Kazi nilizowahi zifanya na zikanishinda kwenye utafutaji

Kuna muda nakupendaga sana ukiacha kile kipengele kimoja tu πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
You are so real.
Nilijua tu hili lazima litaibuka.....

Sisi tuliokulia ushuani ngoja nasi tuanzishe uzi wetu...

JF raha sana. Maana kuna mtu nimemsoma na nikakumbukia kuna thread alivyokuwa anajipa mapromo.... Mpaka sasa sijajua kipi anachosema ukweli, hapa au kwenye ule uzi mwingine


Cha msingi, usiichukulie JF serious sana. Hizi Pen names zinawapa watu nafasi kubwa ya kuficha uhalisia. Tatizo wengine hawajui ili uwe mwongo mzuri unapaswa kuwa na kumbukumbu nzuri pia
 
Don't take JF too serious

Utapotezwa.
 
[emoji23][emoji23][emoji23] umenikumbusha jamaa angu mmoja wa kuitwa bakayoko nakumbukuka aliingia site akiwa nywele fresh tu lakini mpaka kazi ya kumwaga zege inaisha mwamba nywele za katikati ya kichwa akawa hana
Bakayoko ? Mmmmmmh kama namjua ila fresh acha ipite never mind.
 
Kuna kazi ya kuchimba lami kwa sururu ili kupata mtaro mzee mikono inakatika unashika sururu mpaka unasikia vidole vinaishiwa nguvu....hii tulipelekwa kufanya mbagala charambe aisee! Kesho sikurudi....hadi unajiuliza kwa nini wamwage kifusi wakandamize halafu ndio mje kuchimba unapata jibu hizo ni fakin job wanaofanya hawana pa kukimbilia ni shida zao ndio zinawatesa.
 
Kuna kazi ya kutindua zege....kwa kuta za nyumba zinazofanyiwa repair usiombe kukutana na zege ya mkoloni au sakafu uambiwe utindue mzee lazima ukimbie.
Kuna kubeba mfuko wa cement kwa kichwa mzee unasikia kabisa mishipa ya shingo inakaza na kutaka kukatika hiyo muwe mnashusha gari zima mzee lazima uombe sub.
 
unaupiga mwingi mkuu.[emoji16][emoji16]

Matusi, nyimbo vimbwanga vingi mno kwenye zege za maghorofa.

Ila ningendelea na ile kazi nahisi ningemaliza salama.
wanakuambia mtu mzima

"ubwabwa utaitaa uwawa" kwa kazi ile iilivyongumu
 
Ni kweli kabisa mishahara mdogo ya hao walinzi inashawishi wao kuwa wadokozi, nimeshuhudia miaka ya nyuma baadhi ya vitu vya zile hotel kubwa za Dar na JKNIA vikiuzwa mitaani hasa vijiko Uma na glass zenye nembo za hotel hizo au mashirika ya ndege, nilipoulizia mara nyingi jamaa wanasema wanauziwa na walinzi na staffs wa kule kufidia malipo madogo ya mishahara
 
Don't take JF too serious

Utapotezwa.
Mkuu, siwezi potezwa na jf , najua vizuri jf ni jukwaa limebeba watu wa kila aina, watukutu, wahongo,vipenyo, wakweli, wanamapambio, n.k but vipo vitu mtu akiandika vinakugusa MOJA KWa MOJA bila kujali nia ya mtoa mada yoyote, na Kama mada inaendana na hualisia lazima utapata hisia fulani

Mfano ni mada hii, inawagusa wengi nikiwemo Mimi, na wengine, member of JF and non member, hata mwanzilishi wa jukwaa hili pendwa, usione tupo hapa twajimwaga , ila mwanzilishi wa jukwaa hili akianza history wapi ametoka mpaka fikia hapa tutashangaa, maisha ni mapambano, na Kama ndivyo nitapotezwa Kwa lipi? Kama nimeyapitia mengi na leo natumia smartphone kutype hapa, Tengua kauli mkuu
 
Aisee nimeekumbuka na mimi. Ukisikia kazi ya kushusha cement wala usisogee. Nakumbuka 2017 nilipita sehemu nikakuta kuna semi nyingi zimepack, vijana wakiendelea na kazi za kupakua cement toka kwenye gari mpka store, aaah mimi hapo sijala tokea jana halafu njaa inauma nikajisemea ngoja nikomae hapa nipate 15000 niishi...duu...nakumbuka nilibeba mifuko 30 wakati hapo nishachoka balaa jasho kila mahali. Muda huo speed imepungua miguu inatetemeka balaa, nilivochukua mfuko wa 31 nilidondoka nao na kazi ikaishiaa hapohapo nikapepewa buku mbili nakumbuka ..

Nilichogundua sio swala la nguvu pale, maana nguvu nilikuwa nazo isipokuwa ni uzoefu
 
Aisee cement ni nzito bwana asikwambie mtu

Wanakwambia eti simba akikurukia ili akuangushe chini uzito wake ni kama urushiwe mfuko wa cement huudake [emoji1787]
 
Moja ya kazi iliyonishinda ni kuchunga ng'ombe ase
Yaan unawatoa asubuhi unawepeleka kwenye malisho tena kilometer mbili na unakula ugali mwingi ili usurvive mpaka jioni maana hamna kurudi mpaka jioni na mchana yenyewe jua linakupiga balaa halafu kila muda naangalia saa naona jion haifiki dakika haziendi yaani acha tu nkaikacha ase
 
Kweli. Wale mafundi wanahonga mzee sio poa
 
Noma saana. Au ile kupasua zege lilokauka afu la kiwandani kwa sururu na nyundo kubwa. Aisee hizo kazi zinataka watu waliokomaa haswaa. Unapiga nyundo inaruka unapiga sururu inaruka mpaka utoboe hiyo layer aisee mikono imepasuka sio poa
 
Mkuu ukikomaa unatoboa mwanzo mgumu. Sema kesho yake usingeamka maana shingo na joints pia kiuno na mikono vinge kua kama umepooza
unaupiga mwingi mkuu.[emoji16][emoji16]

Matusi, nyimbo vimbwanga vingi mno kwenye zege za maghorofa.

Ila ningendelea na ile kazi nahisi ningemaliza salama.
wanakuambia mtu mzima

"ubwabwa utaitaa uwawa" kwa kazi ile iilivyongumu
 
Mm niliambiwa kuna kaz na jiran yang tigo,yeye alikua anafanya hapo tgo, aisee nikafika pale nashangaa tunaingizwa kwenye gar ya tgo tupo kam 30 hv tukapewa lain, tukapelekwa gongo la mboto tukamwa mtaan tuanze kupita nyumb had nyumba kutafta wateja, aisee niligeuza njia nikapnda daladala nkarud hm..
 
Aisee kumbe ulikua rojo rojo namna hiyo na bahati yako tu ulikua unakaa home ndo maana ulikua unakacha kila ukikutana ugumu kazini.

Ukiwa geto na ukiwaza jion uhakika wa menyu ni 0 aisee hicho kisiki kingeng'oka tu kwa namna yoyote hata ukipata 10k fresh tu. Unaita wana mnakishambulia chap mnagawana kidau.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…