtu hata elimu hiyo hana ila anasumbua watu wote na hela wanampelekea na anawatuma vitu vya ajabu. Akikamatwa kilio.

Niseme kuwa, nguvu iliyo ndani ya positive thinkers ni kubwa kuliko watu wanaodai kuwa na mambo hayo... The power of positive thinking iwafikie wote iwakomboe
 
Iwe club au elimu ila ni ya wachawi. LENGO langu sio kushabikia uchawi. Hayo mengine uko sahihi. Mambo hasi kwenye jamii ni mengi ni lazima tuyashinde ikiwemo na uchawi ili kuwe na jamii yenye maendeleo chanya.
Mkuu uchawi ni nini ?

Kwangu mimi kula rushwa, kuiba mali za watu, uongo uzandiki, kuchonganisha jamii kwamba bibi yako au shangazi yako ndio amekuroga, kutembea uchi kwenye nyumba za watu na kuchafua mazingira yao kufanya vitu visivyoeleweka (kwangu mimi huo ndio uchawi) na kuna sheria za kuweza kuwakabili hao watu sababu ni public nuisance na antisocial behavior

Sasa ukisema tuanze kuhukuma watu kwa definition yako ya uchawi sijui huyu ameingia kwangu ndio maana sipati mali au mtoto wangu kamuua au yule bibi mwenye macho mekundu ndio analeta mkosi mtaani tutaanza kuonea watu na ni hatari sana kwa wale watakaoonewa (persecution)
 
  • Thanks
Reactions: I M
Nimekusoma ila nami hoja yangu ni kuwa, imebaki kuwa dhana ambayo yule aiaminiye ana hasara. Hakuna kuendelea kupitia masharti ya dhana hiyo, halipo hilo. Wasome wapeane digrii ila mwisho wa siku wote hao wanafanya kazi halali na wasipofanya wanakufa masikini tu. Huku sasa kwetu, mtu hata elimu hiyo hana ila anasumbua watu wote na hela wanampelekea na anawatuma vitu vya ajabu. Akikamatwa kilio.

Niseme kuwa, nguvu iliyo ndani ya positive thinkers ni kubwa kuliko watu wanaodai kuwa na mambo hayo... The power of positive thinking iwafikie wote iwakomboe
Hapo nakuunga mkono asilimia zote
 
Nachoona Madam ni unachanganya kati ya "Kiamini uchawi upo" na "Kuamini katika uchawi".....Katika hoja zako unaamini mtu kuamini uchawi upo basi eti anaamini katika uchawi kwamba hawezi fanikiwa bila uchawi nk sihivyo.

Mimi nadhani mapambano hayo unayolenga yalenge kwenye kupambana na fikra za kuamini katika uchawi ndio inaleta madhara katika jamii kama mauji ya albino nk na sio kupambana na watu kufuta imani kuwa uchawi upo hio imani inamzizi mzito wa imani ya kidini pia.

Mimi sijawai kuona tulip lolote la kichawi wala sina ushahidi wowote kushuhudia uchawi tangu nizaliwe ila naamini uchawi upo maana kitabu changu cha Dini ya kiislam kimesema upo, sasa kukataa kuwa haupo hii inakuwa ni sawa na kuoingana na maandiko ya kidini.

Pia nashangaa mtu anayesema anaamini MUNGU then anasema uchawi haupo hii inaonesha kuamini kwako Mungu kuna mashaka sana huna imani na wala huzingatii maandiko yake maana both Islamic and Christian writtings zime eleza uchawi upo.

Kwangu mtu anayeamini uchawi upo na haamini kwenye uchawi so perfect kuliko huyu ambae haamini kua uchawi upo.

Swali kwako Mdam:
Unaamini vipi dini yako na uamini uchawi.
Swali zuri. Imani bila matendo ni bure. Sasa unaamini vipi mambo hujayaona? 😀

Mimi Dini naamini kama Silaha ya kunifanya niwe mtu mwema ambaye, nisiyopenda kutendewa mimi basi nisimfanyie mwingine. Naamini nilisikia njaa lazima niingie jikoni nipike nikitenge mezani jioe na siyo nikae namuomba Mungu akilete.... Kwa Imani yangu lakini. Na tangu nizaliwe mimi sijaona ile neema iliyoandikwa jangwani kuwa mikate ilishuka. Imeandikwa na maandiko naheshimu kuwa, ilikuwa neema ya Kizazi kile wakati ule kwa Sababu za wakati ule. Ila sasa hivi, bila kazi ya mikono yako na kuvipika viive.....😀 inakuwaje
 
Siku utakuja kuamka makaburini sijui utasema sleep walking
 
Ahsanteni sana jamani kwa kubadilishana mawazo. Haya ngoja wengine tuendelee na ratiba zingine, siku moja nitawaalika kwenye kongamano la mgongano wa fikra dhidi ya vikwazo vya maendeleo na ustawi wa jamii kwa jicho la ukatili utokanao na Imani potofu za kishirikina
 
Ahsanteni sana jamani kwa kubadilishana mawazo. Haya ngoja wengine tuendelee na ratiba zingine, siku moja nitawaalika kwenye kongamano la mgongano wa fikra dhidi ya vikwazo vya maendeleo na ustawi wa jamii kwa jicho la ukatili utokanao na Imani potofu za kishirikina
Andaa mh. Kongamano hilo tuje kubadilishana utambuzi na maarifa
 
Mkuu uchawi ni nini ?

Kwangu mimi kula rushwa, kuiba mali za watu, uongo uzandiki, kuchonganisha jamii kwamba bibi yako au shangazi yako ndio amekuroga, kutembea uchi kwenye nyumba za watu na kuchafua mazingira yao kufanya vitu visivyoeleweka (kwangu mimi huo ndio uchawi) na kuna sheria za kuweza kuwakabili hao watu sababu ni public nuisance na antisocial behavior

Sasa ukisema tuanze kuhukuma watu kwa definition yako ya uchawi sijui huyu ameingia kwangu ndio maana sipati mali au mtoto wangu kamuua au yule bibi mwenye macho mekundu ndio analeta mkosi mtaani tutaanza kuonea watu na ni hatari sana kwa wale watakaoonewa (persecution)
Mkuu,
Umeuliza uchawi ni nini, umetoa perception yako kuhusu uchawi na last paragraph I cannot relate. It seems, it's you against youself.
 
Back
Top Bottom