Kesi ya Mbowe: Mbowe na viongozi wa CHADEMA msiposikiliza ushauri wa Godbless Lema anaeshauri muondoe mawakili mahakamani, mtakuja kujiulaumu sana

Wakijitoa sasa hivi MATAGA watasema mawakili wa mboe wameona wamezidiwa na hivyo kuamua kujitoa,kwa hali ilivyo bora wapambane kupAngua ushaidi mpaka mwisho ili wote tuone vioja vinavyoendelea huko mahakamani
Hakuna mtu anaeamini kuwa hii kesi ina uhalali, hivyo wengi watasifu na kupongeza uamuzi huo na labda kusikitika/kulaumu kuwa uamuzi huu umechelewa.
 
Kuondoa mawakili mahakamani maana yake wasuse. Hii ni hatari zaidi. Mbowe atapigwa miaka mingi kuliko umri wake
 
Hoja zako, na hao ulio wananukuu, ni jaribio la kuitisha mahakama
 
Wakijitoa sasa hivi MATAGA watasema mawakili wa mboe wameona wamezidiwa na hivyo kuamua kujitoa,kwa hali ilivyo bora wapambane kupAngua ushaidi mpaka mwisho ili wote tuone vioja vinavyoendelea huko mahakamani

Hao MATAGA hata hiki kitendo cha kususia chaguzi wanasema cdm wameona watashindwa, sijui hawana pesa. Lakini ukweli wote tunaona kwenye chaguzi za kishenzi, kihayawani na ukatili wa wazi ili ccm kutangazwa washindi, tena kwa kushirikiana na tume ya uchaguzi na vyombo vya dola. Ila wananchi wameshaujua ukweli ndio maana sasa hivi zoezi la uchaguzi limepoteza uhalali wa umma. Hivyo usijali wanachosema MATAGA maana hao ni debe tupu, lakini ukweli kila mtu anaujua. Kufikia Ijumaa ya wiki ijayo maamuzi yafanyike maana tayari jaji ameshaonyesha kufuata maagizo toka nje ya uwanja.
 
Wenye nguvu ya maamuzi kesi ya mbowe ni familia na sio chama acheni kujidanganya mitandaoni. Chama kiliisusa kesi,familia wakaingilia kati

Yeye lema katolea mfano uamuzi wa mkewe. Hivyo ujumbe wake ungemlenga mke wa mbowe au mchepuko mkuya(kama ana nguvu za kifamilia)
 
Kukaa kimya mahakamani ndo kufanyeje?Je hii kasi inahusua suala la muda wa MBowe kukaa mahakamani tu?Tuhuma ni Ugaidi,Serikali inaleta Hoja,Lazima hoja ijibiwe kwa ahoja ispokuwa pale ambapo hamna hoja.Binafsi naamni wahatever the outcome of this case.Ni muhimu sana kwa Mbowe et al kushiriki katika kesi mpaka mwisho mintarafu haki na wajibu wake kisiasa na kiraia.

Itoshe tu kusema kwamba kama tunafikiri Mbowe anaonewa kwa sababu tu ya maamuzi ya mahakama kuwa kinyume na amatarajio yetu basi let it be seen so katika process nzima ya kesi yake.
 
Nakuunga mkono kwa mtazamo wangu mbowe amesha hukumiwa kinacho endelea ni kuchelewesha kuidhinisha tu bass
 
Hoja zako, na hao ulio wananukuu, ni jaribio la kuitisha mahakama

Hakuna mtu mwenye muda wa kuitisha mahakama, bali mahakama inashindwa kusimamia utendaji haki. Mifumo yetu kuanzia vyombo vya dola, mihimili kama bunge na mahakama zote kumeingizwa siasa chafu. Kama tumeamua kususia chaguzi za nchi hii kwa uhayawani unaondelea, sioni kwanini tuendelee kupoteza muda huko mahakamani ambako tayari uozo umeshaingia na unaonekana wazi.
 

Kwa nini Serikali ihangaike kumtengeneza Mbowe mashtaka ya kubumba? Ni nguvu gani aliyonayo?, ni hoja yenye nguvu. Na kwa kuwa kesi imevuta hisia za watu wengi, wenye nguvu na wa kawida, ndani na nje ya nchi, ni busara kusubiri hukumu. Tofauti na hilo, ni kuitisha mahakama
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ asusie mahakama sio? Hii nchi hii kazi ipo. Mbowe apambane, yatapita. Amekwepa mishale mingi tayari na serikali ya ccm inajua umuhimu wake na inamuheshimu sana. Kama tu inavyomuheshimu maalim ila wafuasi ndo povu jingi maji machache.
 
Hata wakijitoa sawa tu make dunia imeshajua kinachoendelea.
 
Hizi pumba unazipepeta ukiwa choo gani?
 
Naunga mkono hoja
 
Hakuna mtu anaeamini kuwa hii kesi ina uhalali, hivyo wengi watasifu na kupongeza uamuzi huo na labda kusikitika/kulaumu kuwa uamuzi huu umechelewa.

Kabisa, jaji wa kwanza tulionyesha kupoteza imani na yeye, kwakuwa alijua kabisa ni kesi ya kubumba akakubali haraka, ili asiumize kichwa kutekeleza hukumu isiyoendana na ushahidi. Jaji wa pili akatupilia mbali mapingamizi kwa sababu dhaifu kabisa, na kwakujua nia ovu iliyopo nyuma ya pazia akajitoa. Huyu wa sasa tayari kesi inaanza kumuelemea kwa kuanza kujigeuza sehemu ya ushahidi wa jamuhuri. Hapo tunasita nini kuchukua hatua kufikia Ijumaa ijayo?

Tumesusia kile kikao cha kihuni cha msajili wa vyama vya siasa na IGP, as a result kikao kimeahirishwa maana target ilikuwa ni cdm ili wafundishwe siasa za woga. Chaguzi nyingi tumesusia na sasa zoezi zima la uchaguzi limekosa mashiko na uhalali wa umma. Na sasa tukijitoa kwenye hiyo kesi lazima serikali ikae pabaya maana ndio wahusika wa hizi siasa chafu. Nashauri wakusanye procedings za kesi, ili kufikia Ijumaa ijayo na kujitoa kwenye huo uhuni.
 
Mkuu kwenye shauri hili Chief Hangaya alishamaliza. Rejea mahojiano yake na Mwandishi wa BBC. Bila kusahau upandishwaji wa cheo Kwa Jaji Siyani. Nini kilifanyika kwenye hukumu ya kesi ndogo? Huo ni ushahidi tosha.

Acha wamhukumu wapendavyo kwakuwa ni wamiliki wa Mihimili yote mitatu. Je nn kitawashinda??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…