Kelele zikiwa nyingi na kuwazomoea Bodi Kwa Maamuzi ya Kijinga, msije kushangaa Yanga anapewa Point 3 maana washaanza kuraruana tayar.

Kelele zikiwa nyingi na kuwazomoea Bodi Kwa Maamuzi ya Kijinga, msije kushangaa Yanga anapewa Point 3 maana washaanza kuraruana tayar.

Usilete matusi Yako hapa,
Nimeamka nimepitia Mitandao yangu pendwa miwili X formerly known as Twitter na JF.

Nilichokiona hata waliokua wanatetea swala la Simba mapema Ile wamegeuka nao saiv wanailaumu Bodi.
Utaratibu wa Timu kupewa pointi 3 baada ya timu nyingine kutofika uwanjani upoje? Maana:

1. Ilitakiwa Yanga wafike uwanjani muda wa mchezo husika.

2. Kuwe na viongozi wote wa mechi husika wakiwemo makamishina na refarii uwanjani ambaye atawaongoza waingie uwanjan muda ukifika.

3. Saa moja na robo refarii angepuliza kipyenga kuashiria kuanza kwa mchezo.

4. Refarii angesubiria timu nyingine iingie uwanjani kwa muda wa dakika 15.

5. Baada ya dakika 15 kutimia bila timu nyingine kuingia uwanjani, refarii angemaliza mechi na timu iliyokuwepo uwanjan ingepewa ushindi na alama 3.

Je! kwa jana hayo yote yalikamilika ili Yanga wapewe ushindi na alama 3 kama kichwa cha habari cha bandiko hili kinavyodai?
 
aliyeogopa ni yule aliyemkataza mwenzie asiingie uwanjani akakimbize majini
Hawakutoa taarifa popote, waliibuka kama mzimu. Na Yanga hawashiki funguo za uwanja, na wao walipowasiliana na meneja wa uwanja ndio akawalima ban sio kiongozi wa Yanga.

Kuipakazia Yanga ni kichaka tu ili kosa wamtupie mwananchi.
 
Usilete matusi Yako hapa,
Nimeamka nimepitia Mitandao yangu pendwa miwili X formerly known as Twitter na JF.

Nilichokiona hata waliokua wanatetea swala la Simba mapema Ile wamegeuka nao saiv wanailaumu Bodi.
Naona simba kawashika pabaya msimu huu na mahujuma yenu mshaaza kutoa milio. Mumeona hamuwezi kuhonga refa kama kwa kayoko mkaamua kutumia udhaifu wa sheria ili muhujumu mechi. Mlijua simba ataingiza timu na mtalipa hiyo fine ya mil 1. Sasa mechi imepangwa upya na siku ya mechi mkiruka ukuta, mkijua mtalipa tu fine, simba hawatii timu. Mpka myooke wajinga nyie
 
Usilete matusi Yako hapa,
Nimeamka nimepitia Mitandao yangu pendwa miwili X formerly known as Twitter na JF.

Nilichokiona hata waliokua wanatetea swala la Simba mapema Ile wamegeuka nao saiv wanailaumu Bodi.
Walioahirisha mechi ni nani km sio bodi ya ligi?
 
Usilete matusi Yako hapa,
Nimeamka nimepitia Mitandao yangu pendwa miwili X formerly known as Twitter na JF.

Nilichokiona hata waliokua wanatetea swala la Simba mapema Ile wamegeuka nao saiv wanailaumu Bodi.
Halafu, binafsi nina hili la kanuni ya 22(1) inayosema;

1741500605456.png



Swali, je! 51mba walipeleka malalamika kwa bodi ya ligi juu ya kuzuiwa kufanya mazoezi? Kama hawakupeleka, kwangu mimi, kikao kilichoghairisha mchezo ni batili. Hivyo, mechi ilitakiwa ichezwe. Ambaye hakuja uwanjani, kanuni ziseme naye..!!
Vilevile, 51mba nao waseme, wametumia kanuni gani kutoleta timu uwanjani?

