Kazi nilizowahi zifanya na zikanishinda kwenye utafutaji

Kazi nilizowahi zifanya na zikanishinda kwenye utafutaji

Sio kila hustle wife ajue eti kisa mnapendana. Kuna misala mingi kama mwanaume unatakiwa usimame mwenyewe tu mradi wao wasilale njaa. Kusema kila kitu sio uanaume. Binafsi nilipataga msala job wife alijua nipo likizo ndio baadae nikamwambia nimesimamishwa kazi. Hata baadae nilipotimuliwa alijua ni kwa sababu niliyokua nimemwambia kumbe sababu ni nyingine kabisa ambayo alikuja kuijua kama 4yrs later wakati maisha yalishasonga kivingine. Alijua baada ya kufungua makabrasha yangu kwenye briefcase alishangaa sana kujua kumbe nilikua na msala mkubwa kiasi kile na niliwezaje kupretend niko normal. Ulikua msala mzito wa kula mvua za kutosha ila niliupangua kivyangu na hadi leo akiniangalia hanimalizi
Daaaah teacher kumbe ni wewe daaah pole sana [emoji23] ulikua una fundisha pale ubungo ukatia mtoto mimba ukatimuliwa kazi ukafungua kiduka madale kule daah pole sana maisha hayana formula one
 
Kuna siku nipo maskani nishachoka zanguu,akaja jamaa akasema anaeweza kuchezea mavi twende kuna kazi huko,,

Nikamuuliza kazi gani? akasema mwenye nyumba anataka chemba ya choo tuchote mavi yote na ndooo tukamwage kwenye shamba lake ili ile chemba iongezwe urefu yani pale ilipo ifukuliwe zaidi kwenda chini..

ila huwezi kufukua zaidi bila kutoa kinyesi chote, tukamwambia si aite tu gari ya kunyonya mavi inyonye, Akasema njia ya kufika kwake gari ya mavi haifiki na hata wakifosi gharama ni kubwa mno inafika 1m na huyo mzee hiyo hela hana..

hivyo mzee katoa ofa ya watu kuchota mzgo wote na ndoo na kwenda kuumwaga huko shambani kwake, Tukauliza OFA yake sh ngapi?

Jamaa akasema kazi tunaifanya watu wa 4 tu mzee kasema atatoa 100,000 kwa kila mtu,jamaa mmoja akasema mwambie aongeze walau iwe 150,000 tukapge kazi, nazama chumvini nalamba inye live na ulimi sembuse hiyo harufu inishinde? mwambie aongeze dau...

Jamaa akavuta simu kwa mshua akamwambia vijana wa kazi wamepatikana ila wanasema 100k haitoshi waongeze 50k iwe 150k, mzee akajibu Sawa njooni.

Jamaa akasema oyaa mshua kakubali, Huyo mwingine akawambia sasa sikilizeni hapa tunaenda nunua mafuta ya Taaa kidumu cha lita 5 tunamwaga mwaga mule kwenye chemba mote Harufu inakata kazi tunapga freshi..

Kusikia hivyo tukaona jamaa katoa idea nzuri sana,kweli haooo hadi kwa mangi tukanunua mafuta ya taaa haooo safari ikaanza kwenda site.

Tumefika tukaenda kwenye chemba, ilikua tayari ishabomolewa lile zege la juu hivyo limebaki shimo pana tu unaona inye live live,mafinyo finyo live live, Jamaa akamwaga mafuta ya taaa pwaaaaaa koteee..

Tukaletewa ndooo kila mtu na ndoo yake,gloves kazi ikaanza nikadumbukiza nikachota ndoo ya kwanza nikatoa,jamani jamani jamani nilienda kumwaga shambani nikapitiliza huko huko sikurudi nyuma tena.

Asee inye isikieni tu,ile 150,000 nikaona wala isinipe presha mimi,na niikose tu siwezzi chezea gwede gwede kama vile ni rost... nimeondoka nimefika maskani nasimulia waliobaki,nusu saa haijaisha namuona mwenzangu mwingine huyu hapa karudi, aaah weee kuna kazi za kufanya bwana sio kazi ya kuchezea tope la binadamu..
 
1850 tsh kwa siku??au umekosea kuandika.

