Kauli ya Lissu ya Rais Mzanzibar ni matokeo ya kufumba masikio Tanganyika kuwa na Serikali yake na viongozi wake watakaoamua mambo yao, asilaumiwe!

sijui ulipokuwa unaandika hii ulikuwa usingizini au vipi kijana wa zamani? Ati tumewatawalaje sasa, kwani Zanzibar ina uwezo wa kuchagua raisi, si huwa wanachaguliwa na nyinyi wabara au umesahau?

Hiyo misitu yenu na mashamba makubwa na kila aina za madini mbona munalia njaa na bado ni moja katika nchi masikini kabisa duniani?

Hivi kabla ya muungano Zanzibar ilikuwa watu wanakufa njaa? Chuki zenu tu ndizo zinazowasumbua, hata muungano ukivunjika hakuna atakaekufa njaa Zanzibar.
 
Katika orodha ya mambo ya muungano Ardhi ya tanganyika hakuwemo ni nani aliengiza katika muungano? Na kwa nini Alifanya hivo?
Utaunganishaje nchi pili na useme ardhi haihusiki? Si ndio maana walichanganya udongo? Ila sasa kibuyu cha udongo labda kilipaswa kiwe cha udongo wa bara tu
 
kama kuna kitu kinaitwa kero za muungano, ulishawahi kusikia wapi kuna kero ya watanganyika? yaani ni kama mchepuko vile, kero zote ni zao, sisi hakuna hata tunacholalamika, wakati hakuna hata tunachofaidika. wanini sasa hawa?
Watanganyika wana kero moja tu ya muungano - kuwa na serikali mbili badala ya tatu.
 
Lissu anahitajika kushughulikiwa. Kuchochea ubaguzi haijawahi kuwa uhuru wa kujieleza. Lissu ni kirusi and should be treated as such!
Unajua maana ya ubaguzi? Tupe maana halafu tuambie jambo ambalo ni la kibaguzi katika kauli yake.

Au nikupe mfano? Unaguzi ni kitendo cha kuwaambia watanzania wanaotoka bara hawawezi kuwa na ardhi Zanzibar wakati wazanzibar wanaruhusiwa kuwa na ardhi bara.

Unaguzi ni pale raisi wa Tanzania akitoa amri au kufanya uamuzi wowote kama raisi hauwahusu watu wa Zaznibar bali unawahusu watu wa bara tu

Ubaguzi ni pale Mtanzania wa wa Zaznibar anatoa kauli kwamba Watanzania wa bara watumie passport wanapoenda Zanzibar

Ubaguzi ni pale ambapo waru wa Zanzibar wanawapa majina ya kukebehi wakazi wa bara wanaoishi Zanzibar

Ubaguzi ni wakati ambapo jambo linaloruhusiwa kufanywa ukiwa bara linakuwa ni kosa kisheria ukilifanya Zaznibar japo wote tunaitwa Watanzania

Nk nk nk
 
Hiyo haikuwa hoja yangu, sasa wewe mwenye kutumia akili kwa wingi anzisha thread yako utaje Tanganyika, eboo!
 
Hawa watu wabaguzi Sana walimnyanganya mama wa watu ndizi alizokwenda kuuza Zanzibar wakahawana na kuzila eti haruhusiwi kuuza ndizi Zanzibar Hawa kenge inatakiwa tuwafurushe huko kariakoo na kwingine warudi kwao huko Zanzibar kama wao wafanyavyo alafu Nashangaa hao wakina nape wanamtetea nani kwenye hili? Au ndio wale wasaliti wa taifa Hili?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…