Kauli ya Chongolo ni ufedhuli kwa wasomi wa vyuo vikuu. Ipingwe!

Kauli ya Chongolo ni ufedhuli kwa wasomi wa vyuo vikuu. Ipingwe!

Chongolo amewataka wasomi wa vyuo vikuu kwenda veta ili wakapate uwezo wa kujiajiri.

Kauli hii inatoa tafsiri hasi nyingi sana dhidi ya wasomi wa vyuo vikuu na vyuo vikuu vyenyewe.

Mosi, inatoa tafsiri kwamba elimu ya vyuo vikuu ni dhaifu ukilinganisha na ile ya veta. Kama hivi ndivyo. Je, malengo ya utoaji wa elimu ya vyuo vikuu yamefikiwa? Ikiwa bado hayajafikiwa ni nani wa kulaumiwa, kama siyo CCM na wanaccm?

Pili, inatoa tafsiri kwamba waliohitimu veta wana uwezo wa kujiajiri kuliko waliohitimu vyuo vikuul. Binafsi naona kuwa haya ni madhara ya kusema kabla ya kufanya utafiti. Huku mitaani tunaona watu wengi waliojiri ni wale ambao hawajaenda veta wala vyuo vikuu.

Sasa Chongolo atuambie hawa waliupata wapi uwezo huu? Je, ni shule ya msingi? Kama ndivyo atoe kauli nyingine.

Natoa wito kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini kuandaa maandamano kupinga kauli hii inayotweza na kuidhalilisha elimu ya daraja la juu kabisa duniani. Mkikaa kimya CCM haikawii kuwafanya muonekane kama wahitimu wa darasa la saba.

Yaani Chongolo anawafanya ninyi wasomi wenye madigrii kuwa ni mbumbumbu kuliko kijana wa darasa la nne aliyehitimu ufundi uashi?

MSIKUBALI!
Haya tena! Hapo bosi wako Lucas Mwashambwa anakupa ushauri wa bure kuwa uache maisha ya uchawa, na kisha uende VETA ili uanze mafunzo ya awali ya kuwa fundi mchundo.
 
Haya tena! Hapo bosi wako Lucas Mwashambwa anakupa ushauri wa bure kuwa uache maisha ya uchawa, na kisha uende VETA ili uanze mafunzo ya awali ya kuwa fundi mchundo.
CCM inawafanya watanzania kuwa mazuzu.
 
Chongolo amewataka wasomi wa vyuo vikuu kwenda veta ili wakapate uwezo wa kujiajiri.

Kauli hii inatoa tafsiri hasi nyingi sana dhidi ya wasomi wa vyuo vikuu na vyuo vikuu vyenyewe.

Mosi, inatoa tafsiri kwamba elimu ya vyuo vikuu ni dhaifu ukilinganisha na ile ya veta. Kama hivi ndivyo. Je, malengo ya utoaji wa elimu ya vyuo vikuu yamefikiwa? Ikiwa bado hayajafikiwa ni nani wa kulaumiwa, kama siyo CCM na wanaccm?

Pili, inatoa tafsiri kwamba waliohitimu veta wana uwezo wa kujiajiri kuliko waliohitimu vyuo vikuul. Binafsi naona kuwa haya ni madhara ya kusema kabla ya kufanya utafiti. Huku mitaani tunaona watu wengi waliojiri ni wale ambao hawajaenda veta wala vyuo vikuu.

Sasa Chongolo atuambie hawa waliupata wapi uwezo huu? Je, ni shule ya msingi? Kama ndivyo atoe kauli nyingine.

Natoa wito kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini kuandaa maandamano kupinga kauli hii inayotweza na kuidhalilisha elimu ya daraja la juu kabisa duniani. Mkikaa kimya CCM haikawii kuwafanya muonekane kama wahitimu wa darasa la saba.

