Katika nchi 35 zilizokataa kupiga kura suala la Urusi kuvamia Ukraine 50% ni za Afrika, ikiwemo Tanzania

Katika nchi 35 zilizokataa kupiga kura suala la Urusi kuvamia Ukraine 50% ni za Afrika, ikiwemo Tanzania

Nilimsikia waziri wa mambo ya nje wa Ukraine akidai kwamba kwa kila missile moja ya Urusi inayoilipua Ukraine ubora wa maisha ya watu wa Afrika unaathirika. Sasa sijui pia tumwambie kwa kila round ya mizinga Ukraine wanayoirusha dhidi ya Urusi ubora wa maisha ya waafrika pia yanaathirika? Dharau ya watu weupe dhidi ya waafrika inazidi kujionyesha hapa. Yaani kila ujinga na upuuzi wanaoufanya Ulaya wanataka kuiingiza Afrika humo. Kila kibaya kinachoikuta dunia (corona, vita, mabadiliko tabia nchi) haya majamaa yanataka kuifanya Afrika jalala. Na stupid Africans wanayapa support. Stupid.
 
Sijui umeandika pumba gani..nam ni moja ya misimamo ya hovyo na ya kijinga.

Nikumbushe huyo jkn aliiunga mkono palestina zidi ya uvamizi wa Israel.

Pia huyo huyo jkn ndiye aliyekuwa mstari wa mbele kukomboa nchi zingize zidi ya ukoloni.

Kumbuka pia uvamizi wa libya etc tulikenua meno hiyo siyo nam ni unafiki na uoga kwasababu ya umasikini na ujinga waviongozi.

#MaendeleoHayanaChama
Kwani aliyeivamia Libya na kuivuruga ni waafrika "tuliokenua meno"? Kutoa statement kwa mambo ambayo huwezi kubadilisha nako ni kukosa akili. Tunapokaa kimya haimaanishi tunakubaliana na kila upuuzi wanaoufanya wengine. Ni vile kwamba kuna mambo yetu yanayotuhusu sana katika hayo wala hatusubiri statement kutoka kwa yeyote. Amini alipotuchokoza hatukusubiri statement na ile majuzi kuhusu magaidi wa Kibiti hatukusubiri statement.
 
Nchi ambazo hazikuunga mkono azimio la kuilaani urusi ni 35 tu, lakini hizo nchi 35 zina watu wengi sana kinachozidi nusu ya watu waliomo duniani! Hii ni kwa sababu China na India zimo humo!!
 
Afrika ndiko zilikojaa tawala za kidikteta, nchi zenye marais miungu watu, sawa na ilivyo Russia, North Korea na China. Ni lazima tawala hizizisimame na dikteta mwenzao.
 
Kwanini nchi za kiafrika ziwe na umuhimu kama jambo linawafaidi tu wazungu na siyo vinginevyo?

UN haina nia njema na Afrika and it remains a tool for America and its allies to control other countries.

Of all the organisations, UN is the most bogus institution which must be either restructured or disbanded like yesterday.
Take note: 2003 UN General Assembly lilipinga US kuivamia Iraq. US nao wala jinasibu kuwa UN ni irrelevant katika maslahi yake kiusalama - kama unavyodai hapa. Hivyo wakaivamia Iraq kinyume na UN Charter. Wakaishia kuadhirika.

Madikteta wa Afrika wanajisikia comfortable kuambatana na Putin na Xi ili kupata utetezi. Lakini wamelundika pesa na assests wanazotuibia huko US na Western Europe! Hakuna anayeweza pesa wala kwenda Urusi au China kutalii. Ndio sababu ya Trump kutuita SHTHLS.
 
Naiunga mkono Tanzani 100%. Tuwaache hao nguruwe waupe wauane tu wao kwa wao na wao wajue raha ya vita na ukimbizi. On the other hand Zele kaiuza nchi yake kwa mabwana zake yeye mwenyewe. Ajitetee mwenyewe
 
Hizo zote shobo.Mambo yao waachie wenyewe.

Badala ya kutumia fursa ya matajiri kuwa katika migogoro wenyewe kwa wenyewe ili nchi masikini ziamke kujitafuta, ndiyo kwanza tunazidi kufa njaa eti kisa matajiri wanapigana.

Ukishakuwa masikini uwezekano wa kuwa mpumbavu ni 90%.

Nipo busy na kutafuta ugali wangu sio kuingilia migogoro isiyonihusu.
Tatizo kubwa la Tanzania ni UJINGA ambo ndio sababu ya umasikini na maradhi.
 
Niliweka thread humu JF kwamba suala la Urusi na Ukraine ni dogo sana kwa mtu asie na ukahaba wa kisiasa wa kufuata bwana atakaekupa maslahi bila kujali utu wa mtu huyo.

Nilisema wazi, leo hii wakati tunamkumbuka Nyerere tutafakari angesimamia wapi katika suala la Urusi na Ukraine. Nyerere alisema siku zote mipaka ya nchi zetu inayotambulika kimataifa tunaweza tusiipende, lakini sio sababu za kuvamia nchi nyingine.

