Kwani aliyeivamia Libya na kuivuruga ni waafrika "tuliokenua meno"? Kutoa statement kwa mambo ambayo huwezi kubadilisha nako ni kukosa akili. Tunapokaa kimya haimaanishi tunakubaliana na kila upuuzi wanaoufanya wengine. Ni vile kwamba kuna mambo yetu yanayotuhusu sana katika hayo wala hatusubiri statement kutoka kwa yeyote. Amini alipotuchokoza hatukusubiri statement na ile majuzi kuhusu magaidi wa Kibiti hatukusubiri statement.Sijui umeandika pumba gani..nam ni moja ya misimamo ya hovyo na ya kijinga.
Nikumbushe huyo jkn aliiunga mkono palestina zidi ya uvamizi wa Israel.
Pia huyo huyo jkn ndiye aliyekuwa mstari wa mbele kukomboa nchi zingize zidi ya ukoloni.
Kumbuka pia uvamizi wa libya etc tulikenua meno hiyo siyo nam ni unafiki na uoga kwasababu ya umasikini na ujinga waviongozi.
#MaendeleoHayanaChama
Hivi America huwa havamii nchi za watu,,??Ujinga
Take note: 2003 UN General Assembly lilipinga US kuivamia Iraq. US nao wala jinasibu kuwa UN ni irrelevant katika maslahi yake kiusalama - kama unavyodai hapa. Hivyo wakaivamia Iraq kinyume na UN Charter. Wakaishia kuadhirika.Kwanini nchi za kiafrika ziwe na umuhimu kama jambo linawafaidi tu wazungu na siyo vinginevyo?
UN haina nia njema na Afrika and it remains a tool for America and its allies to control other countries.
Of all the organisations, UN is the most bogus institution which must be either restructured or disbanded like yesterday.
Tatizo kubwa la Tanzania ni UJINGA ambo ndio sababu ya umasikini na maradhi.Hizo zote shobo.Mambo yao waachie wenyewe.
Badala ya kutumia fursa ya matajiri kuwa katika migogoro wenyewe kwa wenyewe ili nchi masikini ziamke kujitafuta, ndiyo kwanza tunazidi kufa njaa eti kisa matajiri wanapigana.
Ukishakuwa masikini uwezekano wa kuwa mpumbavu ni 90%.
Nipo busy na kutafuta ugali wangu sio kuingilia migogoro isiyonihusu.
Samahan mkuu kuna kikaoo chochote kilifanyika kupiga kura juu ya uvamizi wa US hapo Libya? au Sylia? Vilikuwa na matokeo gami? Hatua gani zilichukuliwa baada ya matokeo ya kura? Waliopiga kura kumuunga mkono gaidi wa uvamizi walikuwa na sabbau zipi?Niliweka thread humu JF kwamba suala la Urusi na Ukraine ni dogo sana kwa mtu asie na ukahaba wa kisiasa wa kufuata bwana atakaekupa maslahi bila kujali utu wa mtu huyo.
Nilisema wazi, leo hii wakati tunamkumbuka Nyerere tutafakari angesimamia wapi katika suala la Urusi na Ukraine. Nyerere alisema siku zote mipaka ya nchi zetu inayotambulika kimataifa tunaweza tusiipende, lakini sio sababu za kuvamia nchi nyingine.
Hilo moja, pili ni kwamba, hatupaswi kuwa watumwa wa nchi fulani kwa sababu ya misaada yake, kwamba kwa kuwa tunasaidiwa au tulisaidiwa na nchi fulani, basi hiyo nchi inapofanya mambo kinyume cha maumbile tutakuwa upande wake. Huo ni umalaya wa kisiasa. Dhambi ni dhambi, ifanywe na rafiki au adui.
Angalia kura zilivyopigwa Umoja wa Mataifa juu ya suala la Urusi na Ukraine, na angalia Tanzania ilisimamia wapi. Aibu tupu kwa nchi iliyojiita nchi ya mstari wa mbele kwenye ukombozi wa nchi nyingine. Nasema wazi, tulichofanya hapa ni umalaya wa siasa za kimataifa
Katika hotuba ya mwisho ya Nyerere Umoja wa Mataifa, alisema hiki anachofanya Samia leo hatutafanya hata siku moja! Lakini ndio hivyo tena. Tunafanya. Samia ame-surrender our freedom and dignity. Angalia video hapo chini.
Nchi kama Zambia, Kenya, Rwanda nk wanajitambua sana
View attachment 2387354
Msimamo wa nchi za Afrika juu ya suala la Urusi na Ukraine ni jambo dogo sana linalopaswa kuongozwa na kanuni, sio maslahi ya nchi zetu
Amesimama vizuri Raisi wetu...Unamtukuza Nyerere lkn hujui philosophy zake. Nyerere ndo mwanzilishi na muumini wa "siasa za kutofungamana na uoande wowote" na huo ndo msingi wa Tanzania. Ulitaka Samia aende kinyume na misingi yenu alafu muanze kumnanga?!
Acha theory, ongelea msimamo wa Nyerere kwenye hiliKwa hiyo wewe unaamini Nyerere alikuwa sahihi kwa kila alichosimamia? Kumbuka alikuwa binadamu, hivyo kukosea si ajabu. Hivyo inawezekana kabisa kuna baadhi ya misimamo yake haikua sahihi, au huenda ilikuwa sahihi kwa nyakati zile, lakini kwa sasa ikawa kinyume chake.
Ndio Mkuu, vilifanyika, na kura zilipigwa. Ila sikumbuki kama Tanzania ilipinga US na washirika wake kuvamia Iraq na LibyaSamahan mkuu kuna kikaoo chochote kilifanyika kupiga kura juu ya uvamizi wa US hapo Libya? au Sylia? Vilikuwa na matokeo gami? Hatua gani zilichukuliwa baada ya matokeo ya kura? Waliopiga kura kumuunga mkono gaidi wa uvamizi walikuwa na sabbau zipi?
Najua, ila wasiwasi hapa ni kama wewe Mkuu unajua ninachosema? Alichosema Nyerere na kushangiliwa na kila nchi kwa nguvu sana? Unaelewa?Mleta mada sijui kama unajua unachosema.
Kutokuwapo ni kupiga kura pia.Nadhani ni afadhali hata tusingekuwapo wakati wa huu mkutano uliopiga hii kura ili ijulikane hatukuwapo, kama ilivyokuwa kwa Ethiopia, Togo nk. Hivi hizi ndio siasa za kimataifa za Samia? Very very sad. Pathetic indeed.
Teh kisa humsapoti marekani na wenzieYou have surrendered your freedom and dignity, you are not fit to be called a human being
Hivi unajua aliefanya mauaji ya Wasijulikana kusimamishwa wakati wa Magufuli? Ni USA, na ndio hata wakampiga vikwazo kwenda USA, yeye na mke wake.Naiunga mkono Tanzani 100%. Tuwaache hao nguruwe waupe wauane tu wao kwa wao na wao wajue raha ya vita na ukimbizi. On the other hand Zele kaiuza nchi yake kwa mabwana zake yeye mwenyewe. Ajitetee mwenyewe
Kuna viini macho vingi ila karibuni mambo yatajitokeza.....Najua, ila wasiwasi hapa ni kama wewe Mkuu unajua ninachosema? Alichosema Nyerere na kushangiliwa na kila nchi kwa nguvu sana? Unaelewa?