Kenya Election 2007: Outcomes

Kenya Election 2007: Outcomes

Lakini Museveni Na Kagame Ni Wauaji Wakubwa Pia Nao Wamepitia Udsm Kwanini Nao Wasiwajibishwe ?
 
Naam ni aibu iliyoje kwa wasomi wa UDSM au vyama vya upinzani kutoandamana na kukemea ukiukwaji wa demokrasia na mauji ya wananchi wasio kuwa na hatia nchini Kenya.Tuko katika zama za uwazi na ukweli na hivyo vyama vya upinzani na wasomi ni lazima wawe mstari wa mbele kukemea,kufichua,kupinga na kuwakomboa wananchi ambao wengi wao hawana mtu wa kuwasaidia.
Hivyo basi mimi nawaunga mkono wasomi hao wa UDSM kutumia ujuzi wao wa kisheria,hekima na maono yao katika kukemea ufisadi,uvunjaji wa haki za binadamu,mauaji ya raia wasio na hatia, na ukiukwaji wa demokrasia nchini Kenya kwa kufanya maandamano yao Jumamosi ijayo.

Ni lazima waelewe kuwa serikali ya CCM haipendi uozo huo ufunuliwe na ndiyo maana imekaa kimya kama bakuli la maji! pia cha kushangaza kuna watu hadi hapa JF ambao kwa sababu wanazozijua nao wamechukua msimamo huo huo wa serikali ya CCM kushabikia na kuwanyima haki watanzania kufanya maaandamano ya amani kupinga umwagaji damu na maonezi wanayofanyiwa watu wa Kenya.Ni lazima tuelewe kuwa maisha ni haki ya kila mtu na hakuna mtu au chama au kabila linaloweza kunyima mtu kuishi.Hivyo basi tumeona mauaji yametokea nchini Kenya na hakuna hata sehemu moja inayosema kuwa wapinzani wa Kenya ndiyo waliwauwa wananchi hao.Hivyo suala la kuandamana kwa watanzania wakiwemo wasomi wa UDSM ni suala la muhimu katika kuonyesha msimamo wao katika kutetea haki za wanyonge popote pale duniani ikiwemo Kenya.
Hivyo wale wote ambao wamechukua ile propaganda ya serikali ya CCM na polisi wake ya kuwa maandamano ya amani ni ya kumpa support Raila na hivyo kupendelea upande mmoja wasutwe kwa sauti ya juu na fikra zao wenyewe kwa kuwa wameshindwa si tu kukemea maovu na udhalimu bali wanahalalisha mambo haya kutokea tena katika sehemu nyingine Afrika.
Afrika kama bara tumechoshwa na michezo hii ya ubabe ubabe.Waasisi wetu walisimama kidete kupigania haki,usawa na kukemea maovu ambayo watu wetu walikuwa wanafanyiwa na wakoloni, leo hii kuna baadhi miongoni mwetu wanajikweza na kujifanya wao ndiyo wakoloni wa kipindi cha sasa huku wakitumia nguvu za dola na mahakama kukandamiza na kuuwa wananchi wanyonge! na chakushangaza ni pale wale wanaoamua kukemea mambo hayo kwa kufanya maandamano wanaponyimwa haki hiyo na baadhi yetu tunashabikia uamuzi huo wakiwemo wachache hapa JF.Hii siyo sawa na si haki na kama mambo haya yakiendelea basi inabidi tufikirie njia mbadala kama aliyotumia samora machelli na vikundi vingine vya ukombozi katika kutafuta haki.
Na kwa kuanzia hapa hapa JF tuwapinge kwa sauti zote wale wanaondeleza propaganda za CCM na serikali yake katika kuwanyima wananchi haki zao za msingi.

