Kenya: Godbless Lema aachiwa kutoka kituo cha Polisi Kajiado. Apatiwa hifadhi nchini Kenya

Kenya: Godbless Lema aachiwa kutoka kituo cha Polisi Kajiado. Apatiwa hifadhi nchini Kenya

Makasiriko ya jitu juu ya Kenya na Kenyatta yatazidi maradufu! Wakati ule alichoma vifaranga sijui atachoma nini safari hii.
Mungu akulinde Lema pamoja na familia yako.
Najikuta nacheka at the same time nasikitika.
Yani huyu mzee huwa akili zake sijui zikoje
Ni Mtu wa chuki na visasi..
 
Suala la Kambona lilikuwa uhaini, sio maoni tofauti ya siasa
Uwongo mtupu! Kambona hakuwa na uhaini wowote, rudi kwenye historia za nchi ukajifunze sawaswa, acha kuropoka ropoka. Kwa taarifa yako Nyerere mwenyewe alimruhusu kuondoka kwa kuwa hakuwa tayari kukubaliana na siasa ya Ujamaa Na Kujitegemea.
Sasa huo uhaini ni ndoto zako unatuletea au ni facts za kilevi?
 
Maigizo hayo natizama BBC Swahili sasa hivi anasema ataka kipindi kifupi alafu atarudi Tanzania,yeye si aseme tu anaenda kwa ajili ya likizo ya Christmas na Mwaka mpya.
 
Uchaguzi ukikaribia watarudi tena kugombea.
 
haya yasikie tu kwa mwenzio. mimi na wewe hatujui anajua yeye, Mungu wake na wanaomtishia. tusihukumu. Fikiria pia,wakati Lema "anajifanya" kutaka kuuliwa kuna makumi wameshakufa Zanzibar. huko Tarime kuna makumi wanauguza majeraha makubwa.

Kama hakuna uhakika na usalama wa Maisha Yao afadhali wakimbie, na hicho chama watakikuzaje wakati manyanyaso kutoka kwa polisi ni Kila kukicha? Wakifanya vikao vya ndani ni shida nje Nako hakuna ruksa
Hasa si waseme tu kwamba tunataka kufanyanyia siasa zetu uhamishoni kwa michango ya wafuasi wetu.
 
Nyie ccm mambo ya ukweli mnatia mzaha. Imagine maandamano ya amani mtu unafungwa, halafu unaanza kutumiwa msg ya kijinga
Lema ni chalii wa Arusha hawezi kutishwa na msg akimbie Nchi, ni mchongo tu na Kenya yeye siyo mgeni.
 
Hii tactic ya kujifanya wanataka kuuliwa badala ya kubaki na kukuza chama chao ni usaliti kwa wafuasi wao.
Mkuu, labda wewe unaelewa sana. Hebu nieleweshe, chama chao wanakuzaje?
Mikutano ya kisiasa mlishawazuia,
Wakifanya mikutano ya ndani, mnawakamata,
Wakiitisha press conference mnawakamata
Wakishiriki uchaguzi, mnaiba kura, mnalazimisha matokeo, mnajipa ushindi, mnajipa ulinzi
Wakiitisha maandamano mnawakamata, mnawapiga risasa, mnaua wafuasi wao.
Wakiwakosoa mnawatafuta muwapige risasi.
Hebu nifundishe mkuu, wanajengaje vyama vyao?
 
Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Kaskazini na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mhe. Godblessema ameachiwa muda huu baada ya kukamatwa na polisi Kenya hapo jana.
=======

Mbunge wa zamani wa Arusha Mjini, Godbless Lema aliyekimbia Tanzania na familia yake kuelekea Kenya na kukamatwa na Mamlaka za huko aameachiwa na Polisi katika Kituo cha Kajiado na kupewa hifadhi nchini humo.

Hifadhi ya Lema inakuja wakati Mbunge mwingine wa zamani na Waziri wa Utalii, Lazaro Nyalandu kuzuiliwa na Mamlaka za Tanzania wakati anaelekea Kenya

Pia, soma Amnesty International yaitaka Kenya kumpa hifadhi Godbless Lema kulingana na sheria ya wakimbizi, yasema kumrudisha nchini ni kinyume cha sheria



Kwakweli Dunia tambala bovu
 
Sisi wafuasi tunawaunga mkono so hayo ni ya kwako wewe kada!

Mkuu, labda wewe unaelewa sana. Hebu nieleweshe, chama chao wanakuzaje?
Mikutano ya kisiasa mlishawazuia,
Wakifanya mikutano ya ndani, mnawakamata,
Wakiitisha press conference mnawakamata
Wakishiriki uchaguzi, mnaiba kura, mnalazimisha matokeo, mnajipa ushindi, mnajipa ulinzi
Wakiitisha maandamano mnawakamata, mnawapiga risasa, mnaua wafuasi wao.
Wakiwakosoa mnawatafuta muwapige risasi.
Hebu nifundishe mkuu, wanajengaje vyama vyao?
Waache njaa na siasa za ruzuku,wabaki nyumbani kupigania katiba ambayo wanadai ndiyo inayotumika kuwakandamiza.
 
Uwongo mtupu! Kambona hakuwa na uhaini wowote, rudi kwenye historia za nchi ukajifunze sawaswa, acha kuropoka ropoka. Kwa taarifa yako Nyerere mwenyewe alimruhusu kuondoka kwa kuwa hakuwa tayari kukubaliana na siasa ya Ujamaa Na Kujitegemea.
Sasa huo uhaini ni ndoto zako unatuletea au ni facts za kilevi?
Sasa wewe ndio unapasa kusoma historia ujue kilichofanya Kambona kukimbia katika lile genge la Kambona, Chipaka, Kamaliza, Bibi Titi nk. Sintashangaa kama ulikuwa hata hujazaliwa halafu unajifanya fyokofyoko kusemea puani hapa. Kama Nyerere alimruhusu kuondoka kwa nini Kambona aliogopa kurudi wakati Nyerere yupo madarakani? Kwa nini kina Bibi Titi, Chipaka, Kamaliza wakawekwa ndani? Kwa nini alikimbia akaacha familia nyuma? Kwa Kambona atungiwe nyimbo jeshini? Suala la Kambona kwenda Uingereza lilihusiana na mpango wa kumpindua Nyerere, sio kupishana maoni kati ya ujamaa na ubepari kitu ambacho ndio kililetea watake kumpindua yeye na genge lake. Wenzio hata tuliimba jeshini

Kambona aliagiza hiyoo
Chipaka na Kamaliza
Inueni mkiweza
Nitawalipa mapesa
Nirudipo safarini Uingereza
 
Hii tactic ya kujifanya wanataka kuuliwa badala ya kubaki na kukuza chama chao ni usaliti kwa wafuasi wao.

It's not a "political tactic" as you think, but it's a real threat..

And if you don't take it seriously and take proper measures to save your own life, death is inevitable..

The devil never makes a joke with human beings. He is thief and murderer. Whoever stands on his way, he/she is swallowed..

CCM and Magufuli administration are the devils we are talking about here...!!
 
It's not a "political tactic" as you think, but it's a real threat..

And if you don't take it seriously and take proper measures to save your own life, death is inevitable..

The devil never makes a joke with human beings. He is thief and murderer. Whoever stands on his way, he/she is swallowed..

CCM and Magufuli administration are the devils we are talking about here...!!
🤣😂🤣😂🤣😂 Hahahahaha UPUUUZI MWINGINE WA CHADEMA KWA HIYI LEMA AKIWA KENYA HATAKUFAA
 
Back
Top Bottom