Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
🤣🤣🤣🤣🤣 Aisee.U made my day bro...daa. Smart911 uje ucheke hukuKwenye maisha kuna mambo mengi sana watu wanapitia mengi mpaka unamuona mtu ana biashara akikwambia mapito aliyopitia mpaka kufikia hapo "acha kabisa" (naongelea wapambanaji) wale wapewa mitaji na ndugu/wazazi hampo eneo hili.
Basi bana tutoke huko leo acha tucheke (kwa watao ona inachekesha) tuchangamshane, lakini zaidi tuelimishane na kujifunza mawili matatu,maana hata katika ujinga kuna vya kujifunza,elimu ipo kila mahali.
Katika maisha yangu bana mimi sikuwahi pewa mtaji wa kufanya chochote hadi kufika hapa nilipo,sio ndugu sio wazazi sio BIKO wala any jackpot bali ni akili na kuthubutu kwangu katika sehemu tofauti tofauti.
Leo nitasimulia baadhi ya kazi nilizo thubutu ila yakanishinda, (maisha si mepesi asee) yalinishinda na nilizikimbia bila kuaga wala kuongea kitu na muajiri wangu,wakati naanza maisha niliambiwa na brother angu mmoja kauli yake hii "mdogo angu usije ukachagua kazi,fanya kila kazi ya halali unayoijua"
Huo usemi ulinikaa kichwani kila nilipotembea ulikua ukijirudia rudia kichwani mwangu,ila jamani acheni niwambie wahenga kuna misemo yao sio ya kuifatisha kabisa.,hebu acha nianze simulizi zangu hapa.
ULINZI
Nikiwa katika harakati za kutafuta kazi yakufanya nipate mtaji wakufanya kitu njiani kwenye nguzo ya umeme nikaona tangazo la kampuni ya ulinzi inatafuta vijana wa ulinzi,Kigezo cha elimu kilikua drs la 7 tu,Haina cha mdhamini zaidi ya pasport size zako,kigezo kingine kilichonishawishi nikakamatika waliandika "Hata kama hujapitia mafunzo ya Mgambo" wanakupokea.
Kampuni nyingi za ulinzi usipokua na mafunzo ya mgambo hawakupokei (hili nilishachunguza maana nilishakataliwa kampuni flani flani) kwa kukosa sifa hiyo tu. Basi baada ya kuona hizo vigezo zao nikaona hapa hapa ndio pakutokea, haina kurudi nyuma Huwa nina utaratbu wa kutembea na pasport size kwenye wallet kila ninapoenda,basi kwakua kigezo kikubwa n pasport size na ninayo,nikaona acha niende.
Kufika ofisi zao nikaingia nikajitambulisha nikahojiwa maswali kadhaa basi baada ya hapo wakaniuliza upo tayari kuanza kazi lini? nikawajibu "yani hata sasa hivi" (hapo ndio nilipojichanganya)" wakaniambia safi kabisa kijana,kaa pale subiri tukutaftie uniform.
Nikawa nimekaaa reception pale wakaingia store wakanletea sare,ila sare zilikua OVERSIZE yani kubwa mno kwangu na ilibidi nizivae pale pale,basi sikua na ajizi nikazitupia mwilini kwakua zilikua kubwa sikua na haja ya kuvua nguo nilizokua nimezivaa,nilivaa juu yake zile,viatu nilikua fresh tu (napenda vaa Timberlands) na uzuri hiyo siku nilikua na Black Tims chni hivyo kwenye upande wa viatu nilikua safi.
Baada yakukamilika kimavazi nikawa nimekaa pale kusubiri kupelekwa eneo la kazi,wakati tumekaa pale akaingia kiongozi wao nikaona watu wote wamesimama, kwakua namimi nishakua askari ikabidi nisimame kikakamavu kama askari,ripoti ikatolewa idadi ya askari na mimi nikiwepo,kisha jamaa akapita,tukakaa chini.
Mida ya saa 11 tukafatwa na gari nikapanda kwenye gari safari yakuanza sambazwa vituo vyetu vya kazi ikaanza,basi nikapelekwa kwenye lindo langu Nikamkuta mwamba Kapanda hewani kinoma,basi kufika pale akanielekeza vyakulinda,akanikabidhi daftari la vitu vya kulinda na tukazunguka nae kuvihakiki kwamba vipo kisha tulipomaliza akaniambia yeye anasepa,tukaagana akaniacha.
ilikua ni kama dispensary flani hivi kubwa kubwa,wanafunga saa mbili basi baada ya kufunga haoo wakaniaga wakaondoka,nikabaki peke yangu Usiku huo.
Sijui ikawaje umeme ukakatika eneo hilo tu na nyumba za jirani ambazo nyingi ni ofisi tu za watu sio makazi ya watu kuishi,hivyo kuna ukimya mno,Giza likatawala Uoga ukaja,ukakolea,kama dk 15 hv kupita nikaskia watu wameruka ukuta wamedondokea kwandani, Nikakimbia kujificha kwenye kistore flani, Nikawa nachungulia.
Nikaona majamaa wawili wameingia wanachukua vyuma vyuma ambavyo ni 1 ya vitu niliambiwa nilinde,siwezi sema lolote nawaangalia mkojo umenibana,roho inadunda inataka kuchomoka,Ghafla nawaona wengine wawili wanatokea wakawa wanne ila hawa wawili walikua na nondo wamezishika na mwngine kashka kishoka.