-Wembe

Wapinzani wazimwa Dar




na Happiness Katabazi



JESHI la Polisi jana lilifanikiwa kuzima maandamano yaliyokuwa yawashirikishe wafuasi wa vyama vinne vya upinzani vyenye ushirikiano wa kuunga mkono madai ya kambi ya upinzani nchini Kenya ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Desemba 27.
Tangu saa 12 asubuhi, wakiwa na silaha nzito pamoja na mabomu, polisi walianza kutanda katika vitongoji vya Manzese, Urafiki na eneo la Mahakama ya Ndizi, maeneo ambayo wapinzani walipanga kupita katika maandamano yao.

Wakati polisi wakiwa wametanda katika maeneo hayo, wanachana na wafuasi wa vyama hivyo walianza kuwasili katika maeneo hayo majira ya saa mbili, lakini walipowaona askari walijificha katika nyumba za wakazi wa eneo hilo wakisubiri amri kutoka kwa viongozi wao.

Ilipofika majira saa nne, mmoja wa viongozi wa upinzani aliyesisitiza kuwapo kwa maandamano hayo, Chacha Wangwe alianza kuwasiliana na waandishi wa habari kupitia simu yake ya kiganjani akieleza kuwa yeye pamoja na wafuasi wa upinzani wapatao 100, wako mafichoni eneo hilo, wakipanga mikakati ya kukabiliana na polisi waliokuwa wametanda eneo hilo.

Wangwe alikataa kutaja eneo alilokuwa amejificha pamoja na wafuasi wake kwa kile alichodai kuwa sababu za kiusalama, lakini alisisitiza kuwa wanajiandaa kuvamia eneo hilo ghafla kama mvua.

Baadaye Wangwe aliwasiliana tena na waandishi na kuwaeleza kuwa kutokana na udhibiti wa polisi katika eneo hilo, wamebadilisha sehemu ya kuanzia maandamano hayo na kuwataka waandishi wakashuhudie wanavyoibuka wakitokea eneo la Tandale Uzuri Darajani.

Waandishi waliwahi katika eneo hilo lakini hadi saa saba mchana, waandamanaji hao hawakuwa wamejitokeza katika eneo hilo huku polisi wakiendelea na doria kali.

Wangwe aliwasiliana tena na waandishi wa habari na kuwataka waondoke eneo hilo kwa sababu nalo halikuwa salama, warudi Manzese. Muda mfupi baadaye alipiga tena simu na kueleza kuwa amepata wazo jipya na kuwataka waende eneo la Mkwajuni, Masai Pub ambako alisema angelipua bomu.

Baada ya waandishi wa habari kufika eneo hilo walipokewa na mtu ambaye hawakumfahamu mara moja, aliyewaelekeza waende karibu na msikiti uliokuwa eneo hilo ambako walizungushwa hadi nyumba ambayo haikufahamika pia mmiliki wake ni nani, wakakalishwa chini ya mti.

Wangwe aliungana na waandishi hao dakika chache baadaye na kukiri kuwa wapinzani wameshindwa kuandamana kutokana na nguvu kubwa iliyotumiwa na serikali kuzuia maandamano yao.

Alidai kuwa licha na maandamano hayo kutofanyika, serikali inapaswa itambue kuwa wapinzani wanajua kuwa Serikali ya Tanzania ilishiriki kuiba kura katika uchaguzi wa Kenya uliofanyika hivi karibuni.

Huku akiongea kwa wasiwasi, Wangwe alidai anao ushahidi kuwa Serikali ya Tanzania ilishiriki katika hujuma zilizofanyika kwenye uchaguzi mkuu wa Kenya, kutokana na ziara ya bingwa wa propaganda wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kingunge Ngombale- Mwiru, nchini Kenya wakati wa uchaguzi huo.