Kwababu ya hayo yote hapo juu, kanuni namba 17(44) ambayo inasema;

1741501139694.png

Ichukue mkondo wake

CC bulajunior
 
Hii haiingii akilini kwamba et Simba wamekosea, hapana aisee. Hata kama iwe waliona mbali (kuchezea kichapo), sababu wameipata ya msingi. Timu hizi zinatuhumiana ushirikina, kutokana na hili, taarifa ya siku na saa ya timu mgeni kufanya mazoezi inapotolewa mapema au kujulikana mapema kunaweza kufikiriwa kuwa kutampa nafasi mwenyeji kufanya uhuni wa kishirikina utakakaowaathiri wageni kwa namna moja ama nyingine wakati wa mazoezi hadi wakati wa mechi. Hofu hiyo lazima iwepo kwa mgeni. Kwa kuwa kanuni inatoa muda wa mazoezi kwa timu mgeni kuwa ni wakati ulio sawa na muda wamechi na mwisho iwe ni siku moja kabla ya siku ya mechi, timu mwenyeji alipaswa kutambua kuwa siku yoyote na katika saa iliyopangwa kisheria mgeni anaweza kuja kufanya mazoezi hivyo wahusika (wenyeji) wajipange sawasawa ili wawe tayari kuwakaribisha. Ikiwa mwenyeji ataona kuna viashiria vinavyoleta wasiwasi kwa kuwatilia mashaka wageni, basi angeweza kuwasiliana chap na mamlaka zinazohusika ili zitume wachunguzi ambao wataamua timu kuruhusiwa au kuzuiliwa baada ya uchunguzi.
Sasa hii ya walinzi tu kuwazuia wageni pia kunaweza kutafsiriwa kuwa hwenda nao wameroga vya kutosha humo wakidhani mgeni hana mpango wa kufanyia mazoezi humo, kwamba atakutana na ugumu tu wakati wa mechi kumbe anakuja na anaweza kugundua na kutengua mitego hiyo hivyo solution ni kuwazuia kuingia.
Ki msingi adhabu ianze na waliozuia mazoezi kwa wageni ndipo uangaliwe uamuzi wa wageni kama ulikuwa sahihi au la nao wale adhabu wakipatikana na makosa.
 
Hawakutoa taarifa popote, waliibuka kama mzimu. Na Yanga hawashiki funguo za uwanja, na wao walipowasiliana na meneja wa uwanja ndio akawalima ban sio kiongozi wa Yanga.

Kuipakazia Yanga ni kichaka tu ili kosa wamtupie mwananchi.
meneja wa uwanja hajui kanuni?
wapi kwenye kanuni za tff zinasema ukitaka kwenda kufanya mazoezi utoe taarifa?
 
Usilete matusi Yako hapa,
Nimeamka nimepitia Mitandao yangu pendwa miwili X formerly known as Twitter na JF.

Nilichokiona hata waliokua wanatetea swala la Simba mapema Ile wamegeuka nao saiv wanailaumu Bodi.
Mnaweweseka sana na mtasoma kila mtandao lakini ukweli ni kwamba mechi itachezwa baadae na utopolo lazima aiandae na waruhusu Ubaya Ubwela waingie na watu wao wafupi na meeeeeee😎😎😎
 
Usilete matusi Yako hapa,
Nimeamka nimepitia Mitandao yangu pendwa miwili X formerly known as Twitter na JF.

Nilichokiona hata waliokua wanatetea swala la Simba mapema Ile wamegeuka nao saiv wanailaumu Bodi.
Ni upumbavu kosa la kikanuni kuahirisha mechi na kuwaletea watu hasara za mamilioni na kuwapotezea muda
 
kanuni inasema timu pinzani itafanya mazoezi siku moja kabla ya mechi kwe nye uwanja husika.mlikuwa hamjui hii kanuni?
mnataka mpewe taarifa ili mfiche nini!
Na kanuni hiyo haisemi usipofanya mazoezi kwenye uwanja husika ususie mechi? Ni utoto wa hali ya juu kilichofanywa jana
 
