Uchaguzi 2020 Kawe, Dar: Yaliyojiri mkutano wa Dkt. Magufuli katika viwanja vya Tanganyika Packers

Uchaguzi 2020 Kawe, Dar: Yaliyojiri mkutano wa Dkt. Magufuli katika viwanja vya Tanganyika Packers

Rubbish! Mbunge amuombe Magufuli?? Anamuomba nn?? Magufuli ana hela??
Mbunge anaongea bungeni.

Mtu unavunja taratibu zilizowekwa za nchi hadi unaona ndiyo taratibu sahihi.

Magufuli mwenyewe tunamlipa sisi, kwa kodi zetu.

Everyday is Saturday...............................😎
 
Niko kawe now na nashuhudia watu wengi, rika tofauti kwa mguu yao Wenyewe wakielekea ktk mkutano wa ccm.
 
Vijana wasio na ajira ni wangapi? Hao tu hawana sababu ya kumshabikia Magufuli sababu hajawasaidia lolote miaka hii 5 zaidi aliwadanganya kuhusu ajira million 2.
Bado wakulima ambao nao kila sehemu ni kilio kuanzia korosho mpaka pamba. Watu wanazalisha ila masoko changamoto na serikali haisaidii lolote. Embu nipe sababu ya hao watu kumchagua magufuli?
Serikali itatoa Ajira ngapi wewe ?? Hata akiajiri bado watu wengi watabaki mtaani. Tatizo la ajira halijaanza leo! Mbona zimetolewa ajira za madaktari na walimu , hamulioni Hilo!. Miuondombinu inayojengwa si kuna ajira zinazalishwa mule?? Acheni kujitia upofu!.
 
Rais mpaka aombwe? kwa hiyo asipoambiwa atalala tu maana mambo super. Na hizo halmashauri na viongozi kazi zao ni nini? sasa kama Dar kampeni zinapigwa kama watu wajinga huko vijiini hali ikoje? hatari sana....
 
Jua linachomoza, madimbwi yamekauka kwa Upendo wa Mungu na watu kwa maelfu wanaelekea viwanja vya Kawe Tanganyika packers kumsindikiza kipenzi cha watanzania Dr Magufuli.

Karibuni nyote.

Rip Mwalimu Nyerere

Up dates;

DKT: MAGUFULI: VYAMA VYENYE BENDERA VYENYE RANGI NYEKUNDU VINAASHIRIA MABAYA


Katika Mkutano wa kampeni wa mgombea wa urais wa kupitia CCM, Dkt. Magufuli amesema baba wa Tiafa mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipata uhuru wa nchi hii bila kumwaga damu

Leo tunaadhimisha miaka 21 tangu kifo chake. Lakini anakumbukwa kwa kulipatia uhuru taifa la Tanzania bila mtu yoyote kufa katika harakati za kuutafuta uhuru

Amesema hiyo ndio sababu bendera ya nchi yetu haina rangi nyekundu, tofauti na nchi nyingi za Afrika ambazo zina rangi nyekundu

Amesema kuna baadhi ya vyama vya siasa vina rangi nyekundu, ambavyo haviashirii dalili nzuri. Dkt. Magufuli ameyasema hayo alipokuwa Tegeta kwa Ndevu akielekea Kawe kufanya mkutano wa Kampeni


DKT. MAGUFULI: ALIYEKUWA MBUNGE WA HAPA HAKUWAHI KUNIOMBA

Mgombea urais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Magufuli amesema Oktoba 13, alipigiwa simu na Mgombea Ubunge Jimbo la Kawe kwa tiketi ya CCM kuhusu adha za wananchi wa Basihaya

Amesema aliyekuwa mbunge wa Kawe, jimbo ambalo Bashaya ni sehemu yake, hakuwahi kumuomba kuhusu shida ya mitaro ambayo ilifanya makazi waingiliwe na maji kwa mvua iliyonyesha jana

Aidha amemtaja Gwajima kuwa aliwatembelea wananchi hao na kusaidia kuokoa vitu vyao vilivyokuwa vikichukuliwa na maji

Magufuli ameahidi kutenga Tsh bilioni 5 katika bilioni 32 iliyotengwa kwa ajili ya ukarabati wa mitaro mkoani Dar es Salaam


Dkt. Magufuli akizungumza na wananchi wa Kunduchi, Mtongani
Ndugu zangu wa Mtongani. Mnafahamu…Tunahitaji kufanya mabadiliko makubwa. Jimbo hili linmechelewa sana.