Yaani Chongolo anawafanya ninyi wasomi wenye madigrii kuwa ni mbumbumbu kuliko kijana wa darasa la nne aliyehitimu ufundi uashi?

MSIKUBALI!
JamiiForums1906236051_512x340.jpg
 
Chongolo amewataka wasomi wa vyuo vikuu kwenda veta ili wakapate uwezo wa kujiajiri.

Kauli hii inatoa tafsiri hasi nyingi sana dhidi ya wasomi wa vyuo vikuu na vyuo vikuu vyenyewe.

Mosi, inatoa tafsiri kwamba elimu ya vyuo vikuu ni dhaifu ukilinganisha na ile ya veta. Kama hivi ndivyo. Je, malengo ya utoaji wa elimu ya vyuo vikuu yamefikiwa? Ikiwa bado hayajafikiwa ni nani wa kulaumiwa, kama siyo CCM na wanaccm?

Pili, inatoa tafsiri kwamba waliohitimu veta wana uwezo wa kujiajiri kuliko waliohitimu vyuo vikuul. Binafsi naona kuwa haya ni madhara ya kusema kabla ya kufanya utafiti. Huku mitaani tunaona watu wengi waliojiri ni wale ambao hawajaenda veta wala vyuo vikuu.

Sasa Chongolo atuambie hawa waliupata wapi uwezo huu? Je, ni shule ya msingi? Kama ndivyo atoe kauli nyingine.

Natoa wito kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini kuandaa maandamano kupinga kauli hii inayotweza na kuidhalilisha elimu ya daraja la juu kabisa duniani. Mkikaa kimya CCM haikawii kuwafanya muonekane kama wahitimu wa darasa la saba.

Yaani Chongolo anawafanya ninyi wasomi wenye madigrii kuwa ni mbumbumbu kuliko kijana wa darasa la nne aliyehitimu ufundi uashi?

MSIKUBALI!
Nasubiri tamko la wahitimu wa vyuo kama walivyotoa Watukufu waendesha Bodaboda. Vinginevyo tutaamini tamko la Bodaboda ni la UV CCM.
 
Chongolo amewataka wasomi wa vyuo vikuu kwenda veta ili wakapate uwezo wa kujiajiri.

Kauli hii inatoa tafsiri hasi nyingi sana dhidi ya wasomi wa vyuo vikuu na vyuo vikuu vyenyewe.

Mosi, inatoa tafsiri kwamba elimu ya vyuo vikuu ni dhaifu ukilinganisha na ile ya veta. Kama hivi ndivyo. Je, malengo ya utoaji wa elimu ya vyuo vikuu yamefikiwa? Ikiwa bado hayajafikiwa ni nani wa kulaumiwa, kama siyo CCM na wanaccm?

Pili, inatoa tafsiri kwamba waliohitimu veta wana uwezo wa kujiajiri kuliko waliohitimu vyuo vikuul. Binafsi naona kuwa haya ni madhara ya kusema kabla ya kufanya utafiti. Huku mitaani tunaona watu wengi waliojiri ni wale ambao hawajaenda veta wala vyuo vikuu.

Sasa Chongolo atuambie hawa waliupata wapi uwezo huu? Je, ni shule ya msingi? Kama ndivyo atoe kauli nyingine.

Natoa wito kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini kuandaa maandamano kupinga kauli hii inayotweza na kuidhalilisha elimu ya daraja la juu kabisa duniani. Mkikaa kimya CCM haikawii kuwafanya muonekane kama wahitimu wa darasa la saba.

Yaani Chongolo anawafanya ninyi wasomi wenye madigrii kuwa ni mbumbumbu kuliko kijana wa darasa la nne aliyehitimu ufundi uashi?

MSIKUBALI!
Tusaidie- wanao maliza shahada ya sheria na kwenda shule ya sheria unawaweka wapi?
 
Huo ndio ukweli ndugu, mtu aliehitimu VETA ni bora kwa kila kitu ukilinganisha na wa chuo kikuu, ndivyo ilivyo, The way the cookie crumbles..

