Kero ya Walimu msingi kudai michango mingi; ni makubaliano ya kikao feki cha wazazi feki

Kero ya Walimu msingi kudai michango mingi; ni makubaliano ya kikao feki cha wazazi feki

Hilo nilisikia juzi Waziri mkuu akilikemea shule za sekondari za umma kuchapa joining instruction zenye vifaa vingi sana zaidi ya 200k!

Mkuu nimefurahishwa na kichwa cha habari, lakini kwenye 'content' "umemumunya" maneno.

Kifupi michango ni ya gharama kubwa kuliko ada.

Halafu "vikao vya wazazi" nilishavihudhuria vina mamluki vipandikizi waliojipanga huwashindi hoja.

Hakuna cha wazazi hapo ni wazazi feki kama ulivyoandika kichwa chako cha habari.

Utashangaa hoja za rejareja za kijinga jinga zinazotolewa pale zinaungwa mkono 100%, wanakuwa wanejipanga haswa kwa manufaa binafsi.

Hakuna anayehoji matumizi ya hela ya shule inayoletwa mgao na serikali kwa elimu bila malipo na mchanganuo wake kuonesha zinafanya kazi gani.

Rim za karatasi pamoja na vikorombweso kibao ukiunga gharama zake vinazidi ada.

Marufuku ya michango iliyotolewa na serikali ya awamu ya 5 ingeliendelezwa kukomesha umumiani huu ulioibuka tena kama kweli serikali imeamua kulivalia njuga suala la kubeba gharama za kusomesha watoto.

"Mwenye kuguswa ama mkereketwa" apeleke mchango wake kwa Mkurugenzi kama ilivyokwisha kuagizwa, wanashindwa nini?

Hatukatai harambee za ujenzi wa madarasa kutokana na ongezeko la watoto lisilokuwa na kikomo, lakini double standard ya gharama zinazobebwa na serikali halafu wazazi wanageukiwa kuhamasishwa kuchangia gharama hizo hizo, tunasema hapana.
Umefafanua vyema sana
 
Shule nyingi za msingi za serikali siku hizi zimejaa michango mingi sana ambayo inaleta matabaka kwa watoto!

Walimu wanachangisha hela ya mitihani kila siku 1000.
Ndoo mpya kila term,
Fagio jipya kila mwezi,

Hela ya safari (tour) kwa mgongo wa hiari huku nyuma wanawapiga mkwara watoto kwenda!

Vitabu vidogodogo wanalazimishwa kununua n.k

Hii tabia ukihoji wanasema ni makubaliano ya kikao cha wazazi lakini ajabu kila mzazi analalamika! Sasa hiko kikao huwa wanakalia wapi?

Mambo haya yameshamili sana na maafisa elimu wapo, wakurugenzi wapo, DC na RC wapo, mawaziri wapo, tamisemi wapo, Yaani ni kero mtupu lakini kiiimyaaa!

Walimu wanachukua mikopo halafu wanarudi kulalamika mshahara hautoshi wanasahau mikopo ya anasa ndo tatizo!

Ugumu wa maisha wao kutwa kuchangisha michango isiyo na kichwa wala miguu kila siku!
Kwanza tuition za kulipia za nini kwenye shule za serikali?
Well said mkuu,,
Hayo mambo yapo Sana kwenye hizi shule zetu za serikali.

Halafu ukiuliza wanasema wazazi walikaa na kupanga yote hayo.

Kumbe wazazi fake na vikao fake ..
 
Shule nyingi za msingi za serikali siku hizi zimejaa michango mingi sana ambayo inaleta matabaka kwa watoto!

Walimu wanachangisha hela ya mitihani kila siku 1000.
Ndoo mpya kila term,
Fagio jipya kila mwezi,

Hela ya safari (tour) kwa mgongo wa hiari huku nyuma wanawapiga mkwara watoto kwenda!

Vitabu vidogodogo wanalazimishwa kununua n.k

Hii tabia ukihoji wanasema ni makubaliano ya kikao cha wazazi lakini ajabu kila mzazi analalamika! Sasa hiko kikao huwa wanakalia wapi?

Mambo haya yameshamili sana na maafisa elimu wapo, wakurugenzi wapo, DC na RC wapo, mawaziri wapo, tamisemi wapo, Yaani ni kero mtupu lakini kiiimyaaa!

Walimu wanachukua mikopo halafu wanarudi kulalamika mshahara hautoshi wanasahau mikopo ya anasa ndo tatizo!

Ugumu wa maisha wao kutwa kuchangisha michango isiyo na kichwa wala miguu kila siku!
Kwanza tuition za kulipia za nini kwenye shule za serikali?
1000 kila siku boss? Sema shule gan hiyo watu waifatilie.
 
Labda ni michango yenye baraka
Hakuna baraka zozote kwa wazazi,

Ktk Kila shule kunakuwa na kigenge Cha wahuni ambacho kinajiita wawakilishi wazazi,
Hao ndy wanakula na walimu,

Wao ndy hukaa na walimu na kuamua maamuzi yoyote yenye maslahi nao,
Kwa kisingizio kwamba wao ndy wawakilishi wa wazazi wa wanafunzi wote.

Kumbe janja janja yao ya upigaji.
 