Aliyeongoza kwenye kura za maoni ni mtoto wangu, mtoto wa dada yangu. Anaitwa Furaha. Lakini nikasema hapana. Aliyefuatia aliwahi kuwa Mbunge wa East Africa, nikasema hapana. Nimewaletea Gwajima aje afufue maendeleo ya Kawe.

Wana Kawe musilete mambo ya ubaguzi ya udini na maeneo. Nimekuwa nikiwatetea pembeni pembeni, nikiuliza matatizo ya Kawe wala sipewi.

Mara unaona mtu haingii Bungeni, au anaingia Bungeni akiwa ameziba mdomo. Nataka wanaofungua mdomo ili wanieleze shida za wana Kawe.

Dkt. Magufuli akiwa Boko Basihaya
Ningeweza kutoka Ikulu na kwenda moja kwa moja kwenda Tanganyika Packers. Lakini jana Gwajima pamoja na Diwani waliniambia kuwa kuna sehemu za Kawe zimeharibika kutokana na mvua, nikasema nitapita kuona.

Na mimi nafahamu hapa huwa kunakuwa na maji mengi. Watu wanapata shida. Lakini sijawahi kuombwa hata siku moja kwamba wananchi wa hapa wanapata shida.

Tumetenga bilioni 32 kwaajili ya kushughulikia mitaro [jijini Dar Es Salaam]. Bilioni 5 nitazileta kuja kushughulikia hapa. Lakini tukubaliane, musinichanganyie [na viongozi wa Upinzani]. Huwa naumia sana. Miaka 10 bado hamuelewagi tu?

Tegeta Kwa Ndevu
Marais wote waliopita kabla yangu hawakumwaga damu. N mimi katika miaka yangu mitano sikumwaga damu. Amani nchini Tanzania ni kitu kikubwa sana.
Mimi ni mwana CCM damu, Lakini kuna mengi Raisi wangu anayoyafanya siyakubali. Raisi kama Raisi huhitaji kufatwa na mbunge akuombe kuyatatua matatizo ya jimboni kwake, Una Meya an hata Mkuu wa Mkoa, wote hawa pia wanukuletea habari, mbona huzitimizi, kwa katiba yetu sio Haramu kumchagua kiongozi wa chama cha upinzani, kama ni tatizo basi fungeni vyama vya upinzani tuwe na chama kimoja kama zamani.

Pili Mheshimiwa Raisi, Wana kawe hawana Udini na hawaleti udini, Mtu mdini hapa ni huyu GWAJIMA aliyekuwa chaguzi lako, na udini wake uko recorded. Pia unampigia campaign tofauti na wengine, tunashindwa kukuelewa.
 
Vijana wasio na ajira ni wangapi? Hao tu hawana sababu ya kumshabikia Magufuli sababu hajawasaidia lolote miaka hii 5 zaidi aliwadanganya kuhusu ajira million 2.
Bado wakulima ambao nao kila sehemu ni kilio kuanzia korosho mpaka pamba. Watu wanazalisha ila masoko changamoto na serikali haisaidii lolote. Embu nipe sababu ya hao watu kumchagua magufuli?
Kama miradi yote hii iliyojengwa hukupata ajira ujue wewe ni wale wale ambao wanawza zile ajira za kukaa ofisini kama walivyoambiwa na mababu zao> Mimi nipo kwenye ajira miaka 16 ila kipato cha nje ya ajira ni kikubwa hadi huwa najiuliza huu utumwa wa vyeti ulinipotezea muda sana, njoo kanda ya ziwa kwenye migodi ya wachimbaji wadogo wadogo uone wenzako graduates wa vyuo vyenye heshima kama MUHAS wanavyokamua pesa wewe!
 