“Serikali yetu kupitia Kingunge imeshiriki kuiba kura za Wakenya na ndiyo maana hadi sasa haijatoa tamko la kulaani yanayotokea kwa jirani zetu, kwani nayo ni miongoni mwa walioshiriki kuharibu uchaguzi ule, na ndiyo maana leo (jana) wametumia nguvu kubwa ya dola kutuzuia sisi tusiandamane.” alisema Wakati akiendelea kueleza hayo, askari wawili wa upelelezi walipita eneo hilo na mara Wangwe alipowaona alinyamaza ghafla na kuwataka waandishi wakutane naye Masai Pub, hatua chache kutoka alipokuwa akizungumzia.

Baada ya kuyasema hayo aliondoka haraka eneo hilo akitumia gari aina ya Toyota Corolla lenye namba za usajili T 865 AMR, na haikueleweka alielekea wapi baada ya waandishi kumkosa Masai Pub.

Baadaye ilielezwa kuwa Wangwe alikuwa amekimbilia makao makuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) huko Kinondoni na waandishi walipofika eneo hilo walimkuta na alieleza kuwa alikuwa akiwasubiri waandamanaji waliokuwa na mabango ili maandamano yaanzie hapo.

Dakika chache baadaye aliwaita waandishi wa habari ndani ya ofisi za CHADEMA na kuwaambia kuwa maandamano hayo yamesitishwa lakini yatafanyika siku nyingine kwa nchi nzima, hata hivyo hakutaja siku ya kufanyika maandamano hayo.

Naye Mkuu wa Idara ya Habari wa CHADEMA, Erasto Tumbo, alitaka Kenya itolewe kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki iwapo Rais Kibaki hatajiuzulu, kwa vile ameingia madarakani kwa wizi wa kura.

Kwa ujumla mwenendo mzima wa pilika pilika hizo za jana ambazo zilikuwa kama sinema, zilivuta hisia za watu wengi huku baadhi ya wafanyabiashara wa eneo la Manzese wakiogopa kufanya shughuli zao.

Polisi waliokuwa wakiwafuata waandishi hatua kwa hatua, walisikika wakieleza kuwa iwapo kuna mpinzani atakayeonekana anaandamana barabarani, basi kila hatua yake moja itafuatia rungu la polisi moja.

Baadhi ya wafuasi wa upinzani nao walidai kuwa walichokuwa wakikifanya jana ni kulitikisa na kulihangaisha Jeshi la Polisi ili liendelee kufanya doria siku nzima ya jana chini ya Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Kinondoni, Damas Kasabi.

Nako katika ofisi za Ubalozi wa Kenya zilizo Mtaa wa Mafinga, Kinondoni na katika baadhi ya mitaa ya Jiji la Dar es Salaam, hali ya ulinzi iliimarishwa, huku magari ya polisi ya kurusha maji kwa ajili ya kuwatawanya waandamanaji yakiwa yameegeshwa Kituo cha Polisi Magomeni na Urafiki, yakiwa tayari kuwakabili waandamanaji.

Maandamano hayo yalipigwa marufuku juzi na Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Alfred Tibaigana, kwa maelezo kuwa hali ya usalama hapa nchini kwa sasa si shwari.
 
Hata ODM hakina muda mrefu tangu kuanzaishwa,hiyo siyo issue,swali ni jinsi usanii wa kijinga unaofanywa na viongozi wetu wa Africa
 
The Law Society of Kenya accused electoral officials of "dishonesty and ineptitude", called Kibaki's swearing-in "null and void", and urged a fresh vote.

"Honorable Kibaki lacks legitimacy to govern and this is the cause of the problems that we are facing as a country."
 
May I respond to some people collectively..

Hivi unakumbuka kilichotokea kwenye uchaguzi wa Marekani mwaka 2000 ambapo George Bush alitangazwa Mshindi? Unakumbuka yaliyotokea Florida ya "hanging chad" na wadogo zake. Unajua jinsi gani Supreme Court ya Florida ilivyojaribu "kisheria" kumpa ushindi Gore ambapo baadaye wakawa thwarted na US Supreme Court ambayo nayo ikimpa ushindi George Bush. Unakumbuka Jaji Mkuu Rehnquist baadaye alijuta kwa Mahakama yake kuchukua kesi hiyo?