#MaendeleoHayanaChama
Hajakosea nina hakika,unashangaa hiyo mkuu wakati kuna kiwanda malipo

ilikua ni 3000 per day na mule ndani ukifanya kosa lolote unakatwa jero

hamna mfanyakazi anae ingia akatoka hajakatwa hata buku,mimi day 1

tu niliingia nikakosea makosa ma3 nikalimwa 1500 jioni nikapewa 1500 yangu

kesho yake sikurudi na ndio ilikua forever and for always bye bye,hata uwe malaika

ile kiwanda huwezi salimika ukakosa kosa,hizo kazi sasa,Hata jehanamu hamna kazi ngumu hvyo naamini...
 
all in all pole sana
Asante mkuu,katika kazi naziheshimu hii dunia ni kazi wanazofanya walinzi

binafsi siamini mlinzi 1,huwezi linda kwangu uwe peke ako,pili siwezi kubali mlinzi

wangu apate mshahara mdogo,ki ufupi nawajali walinzi wangu mpka wanashangaaga

wananiona nina pesa labda,ila ukweli ni kwamba naelewa msoto wanaopitia usiku

hasa vipindi vya mvua na baridi,yani walinzi na waheshimiwe ile kazi ni ngumu sana sana sana..
 
Kazi ya kukata nondo nilikuwa nazunguka na fundi tunafunika mashimo ya choo zile chemba per day 20k mda sana nilikuwa kama form three .... Kama hujazoea ni balaa tukawasha moto na tunazipasha kilocal nakumbuka niliota sugu ila pesa tamu sana ilikuwa tunapiga dili ila mi naenda jumamosi na jumapili nikatoka Nina elfu 40 shule naenda na buku mbili daily halafu sio mbali.

Kipindi naanza Kuna siku nilipiga kazi kazi chemba ilikuwa kama ya gesti ikawa kubwa nakumbuka palikuwa ni pongwe -Tanga .. Basi tulikata nondo kibao kazi ya siku mbili tulidamka kama 11 baada ya swala tukapanda gari ya kwenda lushoto inaitwa shashui kama dk 20 au 15 tuko site kutokea Tanga mjini .. tulipigia kazi kukata nondo Mpaka saa 4 kazi tulipiga kwa siku moja muhindi akatupa chetu ilikuwa j2 kesho yake skonga ..

Nimeamka videle vinacheza yaani vinabrate hata mwenyewe sijui kushika kitu siwezi na palikuwa na test kila j3 kipind cha kwanza nikamchana ticha nikaomba ruhusa ya kuumwa .

Siku nyingine nilipiga zege sana kweny gorofa moja msuli ulikaza usiku
 
Kuna siku nipo maskani nishachoka zanguu,akaja jamaa akasema anaeweza kuchezea mavi twende kuna kazi huko,,

Nikamuuliza kazi gani? akasema mwenye nyumba anataka chemba ya choo tuchote mavi yote na ndooo tukamwage kwenye shamba lake ili ile chemba iongezwe urefu yani pale ilipo ifukuliwe zaidi kwenda chini..

ila huwezi kufukua zaidi bila kutoa kinyesi chote, tukamwambia si aite tu gari ya kunyonya mavi inyonye, Akasema njia ya kufika kwake gari ya mavi haifiki na hata wakifosi gharama ni kubwa mno inafika 1m na huyo mzee hiyo hela hana..

hivyo mzee katoa ofa ya watu kuchota mzgo wote na ndoo na kwenda kuumwaga huko shambani kwake, Tukauliza OFA yake sh ngapi?

Jamaa akasema kazi tunaifanya watu wa 4 tu mzee kasema atatoa 100,000 kwa kila mtu,jamaa mmoja akasema mwambie aongeze walau iwe 150,000 tukapge kazi, nazama chumvini nalamba inye live na ulimi sembuse hiyo harufu inishinde? mwambie aongeze dau...

Jamaa akavuta simu kwa mshua akamwambia vijana wa kazi wamepatikana ila wanasema 100k haitoshi waongeze 50k iwe 150k, mzee akajibu Sawa njooni.

Jamaa akasema oyaa mshua kakubali, Huyo mwingine akawambia sasa sikilizeni hapa tunaenda nunua mafuta ya Taaa kidumu cha lita 5 tunamwaga mwaga mule kwenye chema mote Harufu inakata kazi tunapga freshi..

Kusikia hivyo tukaona jamaa katoa idea nzuri sana,kweli haooo hadi kwa mangi tukanunua mafuta ya taaa haooo safari ikaanza kwenda site.

