Keir Starmer kuwa Waziri Mkuu mpya wa Uingereza huku Rishi Sunak akikubali kushindwa

Keir Starmer kuwa Waziri Mkuu mpya wa Uingereza huku Rishi Sunak akikubali kushindwa

Uchaguzi wa Uingereza hata siuelewi. Ndani ya mwezi umetangazwa na kufanyika. Nasikia waziri mkuu anaweza kuitisha uchaguzi muda wowote ilimradi tu ufanyike mara moja ndani ya miaka mitano. Anaeelewa vizuri uchaguzi wa UK anijuze.
 
Uingereza raia wake ni too demanding na wana deko la kuwa na historia ya viongozi wazuri zamani. Hawaridhiki na hawakubali mapungufu kidogo au uwezo pungufu kidogo wa kiongozi. Na hawana muda wa tumpe muda sijui tuwe na imani, mara anashauriwa vibaya. Wao ukifanya kosa moja ndio wamemaliza hivyo hawana imani na wewe.
Yalioikumbuka uingereza sio mapungufu kidogo
Unadhani ma PM wote watano walikua na mapungufu madogo madogo kama usemavyo
Kiukweli UK kuna majambo hayapo sawa haiwezekani nchi kama UK ndani ya miaka 7 sijui 8 wawe washabadilisha PM zaidi ya watatu kisa jambo dogo tuuu
 
Sir Keir Starmer atakuwa waziri mkuu ajaye wa Uingereza baada ya Rishi Sunak kukubali kushindwa katika kukabiliana na chama cha Labour.

Waziri Mkuu Sunak alisema wapiga kura wametoa "uamuzi wa kutisha" juu ya chama chake baada ya miaka 14 madarakani.

Kiongozi wa chama cha Labour Sir Keir Starmer alisema watu kote nchini Uingereza walikuwa wametangaza kuwa "tayari kwa mabadiliko".

Katika hotuba yake ya kukubali kushindwa baada ya kushikilia kiti chake cha Richmond na Northallerton, Bw Sunak alisema: "Chama cha Labour kimeshinda Uchaguzi huu Mkuu na nimempigia simu Sir Keir Starmer kumpongeza kwa ushindi wake."

Bw Sunak aliongeza: “Leo, tutabadilishana mamlaka kwa njia ya amani na yenye utaratibu na nia njema kwa pande zote. "Na ni jambo ambalo linapaswa kutupa imani sote katika utulivu na mustakabali wa nchi yetu."

"Watu wa Uingereza wametoa uamuzi mzito usiku wa leo, kuna mengi ya kujifunza ... na ninawajibika kwa hasara hiyo. Kwa watahiniwa wengi wazuri, wa Kihafidhina waliofanya kazi kwa bidii ambao wamepoteza usiku wa leo, licha ya juhudi zao zisizo na kuchoka, rekodi zao za mitaa na utoaji, na kujitolea kwao kwa jumuiya zao. Samahani."

=====

Pia soma: UK General Election: Waingereza leo kupiga kura kumchagua Waziri Mkuu na Wabunge
Chama chao ilikua inasubiriwa elwction tu,
 
Uingereza raia wake ni too demanding na wana deko la kuwa na historia ya viongozi wazuri zamani. Hawaridhiki na hawakubali mapungufu kidogo au uwezo pungufu kidogo wa kiongozi. Na hawana muda wa tumpe muda sijui tuwe na imani, mara anashauriwa vibaya. Wao ukifanya kosa moja ndio wamemaliza hivyo hawana imani na wewe.
Nimemkumbuka

Liz Truss: I'm a fighter, not a quitter


Nabado akafurushwa


Sema wabunge wa huku naonaga wanapiga sana kelele

View: https://www.bbc.com/news/av/uk-politics-63313539
 
Wamewawekea majasusi kutoka civil services kwenye uongozi wa labour ilikuwa lazima ishinde baada ya chaos ya miaka 6 kwenye uongozi wa juu ndani ya conservatives.

Key player hapo ni ‘Rachel Reeves’ shadow chancellor ‘the city’ (financial and equity markets) wana imani nae uchumi utabaki salama chini yake sio mtu atakepeleka policies hatari kwao. Ndio maana huu uchaguzi wamekaa kimya.

Keir Starmer ni career civil servant last alikuwa DPP

Rachel Reeves kafanya kazi bank kuu, katoka hapo kaenda foreign office, mshauri mkuu wa mambo ya sera za uchumi na dunia, baadae U.K. embassy in US kushauri uchumi. Kurudi U.K. private banking, kaacha kazi ya mshahara wa pound million kadhaa with bonus kwenda kwenye siasa; wakati head hunters wa mabank wanamgombania.

Wamejaza civil servants kadhaa huko juu ambao sio career politicians, kushindwa ilikuwa possibility ndogo sana.
Asante kwa ufafanuzi huu
 
Lilikuwa ni suala tu la muda. Kwanza mtu mwenye aliipata hiyo nafasi kwa bahati nasibu tu. Halafu akajifanya kiherehere kuingia kwenye vita dhidi ya Urusi.

Na bado viherehere wenzake wengine. Wote watatoka madarakani na hivyo kuingia serikali mpya. Na hii ni kuan,ia hapo Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Marekani kwenyewe, nk. Kote wananchi wanafanya mabadiliko baada ya nchi zao kujiingiza kwenye mgogoro wa Urusi vs Ukraine na hivyo kuwasababishia athari za kutosha tu za kiuchumi.
Ulaya na kwingineko zinaingia Serikali ambazo zinapinga uhamiaji holela na dini za kigeni.
 