Punguza uongo, huko VETA wanafundishwa na walimu waliotoka vyuo vikuu, nani Bora hapo, acheni kudhalilisha vyuo vikuu kwa kuvilinganisha na VETA.
 
Mimi ningeshauri serikali kwa vile vyuo vyetu vingi havina sehemu za kufanyia tafiti (research centers) basi watu waliokaa kwenye kazi (field) kwa muda mrefu sana ndo warusishwe vyuoni wakafundishe siyo mtu amebakishwa tutorial..within 5years tayari ni lecture kisa amechukua masters na phd tayari. mfano. Akina Kibatara and likes wakatoe elimu ya sheria huko chuo kikuu..

Wale wataalam wanaotengeneza mitambo ya gesi pale kinyerezi na waotengeneza and the likes wakafundishe chuo kikuu.

Wale wahasibu wabobezi warudi wakafundishe.
Wale wataalam wa mabarabara na ujenzi walioko kwenye field muda mrefu wakafundishe.

Wale miners wabobezi kule GGM na Nyamongo warudishwe wakafundishe...

Tuachaneni na Hao wahadhiri ambao vichwa vyao vimeota kutu na hawafanyi vitu kwa vitendo kwasababu hawaoni vitu katika uhalisia...tuchukue watu waliopo kwenye field. Haiwezekani mwanafunzi amemaliza chuo lakini akipewa mtihani kwa vitendo anaonekana kichekesho..
Hao ndio waliopewa Nchi na mawazo yao ndio haya.

Tz ni zaidi ya uijuavyo.
 
Takataka tupu vyuo vikuuu nani aandamane? kwanza kuna University students wangapi wamejiunga humu au wanasikiliza TV/Radio kujua what is going around thw clock? ? Huu ni ukumbi ambapo mtu unaweza kutoa sauti yako ikasikika! Muulize aliye karibu nawe kama ni member wa JF?

Pili wahadhiri sasa wana wa treat university students kama watoto wa sekondari. Ile heshima ya University haiko tena. WAULIZE VIJANA WA MAZIMBU SUA wanavyokuwa treated, kama watoto wa sekondari. Wanawanyanyasa watoto na mitihani kwa kuwaambia kuwa nahakikisha hutoki hapa kama hujanipa ngono. Nina mifano ya wazi! Nani awakemee

Tatu hata hao wahadhiri wenyewe ni wa mchongo! Ni chekechea hivyo hivyo! Hakuna mwenye sifa/hadhi ya kuwa Lecturer wa chuo kikuu. Kama wako ni very few. Si tunawaona products wanazozitoa....

Mwisho Chongole tunaomba CV yake. naye ni wa mchongo hivyo hivyo. Yuko pale kwa undungunisation wa samia!

Tofautisha quality ya mwanafunzi na qualification ya lecturer. Huwezi kuwa lecturer bila vigezo vya TCU. Lakini quality ya wanafunzi inaanzia mbali.
 
Weka ushabiki wa kivyama pembeni, utaona mantiki halisi ya aliyoysema Katibu Mkuu huyo.

Kuwa na digrii si hoja, hoja ni kuwa na uwezo wa kujiajiri.

Mtu mwenye ujuzi wake toka Veta wa kuunganisha mabomba ya maji taka, na mtu aliye na digrii ya political sayansi ni yupi aliye na urahisi wa kujiajiri mwenyewe?

Na itanoga zaidi, kama huyu msomi wa political sayansi akawa na ujuzi wa kutengeneza vitu na kuitumia kwa upana zaidi hiyo digrii yake, badala ya kukaa nayo tu akiilea huku akiwa tegemezi kwa wengine.

Digrii kwa siku hizi siyo nyenzo tena ya kupatia kazi.

