Uchaguzi 2020 Kibamba: CHADEMA wadai Mwanachama wa CCM amechukua fomu ya kugombea Ubunge kwa jina lao

Uchaguzi 2020 Kibamba: CHADEMA wadai Mwanachama wa CCM amechukua fomu ya kugombea Ubunge kwa jina lao

..hizo fomu zinatolewa KIENYEJI sana.

..msimamizi alitakiwa achukue na nakala ya KITAMBULISHO, pamoja na anuani ya kila anayechukua fomu.

..kwa kilichotokea inatakiwa MAMLAKA za juu za Tume ya Uchaguzi, baada ya kujiridhisha kuhusu mgombea halali wa CDM, zitoe maelekezo chama hicho kipewe fomu nyingine kwa ajili ya mgombea wao.

Nakubaliana na wewe. Chadema wanatakiwa kuzibana Mamlaka ya juu ya Tume ili ichukue hatua kali kukomesha tabia kama hizi kabla hazijaota mizizi.

Anachonishangaza Msimamizi ni kukataa kata kata kuchukua hatua yeyote ya kujiridhisha kuwa watu wenye nia ovu hawajamtumia kama daraja kufanikisha ajenda yao. Anashindwa nini kuwasiliana na uongozi wa chama husika kinachodaiwa kuandika barua ya uthibitisho ili wathibitishe uhalali wa barua hiyo?

Katibu Mkuu wa Chadema anatakiwa kutoa tamko kuhusu suala hili na kuitaka Tume ifute jina la aliyechukua na wamuadhibu. Mambo haya yalianza kwa Meya Boniface na sasa tunayaona yanafanyika Kimamba na Kilombero.

Ukimya wa Chadema unaonyesha kuwa hawako serious kama chama.

Amandla...
 
Alichofanya Msimamizi ni kukwepa majukumu yake kama vile ambavyo baadhi ya mapolisi wanapomtaka mtu aliyefanyiwa kitendo kibaya, amkamate mbaya wake na amlete kwao!

Sijui anashindwaje kuona kuwa institution nzima inachafuliwa kwa kushindwa kudhibiti vitendo na hasa yeye personally. Kwa nini mchezo huu ufanyike mara mbili kwake kama yeye sio complicit? Au wahusika kujua kuwa hana ubavu wa kusimamia integrity ya nafasi yake na ya taasisi yake?

Amandla...
 
Kwani majina yabuteuzi si yako TUME y auchaguzi?
Huyo alie chukua imekuwaje apewe?
Tume haipokei orodha ya wagombea/wateuliwa; yenyewe inapokea barua ya kumtambulisha mgombe toka kwenye chama, Kilichotokea kuna mtu amefoji barua - nadhani ni vema chadema waende polisi kuripoti na waombe stop order ya mahakama ili hiyo fomu iliyotolewa mwanzo, isitambuliwe.
 
Tume haipokei orodha ya wagombea/wateuliwa; yenyewe inapokea barua ya kumtambulisha mgombe toka kwenye chama, Kilichotokea kuna mtu amefoji barua - nadhani ni vema chadema waende polisi kuripoti na waombe stop order ya mahakama ili hiyo fomu iliyotolewa mwanzo, isitambuliwe.

..ushauri wako ni mzuri sana.

..pia utaratibu wa kutoa fomu uboreshwe kwa kuchukua taarifa[kitambulisho, namba za simu, anuani,] za kila anayekabidhiwa fomu na msimamizi wa uchaguzi.
 
Kuna mambo mawili naamini CDM watayafanya
1. Kutoa taarifa polisi, pamoja na hili kupeleka malalamiko yao tume ya uchaguzi kwa kilichotokea

2. Waonyeshe jinsi msimamizi wa uchaguzi anavyo lifanya jambo hili kuwa hawezi kuchukua hatua hadi pale atakaporudishiwa fomu iliyochukuliwa. Nimemsikiliza kiongozi wa CDM akieleza kuwa fomu ilichukuliwa kabla CDM hawajachagua mgombea wao. Katika yote hili ndio rahisi kujiridhisha kama ni kweli na kama ni hivyo basi ile formu ni batili moja kwa moja. Pia kuna list ya CDM je ni nani alichaguliwa?
Sasa mama kushinikiza CDM wamleteee ile fomu anategemea wao watampata wapi huyo "mhalifu"? Cha ajabu kabisa inasemekana hawana namba za simu za wagombea wala anuani za makazi yao. Hivi ni vitu ambavyo havina mjadala vinatakiwa viwepo vinginevyo NEC hawako serious. Mama anashikilia barua aliyoletewa ni halali-anajuaje kuwa ni halali wakati wahusika wana mwambia si halali. Uhalali si signature tu bali na contents za barua. Anasema sio swala la busara ni swala la sheria. Kama sheria ina mapungufu unafanya je.

Matokeo kama haya yanathibitisha bado tuna elements za ushenzi. Badala ya kudhibiti washenzi, tunajaribu kuwakingia kifua kwa manufaa ya kisiasa.
 
Back
Top Bottom