Hilo moja, pili ni kwamba, hatupaswi kuwa watumwa wa nchi fulani kwa sababu ya misaada yake, kwamba kwa kuwa tunasaidiwa au tulisaidiwa na nchi fulani, basi hiyo nchi inapofanya mambo kinyume cha maumbile tutakuwa upande wake. Huo ni umalaya wa kisiasa. Dhambi ni dhambi, ifanywe na rafiki au adui.

Angalia kura zilivyopigwa Umoja wa Mataifa juu ya suala la Urusi na Ukraine, na angalia Tanzania ilisimamia wapi. Aibu tupu kwa nchi iliyojiita nchi ya mstari wa mbele kwenye ukombozi wa nchi nyingine. Nasema wazi, tulichofanya hapa ni umalaya wa siasa za kimataifa

Katika hotuba ya mwisho ya Nyerere Umoja wa Mataifa, alisema hiki anachofanya Samia leo hatutafanya hata siku moja! Lakini ndio hivyo tena. Tunafanya. Samia ame-surrender our freedom and dignity. Angalia video hapo chini.

Nchi kama Zambia, Kenya, Rwanda nk wanajitambua sana

View attachment 2387354

Msimamo wa nchi za Afrika juu ya suala la Urusi na Ukraine ni jambo dogo sana linalopaswa kuongozwa na kanuni, sio maslahi ya nchi zetu

Samahan mkuu kuna kikaoo chochote kilifanyika kupiga kura juu ya uvamizi wa US hapo Libya? au Sylia? Vilikuwa na matokeo gami? Hatua gani zilichukuliwa baada ya matokeo ya kura? Waliopiga kura kumuunga mkono gaidi wa uvamizi walikuwa na sabbau zipi?
 
Hatuna kiongozi sasa hivi tuna incompetent kule juu, suala liko wazi mbona hata kama una penda misaada sio Kwa kiasi hicho, hatujui tusimamie wapi, hata kama una pewa misaada lazima ifike mahali useme hapana Kwa jambo fulani, otherwise una kuwa mtumwa, halafu Kwa nini uwaze misaada miaka yote so utafute pesa zako mwenyewe?
 
Unamtukuza Nyerere lkn hujui philosophy zake. Nyerere ndo mwanzilishi na muumini wa "siasa za kutofungamana na uoande wowote" na huo ndo msingi wa Tanzania. Ulitaka Samia aende kinyume na misingi yenu alafu muanze kumnanga?!
Amesimama vizuri Raisi wetu...
 
Kwa hiyo wewe unaamini Nyerere alikuwa sahihi kwa kila alichosimamia? Kumbuka alikuwa binadamu, hivyo kukosea si ajabu. Hivyo inawezekana kabisa kuna baadhi ya misimamo yake haikua sahihi, au huenda ilikuwa sahihi kwa nyakati zile, lakini kwa sasa ikawa kinyume chake.
Acha theory, ongelea msimamo wa Nyerere kwenye hili
 
Samahan mkuu kuna kikaoo chochote kilifanyika kupiga kura juu ya uvamizi wa US hapo Libya? au Sylia? Vilikuwa na matokeo gami? Hatua gani zilichukuliwa baada ya matokeo ya kura? Waliopiga kura kumuunga mkono gaidi wa uvamizi walikuwa na sabbau zipi?
Ndio Mkuu, vilifanyika, na kura zilipigwa. Ila sikumbuki kama Tanzania ilipinga US na washirika wake kuvamia Iraq na Libya
 
Nadhani ni afadhali hata tusingekuwapo wakati wa huu mkutano uliopiga hii kura ili ijulikane hatukuwapo, kama ilivyokuwa kwa Ethiopia, Togo nk. Hivi hizi ndio siasa za kimataifa za Samia? Very very sad. Pathetic indeed.
Kutokuwapo ni kupiga kura pia.

Ni kupiga kura kwamba hujali matokeo ya kura.
 
Naiunga mkono Tanzani 100%. Tuwaache hao nguruwe waupe wauane tu wao kwa wao na wao wajue raha ya vita na ukimbizi. On the other hand Zele kaiuza nchi yake kwa mabwana zake yeye mwenyewe. Ajitetee mwenyewe
Hivi unajua aliefanya mauaji ya Wasijulikana kusimamishwa wakati wa Magufuli? Ni USA, na ndio hata wakampiga vikwazo kwenda USA, yeye na mke wake.

Sasa vipi kama USA wangesema haituhusu hilo ni suala la ndani la Tanzania? Wewe humu ndani hujalaani kupotezewa kwa Ben Sanane - au hilo pia halikuhusu?

Panapokuwa na ukosefu wa haki za binadamu huwezi kukaa kimya kama una akili sawa
 
Najua, ila wasiwasi hapa ni kama wewe Mkuu unajua ninachosema? Alichosema Nyerere na kushangiliwa na kila nchi kwa nguvu sana? Unaelewa?
Kuna viini macho vingi ila karibuni mambo yatajitokeza.....
 
Back
Top Bottom