Kesi ya Mbowe imetuachia kumbukumbu isiyofutika, kwamba Serikali ilithibitisha Mbowe ana kesi ya kujibu, ushahidi ulitosha!

Hakuna Serikali yeyote duniani inayoweza kumuachia gaidi azurure hovyo mtaani.

Kitendo cha kuachia kesi na kutokuwa na nia ya kuendelea nayo ni ushahidi tosha kwamba Serikali haioni merit yoyote zaidi ya kupotezeana resources (in short, hakuna kesi)

Hii ni sawa na wale mashekhe wa Uamsho mama aliowaachia mara tu baada ya kuukwa Urais. Tena kwa wale ushahidi wa uchochezi ulikuwepo wazi kabisa na unapatikana free kabisa huko Youtube.
 
Ruling ya Mbowe ana kesi ya kujibu iko mtaani for reference, the rest ni academic arguments, itatumika vyuoni, mahakamani kama precedent, hiyo ruling ya Mbowe hakuwa na kesi ya kujibu iko wapi?
Wewe akili yako ni ndogo sana. Mambo haya yamekuzidi kimo. Wewe ambaye hujui hata tofauti ya precedence na precedent, ndiye wa kujadili mambo haya?

Uwezo wako unaishia kupiga vigelegele viongozi wanapopita au kuhutubia.
 
Wewe akili yako ni ndogo sana. Mambo haya yamekuzidi kimo. Wewe ambaye hujui hata tofauti ya precedence na precedent, ndiye wa kujadili mambo haya?

Uwezo wako unaishia kupiga vigelegele viongozi wanapopita au kuhutubia.
Bado unazungusha mikono? Lowasa tayari karudi, babu Duni kawapiga chini
 
Mimi nadhani ni sahihi kwa Mbowe binafsi na watuhimiwa wote waliotajwa kuwa na kesi ya kujibu, wakiongozwa na mawakili wao wasomi wafungue kesi ya madai kwa kudhalilishwa na Serikali na walipwe fidia. 😳[emoji848]
Rais anataka walipwe fidia nje ya mahakama.
 
Matumizi mabaya ya ubongo nimatumizi ya akili kinyume Cha maumbile huna tofauti na anayetumia kiungo kingine kinyume Cha maumbile kamfufueni kayafa Mungu wenu mwl. Aliyewafundisha Chuki na Roho mbaya .mpyuuuuu
 
Msamaha wa Rais ni mkubwa kuliko ushahidi wa uwepo wa kesi ya kujibu. Rais anakwepa mazingira yote ya watu kumlalamikia, ambayo kwa kiasi fulani ni laana zinazodondosha tawala zote maarufu zilizopo duniani.

Rais anakwepa kutembea na dhambi za dhuluma na vilio vya watu. Anataka kufika miaka ya Mzee Mwinyi na JK, huwezi kufika huko ikiwa nafsi yako ni chanzo cha yatima wengi na wajane wanaoteseka na kulalamika kila mara.
 
 
Wewe ni mwendawazimu.

Hakuna ushahidi uliotolewa kuonesha Mbowe ni gaidi. Ruling ya mchongo ilisema Mbowe ana kesi ya kujibu. Hukumu ya kesi kuwa Mbowe ni gaidi au siyo gaidi ingekuja baada ya utetezi. Aliyefungua kesi, akijua ushahidi wa utetezi utakavyomwumbua, akaomba kuondoa mashtaka, na hivyo hata ile hukumu ya kuwa Mbowe ana kesi ya kujibu, kufutika kwa ombi la aliyefungua kesi.
 
Tafsiri ya hili ni kwamba serikali imejivua nguo imeshindwa kuthibitisha hiyo kesi waliosema hao wamba wanayo
 
Mbowe alikuwa anatuma makundi mengi ya watu wamuombee msamaha kwa mama, mama rahimu akamsamehe
Wewe mwendawazimu, endelea kuhangaika. Wenye akili kubwa, Mbowe na Rais, wanajadili maslahi ya Taifa.

Subiria wendawazimu wenzako, akina Kingai, watakavyofanywa. Ndiyo utajua kuwa nchi hii wapo wenye akili, na mpo ninyi mliowatupu vichwani.
 
Serikali Ina uamuzi (ruling) kwamba jamaa Wana kesi ya kujibu, Mbowe hana uamuzi unaosema hana kesi ya kujibu, kisiasa inatosha kumchapa nayo
Finally DPP akabaini hakuna kesi licha ya ruling kumkuta ana kesi ya kujibu, usijisahaulishe kuwa la DPP ndipo uzito ulipo.
 
Je, ana uthibitisho gani kuwa hana hatia katika mashtaka dhidi yake?
Jifunze acha ubishi. Sio kazi ya mtuhumiwa kuthibitisha hana hatia, ni kazi ya anayeshitaki kudhibitisha na mahakama kuamua.

Ni wapi mahakama imeamua kuwa ana hatia? Je kapewa adhabu gani?
 
Jifunze acha ubishi. Sio kazi ya mtuhumiwa kuthibitisha hana hatia, ni kazi ya anayeshitaki kudhibitisha na mahakama kuamua.

Ni wapi mahakama imeamua kuwa ana hatia? Je kapewa adhabu gani?
Ana kesi ya kujibu, ushahidi ulikuwa mwingi sana, ruling ipo
 
Enzi ya jiwe kesi kama hizi ilikuwa ni kuiga kalenda tu.Lakini mama alitaka ziongelewe au zifutwe.tunawashukuru viongozi wa dini.
 
Kweli wewe ni kine.mbe. Kwahiyo kwa akili yako Mbowe ndio ameiondoa kesi mahakamani? [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…