JAMANI HUYU JAMAA VIPI YANI WEWE UNA HALALISHA WIZI????? NAKUSHANGAA, HATA UANDIKE PAGE KUMI ZA KUTUELEWESHA LAKINI YOU CANT CONVINCE US.

WHAT DO YOU WANT MY DAUGHTER AND SON TO LEARN FROM THIS????? YOU CAN STEAL AND STILL GET AWAY WITH IT. WEWE UNATOA MFANO WA USA, IT REALLY HAS COST MANY LIFES BY BUSH BEING IN POWER WATU WAMEKUFA KWA AGILI THE DECISION HE MADE WHEN INVADING IRAQ, HATA UKIANGALIA UONGOZI WAKE ULIKUWA WA UWONGO UWONGO, HE WENT TO IRAQ UNDER THE PRETEXT OF FINDING WEAPON OF MASS DESTRUCTION NA HAZIKUWEPO ALIWADANGANYA KAMA ALIVYOIBA KURA. WEWE UNATAKA TUWE HIVYO? AND BY THE WAY USA IS NOT EVEN A GOOD EXAMPLE BECAUSE HAWAFUATI HATA MAELEKEZO YA UN, THEY USE DEMOCRACY WHEN IT SUITS THEM.

USA GOT OVER THAT BECAUSE IT IS A MATURE DEMOCRATIC COUNTRY, LAKINI KENYA IS AN INFANT DEMOCRATIC COUNTRY.
WEWE UNATAKA AMANI KWA NDIA YOYOTE WITHOUT DIGNITY.
 
Lakini Museveni Na Kagame Ni Wauaji Wakubwa Pia Nao Wamepitia Udsm Kwanini Nao Wasiwajibishwe ?

Nadhani kuwa Kagame hakufika chuo kikuu chochote; elimu yake ya juu iliyowahi kuripotiwa na vyombo vingi vya habari ni ya sekondari, kwa hiyo nina mashaka kama kweli naye kapitia UDSM.
 
The Law Society of Kenya accused electoral officials of "dishonesty and ineptitude", called Kibaki's swearing-in "null and void", and urged a fresh vote.

"Honorable Kibaki lacks legitimacy to govern and this is the cause of the problems that we are facing as a country."

Hivi ile kesi wameshaifungua tayari? Naona internal reporter/analyst wetu KT naye kapotea kidogo.
 
Wakuu,

Hivi niwaulizeni, kwa maoni ya kibinafsi, Mh. Jakaya Kikwete na Tanzania kwa jumla inawezasaidia vipi kwenye kutafuta suluhisho la kudumu kwenye crisis ya kisiasa iliopo Kenya kwa sasa?

Najua Mwalimu angekuwepo hai na mamlakani hangesita kujiuliza swala hili.
 
Kuandika kwa herufi kubwa ina maana "unapiga kelele". Sasa hoja yako haiwezi kuwa na nguvu kwa sababu unapiga kelele. Hoja inakuwa na nguvu kutokana na kilichosema na misingi ya hoja hizo.

[SIZE="3 JAMANI HUYU JAMAA VIPI YANI WEWE UNA HALALISHA WIZI????? NAKUSHANGAA, HATA UANDIKE PAGE KUMI ZA KUTUELEWESHA LAKINI YOU CANT CONVINCE US.

Sasa mtu mbishi atakuwa mbishi hata kama ukweli unamdolea macho. Unaweza kumwambia mtu "kuna mfereji hapo ruka" yeye kwa vile ni mbishi anageuka na kusema "nani wewe kuniambia kuna mfereji" halafu akianguka na kutumbukia anageuka na kuuliza "kwanini hukuniambia kuna mfereji"! Mbishi hashawishiki!


WHAT DO YOU WANT MY DAUGHTER AND SON TO LEARN FROM THIS????? YOU CAN STEAL AND STILL GET AWAY WITH IT.