Wewe ndio unapotosha. Tofautisha employment opportunities na academic opportunities. Huwezi kumdhihaki mtu aliyesoma political science kisa hawezi kujiajiri, unatakiwa kujiuliza aliposoma political science alikuwa na lengo la kujiajiri au kuajiriwa?. Kama kuajiriwa achana naye. Huwezi kucheka academic opportunities kwa sababu ya employment opportunity ya plumbing.
 
Painting & Sign writing (PS)
Kuna dogo anasomea hii course hapo UDSM, sasa akimaliza inabidi aelekee VETA akasome tena kwa mara ya pili?

Wewe kiazi mviringo ongea vizuri na Serikali yako ipanue wigo wa fikra za viongozi sio wanawaza kupokea Posho & Mishahara inachangiwa na walipa Kodi alafu hawafanyi utatuzi wa Ajira zaidi ya kuwafukuzia watu VETA ndio maana naona vyuo vya VETA vinajengwa kwa kasi sana kumbe fikra zao ndio zimeelekea huko?
 
Mtoa mada nahisi uelewa wako ni mdogo na unapenda kukurupuka.Punguza mhemko na papara.Bandiko lako lote limekosa mantiki.

Kupata ajira kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa changamoto karibu dunia nzima!!!!!!!!!!Kwa utamaduni wa elimu yetu humuandaa mwanafunzi kuajiriwa, kwamba ukimaliza masomo yako utakutana na ajira!!!!!!!!!! Hizi zama zimepita na hazitarudi tena!!!!!!!!!!!

Ajira zimekuwa ngumu lakini shughuli za kufanya ziko nyingi!!!!!!!!!!!!!!! Huko vyuo vikuu asilimia kubwa ya mafunzo hasa wanaochukua masomo ya sanaa na hata sayansi hakuna ujuzi wa mikono unaofundishwa zaidi ya kukariri vitini!!!!!!!!!!!!!

Huyu mhitimu akitoka huko hatakuwa na uwezo mkubwa wa kujishughulisha na shughuli mbalimbali ambazo nyingi hutumia ujuzi wa mikono!!!!!!!!!!!

Veta kuna mafunzo mbalimbali ya muda mfupi sana na muda mrefu ambayo kwa kiasi kikubwa hutumia ujuzi wa mikono ambao haupatikani kwa wanafunzi wengi huko vyuoni. Mfano wa mafunzo hayo ni:

Masonry & Bricklaying (MB)

Carpentry & Joinery (CJ)

Road Construction & Maintenance (RCM)

Civil Draughting (CD)

Painting & Sign writing (PS)

Welding & Fabrication (WF)

Fitter Mechanics (FM)

Meat Processing Technology (MPT)

Electronics (ELEC)

Motor Vehicle Mechanics (MVM)

Electrical Installation (EL)

Food Production (FP)

Food & Beverage Services & Sales (FBSS)

Front Office Operations (FO)

Plumbing & Pipe fitting (PPF).

Ukipata haya mafunzo ambayo huchukua muda mfupi utakuwa na uwanda mpana wa kujishughulisha wakati unasubiria muujiza wa ajira!!!!!!!!!!!

Nb 1: Zama zimebadilika. Tujifunze kubadilika!!!!!!!!!

Nb 2: Maarifa ya darasani hutumika kidogo sana mtaani!!!!!!!!!!!!!!

Nb 3: Mtaa una kanuni, sheria na taratibu zake ambazo hutafundishwa chuoni!!!!!!!!!!

Ni mtazamo!!!!!!!!!!!!!!!!

Vyote ulivyoandika hapo na zaidi vinafundishwa chuo kikuu. Tofautisha employment opportunities na academic opportunities.

Tusilazimishe kuidharau academic opportunity kisa haina employment opportunity, tutaaanguka pabaya. Kuwaambia graduates wa uhasibu au procurement kwamba turudi VETA tukasome ujenzi wa nyumba ni sawa nakuua profession yao.
 
Ukiweka siasa pembeni ndugu Chongolo yupo sahihi kabisa.

