Kibatala: Wanaopinga Katiba Mpya wana Maslahi Binafsi

Kibatala: Wanaopinga Katiba Mpya wana Maslahi Binafsi

Wananchi wengi wanawashangaa sana hawa wanaolilia katiba mpya, wakiwa mimacho yamewatoka, mapovu yakiwatoka, mishipa ya shingo imetuna, wameva nguo nyekundu kuashiria kumwaga damu za watu hadi waipate hiyo katiba wanayoitaka. Dhumuni lao nini hasa mpaka wanataka kumwaga damu.

Mbona hii katiba iliyopo tumekuwa nayo miaka mingi tu na nchi ilikuwa imetulia hadi kuwa kinara cha amani Afrika. Mbona katiba hii tuliyo nayo tumekuwa tukiifanyia updates na upgrades ili kwenda na wakati. Mbona katiba hii tuliyonayo tuliifanyia upgrade kubwa mwaka 1984 hadi kuingiza haki zote za binadamu zilizoazimiwa na Umoja wa Mataifa (UN).

Update moja wapo ni ya mwaka 1992 ambayo ilianzisha vyama vingi vya siasa, kitu kilichowezesha hadi chadema ikazaliwa na akina Mbowe kupatikana. Mbona mataifa makubwa duniani kama USA na Germany katiba zao ni zile zile za tangia ujima ila huzifanyia updates na upgrades tu ili kwenda na wakati kama ambavyo sisi tunavyofanya. Haijatokea mataifa haya eti yakadai katiba mpya na kufuta iliyokuwapo.

Ni kitu gani hasa kimetokea hii miaka ya karibuni kilicholifanya kundi hili la wanasiasa hadi kufikia kutaka kumwaga damu za Watanzania? Kwa mtu ye yote mwenye akili timamu jibu lake liko wazi. Wana masilahi binafsi ya kushika Dola. Kwa katiba hii hii tuliyonayo tangia kuanzisha vyama vingi vya siasa, vyama vya upinzani vimekuwa vikiimarika kwa kasi ya kuridhisha na kutoa tumaini ya kuweza kushika dola jinsi miaka ilivyokuwa ikienda.

Uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995, Lyatonga Mrema wa upinzani alimtoa kamasi Benjamini Mkapa wa chama tawala. Ilibidi Nyerere atoke ustafuni na kuzunguka nchi nzima kuokoa jahazi. Kama Nyerere hangalifanya hivyo, Mrema alikuwa anachukua Dola kwa katiba hii hii tuliyonayo. Hivyo hivyo uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 Dr Willbrad Silaa wa upinzani alimtoa jasho Jakaya wa chama tawala na hatasahau. Mwaka 2015 ilikuwa balaa zaidi. JPM wa chama tawala alipita kwa taabu dhidi ya Edward wa upinani.

Tatizo chama kilichokuwa kikuu cha upinzani kati ya mwaka 2015 hadi 2020 kikajivuruga chenyewe kwa sababu ya ubinafsi wa mwenyekiti wake. Watu muhimu kwenye chama hicho wakakikimbia hadi ilipofika uchaguzi mkuu wa 2020 kikafa kifo cha mende. Kinasingizia Tume ya Uchaguzi kwamba muundo wake hauko vizuri. Hili ni jambo dogo sana halihitaji katiba mpya. Sheria husika ya NEC inaweza kurekebishwa. Returning Officers huko wilayani badala ya kuwa wakurugenzi wa halimashauri wanaweza wakawa District Magistrates kama ilivyo huko India. Ni kubadilisha sheria tu.
 
Hayo yote unayodhani yatawezeshwa na Katiba Mpya yanaweza kubaki ndoto za alinacha. Kwa sababu moja kuu: tatizo sio sheria mpya, nzuri au kali bali tatizo kubwa si kwa watawala wetu bali Watanzania kwa ujumla ni katika kuheshimu sheria. Hebu tupia jicho hapo mtaani unapoishi, ni watu wangapi wanakiuka "sheria za ndoa"? Sasa kama watu hawaheshimu sheria "binafsi," miujiza gani itafanya sheria za kwenye Katiba mpya ziheshimiwe?
Daah Kaka Chahali sawa Bwana. Lakini Ulikuwa hapo awali unatulaumu sisi wapinzani kwanini hatuanzishi michakato ya kudai katiba mpya na tume huru na ukaenda mbele zaidi kusema huwa tunadfnya hivyo wakati wa uchaguzi too late. Lakini leo unataka kutusaliti na kutaka kuonesha kuwa katiba mpya sio muhimu.
 