Uangalie mtu kasema nini kuliko kuamua kumuwekea mtu maneno kinywani!

WEWE UNATOA MFANO WA USA, IT REALLY HAS COST MANY LIFES BY BUSH BEING IN POWER WATU WAMEKUFA KWA AGILI THE DECISION HE MADE WHEN INVADING IRAQ, HATA UKIANGALIA UONGOZI WAKE ULIKUWA WA UWONGO UWONGO, HE WENT TO IRAQ UNDER THE PRETEXT OF FINDING WEAPON OF MASS DESTRUCTION NA HAZIKUWEPO ALIWADANGANYA KAMA ALIVYOIBA KURA. WEWE UNATAKA TUWE HIVYO? AND BY THE WAY USA IS NOT EVEN A GOOD EXAMPLE BECAUSE HAWAFUATI HATA MAELEKEZO YA UN, THEY USE DEMOCRACY WHEN IT SUITS THEM.

and...

[/quote]USA GOT OVER THAT BECAUSE IT IS A MATURE DEMOCRATIC COUNTRY, LAKINI KENYA IS AN INFANT DEMOCRATIC COUNTRY.
WEWE UNATAKA AMANI KWA NDIA YOYOTE WITHOUT DIGNITY.
[/SIZE][/QUOTE]

yaani watu zaidi ya mia tatu wameuawa kwa sababu ya "intant democracy"? Ndiyo maana nimesema wote hawa Kibaki na Raila wana damu ya watu mikononi kwa namna moja au nyingine na hawastahili kuiongoza Kenya. Kama wameshindwa kuongoza demokrasia changa namna hii basi washindwe na kulegea!
 
Na huyu odinga yuko dar es salaam sasa hivi kwa mazungumzo na baadhi ya viongozi wa tanzania wakati mkapa ameelekea kenya kusulugisha mambo
 
Wakuu,

Hivi niwaulizeni, kwa maoni ya kibinafsi, Mh. Jakaya Kikwete na Tanzania kwa jumla inawezasaidia vipi kwenye kutafuta suluhisho la kudumu kwenye crisis ya kisiasa iliopo Kenya kwa sasa?

Najua Mwalimu angekuwepo hai na mamlakani hangesita kujiuliza swala hili.

K-T

Tatizo la Kikwete na serikali ya Tanzania kwa sasa hivi ni kuwa wako kama wanaishi kwenye nyumba ya vioo. Kwa namna moja ama nyingine walishafanya kama yale aliyofanya Kibaka. Kukosekana kwa moral integrity baina ya viongozi wetu ni jambo linalowakosesha authority kwa kiasi kikubwa sana kaitika kushugulikia mambo mbalimbali.

Jambo ambalo Kikwete (na Museveni pia) angeweza kulifanya ni kumpa moyo bwana Kibaki kuwa awe statesman zaidi na kukubali uchaguzi urudiwe kwa vile hiyo ndiyo njia pekee inayoelekea kuondoa tension iliyozuka hapo Kenya. Endapo anaona uwezekano wa kushindwa uchaguzi ukirudiwa na hivyo kufedheheshwa, basi asigombee tena kusudi apewe heshima ya kuwa rais mstaafu; tena kwa sasa hivi ana kisingizio kizuri sana cha kutogombea.
 
K-T

Tatizo la Kikwete na serikali ya Tanzania kwa sasa hivi ni kuwa wako kama wanaishi kwenye nyumba ya vioo. Kwa namna moja ama nyingine walishafanya kama yale aliyofanya Kibaka. Kukosekana kwa moral integrity baina ya viongozi wetu ni jambo linalowakosesha authority kwa kiasi kikubwa sana kaitika kushugulikia mambo mbalimbali.