Mkojo ukazidi nibana nikawa naona haya leo ndio mwisho wangu,kupgana siwezi mimi hawa watu wote nawafanyaje,hapo store kulikua na pipa nikadumbukia,ila kabla sijadumbukia nikawapgia kelele wajamaa nikawambia "Nyie tokeni Hapo" halafu nikadumbukia kwenye pipa nikajifunika.
Nikawasikia na wao wamekurupuka wamekimbia,nikawa nimekaa kwenye pipa kama dk 10 nilisikia ukimya umezidi nikatoka kimya kimya kiminyato,kuchungulia kweli sioni mtu,Pale Pale nikasema Hapana ntakufa mimi siwezi hii kazi,nikavua nguo zao nikafungua geti nikapita na mishe zangu nikaondoka na kazi ikaishia hapo Hiyo ni saa nane usiku inaenda saa tisa huko.
KUNG'OA KISIKI
Nikiwa katika tafuta tafuta`nikafika nyumba 1 nikaomba kazi,akatoka maza mmoja akaniambia kuna kisiki cha kutoa unaweza,nikamwambia bila shaka nipate tu jembe,Akasema vifaa vyote vipo Je kazi nitaifanya kwa sh ngapi? nikjisemea kimoyo moyo,yani najipangia mwenyewe malipo? Nikaropoka Nikamwambia Boss hii kazi nzito ukinipa 15,000 itantosha.
Akasema sawa kijana ukikitoa vizuri ntakuongeza 15,000 nyingine, nikamwambia sawa boss Hapo nina mizuka kama yote,nikawa najisemea hapa nina 30k ya chap chap,Kazi ikaanza..
Piga jembe,piga shoka natikisa kisiki kinaniangalia kama hamna nilichokifanya, Lima sana kwatua sana natingisha kisiki kinantolea macho tu,Boss anakuja anauliza maendeleo namwambia Shaka ondoa hiki kinatoka chote utafurahia...
Akiondoka naanza kazi tena pga shoka kata mizizi lakini wapi,nilianza kazi saa nne asubuhi kufika saa tisa mchana kazi haielekei kuisha au kukamilika,nikamwambia Boss nakuja naenda Dukani fata vocha nimpgie maza mara moja home, Nilivyopita huko huko sikurudi nyuma,nikaona ntaja kufa mimi.
Duniani kuna visiki nyie acheni kabisa kuna miti ukiambiwa utoe kisiki chake hata upewe wiki unaweza usiweze kwa namna ardhi ilivyo ngumu,mti una mizizi kama mkia wa pweza kuupata huo mzizi mkuu tu ni kazi ya masiku,Aaaah nilikimbia mimi.
KUUZA LOTION NA VYOMBO VYA PLASTIK
Kama kawaida niko zangu barabarani natembea sina hili wala lile nikaona tangazo wanatafutwa wafanyakazi watu wa SALES AND MARKETING kigezo kikubwa uwe umefika chuo kwa level yoyote uwe na vyeti vyako tu kuthibitisha elimu yako. Mshahara kuanzia 300,000 - 500,000 NIKAONA yes HAPA HAPA nikachukua namba za simu nikarudi home kusanya vyeti vyangu,kesho yake asubuhi sana nikapga simu nikiwa nimekamilika.
Nikaelekezwa ofisi zilipo kufika pale tukaambiwa wale mliokuja na vyeti vyenu mtakua viongozi kwahyo leo leo mtaanza kazi hii,tukaelekezwa majukumu Ajabu nikaona tunaletea mabeseni,malotion lotion (yale wanayopaka wadada wa kazi) kisha tukaambiwaa Viongozi nyie mtazunguka kutangaza hizi biashara za kampuni kampuni ikishajulikana basi kazi rasmi ya mshahara wa 300k to 500k itaanza,
kwasasa tutalipwa kulingana na mauzo ya siku, sisi viongozi tukapewa mzigo wetu na mabegi na lotion zetu kila kundi tulikua na mwenyeji mmoja aliekua anatutembeza huko mtaani,basi bwana tukatoka pale na mabeseni yetu tukaingia mtaani kila kikundi tupo mtu 4, tukifika sehemu watu wamekaa yule mwenyeji anajitambulisha anaongea maneno 20 kidogo kisha anasema leo ana ofaa ya vitu flani flani, (nilipooona vile nkakumbuka aina ya kazi niliyoipata)
tulizunguka anzia ile asubuhi hadi jioni kwa mguu sijala hata kitu yule mwenyeji wetu alinunua maji ya kandoro akatugaia na sisi kidogo,asee imefika jioni muda wa kurudi nikikumbuka tulipotoka ni wapi halafu tunatakiwa kurudi kwa miguu tena,nikaona Enough is Enough,Nikawambia wazee nimebanwa haja kubwa ngoja ntafute pori nakuja. Niikaingia pori flani nikatokea mbele panda boda boda straight hadi stand,nikalipa kisha panda dala dala hadi home nafika maskani saa 1 nina njaa sio kawaida,na vyeti vyangu kwenye begi kazi ikaishia hapo.
