Kesi ya Mbowe imetuachia kumbukumbu isiyofutika, kwamba Serikali ilithibitisha Mbowe ana kesi ya kujibu, ushahidi ulitosha!

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Vitabu vya sheria vimebaki na kumbukumbu moja, serikali ilithibitisha ugaidi wa Mbowe, akaonekana ana kesi ya kujibu, hivyo kutakiwa ajitetee.

Mbowe hana hukumu ya kurejea kumsafisha!! Serikali Ina hukumu ya kuonyesha ilithibitisha Mbowe gaidi na ana kesi ya kujibu
 
Unafahamu maana ya " kuweka mpira kwapani"?
Serikali Ina uamuzi (ruling) kwamba jamaa Wana kesi ya kujibu, Mbowe hana uamuzi unaosema hana kesi ya kujibu, kisiasa inatosha kumchapa nayo
 

Nakumbuka kuna siku ulimkorofisha Pascal Mayalla kiasi cha kukuita jina fulani hivi linalo fanana na hili jina lako chinembe. Sasa naona ni kwa namna gani alikuwa sahihi.
 
sidhani kama kila kesi dpp anaweza ifuta,kama mahakama imeona wana kesi ya kujibu na imeridhika na maelezo ya upande wamashitaka kwanini dpp ameondoa kesi hiyo mahakamani ? Hili jambo ni baya hasa kwakuchafuana inabidi kina kibatara wafanye jambo ili kuwasafisha kina mbowe na iwe mwisho wakuonea watu''
 

Tubu ndugu yangu. Inaonekana unapenda Sana ugaidi. Tanzania hakuna ugaidi Kama unataka ugaidi kawaulize West gate Nairobi au Mogadishu Somalia. Kuna baadhi ya Mambo jaribu kuondoa siasa Bali angalia ukweli.

Unapodai ugaidi, ugaidi gani ulifanyika na wapi?. Uwe na reasoning usiwe mtu wa kudakia Mambo. Case to answer ni rulling sio hukumu ya kumtia mtu hatiani.
 
Nimeshangaa Samia amechezea mihimili yote tena wazi kweupe lakini kashangiliwa tu!

Nikajiuliza kwa staili hii kuna mtu atakuja kurudisha Rasimj ya pili ya Katiba? Leo tukimuuliza mzee Warioba, kwa mwenendo wa siasa za taifa lake anaona kuna mtu atakuja kurudisha ile Rasimj ya 2?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
chamsingi nikudai katiba tu! Kwa sasa watatoa uhuru wakufanya siasa nahapo ndipo chadema watumie mwanya huo.
 
Sasa kama ilithibitisha kwanini inaogopa watu wasijitetee
 
Reactions: Qwy
Tatizo liko wapi...DPP ndio mwenye Mamlaka kisheria na ametumia sheria
 
Kimsingi Mbowe kalishwa tango pori. Kama hajatambua hilo hastahili kuwa kiongozi wa chama cha Siasa. Hata jopo la mawakili wake ni zigo katika medani ya kisheria. Wanapaswa kuthibitisha, pasipo shaka, kuwa mashtaka dhidi ya mteja wao ni uwongo mtupu. Hivyo tungetegemea wangeweka pingamizi dhidi ya hiyo "nolle prosequi" (mashtaka kuondolewa) ya Serikali.

Hivyo basi, furaha, nderemo, na shangwe zinazoendelea kuhusu Mbowe kuwa huru (mawakili wake na wanachama wa CHADEMA) ni ushahidi kuwa mashtaka dhidi ya Mbowe na wenzake ni ya kweli.

Kwa hoja zangu hizo mshindi ni viongozi wa dini waliomwomba Rais amwondolee Mbowe mashtaka. Wakati Rais, kama M/kiti wa CCM, chama tawala, na Serikali yake amevuna imani ya WaTz, Mbowe bado anawajibika kuthibitisha kuwa hana hatia kwa mashtaka dhidi yake.
 
Nyie extremist wa Magufuli mtapata tabu sana... Tanzania mpya inasonga bila chuki zenu za kijinga wapuuzi nyie
 
Reactions: Qwy
Umeongea takataka tupu hapa

Everyone is innocent until proven guilty.

Hakuna kitabu kitakachoandika Mbowe ni gaidi. Wewe jifurahishe tu.
 
Walipaswa kuweka pingamizi dhidi ya hiyo "nolle prosequi", kama walivyokuwa wanafanya wakati kesi ikiendelea. Kutokufanya hivyo kunamwacha Mbowe na tuhuma dhidi yake maana tayari ushahidi uliotolewa mahakamani umethibitisha alikuwa na kesi ya kujibu
 
Umeongea takataka tupu hapa

Everyone is innocent until proven guilty.

Hakuna kitabu kitakachoandika Mbowe ni gaidi. Wewe jifurahishe tu.
Je, ana uthibitisho gani kuwa hana hatia katika mashtaka dhidi yake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…