Jambo ambalo Kikwete (na Museveni pia) angeweza kulifanya ni kumpa moyo bwana Kibaki kuwa awe statesman zaidi na kukubali uchaguzi urudiwe kwa vile hiyo ndiyo njia pekee inayoelekea kuondoa tension iliyozuka hapo Kenya. Endapo anaona uwezekano wa kushindwa uchaguzi ukirudiwa na hivyo kufedheheshwa, basi asigombee tena kusudi apewe heshima ya kuwa rais mstaafu; tena kwa sasa hivi ana kisingizio kizuri sana cha kutogombea.

Asante Kichuguu,

Inatia moyo sana kusoma maneno kama haya. Agents wa Kikwete kama wakifungua minds zao na kumfikishia JK huu ujumbe natumaini naye anaweza kufanya kitu kizuri. Tatizo dhamira inamsuta hata yeye.

Uchaguzi wa 2005 ulishuhudia mbinu mbali mbali zikitumika kuhakikisha kuwa upinzani unapata viti vichache (labda vya pemba pekee) katika bunge na kikwete anapata kura nyingi sana (show off) chini ya mbinu hatari za mzee malecela. Nani ana moral authority ya kusimama against Kibaki?
 
Kichuguu, pointi nzito. Ukweli ni kuwa ni kuwa Kibaki anaweza kuendelea kuwa Rais na kuonesha kutokujali maslahi ya Taifa lake. Kama yeye ni mtu wa haki basi njia pekee ni kuamua kujiuzulu mara moja na kufuata taratibu za Kikatiba za kupokezana Urais.

a. Sijui makamu wa Rais wa Kenya anachaguliwa at the same time na Rais na hivyo Rais akishindwa basi anachukua Urais?

b. Kama sivyo basi lazima kuwe na utaratibu wa kubadilisha madaraka kuliko kuiacha nchi kwenye vacuum. Wazo la caretaker government silioni kikatiba au kisheria. Labda ndugu zetu wa Kenya wanaweza kutusaidia, Kibaki akijiuzulu nani Kikatiba anaweza kuchukua nafasi yake?

c. Tatizo jingine ni kuwa kina Raila hawataki mtu mwingine kuchukua Urais badala ya Kibaki kwenye chain of succession bali wanataka uchaguzi mzima urudiwe. Je, Sheria ya Kenya inatoa nafasi ya uchaguzi kurudiwa kutokana na election irregularities...?
 




images



Where Our Land Once Stood…



It
stood here upon these hills
what yesterday, was our land.
On these slopes we stand today
Stood that which you and I,
Side by side
Brought burning down
By our endless
Furious ethnic
Fists and blows



Now
grey smokes of sadness
spiral off these ruins,
where piles of your crushed bones
And mine,
Forever sleep side by side
next to the river of blood
in this vast valley of skulls…
Wild winds of regret
Whistle here
And whistle there…
Spreading the sad news of
Of our fallen hopes
And burnt homes
To shocked homes
Across the whole globe…



The soothsayers'll say
in folklore of years to come,
You and I
Failed to abide by the Law
choosing instead blow upon blow
smashing our past, present and tomorrow
until all that remained was only sorrow...



Sadly
Then
as now...
Our ghosts
Will stand side by side
upon these ruins
Of our failed State
and hear them tell
And retell with regrets...
The teary tale
Of how you and I
Blinded by ethnic hate
Sealed our national fate
By killing the State.





By Kenyan-Tanzanian



 
Wakuu,

Hivi niwaulizeni, kwa maoni ya kibinafsi, Mh. Jakaya Kikwete na Tanzania kwa jumla inawezasaidia vipi kwenye kutafuta suluhisho la kudumu kwenye crisis ya kisiasa iliopo Kenya kwa sasa?

Najua Mwalimu angekuwepo hai na mamlakani hangesita kujiuliza swala hili.

