Uchaguzi 2020 Kauli ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kusema Wagombea wa Upinzani wasiwachafue wagombea wa chama tawala una lengo la kutaka kuwatisha

Uchaguzi 2020 Kauli ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kusema Wagombea wa Upinzani wasiwachafue wagombea wa chama tawala una lengo la kutaka kuwatisha

Hivi yale maneno ya boss mkubwa, kwamba wapinzani wakichumua madaraka watavunja madaraja na kuyauza kama skrepa... SIYO KUWACHAFUA WAPINZANI..!?? Au uchafu ni upande mmoja!?
Ndo dabo standard yenyewe hio sawa na ya musiba ruksa kuongea akiongea ponda ndani
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Kweli kabisa wala haijengwi kwa kuteka na kupiga watu risasi 18 na wengine kupigwa mapanga na wengine kupotezwa!
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Hili limekuwa likipiganiwa sana na wapinzani.

Sisi CCM ndio tunatakiwa tuwajibu wapinzani na wananchi kwa hoja na sio kuwafunga na kuwapiga tu.

Mfano, sheikh Ponda na waislam juzi walikuja na waraka wao, Sisi baada ya kuwajibu kwa hoja tukakimbilia kumkamata na kumuweka rumande siku tele.

By the way usije ukasema mimi ni wa ufipa mimi ni mwana CCM mpenda haki
 
Hawa akina majaliwa vichwa vyao vimejaa misifa mpaka wanajisahau kwamba kampeni ni kuonyesha mapungufu na madhaifu ya mpinzani wako na kuelezea wewe utavyoyatatuwa.wasidhani uchaguzi mkuu ni mikutano ya serikali au ya ccm ambako wao wanasemana kufoka foka huku wanachama na wafanyakazi wakiomba radhi hata wasipokuwa na kosa .Tatizo lao hawajaamini wao ni wangombea kama wengine walivyo wa namrisha askali watafsiri wao matusi kweli wanaendekeza ujinga. Na umbumbu na kulewa madaraka
 
Ndo dabo standard yenyewe hio sawa na ya musiba ruksa kuongea akiongea ponda ndani
Kama hawa watawala wetu wangekuwa fair, wangekuwa weshamchukulia hatua za.kisheria siku nyingi tu huyo mtu "wao" Musiba, kutokana na maneno yake ya uzushi, kuwatukana, kuwakashifu na hata kutishia kutaka kuwaua viongozi wa upinzani.

Lakini kwa kuwa huyo Musiba anakumbatiwa na Jiwe, basi kila analolifanya, vyombo vya usalama vimepigwa upofu na kuviona viko sawa!
 
Habari kubwa kwenye magazeti ya Leo ni kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kuwapiga mkwara mzito, wagombea wa vyama vya upinzani kuwa wasitumie majukwaa ya kisiasa katika kipindi hiki cha kampeni kuwachafua wagombea wenzao.

Ingawa hakuwataja kwa majina wagombea hao, ni dhahiri alikuwa na maana ya wagombea wa Chadema na ACT Wazalendo, ambao kwao CCM ndiyo wanawaona kuwa ni tishio kubwa kwao.

Ni jambo la kushangaza kauli hiyo kutolewa na kiongozi wa ngazi ya juu wa CCM, kwa kuwa katika kipindi chote cha miaka 5 iliyopita, chama cha CCM "kilijipendelea" kwa kufanya kampeni peke yao, nchi nzima, wakiwachafua viongozi wenzao wa upinzani, huku wakivipiga marufuku vyama vya upinzani, kutofanya mikutano yoyote ya kisiasa.

Sasa inashangaza mno kwa viongozi hao wa upinzani wanapotumia fursa hii ya kufanya kampeni kujieleza, Waziri mkuu anasema wasiwachafue viongozi wa CCM!

Hivi kwa mfano kauli iliyotolewa na kiongozi wa Chadema, ambaye pia ni mgombea wa nafasi ya Urais Tundu Lissu, kuwa Rais Magufuli ametumia nafasi yake ya Urais kujenga kiwanja cha ndege cha kimataifa, huko kijijini kwake Chato na "kulazimisha" kuwa na mbuga yao ya wanyama ya Burigi, kwa Maelezo ya waziri mkuu, ni kumchafua Rais Magufuli?

Ninavyoona Mimi kama raia wa Tanzania, ambaye nina haki ya kutoa maoni yangu, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 18(1) uamuzi wa busara kwa viongozi wa CCM ni kwa Rais Magufuli kujitokeza hadharani na kujibu mapigo hayo ni kwanini yeye ameamua kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa kwenye kijiji chake, kinyume cha viongozi waliomtangulia, akina Mwalimu Nyerere, Alli Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete, hawajafanya kama yeye, kwenye majukwaa ya kisiasa, kama maelezo aliyoyatoa Tundu Lissu ni ya uwongo. OVA
Magufuli anachafuliwaje wakati amejisafisha na kujifagilia kwa Miaka yote mitano peke yake?
 