KUTEMBEZA MAJI NA SODA
Nakumbuka ndio miaka hiyo naingia Dar nikapata wana siwajui ila niliwaona tu ni wapambanaji nikawaelezea nia yangu,shida yangu wakaniambia "imeisha hiyo wakwetu" twende ukachukue mzigo upge kazi,huyu jamaa yeye alikua anauza maji ya kutembeza,juice,soda za take away,biskut,nk
Nikamwambia mimi mtaji sina lakini,akasema usijali nakupeleka kwa boss wangu atakupa mzigo,kweli tukatoka haoo tukafika kwa muhindi mmoja hivi akanitambulisha akamwambia "mimi iko letea wewe kijana ya kaziii", muhindi akauliza "hii hapana sumbua kama ile nyingine"? jamaa akamwambia hii iko safi kabisa, basi baada ya hapo nikapewa kitrey Jamaa akanipakia mzigo wa kwenda kuzungusha..
Unachotakiwa n unaenda na mzigo unauza kwa bei ya reja reja il wewe unachukua kwa bei ya jumla,take away pale tulikua tunachukua kwa 800 wewe unauza 1000 faida 200,basi jioni mzigo utaobaki unarudsha kwa muhindi Fresh maisha yanaenda.
Basi bana jamaa akanipakia trei langu kajaza soda,maji,vinywaji vyotee muhimu mzigo huooo,yani kujitwisha tu lazima mtu akutwishe,tukatoka haooo jamaa akaniambia sasa mwanangu hapa tunagawana mitaa wewe pita kule mimi kule tutakutana badae... Nikamwambia fresh...
Tukaachana, tembea tembea na wewe mzigo ni mzito sina mfano,Kujitwisha peke ako huwezi Napishana na watu hata kununua maji hawanunui,Mchana ukakolea jua likakolea kiu ikanikamata,Acha kabisa Kuhusu Kiu Bora ushikwe na njaa utavumilia ila sio kiu cha maji.
hapo nimejikaza imefika saa 11 inaenda 12 jioni sijauza hata biskuti,ki ukweli ilifika mahali nikaona hapa ninapoendea ni kufa Kizembe,nikatafuta kivuli nikajitua mzigo wangu, Nikachukua fanta passion nikafungua Nikainywa yoteee,Kiu hakijaisha njaa ndio imekolea,Nikachukua Biskuti na fanta nyingine nikashushia.
Baada ya hapo nikaamka nikaomba kutwishwa safari moja kwa moja mpaka kwa muhindi,kufika pale ashukuriwe Mungu sikumkuta,nilikuta wafanyakazi,nikawambia mzigo wangu msiguse naenda chooni mara 1 nakuja,Nikauweka pale nilivyotoka ndio kimoja yani sikugeuza shingo...Nilijiona ntaja kufa kwenye kazi za wahindi kizembe..
Basi kuna kazi nyingi sana nimeshazifanya hadi kufikia hapa nilipo,bandiko lenyewe hili naliandika nafuta naliandika nafuta yani tangu Wiki iliyopita naandikaga tu,kazi zingine nitaziendeleza kwenye comment maana kama ni kujaribu tu wanangu nimejaribu sanaa tu...
Naomba kuishia hapa tukutane kwenye comment hapo tuendelezeane mikasa,ila yote kwa yote Tufahamu jambo moja ktika utafutaji Ni marufuku kukata tamaa,fanya kila uwezalo feli kosea anguko zomewa ila mwiko kukata tamaa,uta aibika lakini nakuhakikishia mwisho wake huwa ni mzuri tu.
Hakunaga mwisho mbaya au mbovu kwa mtafutaji mpambanaji,nimeshuhudia na nimeliona kwangu binafsi hamna kitu na enjoy kama background ya maisha yangu ya nyuma,i have many many untold stories ambazo ki ukweli ndio siri ya mafanikio yangu,siku ntakuja na ID feki ntaachia makombora .
Haya ninayo yasimulia ni ma trailer tu mapicha kamili yapo nitayasimulia siku 1 all in all tupambane tusikate tamaa maisha ni mazuri sana ukijishughulisha no matter what fanya unachoona ni sahihi kikikushinda usilazimishe Jaribu kingine,usigande na jambo 1 yawezekana bahati yako haipo kwenye hilo unalofanya.
Ushauri ni mwingi nazidi kurefusha tu thread asee,tukutane chini hapo,sema mwanangu Mbekenga unazingua yani unaosha vyombo ughaibuni unaogopa mwambia wife? au umekosea hukumaanisha wife ulimaanisha mchepuko au kimanzi flani?
Men we dont hide our hustles kwa wake zetu,we tell them ukweli mweupe uamuzi ni wao wauchukie au waupokee,kuna heshima katika hiyo kazi yako ya kuosha vyombo mkuu Mwambie waifu utaona atavyo kuheshimu. Change brother mfanye mke rafiki ako acha mambo za kizamani...
Ila umepambana japo wewe hiyo haijakushinda tuambie kilichokushinda maaana vyombo unaendelea kuosha means hamna changamoto yyte eneo hilo... Tupe zile ngumu kumeza ulizoona hapana hizi siwezi...