Na sio shule za msingi pekee bali ni shule zote za serikali zina mambo hayo ya michango ya hovyo hovyo.
 
Shule nyingi za msingi za serikali siku hizi zimejaa michango mingi sana ambayo inaleta matabaka kwa watoto!

Walimu wanachangisha hela ya mitihani kila siku 1000.
Ndoo mpya kila term,
Fagio jipya kila mwezi,

Hela ya safari (tour) kwa mgongo wa hiari huku nyuma wanawapiga mkwara watoto kwenda!

Vitabu vidogodogo wanalazimishwa kununua n.k

Hii tabia ukihoji wanasema ni makubaliano ya kikao cha wazazi lakini ajabu kila mzazi analalamika! Sasa hiko kikao huwa wanakalia wapi?

Mambo haya yameshamili sana na maafisa elimu wapo, wakurugenzi wapo, DC na RC wapo, mawaziri wapo, tamisemi wapo, Yaani ni kero mtupu lakini kiiimyaaa!

Walimu wanachukua mikopo halafu wanarudi kulalamika mshahara hautoshi wanasahau mikopo ya anasa ndo tatizo!

Ugumu wa maisha wao kutwa kuchangisha michango isiyo na kichwa wala miguu kila siku!
Kwanza tuition za kulipia za nini kwenye shule za serikali?

Wewe huwa unaenda kwenye vikao cha shule?
Mara nyingi wengi huwa hawaendi halafu wanalalamikia maamuzi ya walioenda
Dawa ni kwenda na kutoa maoni yako au kukataa hiyo michango kabla ya utekelezwaji wa maazimio ya vikao
 
Hakuna baraka zozote kwa wazazi,

Ktk Kila shule kunakuwa na kigenge Cha wahuni ambacho kinajiita wawakilishi wazazi,
Hao ndy wanakula na walimu,

Wao ndy hukaa na walimu na kuamua maamuzi yoyote yenye maslahi nao,
Kwa kisingizio kwamba wao ndy wawakilishi wa wazazi wa wanafunzi wote.

Kumbe janja janja yao ya upigaji.

Ndio uwe unaenda kwenye vikao ili upingie huko
 
Shule nyingi za msingi za serikali siku hizi zimejaa michango mingi sana ambayo inaleta matabaka kwa watoto!

Walimu wanachangisha hela ya mitihani kila siku 1000.
Ndoo mpya kila term,
Fagio jipya kila mwezi,

Hela ya safari (tour) kwa mgongo wa hiari huku nyuma wanawapiga mkwara watoto kwenda!

Vitabu vidogodogo wanalazimishwa kununua n.k

Hii tabia ukihoji wanasema ni makubaliano ya kikao cha wazazi lakini ajabu kila mzazi analalamika! Sasa hiko kikao huwa wanakalia wapi?

Mambo haya yameshamili sana na maafisa elimu wapo, wakurugenzi wapo, DC na RC wapo, mawaziri wapo, tamisemi wapo, Yaani ni kero mtupu lakini kiiimyaaa!

Walimu wanachukua mikopo halafu wanarudi kulalamika mshahara hautoshi wanasahau mikopo ya anasa ndo tatizo!

Ugumu wa maisha wao kutwa kuchangisha michango isiyo na kichwa wala miguu kila siku!
Kwanza tuition za kulipia za nini kwenye shule za serikali?
Sasa unataka walimu waishije?
 
Wapeni support walimu wapate chochote kupitia hyo michango , hawa watu ni wa mhimu na wanapitia wakat mgumu kuliko wafanyakazi wote.... Hawana semina hawana marupu tupu yyte , mwisho wa sku wanakopa mpak Kwa boda
Sasa huyo unayemtaka atoe support yeye anapewa na nani?.

Yeye Mwalimu ana mshahara mwisho wa uhakika kila Mwezi anataka support ya Saidia Fundi asiye na uhakika wa kazi kwa siku zote 30 za mwezi.
 
Yaani fagio na ndoo ndio waalimu wanapiga, kwa Nini msishauri hao watoto wenu wakifanya usafi warudi na ndoo na mifagio nyumbani kila siku ili kuepuka waalimu kupiga? Na hio hela ya copy za mitihani, mzazi mmoja mwenye photocopy ajitolee wenzie wamchangie awe anadurufu yeye hio mitihani yote
 
Toeni hela, acheni kulalamika lalamika kama watoto.
 
Yaani unataka mwanao apewe kila kitu na serikali? Acheni uvivu wazazi mfanye kazi msapiti kidogo
 
Well said mkuu,,
Hayo mambo yapo Sana kwenye hizi shule zetu za serikali.

Halafu ukiuliza wanasema wazazi walikaa na kupanga yote hayo.

Kumbe wazazi fake na vikao fake ..
Wazazi wa mchongo
 
Yaani unataka mwanao apewe kila kitu na serikali? Acheni uvivu wazazi mfanye kazi msapiti kidogo
Basi Ijulikane ya jumla ya mwaka mzima tujue moja siyo kila siku kidogo kidogo ni kero
 
Basi Ijulikane ya jumla ya mwaka mzima tujue moja siyo kila siku kidogo kidogo ni kero
Wakipiga hesabu ya mwaka itashtua watu. Kwa hiyo wanaona bora waende na hesabu ya wiki wiki
 
Back
Top Bottom