Kesi ya Mbowe: Thamani ya ushahidi wa shahidi #4 ni ipi?

Kesi ya Mbowe: Thamani ya ushahidi wa shahidi #4 ni ipi?

Hilo ndilo linaloendelea kwenye dodoso za huyu shahidi #4. Tusubiri hitimisho la dodoso kwa huyu shahidi.

Kuweka rekodi sawa sawa, dodoso kwa shahidi #4 limekwisha na kesho inshallah anapanda kizimbani moja kwa moja shahidi #5.
 
Wewe kwa akili zako hayo maelezo ya polisi yana ukweli gani kama waliwakamata watuhumiwa saa saba wakamfanyia mahojiano kwa 45mins it means walimaliza naye saa 13:45 kisha maelezo hayo hayo akayasaini saa saba kamili.....inakuingia akilini?

Hapo hizo hesabu zao waligawanya walizidisha au walitoa?may be walijumlisha who knows!
Tena yamesainiwa kituo kikuu Cha Polisi Moshi siyo hapo Rau ili hesabu ziendane na na saa 7.Au walirudisha mahare wa saa nyuma?
 
Ndio maana kitabibu ni kweli baadhi ya watu wana uwezo wa kuona mbali au karibu kwa hiyo hakuna tatizo katika maelezo yake ya ushahidi.

Wakili ameshindwa kuhoji kama ana matatizo ya kuona na kwamba alishathibishwa hospitalini ili adai cheti cha kupimwa kwake. Mawakili wanaojifunza wanafikiri kila kinachofundishwa darasani ndicho kilichoko kwenye uhalisia ndio maana pakawepo na shule ya sheria (Law School) kumwandaa na uwanja wa hoja tunduizi
Inabidi uwe zuzu ndiyo mtu anaweza kukubaliana na wewe.
 
Mimi huwa kuna kamsemo nakapenda sanaa wkt wa mahojiano...unakuta shahidi kaingia chaka...unaskia tu wakili anamwambia...iambie mahaka au jaji kwamba hapa nmedanganyaa...dizain kama unasnitch kwa jaji....ila ukijua sheria ni raha sanaaa
 
Daaa sikufuatilia maana nilijua leo ni upande wa serikali
Huwa upande wa Jamhuri ni hapo hapo, cross examination kutoka mawakili wa upande wa utetezi ni hapo hapo na hata re-examination kutoka mawakili wa upande wa Jamhuri ni hapo hapo. Leo ambacho hakijafika mwisho ni re-examination ingawa ilifanyika hadi mahakama ilipoahirishwa. Hivyo kesho ni kumalizia re-examination kutoka upande wa mawakili wa upande wa Jamhuri. Lengo la hii re-examination kutoka mawakili wa upande wa Jamhuri ni "ku repair damage" iliyosababishwa na mawakili wa upande wa utetezi kwa shahidi wao wakati wa cross examination.
 
Huwa upande wa Jamhuri ni hapo hapo, cross examination kutoka mawakili wa upande wa utetezi ni hapo hapo na hata re-examination kutoka mawakili wa upande wa Jamhuri ni hapo hapo. Leo ambacho hakijafika mwisho ni re-examination ingawa ilifanyika hadi mahakama ilipoahirishwa. Hivyo kesho ni kumalizia re-examination kutoka upande wa mawakili wa upande wa Jamhuri. Lengo la hii re-examination kutoka mawakili wa upande wa Jamhuri ni "ku repair damage" iliyosababishwa na mawakili wa upande wa utetezi kwa shahidi wao wakati wa cross examination.
Asante sana mkuu ufafanuzi wa kina.
 
Atamaliziwa huyu #4 kufanya "repairs" na mawakili wa upande wa Jamhuri kabla ya #5 kuanza.

Umeona hapo kwenye red mkuu wangu?

IMG_20211101_213222_147.jpg
 
Shahidi ana ugonjwa wa macho pia hakumbuki vizuri lakini ameweza kukumbuka namba ya bunduki haleluya
Hii kesi imejaa maruwe ruwe! Naamini hata Majaji wanaiendeleza hii kesi kwa lengo la kutaka kutoa mafunzo kwa Majaji na Mawakili wengine siku za usoni!

Kinyume na hapo, hii kesi ni ya kufutilia mbali. Maana haina uhalisia hata kidogo.
 
Huwa upande wa Jamhuri ni hapo hapo, cross examination kutoka mawakili wa upande wa utetezi ni hapo hapo na hata re-examination kutoka mawakili wa upande wa Jamhuri ni hapo hapo. Leo ambacho hakijafika mwisho ni re-examination ingawa ilifanyika hadi mahakama ilipoahirishwa. Hivyo kesho ni kumalizia re-examination kutoka upande wa mawakili wa upande wa Jamhuri. Lengo la hii re-examination kutoka mawakili wa upande wa Jamhuri ni "ku repair damage" iliyosababishwa na mawakili wa upande wa utetezi kwa shahidi wao wakati wa cross examination.

Shahidi #4 imetoka. Kesho straight #5.

IMG_20211101_213222_147.jpg
 
Back
Top Bottom