Kero ya kuripoti kazini baada ya kupangiwa ajira na sekretarieti ya ajira, halafu unaambiwa urudi nyumbani mpaka upigiwe simu kuitwa!

Kijana ukimaliza probation yako ya miezi isiyopungua 9 ndio utaelewa kiasi fulani taratibu za kiserikali...
Nimekupa hints muhimu za kukuongoza otherwise fanya unavyotaka wewe kwa experience ya kukaa home na story za vijiweni...
 
Hapo Kwa mdada unataka uanze ugomvi na mkeo
 
Ajira zenyewe za Halmashauri 😂😅 mnakuja kutupigia kelele JF.. mnaelekezwa mnajifanya wajuaji haya kalaleni getini basi muone kama mtafanyiwa mnavyotaka nyie... Serikal ina taratibu zake hawawez kufanya kazi na kukupa stahiki za kiutumishi kwasabab umeenda tu na barua yako... Rudi kijijini kamalizie kupalilia alizet
 
Ukisoma Barua Ile ya kupangiwa Kituo inamtaka mwajiri afanye uhakiki Wa vyeti vyako Kwanza ndipo akupokee rasmi. Nadhani hicho ndo kinakula muda

Huu ni upuuzi pia linapokuja suala la uhakiki wa vyeti.

Kwa nini utumishi wanahamisha majukumu. Wao ndio wanaajiri, na michakato yote wasailiwa wanaaenda na vyeti halisi kila hatua ya usaili.

Inamaana gani tena kuendelea kudai vyeti halisi siku ya kwenda kuripoti.

Tujifunze namna ya kuhakiki taarifa za wajiriwa bila kuleta usumbufu.

Tuna watu wenye elimu lakini hawajaelimika kutumia elimu zao kurahisisha changamoto/taratibu.
 
Ndugu yangu Mstaafu;

1. Mimi sijapingana na wewe. Uko sawa kabisa na hicho inachofanya serikali ni kuonesha kuwa hawakujiandaa vyema. Na ishu hapo huwa ni fedha tu, hakuna kingine. Yaani unaajiri mtu, lakini fedha zinakuwa bado hazipo!!

2. Ishu siyo uvivu wa kusoma. Nimekusoma na kukielewa vyema kabisa

3. Mwishoni nilikushauri tu kuwa, weka andiko lako kwenye paragraphs.

Au nimefanya vibaya kukushauri hivyo ndugu Mstaafu?
 
Hilo kokoro linaloitwa serikali linakera sana . Hapo unatakiwa ulipowe nauli ya kwenda na kurudi na pesa ya kulala mpaka zoezi likamilike. Wewe na wategemezi wako Na pesa ya ya kusafirishIa mizigo yako
Muone hr au mkuu wa idara acha kulalamika jf
Adui mkubwa wa mtz ni uwoga
 
Mimi nina mfano wa vijana wawili.
Waliitwa kazini na kurudi.
Nlipongea nao kila mmoja anasema aliambiwa taratibu za mshahara zitachelewa hivyo either ajaze fomu ya ruhusa kurudi mpk atakapopigiwa au aendelee na kazi huku akisubiri taratibu za mshahara.
Mmoja aliitwa Baada ya miezi miwili, mwingine Baada ya km wiki tano na wote waliingiziwa mishahara yao yote walipofika tu
 
Hii nchi bado kuna ujinga ujinga mwingi sana usio na sababu.
 

Hii ni shida kubwa sana. Hebu tazama mfumo wa uombaji ajira kwa sasa ulivyo.

Hii inahitaji hata siku 3 kuhakiki taarifa za mwajirirwa.

Tunashida kubwa sana kama taifa.

Binafsi nachukia sana kushindwa kutumia teknolojia tena katika taasisi zetu wenyewe.

Necta, vyuo vya elimu ya juu, Nida hizi zote ni taasis za serikali.
Facts findings inakuchukuaje miezi.

Elimu zetu zitusaidie kufanya mambo kwa wepesi na kwa usahihi.
 
Kijana ukimaliza probation yako ya miezi isiyopungua 9 ndio utaelewa kiasi fulani taratibu za kiserikali...
Nimekupa hints muhimu za kukuongoza otherwise fanya unavyotaka wewe kwa experience ya kukaa home na story za vijiweni...
Taratibu za serikali nazijua sana!! Mimi ni mumishi wa umma mstaafu!! Niliajiriwa katika utumishi wa umma mwaka 1986 baada ya kuhitimu chuo kikuu cha Dar, na nimestaafu mwaka 2019!! Kinachofanyika sio taratibu za utumishi wa umma bali uhuni. Taratibu za utumishi wa umma zinaongozwa na Government standing orders toleo la 2009 na marekabisho yake ya mwaka 2011!! Huo utaratibu wa mtu kuripoti kazini kwa wito rasmi halafu unarudishwa nyumbani bila kuhudumiwa kwa lolote ni uhuni wa watu!! Naomba unukuu hapa waraka wowote rasmi wa serikali unaoelekeza hivyo!!
 
Mkuu hapana,Mimi nimelsaidia watu wengi sana nikiwa na mke wangu so worry not.Anayepata shida wa mkoani siyo wa mjini
Basi wako ni mwelewa Kuna mtu alikuwa wakusaidia mkewe alijua ni mdada anaenda kuharibu uko sasa sijui ndio uchawi na roho mbaya
 

Ukisharipoti ni ajira imekamilika. Hizo ni taratibu tu.
Ilipaswa kumpa hata barua kuwa ameripoti na sasa wanakamilisha taratibu nyingine arudi tarehe fulani.
 
Miongozo na taratibu zozote zinazopangwa ambazo hazizingatii Government standing orders toleo la 2009 na ,marekebisho yake ya mwaka 2011 ni batili!!
 
Serikali irekebishwe huu upumba.vu na usumbufu ndio maana umaskini hauishi hii kitu ya taratibu ingeweza kufanyika na Kila jambo kukamilika ndio mtu aitwe Sasa huu mlolongo mrefu wa Nini in the name eti taratibu na mtu anajiona yuko kazini huku hawezi ku solve changamoto mapema.
Pia ka watu vyeti vimetolewa na vyuo na vimehakikiwa Kwa mwanasheria huo usumbufu Huwa wanini Ina maana hamna coordination.
Ni huko serikalini jambo la siku moja waweza zungushwa miezi miwili kisingizio mara kiwe mfumo uko chini mara kile, ni mdada Sasa watu waanze kulipwa kulingana na huduma wanafanya uone ka itachukua mda
 
Jamaa unajua kulalamika unaandika gazette wewe unachembe chembe ya umbea
 
Unapofikiria una Kila kitu kuwa makini sana unaweza kupoteza Kila kitu ukahitaji msaada Kwa mtu ambaye hakuwa na kitu sasa hivi anacho na yeye.
 
Ingetakiwa akae hotelini siku zote hzo akisubiria
 
Tangazo la ajira likitoka maana yake ni kuwa: 1. Nafasi hizo ziko wazi. 2. Kibali cha ajira kimeshatolewa. 3. Pesa za kushughulikia mchakato huo wa kujaza nafasi hizo zipo. 4. Pesa za mishahara na malipo mengine yanayoambatana na ajira mpya zipo. Kama ndivyo kwa nini mchakato uchukuwe muda mrefu sana kiasi cha zaidi ya miezi sita hadi mwaka mzima?? Lazima kuna tatizo mahali fulani!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…