Uchaguzi 2020 Kibamba: CHADEMA wadai Mwanachama wa CCM amechukua fomu ya kugombea Ubunge kwa jina lao

hujui ni sawa na kusema musiba akigombea uraisi badala ya magufuli ccm watapata hasara gani
 
Duh! Wanatoaje form kwa mtu bila kujua jina lake, address yake na namba yake ya simu? Na wanatoaje form kwa mgombea kabla chama husika hakijateua mgombea wake?😳

Their record keeping is ZERO.

Huu ni uhuni wa hali ya juu.
 
Ishu nyeti km hii mtu anatoa fomu kienyeji hivi kweli! Loose stool! NEC toeni muongozo kwa hao wasimamizi wenu kuepusha huu uzezeta! Ikiwezekana mgombea alieteuliwa na chama aambatane na viongozi waandamizi wa chama ndani ya jimbo husika! Mnafanya mambo ya hovyo watu wakireact mnasema vyama vya upinzani vinasababisha vurugu..hivi kweli mtu anapewa fomu bila kutoa taarifa zozote kwenye ofisi ya mkurugenzi?? Huyo mama aondolewe mara moja atatuharibia uchaguzi!
 
Hapo yupo mbele ya camera bado anajibu majibu yanayodhihirisha nia ovu. He wayafanyayo gizani?
 

Mambo yafuatayo yametokea.

1. Mhusika amechukua fomu ya kugombea siku ambayo CDM ilikuwa bado haijatangaza mgombea wa jimbo la Kibamba.

2. Aliyechukua fomu jina lake halipo kabisa ktk orodha ya wanachama wa CDM waliotia nia kugombea jimbo la Kibamba.

3. Mhusika hakuacha copy ya kitambulisho chake, pia hakuacha anuani yake wala nambari za simu kwa msimamizi wa Uchaguzi.

4.CDM wana utaratibu wa kuwasindikiza wagombea wao kuchukua fomu. Mhusika aliyechukua fomu aliambatana na mtu mmoja tu.

5.Barua haiwezi kuwa halali kwasababu imeandikwa wakati vikao vya chama havijafanya uteuzi wa mgombea wa ubunge jimbo la Kibamba.
 
Nitaendelea kuomba tafasiri ya kauli "Sasa basi" japo hakuna wa kunijibu. Why is it not applied in such circumstance!!
 
Ninawashauri Chadema wasipoteze muda kubishana na hao wahuni. Wafanye coordination na Act Wazalendo kuona iwapo kuna mgombea competent basi huyu wa Chadema amuunge mkono, Kama Act- Wazalendo hawana mgombea basi huyo wa Chadema ahamie huko achukue form na kugombea kupitia Act-Wazalendo. Wanatakiwa kuwa pragmatic, hakuna haja ya kubishana na kupoteza muda kwa kuwa hawa wahuni wa CCM wanataka kuchukua jimbo bila kupingwa. Fikirini kijeshi and smartly.
 
Mbona simple tu, yeye atoe fomu nyingine halafu utaratibu wakati wa kurudisha hiyo fomu awepo kiongozi wa ngazi za juu za CDM( Mwenyekiti au katibu) Hapo atajulikana halali ni yupi.

Hayo anayosema CHADEMA waende polisi wamtafute huyo mgombea fake fomu irudishwe kwake ndiyo atoe fomu nyingine, huko ni kupoteza muda, na kuweka mazingira ya CDM kukosa mgombea.

Huyu mkurugenzi kwa jinsi alivyokuwa anajieleza inaelekea anajua kabisa kuwa huyo mgombea alikuwa fake na hawezi kurudisha hiyo fomu.
 
Si ajabu hili alilotenda linaweza kufanyika katika vituo vingi nchini. Mtu akajichukulia form halafu hawana hata rekodi yoyote ile ya kuweza kumtambua. Na kama form ilitolewa kabla ya Chama kuteua mgombea hiyo form ni BATILI mgombea husika apewe form nyingine.

NEC imshugulikie huyu mama, ana mambo ya kipumbavu kabisa.
 
Watu kama huyo mama ndio tatizo ugumu huko wapi hapo wa kutoa form nyingine. Huyo mwingine akirudisha si ndio awaite polisi.

Mambo kama hayo CDM sasa ndio wanatakiwa wakaripoti NEC kwa mtu yeyote atakaesikiliza ni ubabaifu; it doesn’t make sense wape watu form.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…