Kero: Tabia ya ajabu Mbeya kuchangisha pesa za misiba imezidi mno

Kero: Tabia ya ajabu Mbeya kuchangisha pesa za misiba imezidi mno

Nakuunga mguu mia kwa mia! Hii tabia inakera sana pale Mbeya! Mwenyewe nimeishi Mby na nimeshuhudia ujinga huu sanaa! Hasa ile barabara ya Makunguru! Na fedha nyingi zinazochangishwa zinasimamiwa na vibaka, hadi wengine wanakuonyesha picha kumbe mtu alikufa miaka mitatu iliyopita au hata wanakurupua tu lipicha la mtu huko studio na kutembeza kuwa ni marehemu! Shenzi kabisa hawa!
Nimewahi kupita ile barabara ya kiwira pale soweto inayotokea makunguru nimefika sehemu kuna nyumba ina msiba kweli na hapo hapo kuna vijana wa msibani hapo barabarani wana picha ya marehemu wanatusimamisha wenye magari, kiukweli nilisikitika japo nlitoa buku, hata wakiandika jina haina maana, mimi mpita njia tu hivi hela inakofika huko watanijuaje.
 
Kweli home michango ni tatizo sio uongo unakuta wengine washazikwa wao wapo busy na mchango ili iweje mkuu upo sahihi na michango ifanywe kwa wahusika wenyewe sio kila mtu ahusike kwenye msiba usiomuhusu...
 
Mbeya sehemu gani?? Mama John??

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Tatizo tumeaminishwa na kuamini kuwa Mtu akifa lazima azikwe na watu wengi na hapo eti ndio msiba ukifana. Kumbe ukiangalia kwa upana zaidi ni kupoteza muda na rasilimali tuu, mtu unaweza kufa na kuzikwa hata na Kikundi cha watu kumi tuu na ikawa poa tuu..Sababu hata uzikwe na watu milioni 1 haufufuki.

Na hiyo michango binafsi huwa naona ni ya kinafiki tuu sababu mtu unakuta kaugua Mwaka mzima hata Unga hajawahi changiwa ila akifa ndio upendo unaanza kuonekana!
 
NDOMANA NLISHAWAHIGI KULA MICHANGO WALIYOCHANGISHANA WATU,WAKANIPA KAMA NIWAWEKE HAPO HAPO NKAJIPATIA NAULI NKAWAACHIA MANYOYAAA

ova
 
Usipochanga nini kinatokea mkuu??
Mkuu wengi tunapenda kuishi kijamii kuepukana na kero, basi tena tufenyeje, tunatoa ila kwa shingo upande, yani hata msiba siambiwi ulipo hadi niwaambie wao ila wanataka pesa
 
Usiwalaumu ndugu yang, hiyo tabia ya kuomba omba na kuchangishana kila wakati wameiga kutoka chadema. Kumbuka Mbeya ni moja ya ngome za chadema na wengi wanaishi kwa kufuata misingi na tabia za viongozi wa chama.
Mkuu waambie wakurudishie kichwa chako.Tunapoelekea utaanza kutembea kwenye soko la kijiji umevaa shumizi.😝😝😝😝
 
Mkuu wengi tunapenda kuishi kijamii kuepukana na kero, basi tena tufenyeje, tunatoa ila kwa shingo upande, yani hata msiba siambiwi ulipo hadi niwaambie wao ila wanataka pesa
Itakua vizuri kama utakua unatoa kwa kiasi mkuu. Kama unacho unatoa kama huna unawaambia biashara mbaya, kuliko kuendekeza kutoa tu kila wanapokuja.
Na pia kuna kuna kipindi apo mbeya kulikua na tabia ya omba omba kupita madukani vipi nado inaendelea!!?
 
Mara ya kwanza kufika mbeya jambo lililonishangaza ni PA za msiba barabarani utadhani harusi yaani!
 
Chadema imewekeza zaidi kwa vibaka, wanywa viloba, wanywa gongo, mateja nk. Na hayo makundi hapo juu wengi wao huwa hawapigi kura.
Ni huna akili au ushabiki?nimeuliza kama mbeya ni ngome ya chadema kama ulivyodai mbona alishinda Tulia!weka sawa akili yako au kama vipi insta kunakufaa zaidi kuliko huku.
 
Chadema imewekeza zaidi kwa vibaka, wanywa viloba, wanywa gongo, mateja nk. Na hayo makundi hapo juu wengi wao huwa hawapigi kura.
Ni huna akili au ushabiki?nimeuliza kama mbeya ni ngome ya chadema kama ulivyodai mbona alishinda Tulia!weka sawa akili yako au kama vipi insta kunakufaa zaidi kuliko huku.
 
Back
Top Bottom