Kazi nilizowahi zifanya na zikanishinda kwenye utafutaji

Kazi za ZEGE ni ngumu sana. Kwa siku ya kwanza ,



Mie nilijitoa ufahamu nikavamia site ya ujenzi moja hapa moshi , pale panapojengwa. St.magreth day care and nursery maana nimekaa kitaa sina hata jiti , so nkaona nijitutumue tuuu kiume dah nkatinga hapo site mashallaah. Kazi zilizipo ni za zege




Asalaleeeeeeeeeeeeeeee. Nilijuta sana ila nikishangaa kukuta vijana wadofo kwangu wakipiga job za zege kama kawaida tofauti na mm nilieanza aseeeeeeeeeee. Nilipiga siku mbili tuuu siku ya 3 sikurudi nkasu biri ,jmos ya malipo nkajitokeza. Nkapata 20k zangu nkaamsha
 

Nimecheka kwa sauti [emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
Pole sana mkuu
 
Dah mkuu si bora ungeniita mim mkuuu wangu
 
Hahaaaaaa.
Ila we jamaa bingwa wa kukimbia kazi.
Mimi kinyesi nazoa vizuuri kabisa bila tabu.
Mkuu kuna Kinyesi na Vinyesi, pale tulikua tunazoa Vinyesi

bobu acha masihara,imagine tu mtu akijamba unaziba pua

vuta picha uko live kwa live na kile kinachochujwa tumboni

halafu ni rojo rojo na halipo peke ake lina wadudu wengine hata

hujawahi washuhudia kwenye dunia hii hii tuliyopo,boss ule ni mtiti...

Japo najua kuna watu hamna kazi zina washinda,nyie ni special case.
 
Ungekufaaaa 😆😆🤣
 
Nacheka hapa naonekana kichaa 🤣🤣🤣
 
Hii kazi ya freelancer nilifanya back 2010 to 2013 na ndio ilipa taff kwenye kusoma advance nilikuwa napata commission 80k to 150 every month...remind you kuna freelancer wengi tu wamejengaa nyumba nzuri na wanaendesha familia up to day kwa kazi hii hii..
 
Umenikumbusha mbalii kwenye haya maisha tunapitia mengi sanaa

back to 2020 kwa nilichopitia hapo mbezi mwisho stand ya magufuli kipindi inajegwaa hapana isee zile bodi zioneni zinapendeza tu hivyohivyo ila kuzipandisha huko juu ilikuwa habari nyingine alafu hicho ndio kilikuwa kitengo cha bata sasa, kwenye zege huko ndio ilikuwa uuwajii kabisaa..
 
Alcoboard ni nzito sio kawaida,kuzipandisha huko napata picha kazi mliyokua nayo asee
 
Hahaaaaaa. Mgetafuta masks kazi iendelee. Daadeki Mimi laki siiachi. Nimewahi kushusha cement kwenye semi. Asee vumbi la cement ni hatari. Kifua kilibana, mate yalikauka kabisaa
Siku nyingine nikawa nasomba maharage kwa kubeba kichwani kupeleka Kijiji ambapo gari inakuja kupakia. Niliumwa shingo mwezi mzima, mpaka Sasa vitu vizito siwezi.
 
Nitakuwa nakufahamu nimefanya kazi Mofed kipindi cha hayo matukio nilikuwepo
 
Bububuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…