Tumefika tukaenda kwenye chemba, ilikua tayari ishabomolewa lile zege la juu hivyo limebaki shimo pana tu unaona inye live live,mafinyo finyo live live, Jamaa akamwaga mafuta ya taaa pwaaaaaa koteee..

Tukaletewa ndooo kila mtu na ndoo yake,gloves kazi ikaanza nikadumbukiza nikachota ndoo ya kwanza nikatoa,jamani jamani jamani nilienda kumwaga shambani nikapitiliza huko huko sikurudi nyuma tena.

Asee inye isikieni tu,ile 150,000 nikaona wala isinipe presha mimi,na niikose tu siwezzi chezea gwede gwede kama vile ni rost... nimeondoka nimefika maskani nasimulia waliobaki,nusu saa haijaisha namuona mwenzangu mwingine huyu hapa karudi, aaah weee kuna kazi za kufanya bwana sio kazi ya kuchezea tope la binadamu..
Ukaona ya nini kujifia
 
Asante sana mtoa mada !! Nyakati kama hizo za kupambania kombe mwanaume unakua umejikataa kabisa !!

Mimi kazi ngumu niliyosema sitawahi kurudi ni kazi ya ujenzi !! Siku moja nikasema ngoja nikacheki site !! Nilivyofika nikakuta wahuni washaanza kazi ila yule msimamizi akanambia Dogo subiri hapa nyie mtashusha Cement ! Mara Gari likaingia limefunga mifuko 400 ya cement nilikua na mwanagu mmoja tukapata na mtu mmoja tukawa watatu

Tunahamisha mifuko kutoka kwenye gari kuipeleka store moja inawekwa kwa kupangwa kwenda tuliahidiwa kila mfuko tunaubeba kwa sh 100 hivyo tuna 40k tugawane !! Nilichubuka sana maeneo ya mgongo !! Kesho sikurudi

Nikaenda site nyingine huko nilikuta ndo wanatengeneza foundation ya chini kabisa ya Ghorofa , kwa hiyo ilikua kumwaga zege wenyewe wanaita "Ghala' tulipiga kazi toka saa mbili asubuhi unaambiwa zege hailali mpaka saa sita usiku muhindi akatulipa 12500.
Ila kuna watu wanakua wameridhika na kazi tu fresh
 
"UTAPIGA KAZI MPAKA UITEE MMAA"

Nakumbuka enzi zile sina mishe yoyote na nasaka pesa.niliamka asubuhi moja na kuiingia mtaani, kupita mtaa fulani nkaona watu wamesimama nje ya geti ya site ya ujenzi wanahesabiwa.

Nikaona wanapangiwa kazi za kufanya, walikuwa watu kati 40 mpaka 50 hivi.Kidume mbio nkajipenyeza.

Sasa yule Mhandisi(nilikuja kumjua badae) aliyekuwa anahesabu watu na kupanga majukumu akaniweka kwenye kundi la 2( watu 23 maana yake tukawekwa magroup ma2 ya watu 23, 23 kama sikosei).

nikasikia yule mhandisi anatoa majukumu kwa group letu kuwa "" nyinyi wazee ni wazee wa MMAA"" na natoa 40,000 kwa kila mmoja kazi ikiisha.
Daah kusikia 40,000, nkaona kazi si ndo hii jamani.
Ila sasa sikuelewa alivyomaanisha "wazee wa mmaa",

kumbe banaaa ni wazee wa zege la jamvi la juu ya GHOROFA ya tatu.zege la kukesha, zege la kufa mtu,aaah manina

wenzetu wao yani kundi la pili wao ni kazi za chini.

*****************************************

Picha linaanza tulianza kupakua mifuko kama 300 ya cement, mchanga lori, kokoto lori, mixer na gari la maji .halafu kilichonitisha walishusha ndoo kubwakubwa za kubebea zege kama 200 hivi.

AISEEEEE, AISEEEE. ndo nilijua kwanini sisi tunaitwa"" wazee wa MMAAA" yani utapiga kazi mpaka uombe maji kama mtoto.


Zege linakorogwa chini unalipandisha kwa kichwa mpaka ghorofa ya 3.MANINAAAAAA

nilipiga trip kama 6 hivi,nikiwa napandisha trip ya 6, nkasikia lijamaa limoja eti kwann mimi mchumba nimekuja kwenye kazi za wanaume. Niliumia sana, nkajikaza trip kama 5 zingine.
ile trip ya mwisho, nkasikia shingo imekaza.[emoji16][emoji16][emoji16]nikajiuliza kwanini nifie site??