Duuh hilo kontena hebu simulia kidogo mkuuMimi nimelinda sana, Agakhan University, Agakhan Hospital, Jamatin msikini Kariakoo, Mahotel Kama Serena, New Africa, Ramada, Regency.
Bandari Kama TICTS, IMPALA, MOFED.
Residence za Wahindi ( Vibibi vya kihindi havilali, vinakuchungulia usiku mzima ).
Binafsi, Sina nguvu na Nina mwili mdogo ila Nina UNASIRI TANI 200.
Nilikiwa napiga bit watu wakubwa na wenye vyeo vikubwa sana huweni kuamini.
Nimewahi kumfungia Nje ofisa mkubwa sana wa kampuni, kwasababu nilikuwa namwambia afungue buti la gari nikague hataki.
Nimewahi kutishiwa kupigwa bastola na Maafisa Usalama usiku waliokuwa wanalinda makinikia.
Pia, tumewahi kufungwa pingu na watu wa usalama wa Ikulu waliokuwa wamekuja kuchukua sample ya makinikia ya dhahabu tulipokuwa tunalinda.
Kitu kingine, nisichosahau Ni pale kontena la 40 feet, lililojaa KOROSHO zilizobanguliwa lilipoibwa na Bandarini wakakuta mawe, yaani kwenda Polisi na kukaa Mahabusu ilikuwa ni Kama kunywa maji.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Aliyeugundua mchanganyiko wa kokoto, mchanga, saruji na maji, visa yake ya mbinguni itasumbua sana
😂😂🤣 Daah we jamaaa 🙌🙌🙌Mimi nishawahi kutwa na msala wa gerezani wa kazi flani Ngumu sana kuifanya,nikaona huu ushenzi
hiii kazi nisipoangalia ntaja fia hapa hapa,nikaangalia huku na kule kisha nikajidondosha chini puuuu
nikaanza kurusha miguuu kama nina dege dege,huku natoa mapovu( hapo nishakusanya mate kibaooo)
nikawa nayatema kwa pembeni kidogo kidogo,nikaskia wana wanasema Oyaa huyu atakua ana dege dege
askari akaitwa akaja akasema mbebeni muwekeni pale kivulini,nilipopelekwa kivulini nikasema hapa nikitulia
tuu ntalishwa rungu kwa sana watanishtukia, basi nikazidisha drama nikajirusha kama jongooo nakwambia
askari akaona huu msala atatufia huyu,nikabebwa ikaitwa TAX dakwa speed hadi gerezani,kufika gerezani nikajifanya
napumua haaaaaa huku nakoromaa,ndio ikawa pona yangu ila bila ile tekniki Ningefia pale walahi vile...
Mpemba noma3.Kuvua bahari ya upande wa sahare Tanga
Nilikuwa nina shida na nauli nikimbie Lusanga kuna mishe mchizi alinisanua nikapata kazi ya kuvua mwana aliniunga tu picha linaanza jioni ile nikatokea na ka t-shirt kangu manga nyepesi maana tulienda vua maji ya usiku [emoji3] wale wadigo na Wapemba wa ile mashua sijui boat whatever the case .. walikuwa wanacheka
Niligundua kwa nini wanacheka tupo katika ya bahari ule upepo wa baridi niliokuwa napigiwa nao plus yale maji yakikurukia ushapata picha
Kwa nini nilijuta kuna kitu wenyeji wanaita sijui bawa la mvua wataalamu mtaiweka sawa ile maji yanaongezeka yanapanda juu kwa kasi yanavuka hadi kingo za beach ambapo watu wanakaa kunakuwa na maji yanasogea hio ishu ilitukutia usiku plus mawimbi maji yakawa yanaingia kwenye chombo chetu tuna kazi ya kuyatoa na visado boti linapigwa pushi na mawimbi mara chemli imeanguka imepasuka mpemba mmoja akanambia "wajua kuogelea weye ..mimi siokoi ntu nanusuru roho yangu mie " wengine wanakazi ya kutoa maji na visado huku wakisema "shahada" yaani kwa imani ya dini ya kiislamu unaenda peponi ukifa kama utaisema
Nilisema sirudii tena [emoji1787][emoji1787]
Nimecheka sana aisee.Kwenye maisha kuna mambo mengi sana watu wanapitia mengi mpaka unamuona mtu ana biashara akikwambia mapito aliyopitia mpaka kufikia hapo "acha kabisa" (naongelea wapambanaji) wale wapewa mitaji na ndugu/wazazi hampo eneo hili.
Basi bana tutoke huko leo acha tucheke (kwa watao ona inachekesha) tuchangamshane, lakini zaidi tuelimishane na kujifunza mawili matatu,maana hata katika ujinga kuna vya kujifunza,elimu ipo kila mahali.
Katika maisha yangu bana mimi sikuwahi pewa mtaji wa kufanya chochote hadi kufika hapa nilipo,sio ndugu sio wazazi sio BIKO wala any jackpot bali ni akili na kuthubutu kwangu katika sehemu tofauti tofauti.
Leo nitasimulia baadhi ya kazi nilizo thubutu ila yakanishinda, (maisha si mepesi asee) yalinishinda na nilizikimbia bila kuaga wala kuongea kitu na muajiri wangu,wakati naanza maisha niliambiwa na brother angu mmoja kauli yake hii "mdogo angu usije ukachagua kazi,fanya kila kazi ya halali unayoijua"
Huo usemi ulinikaa kichwani kila nilipotembea ulikua ukijirudia rudia kichwani mwangu,ila jamani acheni niwambie wahenga kuna misemo yao sio ya kuifatisha kabisa.,hebu acha nianze simulizi zangu hapa.
