Kazi uliyokuwa ukiipenda pindi ungali mdogo ndo unaifanya Sasa?

Utotoni kabisa nilikuwa nataka kuwa rubani, baadae nilivyofika sekondari nikataka kuwa surgeon nilipofika advance nikataka kuwa mfamasia au telecom engineer na vyote hapo hakuna hata kimoja nilisomea chuoni ila nafikiria kutimiza kimoja kati ya hivyo nikijaaliwa uhai na uzima.
 
pindi zitakapofika nyakati ambazo kila mtu atakuwa anafanya jambo la ndoto yake basi na dunia itakuwa imekaribia kufika mwisho......
 

Nilitamani kuwa Kama huyo pichani!..
Hivi mganga wa kienyeji ndo anaitwa witch doctor..?
Nauliza tu!..😎
 
Kwa mwenye mafikirio huu uzi ni sad story kwa watu wengi humu.
Nakumbuka familia ilipenda niwe mwanasheria.

Mimi nilipenda niwe administrator.

Nikiwa ktk masomo ya juu kuna jamaa akawa anachukua certificate ya sheria masomo ya jioni angali ansoma kitu kingine hapo hapo chuoni. Nilimuuliza hii certificate ya nini akasema ni kwa ajili ya ulinzi tu.

Nikakumbuka ndoto ya kuwa mwanasheria na hata ya kuwa administrator nayo ikipotea.

In my next 10 years life I wish kutimiza one of them.
Maisha mengi ya waafrika si yakutimiza ndoto bali ni kuutafuta kula, kuvaa, kujenga familia na kufa
 
Yes nilipenda kuwa Mhasibu na imekuwa hivo paka Sasa
 
Nilikuwa napenda kuwa mwanajeshi nilikuwa napenda mavazi yale na kofia na Traffic police nguo zao na kuelekeza magari unajiona na wewe umevalia lakini huku ukubwani hutaki hata kusikia kazi hizo..
 
Hivi mtu anaweza piga postgraduate ya law pale open akatambuliwa kama mwanasheria?

#MaendeleoHayanaChama
 
Nilitamani sana urubani, ila nimeishia kushika mikoba ya mwanasiasa kila aendapo ninaye (niko na yeye)
 
Nilitamani sana urubani, ila nimeishia kushika mikoba ya mwanasiasa kila aendapo ninaye (niko na yeye)
Na anza kuamini Moja Kati ya ndoto inayo ongoza kwa kutotimia ukizaliwa kusini mwa jangwa la sahara basi ni urubani.....
 
Wakuu mimi nina ndoto nyingi sana.

1.nilitamani kuwa daktari.

2.nilitamani sana kuwa kiongozi mkubwa ambae nitawasimamia watu na kuwahamasisha kuhusu maendeleo ya nchi huku mimi nikiwa nimesimama kidete.

Ila cha ajabu sijui hata kama nilikuwa serious na ndoto hizi.

Nikifikiria uongozi wenyewe unavyoupata sina watu chamani,mama yangu alikuwa mwenyekiti wa wanawake CCM katika kata tu,sina connection yoyote.

Najiona kabisa naweza kuwa kionggozi na nisiwe fisadi ila acha tu nifanye mambo mengine.

Naumia sana na tanzania yangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…