Vipi leo mnasomba watu kama ng'ombe kutoka wapi, juzi hapa kinyerezi walilazimisha kila mwenyekiti wa mtaa alazimishe watu 30 na makosta yanabeba,kama mnapendwa watu watakuja wenyewe kwanini mnaforce watu?yaani mnajitekenya aibu gani hii kwa chama tawala ,mmekosa mvuto
Wamesombwa kama wote wa mbagala. Kisarawe n.k

Sent from my BLL-L22 using JamiiForums mobile app
 
Mimi ni mwana CCM damu, Lakini kuna mengi Raisi wangu anayoyafanya siyakubali. Raisi kama Raisi huhitaji kufatwa na mbunge akuombe kuyatatua matatizo ya jimboni kwake, Una Meya an hata Mkuu wa Mkoa, wote hawa pia wanukuletea habari, mbona huzitimizi, kwa katiba yetu sio Haramu kumchagua kiongozi wa chama cha upinzani, kama ni tatizo basi fungeni vyama vya upinzani tuwe na chama kimoja kama zamani.

Pili Mheshimiwa Raisi, Wana kawe hawana Udini na hawaleti udini, Mtu mdini hapa ni huyu GWAJIMA aliyekuwa chaguzi lako, na udini wake uko recorded. Pia unampigia campaign tofauti na wengine, tunashindwa kukuelewa.
Wabunge ambao wanafunga plaster midomo yao, wanajiweka karanti baa na konyagi pembeni zikiwazidi wanaanguka na kuumia na kuuambia umma kuwa wamepigwa na wasiojulikana!
 
Serikali itatoa Ajira ngapi wewe ?? Hata akiajiri bado watu wengi watabaki mtaani. Tatizo la ajira halijaanza leo! Mbona zimetolewa ajira za madaktari na walimu , hamulioni Hilo!. Miuondombinu inayojengwa si kuna ajira zinazalishwa mule?? Acheni kujitia upofu!.
Wakati wa Kikwete mbona aliajiri kila mwaka? Hilo ndio jukumu la serekali kuhakikisha ustawi wa jamii.

Kama haiwezi kuajiri wapishe wanaoweza
 
Niende Moja kwa Moja kwwnye mada
Napenda kumpa sifa Sana magu kwa kujiamini
Katika kampeni zake unaona jinsi ambavyo hahitaji kusindikizwa na wazee wastaafu Wala Nini

Hahitaji support ya JK Wala mwinyi Wala sijui Nani anaenda mwenyewe na anamaliza

Watu wameongea Sana kwamba atafeli kwa vile amewatenga wastaafu lakini ndio kwanzaaaa anazidi kupaaa

Binadamu tunakosa Sana kujiamini Katika mabo Yetu ya kila siku ndio maana tunafeli
Tukiona watu Fulani hawatuungi mkono basi tunakata tamaa kabisaa tunaacha
 
Halima mdee uchaguzi huu hana chake, ni muda muafaka wakujifungia ndani na bulaya
 
Achana na Mimi! Nyie si mnajifanyaga vipofu hamuoni !! Tunawapiga spana tu mpaka akili ziwakae sawa!.
spana anapigwa magu ndo maana bila baada ya kampeni lazima aingie gereji ,nye mbuzi katoliki kweli
 
Wakati wa Kikwete mbona aliajiri kila mwaka? Hilo ndio jukumu la serekali kuhakikisha ustawi wa jamii.

Kama haiwezi kuajiri wapishe wanaoweza
Kikwete alijitahidi kuajiri! lakini bado watu wengi tu walikua hawana ajira mtaani..msifikiri tatizo la ajira kalileta Jpm ! Mbona kaajiri walimu na madaktari hamlioni hilo?? .
 
Ameyasema haya akiwa ktk viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe.

Amemuombea dua Rais Magufuli na akasema wanao mpinga yatawapata mabaya, lakini pia amewaombea wagombea wote wa CCM nafasi mbali mbali nchini na akasisitiza juu ya ushindi wao.

My Take; Shekhe mkuu wa Dar bwana al haji Mussa anaonesha makucha yake ni nani haswaa, ni mwana ccm na mfuasi mzuri wa ccm, sio makosa kisheria, ila ki maadili sijui anakua ktk nafasi gani?

Bakwata wanapaswa kumpa ushauri huyu na akumbushwe kwamba waumini wake wengine ni wavyama vingine, alipaswa kutoa dua tu na sio kupiga kampeni.
 
Back
Top Bottom