Ni ukweli uliowazi Sasa kwamba mgombea Urais kupitia Chadema Tundu Lissu ni kama amewameza wagombea wenzake na hawasikiki tena.
Tangu ateuliwe na chama chake CHADEMA na kisha kuchukua fomu za kuteuliwa kutoka tume ya uchaguzi NEC Lissu amekuwa gumzo kila kona huku akijadiliwa zaidi kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii.
Lissu amekuwa akifanya ziara mikoa mbalimbali ya kusaka wadhamini huku akilakiwa na Maelfu kwa maelfu kokote anakopita.
Mojawapo ya sababu kubwa ya kupata uungwaji mkono huo kutoka kwa wananchi hasa waliohojiwa kila anakopita ni kauli Mbiu yake ya 'Uhuru na Kazi' akimaanisha pamoja na kutakiwa kufanya kazi lakini katika serikali yake wananchi watakuwa huru hasa katika kufanya siasa, kupata habari mbalimbali bila ubaguzi, vyombo vya Habari kuwa huru bila kufungiwa hovyo, waandishi wa habari kutokunyanyaswa na watu kuwa huru kukosoa serikali yao bila kuogopa kukamatwa na kufungwa.
Pia Lissu amekuwa akijinasibu katika serikali yake ni mwiko kuingilia Bunge na mahakama bali kuiacha mihimili hiyo kuwa huru katika maamuzi yake. Pia wananchi kuwa huru kuangalia LIVE Bunge lao.
Mgombea huyo wa Chadema anasema kutaka watu wafanye kazi tu huku ukiwanyima Uhuru wao ni dhambi kubwa ambayo kamwe serikali yake haitafanya.
Tangu ateuliwe na chama chake CHADEMA na kisha kuchukua fomu za kuteuliwa kutoka tume ya uchaguzi NEC Lissu amekuwa gumzo kila kona huku akijadiliwa zaidi kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii.
Lissu amekuwa akifanya ziara mikoa mbalimbali ya kusaka wadhamini huku akilakiwa na Maelfu kwa maelfu kokote anakopita.
Mojawapo ya sababu kubwa ya kupata uungwaji mkono huo kutoka kwa wananchi hasa waliohojiwa kila anakopita ni kauli Mbiu yake ya 'Uhuru na Kazi' akimaanisha pamoja na kutakiwa kufanya kazi lakini katika serikali yake wananchi watakuwa huru hasa katika kufanya siasa, kupata habari mbalimbali bila ubaguzi, vyombo vya Habari kuwa huru bila kufungiwa hovyo, waandishi wa habari kutokunyanyaswa na watu kuwa huru kukosoa serikali yao bila kuogopa kukamatwa na kufungwa.
Pia Lissu amekuwa akijinasibu katika serikali yake ni mwiko kuingilia Bunge na mahakama bali kuiacha mihimili hiyo kuwa huru katika maamuzi yake. Pia wananchi kuwa huru kuangalia LIVE Bunge lao.
Mgombea huyo wa Chadema anasema kutaka watu wafanye kazi tu huku ukiwanyima Uhuru wao ni dhambi kubwa ambayo kamwe serikali yake haitafanya.