ULINZI
Nikiwa katika harakati za kutafuta kazi yakufanya nipate mtaji wakufanya kitu njiani kwenye nguzo ya umeme nikaona tangazo la kampuni ya ulinzi inatafuta vijana wa ulinzi,Kigezo cha elimu kilikua drs la 7 tu,Haina cha mdhamini zaidi ya pasport size zako,kigezo kingine kilichonishawishi nikakamatika waliandika "Hata kama hujapitia mafunzo ya Mgambo" wanakupokea.
Kampuni nyingi za ulinzi usipokua na mafunzo ya mgambo hawakupokei (hili nilishachunguza maana nilishakataliwa kampuni flani flani) kwa kukosa sifa hiyo tu. Basi baada ya kuona hizo vigezo zao nikaona hapa hapa ndio pakutokea, haina kurudi nyuma Huwa nina utaratbu wa kutembea na pasport size kwenye wallet kila ninapoenda,basi kwakua kigezo kikubwa n pasport size na ninayo,nikaona acha niende.
Kufika ofisi zao nikaingia nikajitambulisha nikahojiwa maswali kadhaa basi baada ya hapo wakaniuliza upo tayari kuanza kazi lini? nikawajibu "yani hata sasa hivi" (hapo ndio nilipojichanganya)" wakaniambia safi kabisa kijana,kaa pale subiri tukutaftie uniform.
Nikawa nimekaaa reception pale wakaingia store wakanletea sare,ila sare zilikua OVERSIZE yani kubwa mno kwangu na ilibidi nizivae pale pale,basi sikua na ajizi nikazitupia mwilini kwakua zilikua kubwa sikua na haja ya kuvua nguo nilizokua nimezivaa,nilivaa juu yake zile,viatu nilikua fresh tu (napenda vaa Timberlands) na uzuri hiyo siku nilikua na Black Tims chni hivyo kwenye upande wa viatu nilikua safi.
Baada yakukamilika kimavazi nikawa nimekaa pale kusubiri kupelekwa eneo la kazi,wakati tumekaa pale akaingia kiongozi wao nikaona watu wote wamesimama, kwakua namimi nishakua askari ikabidi nisimame kikakamavu kama askari,ripoti ikatolewa idadi ya askari na mimi nikiwepo,kisha jamaa akapita,tukakaa chini.
Mida ya saa 11 tukafatwa na gari nikapanda kwenye gari safari yakuanza sambazwa vituo vyetu vya kazi ikaanza,basi nikapelekwa kwenye lindo langu Nikamkuta mwamba Kapanda hewani kinoma,basi kufika pale akanielekeza vyakulinda,akanikabidhi daftari la vitu vya kulinda na tukazunguka nae kuvihakiki kwamba vipo kisha tulipomaliza akaniambia yeye anasepa,tukaagana akaniacha.
ilikua ni kama dispensary flani hivi kubwa kubwa,wanafunga saa mbili basi baada ya kufunga haoo wakaniaga wakaondoka,nikabaki peke yangu Usiku huo.
Sijui ikawaje umeme ukakatika eneo hilo tu na nyumba za jirani ambazo nyingi ni ofisi tu za watu sio makazi ya watu kuishi,hivyo kuna ukimya mno,Giza likatawala Uoga ukaja,ukakolea,kama dk 15 hv kupita nikaskia watu wameruka ukuta wamedondokea kwandani, Nikakimbia kujificha kwenye kistore flani, Nikawa nachungulia.
Nikaona majamaa wawili wameingia wanachukua vyuma vyuma ambavyo ni 1 ya vitu niliambiwa nilinde,siwezi sema lolote nawaangalia mkojo umenibana,roho inadunda inataka kuchomoka,Ghafla nawaona wengine wawili wanatokea wakawa wanne ila hawa wawili walikua na nondo wamezishika na mwngine kashka kishoka.
Mkojo ukazidi nibana nikawa naona haya leo ndio mwisho wangu,kupgana siwezi mimi hawa watu wote nawafanyaje,hapo store kulikua na pipa nikadumbukia,ila kabla sijadumbukia nikawapgia kelele wajamaa nikawambia "Nyie tokeni Hapo" halafu nikadumbukia kwenye pipa nikajifunika.
Nikawasikia na wao wamekurupuka wamekimbia,nikawa nimekaa kwenye pipa kama dk 10 nilisikia ukimya umezidi nikatoka kimya kimya kiminyato,kuchungulia kweli sioni mtu,Pale Pale nikasema Hapana ntakufa mimi siwezi hii kazi,nikavua nguo zao nikafungua geti nikapita na mishe zangu nikaondoka na kazi ikaishia hapo Hiyo ni saa nane usiku inaenda saa tisa huko.