Habari kubwa kwenye magazeti ya Leo ni kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kuwapiga mkwara mzito, wagombea wa vyama vya upinzani kuwa wasitumie majukwaa ya kisiasa katika kipindi hiki cha kampeni kuwachafua wagombea wenzao.

Ingawa hakuwataja kwa majina wagombea hao, ni dhahiri alikuwa na maana ya wagombea wa Chadema na ACT Wazalendo, ambao kwao CCM ndiyo wanawaona kuwa ni tishio kubwa kwao.

Ni jambo la kushangaza kauli hiyo kutolewa na kiongozi wa ngazi ya juu wa CCM, kwa kuwa katika kipindi chote cha miaka 5 iliyopita, chama cha CCM "kilijipendelea" kwa kufanya kampeni peke yao, nchi nzima, wakiwachafua viongozi wenzao wa upinzani, huku wakivipiga marufuku vyama vya upinzani, kutofanya mikutano yoyote ya kisiasa.

Sasa inashangaza mno kwa viongozi hao wa upinzani wanapotumia fursa hii ya kufanya kampeni kujieleza, Waziri mkuu anasema wasiwachafue viongozi wa CCM!

Hivi kwa mfano kauli iliyotolewa na kiongozi wa Chadema, ambaye pia ni mgombea wa nafasi ya Urais Tundu Lissu, kuwa Rais Magufuli ametumia nafasi yake ya Urais kujenga kiwanja cha ndege cha kimataifa, huko kijijini kwake Chato na "kulazimisha" kuwa na mbuga yao ya wanyama ya Burigi, kwa Maelezo ya waziri mkuu, ni kumchafua Rais Magufuli?

Ninavyoona Mimi kama raia wa Tanzania, ambaye nina haki ya kutoa maoni yangu, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 18(1) uamuzi wa busara kwa viongozi wa CCM ni kwa Rais Magufuli kujitokeza hadharani na kujibu mapigo hayo ni kwanini yeye ameamua kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa kwenye kijiji chake, kinyume cha viongozi waliomtangulia, akina Mwalimu Nyerere, Alli Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete, hawajafanya kama yeye, kwenye majukwaa ya kisiasa, kama maelezo aliyoyatoa Tundu Lissu ni ya uwongo. OVA

Yule huwa hawezi ongea😀
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.

We sijui hata umeandika nini..hivi kati ya lisu na uliowataja ni nan habishan kwa hoja...?? Unaeza sema lisu kamtusije huyo?
 
Hiyo ni hofu imewajaa tu maana waliyoyafanya na yaliyozungumzwa sana katika uhalisia ni madogo mno kuliko yalivyokuzwa sasa wanahisi itaonekana wazi hawajafanya makubwa ndiyo maana wanajihami
 
Kweli kabisa......

Hivi kwa tafsiri yao CCM, kuchafuliwa ni kwa upande mmoja tu pale wapinzani wanaopokosoa viongozi wa CCM, lakini wakati huo huo viongozi wa CCM wakiwatukana na kuwachafua viongozi wa upinzani ni ruksa?

Yataisha tu mkuu one day itakuwa ni historia wacha tupiganie wajukuu wetu dhidi ya utawala huu
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Mbona wapinzani wakitukanwa (wanaitwa vibaraka wa mabeberu, wazinzi, wana mahusiano ya jinsia moja, mafisadi wa ruzuku, wauaji wa Akwilina n.k.) na wafuasi wa Chama Tawala hatuwasikii mkiwatetea? Watu wamewatishia vifo na kuwatia vilema lakini hatuwasikii mkisema kuwa hiyo sio sahihi!
Watanzania kweli ni waelewa na wanajua nani anamtukana nani.

Amandla...
 
Kuna li jamaa limoja huwa linasema.

Maendeleo hayana chama.

Halafu baada ya muda linawaambia raia wakitaka wapate maendeleo wachague lichama lake.

Sijui ni akili gani huwa zinatumika kwenye kuongea hayo.
😁😁 simuelewagi kabisa
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Uko sahihi.
Unakumbushwa pia kwamba Nchi haijengwi kwa kuwapiga Raia risasi.
 
Serikali ya CCM wana mambo ya kishenzi sana.
Wanakwambia vizuri "Uhuru unao LAKINI" maneno yanayofata mbele ya hiyo lakini yanabana uhuru wote, ni sawa na kumwambia mtu, unaweza kula hii keki lakini hutakiwi kutumia mdomo wala mkono, ile kwa macho. Ni ujinga ambao hau-make sense. Huyu aliyejaliwa ni mbaya kuliko hata jiwe basi tu mchukulieni poa kwa kua hua haongei.
Yaleyale ya jiwe "maendeleo hayana vyama" kesho yake "mmemchagua wa upinzani kamuombeni huyohuyo maendeleo". Words from kiongozi wa nchi hahaha! watu wanapewa cheo na wananchi wanakaa wanajisahau wanahisi wamegeuka miungu. AH
 
Back
Top Bottom