Kikwete anaweza tu kama akimweleza Kibaki kwamba kama akikataa kujiuzulu, Tanzania itamtenga katika EAC na haitamtambua! Na kwamba Tanzania itakwenda mbele zaidi kutumia nafasi yake kushawishi nchi zingine duniani nazo zisimtenge. Kibaka akimuuliza Kikwete mbona na wewe uliiba Zanzibar, Kikwete atamjibu mimi sikukamatwa ready handed. Wewe umekamatwa mchana kweupe. Tatizo ni M7 ambaye ameshamtambua Kibaka na ndiye mwenyekiti wa EAC. Leo alikuwa na fursa ya kubadili msimamo wake kama walivyofanya Marekani lakini ameendelea kusisitiza kumtambua kwa kuwa tu "Kivuitu alimtambua". M7 anashindwa kujua kuwa Kivuitu tayari ameshampa pa kutokea kwa kusema kwamba hata yeye hajui kama Kibaka alishinda. Tatizo kuwa ni kubwa ni kuwa M7 alishiriki moja kwa moja kuiba kura kuliko Kikwete hapo Kenya. Anakazi ya kulinda na kutetea uwizi alioshiriki. ODM endeleeni kumbana Kibaka kwenye kona, mpaka akimbie mwenyewe. Nawapongeza kwa kufuta maandamano ya kesho, lakini jamaa asipokubali tu kuitishia uchaguzi mwingine rudisheni tena orange movement! Mapinduzi ya machungwa yamtoe kibaka, tena safari hii apondwe na machungwa mabovu na wanawake kila ziara atakayofanya popote. Ni aibu kutawaliwa na kibaka aliyekamatwa hadharani.

Asha
 
1. Bunge la 10 la Kenya litaapishwa tarehe 15 Januari, 2008 yaan Jumanne wiki ijayo.

2. Rais Kufuor aingia Nairobi kesho kuanza mediation talks.

3. Kibaki ajaribu kumualika Raila ikulu waonngee ana kwa ana. Raila amekataa akisema kwamba hii ni njama ya kujaribu kuinfluence jamii ya kimataifa na wasuluhishi kama kina AU. Amesema atakutana na PNU only wakati wapatanishi watakapofika nakuanza kazi yao.

4. Law Society of Kenya (LSK) imesoma ripoti za ECK na imesemea kulingana na sheria za Kenya:
a) Wamemfuta Kivuitu toka kwenye Roll of Honors or rejista ya mawakili na wanasheria
b) Kibaki is in State-House illegaly and he is technically not the President of Kenya for being sworn in illegally
c) AG and Cj waliomuapisha Kibaki wajiuzulu na washtakiwe mbele ya mahakama. Mkuu wa polisi vile vile.
d) ECK na mkuu wao Kivuitu wafutiliwe mbali mara moja na kufunguliwa mashtaka.
d). Uchaguzi mwengine ufanywe mara moja lakini uwe tu wa Urais kwajili ule wa Ubunge hauna utata.
e). Jendayi Fraser, naibu wa Condoleeza Rice asema kwamba Kibaki na Raila wote wako ready kwa talks lakini wana masharti makubwa kila mmoja.
f) British Foreign Secretary awaambia House of Commons/Parliament kwamba power-sharing eti ndio the only way forward.
g) Alisema all the allegations of fraud in the elections should be investigated and the criminals brought to justice.
h) Kufikia sasa watu 486 wamefariki, 250,000 wameachwa bila makao.
i) Kenyans abroad esp in US, Germany and UK wafanya maandamano wakiitisha kujiuzulu kwa Mr Mwai Kibaki mara moja.
j) Kibaki aingia woga marais wa Afrika wanamsusa na atuma Uhuru kwa JK kujaribu kuomba sapot. JK akataa. Tunashukuru kwa hilo. Mungu ibarike Tanzania.
k). The only peaceful solution is for Mr. Kibaki to resign immediately. (Nafahamu kuna walouliza maswali kuhusu hili. Ntarejea na hili kwa post nyingine baada ya kupata cha jioni.)
 
Back
Top Bottom