KUNG'OA KISIKI
Nikiwa katika tafuta tafuta`nikafika nyumba 1 nikaomba kazi,akatoka maza mmoja akaniambia kuna kisiki cha kutoa unaweza,nikamwambia bila shaka nipate tu jembe,Akasema vifaa vyote vipo Je kazi nitaifanya kwa sh ngapi? nikjisemea kimoyo moyo,yani najipangia mwenyewe malipo? Nikaropoka Nikamwambia Boss hii kazi nzito ukinipa 15,000 itantosha.
Akasema sawa kijana ukikitoa vizuri ntakuongeza 15,000 nyingine, nikamwambia sawa boss Hapo nina mizuka kama yote,nikawa najisemea hapa nina 30k ya chap chap,Kazi ikaanza..
Piga jembe,piga shoka natikisa kisiki kinaniangalia kama hamna nilichokifanya, Lima sana kwatua sana natingisha kisiki kinantolea macho tu,Boss anakuja anauliza maendeleo namwambia Shaka ondoa hiki kinatoka chote utafurahia...
Akiondoka naanza kazi tena pga shoka kata mizizi lakini wapi,nilianza kazi saa nne asubuhi kufika saa tisa mchana kazi haielekei kuisha au kukamilika,nikamwambia Boss nakuja naenda Dukani fata vocha nimpgie maza mara moja home, Nilivyopita huko huko sikurudi nyuma,nikaona ntaja kufa mimi.
Duniani kuna visiki nyie acheni kabisa kuna miti ukiambiwa utoe kisiki chake hata upewe wiki unaweza usiweze kwa namna ardhi ilivyo ngumu,mti una mizizi kama mkia wa pweza kuupata huo mzizi mkuu tu ni kazi ya masiku,Aaaah nilikimbia mimi.
KUUZA LOTION NA VYOMBO VYA PLASTIK
Kama kawaida niko zangu barabarani natembea sina hili wala lile nikaona tangazo wanatafutwa wafanyakazi watu wa SALES AND MARKETING kigezo kikubwa uwe umefika chuo kwa level yoyote uwe na vyeti vyako tu kuthibitisha elimu yako. Mshahara kuanzia 300,000 - 500,000 NIKAONA yes HAPA HAPA nikachukua namba za simu nikarudi home kusanya vyeti vyangu,kesho yake asubuhi sana nikapga simu nikiwa nimekamilika.
Nikaelekezwa ofisi zilipo kufika pale tukaambiwa wale mliokuja na vyeti vyenu mtakua viongozi kwahyo leo leo mtaanza kazi hii,tukaelekezwa majukumu Ajabu nikaona tunaletea mabeseni,malotion lotion (yale wanayopaka wadada wa kazi) kisha tukaambiwaa Viongozi nyie mtazunguka kutangaza hizi biashara za kampuni kampuni ikishajulikana basi kazi rasmi ya mshahara wa 300k to 500k itaanza,
kwasasa tutalipwa kulingana na mauzo ya siku, sisi viongozi tukapewa mzigo wetu na mabegi na lotion zetu kila kundi tulikua na mwenyeji mmoja aliekua anatutembeza huko mtaani,basi bwana tukatoka pale na mabeseni yetu tukaingia mtaani kila kikundi tupo mtu 4, tukifika sehemu watu wamekaa yule mwenyeji anajitambulisha anaongea maneno 20 kidogo kisha anasema leo ana ofaa ya vitu flani flani, (nilipooona vile nkakumbuka aina ya kazi niliyoipata)
tulizunguka anzia ile asubuhi hadi jioni kwa mguu sijala hata kitu yule mwenyeji wetu alinunua maji ya kandoro akatugaia na sisi kidogo,asee imefika jioni muda wa kurudi nikikumbuka tulipotoka ni wapi halafu tunatakiwa kurudi kwa miguu tena,nikaona Enough is Enough,Nikawambia wazee nimebanwa haja kubwa ngoja ntafute pori nakuja. Niikaingia pori flani nikatokea mbele panda boda boda straight hadi stand,nikalipa kisha panda dala dala hadi home nafika maskani saa 1 nina njaa sio kawaida,na vyeti vyangu kwenye begi kazi ikaishia hapo.
KUTEMBEZA MAJI NA SODA
Nakumbuka ndio miaka hiyo naingia Dar nikapata wana siwajui ila niliwaona tu ni wapambanaji nikawaelezea nia yangu,shida yangu wakaniambia "imeisha hiyo wakwetu" twende ukachukue mzigo upge kazi,huyu jamaa yeye alikua anauza maji ya kutembeza,juice,soda za take away,biskut,nk
Nikamwambia mimi mtaji sina lakini,akasema usijali nakupeleka kwa boss wangu atakupa mzigo,kweli tukatoka haoo tukafika kwa muhindi mmoja hivi akanitambulisha akamwambia "mimi iko letea wewe kijana ya kaziii", muhindi akauliza "hii hapana sumbua kama ile nyingine"? jamaa akamwambia hii iko safi kabisa, basi baada ya hapo nikapewa kitrey Jamaa akanipakia mzigo wa kwenda kuzungusha..
Unachotakiwa n unaenda na mzigo unauza kwa bei ya reja reja il wewe unachukua kwa bei ya jumla,take away pale tulikua tunachukua kwa 800 wewe unauza 1000 faida 200,basi jioni mzigo utaobaki unarudsha kwa muhindi Fresh maisha yanaenda.