Wanufaika wa moja kwa moja wa hali iliyopo wanafahamika kwa maandiko yao. Uzi huu uliwahusu wao:

Machafuko na ukatili uliotokea wakati wa uchaguzi 2019 serikali za kitaa na 2020 uchaguzi mkuu ni matokea ya Katiba ua hovyo. Anayepinga ujue ni wale wale tu.
 
Ni Dhahiri Katiba iliyopo kuna Viongozi Wengi Wananufaika nayo kutoka na UBOVU wa KATIBA.Wapo Waliopata UWAZIRI na UBUNGE na Wapo WALIOIBA PESA za SERIKALI lakini Kutokana na UBOVU wa KATIBA wapo HURU MITAANI.

Polepole wa Mchakato wa KATIBA MPYA sio Polepole ambaye sasa ni MBUNGE

Bashiru wa Bunge la Katiba Sio huyu Bashiru MBUNGE

KABUDI wa Kukusanya Maoni ya Wananchi na Bunge la Katiba Sio huyu WAZIRI.

Kigwangala wa Bunge la Katiba na Waziri Aliyepiga PESA za TANAPA na kuchonga SANAMU ya Hayati Baba Wa Taifa sio huyu Wa sasa hawa ni Baadhi ya Wanufaika na Katiba Iliyopo ni lazima WAIPINGE KATIBA MPYA.

Screenshot_20210615-225216_Twitter.jpg
 
Hawa ni wanafiki kwani hata jaji Warioba alipomaliza kuwakilisha rasimu ya Katiba mpya bungeni, wengi wa wabunge wa CCM walimpogeza Mimi nikiwa naangalia luninga yangu; wanafiki tu tena wanasahau wameajiriwa na wananchi ambao ndio wanaotaka katiba ya uajibikaji.
Na Jaji Werema (mstaafu asiyeeleweka) ameongea Ila mnajua kwa nini aliondolewa hadi ujaji kabla ya umri wa kustaafu? Maana Jaji akishateuliwa haondoki kazini mpaka atimize umri wa kustaafu (65 yrs)

Nae ana mambo yake fudenge no wonder leo anaamka kutafuta audacity.
 
Daah Kaka Chahali sawa Bwana. Lakini Ulikuwa hapo awali unatulaumu sisi wapinzani kwanini hatuanzishi michakato ya kudai katiba mpya na tume huru na ukaenda mbele zaidi kusema huwa tunadfnya hivyo wakati wa uchaguzi too late. Lakini leo unataka kutusaliti na kutaka kuonesha kuwa katiba mpya sio muhimu.

Yaonesha huyo bwana anasoma kwa akina Kafulila, Mashinji, Nassari, Lijualikali, Sumaye, Lowassa, Nyalandu na wa namna hiyo.

Atakuwa amerudi nyumbani au yu njiani kurudi nyumbani. Wenyewe wanaita Ku switch sides. Atakuwa kaona nyimbo za Sayuni haziimbiki ugenini.

Hapa ndipo inapokuja suala zima la Mbowe kuendelea kuongoza Chadema. Wengi hawaaminiki. Machoni kama watu kumbe ni vinyonga!

Hili pia lilikuwa bandiko lake la kushangaza la siku za karibuni:

IMG_20210706_060201_162.jpg


Comment #72 kwenye uzi huu:


Kulikoni bwana Evarist Chahali, nyumbani kumenoga?

Cc: BAK Mmawia imhotep JokaKuu
 
Kwa nini kipindi cha lile lisanamu la Chato hakukukuwa na hizi hamsha hamsha.
Inakuwaje linapotokea tetemeko la ardhi mukiwa ndani ya Pub munastarehee?

Ni dhahiri mutakimbia nje kuokoa maisha yenu.

BARIKIWA NA UWE NA SIKU NJEMA.

Ole wako ukamatwe unataka kujiuwa (suicide) utapandishwa kizimbani na hakimu atakufunga tu.