Hawa wahitimu lazima wawe na skills nyingine za kuleta ugali mezani .

VETA isimame Kama VETA , na Vyuo vikuu visimame Kama vyuo vikuu, tukianza ujinga wa kuonesha VETA ni Bora kuliko chuo kikuu ndio tutaua kila kitu.
 
Chongolo amewataka wasomi wa vyuo vikuu kwenda veta ili wakapate uwezo wa kujiajiri.

Kauli hii inatoa tafsiri hasi nyingi sana dhidi ya wasomi wa vyuo vikuu na vyuo vikuu vyenyewe.

Mosi, inatoa tafsiri kwamba elimu ya vyuo vikuu ni dhaifu ukilinganisha na ile ya veta. Kama hivi ndivyo. Je, malengo ya utoaji wa elimu ya vyuo vikuu yamefikiwa? Ikiwa bado hayajafikiwa ni nani wa kulaumiwa, kama siyo CCM na wanaccm?

Pili, inatoa tafsiri kwamba waliohitimu veta wana uwezo wa kujiajiri kuliko waliohitimu vyuo vikuul. Binafsi naona kuwa haya ni madhara ya kusema kabla ya kufanya utafiti. Huku mitaani tunaona watu wengi waliojiri ni wale ambao hawajaenda veta wala vyuo vikuu.

Sasa Chongolo atuambie hawa waliupata wapi uwezo huu? Je, ni shule ya msingi? Kama ndivyo atoe kauli nyingine.

Natoa wito kwa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini kuandaa maandamano kupinga kauli hii inayotweza na kuidhalilisha elimu ya daraja la juu kabisa duniani. Mkikaa kimya CCM haikawii kuwafanya muonekane kama wahitimu wa darasa la saba.

Yaani Chongolo anawafanya ninyi wasomi wenye madigrii kuwa ni mbumbumbu kuliko kijana wa darasa la nne aliyehitimu ufundi uashi?

MSIKUBALI!
Katika wasomi, Chongolo hayumo kabisaa.
Na karibu atapewa PhD ya Heshima na VETA.
 
Kama vip elimu ya. Vyuo vikuu ifutwe sasa,ili watu wote wenye shida na shule waende veta,maana wasomi wa vyuo vikuu Wana pondwa na kulushiwa mawe kutoka Kila Kona.
 
Yaani watanzania tuna Shida, watu wanadhani Chongolo amekosea lakini mimi sioni jipya huko vyuo vikuu haswa Kwa baadhi ya kozi maana ziko ki nadharia tu Wala hazina mchango wa maana . Mtu aliyeenda Veta ni Bora zaidi kuliko KWENDA ELIMU ya juu haswa Tanzania

Wewe ndio mwenye shida. Kila chuo kina muda wa practicals, kila course, Sasa nadharia imetoka wapi?. Kwa maono yako graduates wa SUA, Bugando, Muhimbili, UDSM, Mzumbe hawana maana, ila std seven aliyeenda VETA na kufundishwa na graduate wa chuo kikuu ndio wa maana. Punguza unafiki. Mnatukana elimu kisa ajira hamna. Kwenu elimu Ni ajira tu, punguza mhemko, Yani vyuo vyote havina maana kisa
 
"waliohitimu veta wana uwezo wa kujiajiri kuliko waliohitimu vyuo vikuu", kwa hili yuko sahihi, huku kwetu ukihitimu chuo kikuu unategemea uwe mtawala na si mshika spana na nyundo! Tangu tuanze kuwa na vyuo vikuu mpaka sasa hatuna hata kitu kimoja cha kumbukumbu kilchoundwa na wahitimu wa vyuo vikuu!

Hao VETA wanafundishwa na wahitimu wa vyuo vikuu, sasa sijui unongea Nini. Tatizo mnashabikia kauli za wanasiasa bila kufanya utafiti.
 
Back
Top Bottom