Na kanuni hiyo haisemi usipofanya mazoezi kwenye uwanja husika ususie mechi? Ni utoto wa hali ya juu kilichofanywa jana
kama walianza?....
kwani tff walipopeleka muda mbele kanuni ilisema timu isiingie uwanjani!?mbona hamjaja?kufanya mfanye nyie ila wakifanya wenzenu wamekosea
 
Yanga hawezi kupewa pointi tatu za bure maana kanuni za mchezo zinataka refarii na wasaidizi wake wote wawepo uwanjani na timu moja iwepo uwanjani kisha baada ya muda fulani kama timu pinzani haijaingia uwanjani refarii anamaliza mpira.

Hapo ndiyo utaratibu wa kikanuni utakuwa umefuatwa na ni halali kwa timu iliyofika uwanjani kupewa pointi tatu.

Sasa jana Uto wamepeleka timu bila uwepo wa maafisa wa mchezo husika unadhani wanapata wapi hizo pointi tatu?

Vitu vingine ni kutumia common sense tu.
 
Maamuzi ya kuahirisha mpira wa jana ni kati ya maamuzi mabovu kuwahi kufanyika
Kwa sababu sababu zilizokuwepo hazikuwa na uzito wa kutosha kuahirisha mpira

1. Kitendo cha Simba kupeleka team uwanjani bila taarifa jioni/usiku, kilitosha kabisa kuwazuia kwa sababu; uongozi wa Uwanja unatakiwa kuwa na taarifa ili kuweka mazingira sawa ikiwepo kuwa na walinzi, wafanyakazi nk kwa ajili ya kusimamia taratibu za uwanja.

2. Kimsingi waliozuia Simba isiingie uwanjani ni walinzi wa uwanja, hata kama kulikuwa na washabiki wanao dhaniwa ni wa Yanga maeneo ya uwanjani....

3. Tusiaminishwe kuwa washabiki wachache tu ndio wenye nguvu ya kufanya kazi ya ulinzi wa uwanja kuliko wafanyakazi/walinzi wa uwanja walio ajiriwa.....tukiamini hivyo kuna siku team zitazuiwa kwenda uwanjani ili team nyingine ipate point tatu....

4. Mimi bado naamini team ya SIMBA ILIZUILIWA na walinzi wa uwanja kwa kutokufuata taratibu (kwenda uwanjani jioni/usiku bila taarifa) hayo ya mashabiki wa Yanga yamejazilishiwa tu.....

Kimsingi sababu zilikuwa Nyepesi ukiangalia gharama za maandalizi na washabiki ambao wengi tu walisafiri kutoka mikoani na Nnje ya Nchi. Inamaana mechi za Yanga na simba wanaenda kuzipunguzia ushabiki (fedha) kwani hakuna mtu ataliipa hela yake kwenda dar wakati kwa sababu nyepesi nyepesi mechi inaweza kuaharishwa!
Haya madini sana kama TFF na BODI wapo humu huu uzi wa usome kwa makini sana.
 
Shida pale simba mangungu anapelekwa pelekwa sana na kina magori na jaribu tena
 
Usilete matusi Yako hapa,
Nimeamka nimepitia Mitandao yangu pendwa miwili X formerly known as Twitter na JF.

Nilichokiona hata waliokua wanatetea swala la Simba mapema Ile wamegeuka nao saiv wanailaumu Bodi.
Kwa ufupi bodi ya ligi wameingia kwenye mtego ambao nilisema utakuja kuwagharimu maana washakosa meno ya kuihukumu timu nyingine yoyote endapo itatokea scenario kama hii Tena,,wameshindwa kusimama na Sheria na kanuni walizojiwekea wao wameingia kwenye siasa za Mpira wa Tanzania
 
Point 3 lazima watoe na magoli matatu.
Mana timu ilipelekwa uwanjani walikua wanasubiriwa wao tu waahirishaji hio ni zaidi ya evidence
 
Back
Top Bottom