Basi bana jamaa akanipakia trei langu kajaza soda,maji,vinywaji vyotee muhimu mzigo huooo,yani kujitwisha tu lazima mtu akutwishe,tukatoka haooo jamaa akaniambia sasa mwanangu hapa tunagawana mitaa wewe pita kule mimi kule tutakutana badae... Nikamwambia fresh...
Tukaachana, tembea tembea na wewe mzigo ni mzito sina mfano,Kujitwisha peke ako huwezi Napishana na watu hata kununua maji hawanunui,Mchana ukakolea jua likakolea kiu ikanikamata,Acha kabisa Kuhusu Kiu Bora ushikwe na njaa utavumilia ila sio kiu cha maji.
hapo nimejikaza imefika saa 11 inaenda 12 jioni sijauza hata biskuti,ki ukweli ilifika mahali nikaona hapa ninapoendea ni kufa Kizembe,nikatafuta kivuli nikajitua mzigo wangu, Nikachukua fanta passion nikafungua Nikainywa yoteee,Kiu hakijaisha njaa ndio imekolea,Nikachukua Biskuti na fanta nyingine nikashushia.
Baada ya hapo nikaamka nikaomba kutwishwa safari moja kwa moja mpaka kwa muhindi,kufika pale ashukuriwe Mungu sikumkuta,nilikuta wafanyakazi,nikawambia mzigo wangu msiguse naenda chooni mara 1 nakuja,Nikauweka pale nilivyotoka ndio kimoja yani sikugeuza shingo...Nilijiona ntaja kufa kwenye kazi za wahindi kizembe..
Basi kuna kazi nyingi sana nimeshazifanya hadi kufikia hapa nilipo,bandiko lenyewe hili naliandika nafuta naliandika nafuta yani tangu Wiki iliyopita naandikaga tu,kazi zingine nitaziendeleza kwenye comment maana kama ni kujaribu tu wanangu nimejaribu sanaa tu...
Naomba kuishia hapa tukutane kwenye comment hapo tuendelezeane mikasa,ila yote kwa yote Tufahamu jambo moja ktika utafutaji Ni marufuku kukata tamaa,fanya kila uwezalo feli kosea anguko zomewa ila mwiko kukata tamaa,uta aibika lakini nakuhakikishia mwisho wake huwa ni mzuri tu.
Hakunaga mwisho mbaya au mbovu kwa mtafutaji mpambanaji,nimeshuhudia na nimeliona kwangu binafsi hamna kitu na enjoy kama background ya maisha yangu ya nyuma,i have many many untold stories ambazo ki ukweli ndio siri ya mafanikio yangu,siku ntakuja na ID feki ntaachia makombora .
Haya ninayo yasimulia ni ma trailer tu mapicha kamili yapo nitayasimulia siku 1 all in all tupambane tusikate tamaa maisha ni mazuri sana ukijishughulisha no matter what fanya unachoona ni sahihi kikikushinda usilazimishe Jaribu kingine,usigande na jambo 1 yawezekana bahati yako haipo kwenye hilo unalofanya.
Ushauri ni mwingi nazidi kurefusha tu thread asee,tukutane chini hapo,sema mwanangu Mbekenga unazingua yani unaosha vyombo ughaibuni unaogopa mwambia wife? au umekosea hukumaanisha wife ulimaanisha mchepuko au kimanzi flani?
Men we dont hide our hustles kwa wake zetu,we tell them ukweli mweupe uamuzi ni wao wauchukie au waupokee,kuna heshima katika hiyo kazi yako ya kuosha vyombo mkuu Mwambie waifu utaona atavyo kuheshimu. Change brother mfanye mke rafiki ako acha mambo za kizamani...
Ila umepambana japo wewe hiyo haijakushinda tuambie kilichokushinda maaana vyombo unaendelea kuosha means hamna changamoto yyte eneo hilo... Tupe zile ngumu kumeza ulizoona hapana hizi siwezi...
[emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] Pole sana,Kuchimba kisiki ni msala nakumbuka nikiwa gerezani nilikutana na hiyo kazi vilikua visiki kama kumi na sita afu tupo mtu tano asikuambie mtu tulivuja jasho.
Swali kutoka kwa juniyaUmewahi kufungwa jela?
😂😂😂Swali kutoka kwa juniya
Kama kazi gani Dina? Manake mimi hadi kazi ya kuzibua vyoo nishazibua sana, ila niko sawa tu!Ila kuna kazi ukizifanya unaweza kuwa kichaa kabisa
"UTAPIGA KAZI MPAKA UITEE MMAA"
Nakumbuka enzi zile sina mishe yoyote na nasaka pesa.niliamka asubuhi moja na kuiingia mtaani, kupita mtaa fulani nkaona watu wamesimama nje ya geti ya site ya ujenzi wanahesabiwa.
Nikaona wanapangiwa kazi za kufanya, walikuwa watu kati 40 mpaka 50 hivi.Kidume mbio nkajipenyeza.
Sasa yule Mhandisi(nilikuja kumjua badae) aliyekuwa anahesabu watu na kupanga majukumu akaniweka kwenye kundi la 2( watu 23 maana yake tukawekwa magroup ma2 ya watu 23, 23 kama sikosei).
nikasikia yule mhandisi anatoa majukumu kwa group letu kuwa "" nyinyi wazee ni wazee wa MMAA"" na natoa 40,000 kwa kila mmoja kazi ikiisha.