Nilimuaga msimamizi kuwa naiingia toilet 2mins , Akajibu ""chapu chapu dogo huu si muda wa kulemba kanye huku umesimama maana hii ngoma tunakesha mpaka uitee mmaa""

nilivyokata kona, nilikimbia mnooooo,zile trip 11 nilizopiga niliumwa 2 days[emoji2]
Sikuwahi kufanya kazi ya zege tena.

Kwa jinsi nilivyo- kila nkimhadithia wife kuwa nilipiga kazi za hovyo huwa anakataaa sanaaa, sijui why but anyway.

wakuu tusikate tamaaa maishani.

"wazee wa mmaa"[emoji23][emoji23]
Dah nimecheka Sana pole Sana mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu uzi umenikumbusha muda kidogo miaka kama 3 nyuma tunaunga kazi za zege kwa mafundi ujenzi na kwenye majengo makubwa. Sasa bwana kuna kazi ya kuondoa brown zile kwenye magorofa ilikua kiwandani yale majengo yao ni marefu maana ni maalumu kwa mitambo hivyo yameenda juu. Kuanzia chini mpaka juu kuna urefu sio kdgo. Tukapewa kazi pale nikapanda juu na spana zile ili nianze kufungua bomba zile zilizokamata brown na mbao kazi ianze. Kufika juu nikafingua chuma ya kwanza nikaangalia urefu chini nikaangalia namna ya kuset nitakapo simama, nikapiga hesabu zangu nikatafakari malipo yale nguvu zikakata. Niliona risk ya kudondoka ni kubwa na kazi ile ni ngumu nikashuka nikaenda kumpa msimamizi spana nikamuuliza kuna kazi zingine hii hapana. Kajibu labda wiki nnyingine mimi huyooo nikasepa. Kazi zingine we sikia tu
 
Asante sana mtoa mada !! Nyakati kama hizo za kupambania kombe mwanaume unakua umejikataa kabisa !!

Mimi kazi ngumu niliyosema sitawahi kurudi ni kazi ya ujenzi !! Siku moja nikasema ngoja nikacheki site !! Nilivyofika nikakuta wahuni washaanza kazi ila yule msimamizi akanambia Dogo subiri hapa nyie mtashusha Cement ! Mara Gari likaingia limefunga mifuko 400 ya cement nilikua na mwanagu mmoja tukapata na mtu mmoja tukawa watatu

Tunahamisha mifuko kutoka kwenye gari kuipeleka store moja inawekwa kwa kupangwa kwenda tuliahidiwa kila mfuko tunaubeba kwa sh 100 hivyo tuna 40k tugawane !! Nilichubuka sana maeneo ya mgongo !! Kesho sikurudi

Nikaenda site nyingine huko nilikuta ndo wanatengeneza foundation ya chini kabisa ya Ghorofa , kwa hiyo ilikua kumwaga zege wenyewe wanaita "Ghala' tulipiga kazi toka saa mbili asubuhi unaambiwa zege hailali mpaka saa sita usiku muhindi akatulipa 12500.
Ila kuna watu wanakua wameridhika na kazi tu fresh
Mkuu hii ya ujenzi bora kwa waswahili wenzetu kwa mhindi au mchina wanaua mzee kaI mlima malipp kijiko
 
Asante mkuu,katika kazi naziheshimu hii dunia ni kazi wanazofanya walinzi

binafsi siamini mlinzi 1,huwezi linda kwangu uwe peke ako,pili siwezi kubali mlinzi

wangu apate mshahara mdogo,ki ufupi nawajali walinzi wangu mpka wanashangaaga

wananiona nina pesa labda,ila ukweli ni kwamba naelewa msoto wanaopitia usiku

hasa vipindi vya mvua na baridi,yani walinzi na waheshimiwe ile kazi ni ngumu sana sana sana..
Da kweli mkuu ,kazi ukishaipitia lazima twaswira na huruma itakujia , ila sio wote hufikili haya mkuu, Sema ni Mungu amekuinua na kutambua ulipotoka ndo maana unawatendea yaliyo mazuri walinzi wako
 
Back
Top Bottom