Sir Keir Starmer atakuwa waziri mkuu ajaye wa Uingereza baada ya Rishi Sunak kukubali kushindwa katika kukabiliana na chama cha Labour.

Waziri Mkuu Sunak alisema wapiga kura wametoa "uamuzi wa kutisha" juu ya chama chake baada ya miaka 14 madarakani.

Kiongozi wa chama cha Labour Sir Keir Starmer alisema watu kote nchini Uingereza walikuwa wametangaza kuwa "tayari kwa mabadiliko".

Katika hotuba yake ya kukubali kushindwa baada ya kushikilia kiti chake cha Richmond na Northallerton, Bw Sunak alisema: "Chama cha Labour kimeshinda Uchaguzi huu Mkuu na nimempigia simu Sir Keir Starmer kumpongeza kwa ushindi wake."

Bw Sunak aliongeza: “Leo, tutabadilishana mamlaka kwa njia ya amani na yenye utaratibu na nia njema kwa pande zote. "Na ni jambo ambalo linapaswa kutupa imani sote katika utulivu na mustakabali wa nchi yetu."

"Watu wa Uingereza wametoa uamuzi mzito usiku wa leo, kuna mengi ya kujifunza ... na ninawajibika kwa hasara hiyo. Kwa watahiniwa wengi wazuri, wa Kihafidhina waliofanya kazi kwa bidii ambao wamepoteza usiku wa leo, licha ya juhudi zao zisizo na kuchoka, rekodi zao za mitaa na utoaji, na kujitolea kwao kwa jumuiya zao. Samahani."

=====

Pia soma: UK General Election: Waingereza leo kupiga kura kumchagua Waziri Mkuu na Wabunge
Safi Sana
 
Sema kwa viongozi sio wananchi.
Viongozi wanaojitambua ama taasisi ama serikali inayojitambua.
Kama wananchi hawajitambui uhangaike kuiba kura ili iweje!?
Wananchi ndio chanzo!! Sasa hata unapoiba kura hakuna wanaloweza fanya, unategemea nini??! Viongozi wa kizungu wanajitambua toka utotoni, na hawana njaa, AFrica shida ni njaa na ubinafsi wetu.
 
Fuatilia vizuri siasa za UK kabla ya kutoa maoni yako. Nahisi hapa unatumia mihemko zaidi kuliko hali halisi ilivyo. Huyo Sunak alikuwa Waziri Mkuu wa tatu kipindi cha miaka mitano.
Ni vizuri ukijikita kwenye kutoa maoni yako. Masuala ya kuhisi mimi natumia mihemko zaidi, yanaingiaje hapa? Kama unazifahamu vizuri hizo siasa za Uingereza, ziweke hapa jukwaani na tutakuelewa vizuri tu. Huo ni mtazamo wangu tu.
 
Lilikuwa ni suala tu la muda. Kwanza mtu mwenye aliipata hiyo nafasi kwa bahati nasibu tu. Halafu akajifanya kiherehere kuingia kwenye vita dhidi ya Urusi.

Na bado viherehere wenzake wengine. Wote watatoka madarakani na hivyo kuingia serikali mpya. Na hii ni kuan,ia hapo Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Marekani kwenyewe, nk. Kote wananchi wanafanya mabadiliko baada ya nchi zao kujiingiza kwenye mgogoro wa Urusi vs Ukraine na hivyo kuwasababishia athari za kutosha tu za kiuchumi.
Urusi ni noma sana, wamemuondoa madarakani waziri mkuu wa Uingereza huku wakimuweka wanayemtaka
 
hajatoka kwasababu ya kuipiga vita urusi bali kwasababu Rish hakuwa strong hivyo wanahitaj mtu atakae irudisha heshima ya UK na kulinda tamaduni zao UK
Lilikuwa ni suala tu la muda. Kwanza mtu mwenye aliipata hiyo nafasi kwa bahati nasibu tu. Halafu akajifanya kiherehere kuingia kwenye vita dhidi ya Urusi.

Na bado viherehere wenzake wengine. Wote watatoka madarakani na hivyo kuingia serikali mpya. Na hii ni kuan,ia hapo Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Marekani kwenyewe, nk. Kote wananchi wanafanya mabadiliko baada ya nchi zao kujiingiza kwenye mgogoro wa Urusi vs Ukraine na hivyo kuwasababishia athari za kutosha tu za kiuchumi.
 
Wananchi ndio chanzo!! Sasa hata unapoiba kura hakuna wanaloweza fanya, unategemea nini??! Viongozi wa kizungu wanajitambua toka utotoni, na hawana njaa, AFrica shida ni njaa na ubinafsi wetu.
Hehehehe.
Umeongea vise versa mkuu.
Mtu keshakufa,unaweza kuwa na hofu naye!?
Viongozi wetu hawajielewi ndio maana wanatumia udanganyifu kukaa madarakani kwasababu uroho wao wa madaraka umewatoa akili.
Sio kwamba hawajui na hawaoni kama raia wanajua utumbo wanaofanya,wanaona na wanajua,ila kwa kutokuelewa kwao wanatumia nguvu kuwatuliza hao raia.
Viongozi wa wenzetu wanajielewa ndio maana wanafanya maamuzi sahihi kwa ustawi wao na raia wao.
Shida ni viongozi sio raia.
 
Back
Top Bottom