Kaya 644 Magomeni kota zagomea kusaini mkataba kununua nyumba

Hali ya kiuchumi ya wapangaji hao ukilinganisha na mwaka 2015 imeporomoka mara dufu.

Hizo gharama walizoomba wauziwe ml 17 zilitakiwa zishuke Hadi ml 12 na walipe Kwa miaka Hadi 20.

Narudia, mkitaka faida, Serikali haipo Kwa ajili ya kumake PROFIT, IPO kusaidia raia.

Jengeni nyumba zenu binafsi ndo mpange faida,

Ukipewa nafasi ktk kuutumikia Umma wa Watanzania, tanguliza maslah ya umma mbele.

Aaamen
 
Nashauri bei iongezwe ili hao masikini wakajengewe nje ya mji huko kimbiji, chekeni mwasonga, kimanzichana ama mohoro.

Hapo mjini wacha wakae matajiri wenye pesa ili mji uzidi kupendeza.

Unamuuziaje mtu city center kwa m50?
Hizo nyimba wapewe wenye uwezo nazo. Wakiwapa watu wasio na uwezo kesho hapatamaniki hapo maana maisha waliyozoea kuishi ya kiswahiliswahili uchafu mtupu.

Hizo nyumba sio za msaada bali biashara, asieweza kulipa aende kuishi kimanzichana.

Huna kipato unataka ukae city center ili usumbue watu? Si uende kijijini ukalime huko

Hakuna kuoneana huruma kwenye biashara.

Wazee wengi wa hapo kota walikuwa watumishi wa serikali ambao maisha yao yote ilikuwa ni kula bata mpaka kiinua mgongo wakalia bata, wachache sana walikuwa na akili ya kujenga.

Kuna mzee mmoja ni jamaa yangu alikuwa mtumishi serikalini ye maisha yake ilikuwa ni bata tu mpaka kiinua mgongo. hakuwahi jenga kwa sababu kota ilikuwa kodi sawa na bure.
 
Angalizo:

Mahusiano ya Serikali na wananchi ni kama ya mtu na bosi wake,

Wananchi ni Bosses na Serikali ni watumishi wa wananchi.

Viongozi wamegeuza ionekane Serikali ni bosses wa raia, NO, NO NO!!!

Hatukuiweka Serikali madarakani Ili ifanye Biashara na kuwafanya raia kuwa wateja, HAPANA.

Serikali KAZI kuu ni kuhudumia raia, imetumwa na wananchi KAZI Fulani Fulani Kwa maslah ya wananchi.

Aaamen
 
Magomeni mjini kati,kota za ghorofa alafu wakae malofa kizembe zembe tu iyo aipo nilijua tu ipo namna hao malofa wenzetu watapigwa chini kiaina flani.
Kama wananchi wengi ni malofa, Serikali pia ni Malofa.

Kila siku wanatembeza bakuli kukopa, iweje wawadharau wananchi malofa, wao Si wanatokana na wananchi malofa?

Viongozi Wachache ndo wanahusika na uhuni huu.
 
Wahame wakatafute sehemu nyingine ya kununua kwa bei wanayoitaka wao hakuna mtu anaweza kukuuzia nyumba yake eti kwa bei inayoendana na uchumi wako bali atauza kwa bei inayomlipa, hivyo kama hali zao za kiuchumi haziendani na hapo wakatafute sehemu itakayoendana na uchumi wao.
 
Hoja zako ni dhaifu sana.
Serikali haikujenga zile nyumba pale magomeni ili kutoa huduma, wamejenga kufanya biashara. Lengo ni kuzalisha faida.

Wale wakazi wa Magomeni ni wapangaji tu, na mpangaji hawezi kumpangia mwenye nyumba kiasi cha kulipa.
 
Nyumba zimejengwa na serikali na wala si ngedere yeyote yule.
 
Kama wananchi wengi ni malofa, Serikali pia ni Malofa.

Kila siku wanatembeza bakuli kukopa, iweje wawadharau wananchi malofa, wao Si wanatokana na wananchi malofa?

Viongozi Wachache ndo wanahusika na uhuni huu.
naibu waziri wa ardhi na makazi ajawekwa pale kwa kubahatisha.
madili yatafunguliwa kusini na kaskazini.malofa awana chao ni kulalama tu.
 
Nyumba za makazi zikijengwa Chanika hizo biashara kwenye hayo maeneo zitafanywa na wanyama au wadudu?
 
Kwani ni lazima hao wakazi wakae hapo hapo Magomeni kwenye hizo nyumba?
Kwani ni wao tu wenye uhuhitaji wa nyumba bora hapa Tz?
Wanazing'ang'ania kwani ni mali yao?

Kama wanaona gharama ya kuzinunua ni kubwa, basi waende wakanunue huko kwenye gharama nafuu au wajenge nyumba zao.
 
Hivi hao wakazi wa Kota walikuwa Ni wapangaji au wemye nyumba?

Vitu vingine havihitaji elimu kubwa kujielewa.

Mlikuwa mnaishi bure pale Kota,
Mkalipwa na pesa za kwenda kupanga vyumba,

Bado mmepewa offer mkae bure miezi kadhaa ili baadae mnunuwe nyumba hizo.


Mnagomea kununuwa mnasema pesa kubwa,,,

Mnagomea mwenye nyumba zake?

Nyumba za serikali sio za wapangaji wa Kota.,
Serikali itoe bei elekezi kwa anayetaka kununuwa tujitose kununuwa,,

Vitu vingine hovyo kabisa...

Sent from my 2201117SG using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…