Daah kusikia 40,000, nkaona kazi si ndo hii jamani.
Ila sasa sikuelewa alivyomaanisha "wazee wa mmaa",
kumbe banaaa ni wazee wa zege la jamvi la juu ya GHOROFA ya tatu.zege la kukesha, zege la kufa mtu,aaah manina
wenzetu wao yani kundi la pili wao ni kazi za chini.
*****************************************
Picha linaanza tulianza kupakua mifuko kama 300 ya cement, mchanga lori, kokoto lori, mixer na gari la maji .halafu kilichonitisha walishusha ndoo kubwakubwa za kubebea zege kama 200 hivi.
AISEEEEE, AISEEEE. ndo nilijua kwanini sisi tunaitwa"" wazee wa MMAAA" yani utapiga kazi mpaka uombe maji kama mtoto.
Zege linakorogwa chini unalipandisha kwa kichwa mpaka ghorofa ya 3.MANINAAAAAA
nilipiga trip kama 6 hivi,nikiwa napandisha trip ya 6, nkasikia lijamaa limoja eti kwann mimi mchumba nimekuja kwenye kazi za wanaume. Niliumia sana, nkajikaza trip kama 5 zingine.
ile trip ya mwisho, nkasikia shingo imekaza.[emoji16][emoji16][emoji16]nikajiuliza kwanini nifie site??
Nilimuaga msimamizi kuwa naiingia toilet 2mins , Akajibu ""chapu chapu dogo huu si muda wa kulemba kanye huku umesimama maana hii ngoma tunakesha mpaka uitee mmaa""
nilivyokata kona, nilikimbia mnooooo,zile trip 11 nilizopiga niliumwa 2 days[emoji2]
Sikuwahi kufanya kazi ya zege tena.
Kwa jinsi nilivyo- kila nkimhadithia wife kuwa nilipiga kazi za hovyo huwa anakataaa sanaaa, sijui why but anyway.
wakuu tusikate tamaaa maishani.
"wazee wa mmaa"[emoji23][emoji23]
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]"UTAPIGA KAZI MPAKA UITEE MMAA"
Nakumbuka enzi zile sina mishe yoyote na nasaka pesa.niliamka asubuhi moja na kuiingia mtaani, kupita mtaa fulani nkaona watu wamesimama nje ya geti ya site ya ujenzi wanahesabiwa.
Nikaona wanapangiwa kazi za kufanya, walikuwa watu kati 40 mpaka 50 hivi.Kidume mbio nkajipenyeza.
Sasa yule Mhandisi(nilikuja kumjua badae) aliyekuwa anahesabu watu na kupanga majukumu akaniweka kwenye kundi la 2( watu 23 maana yake tukawekwa magroup ma2 ya watu 23, 23 kama sikosei).
nikasikia yule mhandisi anatoa majukumu kwa group letu kuwa "" nyinyi wazee ni wazee wa MMAA"" na natoa 40,000 kwa kila mmoja kazi ikiisha.
Daah kusikia 40,000, nkaona kazi si ndo hii jamani.
Ila sasa sikuelewa alivyomaanisha "wazee wa mmaa",
kumbe banaaa ni wazee wa zege la jamvi la juu ya GHOROFA ya tatu.zege la kukesha, zege la kufa mtu,aaah manina
wenzetu wao yani kundi la pili wao ni kazi za chini.
*****************************************
Picha linaanza tulianza kupakua mifuko kama 300 ya cement, mchanga lori, kokoto lori, mixer na gari la maji .halafu kilichonitisha walishusha ndoo kubwakubwa za kubebea zege kama 200 hivi.
AISEEEEE, AISEEEE. ndo nilijua kwanini sisi tunaitwa"" wazee wa MMAAA" yani utapiga kazi mpaka uombe maji kama mtoto.
Zege linakorogwa chini unalipandisha kwa kichwa mpaka ghorofa ya 3.MANINAAAAAA
nilipiga trip kama 6 hivi,nikiwa napandisha trip ya 6, nkasikia lijamaa limoja eti kwann mimi mchumba nimekuja kwenye kazi za wanaume. Niliumia sana, nkajikaza trip kama 5 zingine.
ile trip ya mwisho, nkasikia shingo imekaza.[emoji16][emoji16][emoji16]nikajiuliza kwanini nifie site??
Nilimuaga msimamizi kuwa naiingia toilet 2mins , Akajibu ""chapu chapu dogo huu si muda wa kulemba kanye huku umesimama maana hii ngoma tunakesha mpaka uitee mmaa""
nilivyokata kona, nilikimbia mnooooo,zile trip 11 nilizopiga niliumwa 2 days[emoji2]
Sikuwahi kufanya kazi ya zege tena.
Kwa jinsi nilivyo- kila nkimhadithia wife kuwa nilipiga kazi za hovyo huwa anakataaa sanaaa, sijui why but anyway.
wakuu tusikate tamaaa maishani.
"wazee wa mmaa"[emoji23][emoji23]
Alikuwa sahihi ukimuokoa mtu ambaye hajui kuogelea usipokuwa makini mnakufa wote[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Nimecheka sana aisee