Wakati ule kujitokeza na mambo haya ni sawa na kujiuwa.

USIRUHUSU KIZAZI CHAKO KIWE NA AKILI KAMA ZAKO
 
Wengine ni kweli hawaelewi chochote na hata JF wamo.

Utawasikia, watu wanahitaji umeme na maji'' utadhani katiba mpya itazuia watu kupata umeme na maji.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Wananchi wengi wanawashangaa sana hawa wanaolilia katiba mpya, wakiwa mimacho yamewatoka, mapovu yakiwatoka, mishipa ya shingo imetuna, wameva nguo nyekundu kuashiria kumwaga damu za watu hadi waipate hiyo katiba wanayoitaka. Dhumuni lao nini hasa mpaka wanataka kumwaga damu. Mbona hii katiba iliyopo tumekuwa nayo miaka mingi tu na nchi ilikuwa imetulia hadi kuwa kinara cha amani Afrika. Mbona katiba hii tuliyo nayo tumekuwa tukiifanyia updates na upgrades ili kwenda na wakati. Mbona katiba hii tuliyonayo tuliifanyia upgrade kubwa mwaka 1984 hadi kuingiza haki zote za binadamu zilizoazimiwa na Umoja wa Mataifa (UN). Update moja wapo ni ya mwaka 1992 ambayo ilianzisha vyama vingi vya siasa, kitu kilichowezesha hadi chadema ikazaliwa na akina Mbowe kupatikana. Mbona mataifa makubwa duniani kama USA na Germany katiba zao ni zile zile za tangia ujima ila huzifanyia updates na upgrades tu ili kwenda na wakati kama ambavyo sisi tunavyofanya. Haijatokea mataifa haya eti yakadai katiba mpya na kufuta iliyokuwapo.

Ni kitu gani hasa kimetokea hii miaka ya karibuni kilicholifanya kundi hili la wanasiasa hadi kufikia kutaka kumwaga damu za Watanzania? Kwa mtu ye yote mwenye akili timamu jibu lake liko wazi. Wana masilahi binafsi ya kushika Dola. Kwa katiba hii hii tuliyonayo tangia kuanzisha vyama vingi vya siasa, vyama vya upinzani vimekuwa vikiimarika kwa kasi ya kuridhisha na kutoa tumaini ya kuweza kushika dola jinsi miaka ilivyokuwa ikienda. Uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995, Lyatonga Mrema wa upinzani alimtoa kamasi Benjamini Mkapa wa chama tawala. Ilibidi Nyerere atoke ustafuni na kuzunguka nchi nzima kuokoa jahazi. Kama Nyerere hangalifanya hivyo, Mrema alikuwa anachukua Dola kwa katiba hii hii tuliyonayo. Hivyo hivyo uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 Dr Willbrad Silaa wa upinzani alimtoa jasho Jakaya wa chama tawala na hatasahau. Mwaka 2015 ilikuwa balaa zaidi. JPM wa chama tawala alipita kwa taabu dhidi ya Edward wa upinani.

Tatizo chama kilichokuwa kikuu cha upinzani kati ya mwaka 2015 hadi 2020 kikajivuruga chenyewe kwa sababu ya ubinafsi wa mwenyekiti wake. Watu muhimu kwenye chama hicho wakakikimbia hadi ilipofika uchaguzi mkuu wa 2020 kikafa kifo cha mende. Kinasingizia Tume ya Uchaguzi kwamba muundo wake hauko vizuri. Hili ni jambo dogo sana halihitaji katiba mpya. Sheria husika ya NEC inaweza kurekebishwa. Returning Officers huko wilayani badala ya kuwa wakurugenzi wa halimashauri wanaweza wakawa District Magistrates kama ilivyo huko India. Ni kubadilisha sheria tu.
Kwamba?

"Wananchi wengi wanawashangaa sana hawa wanaolilia katiba mpya, wakiwa mimacho yamewatoka, mapovu yakiwatoka, mishipa ya shingo imetuna, ..."

Hao wananchi ni hawa ambao
:

IMG_20210706_062420_640.jpg


You must be kidding!
 
Wengine ni kweli hawaelewi chochote na hata jf wamo.
Utawasikia ,,watu wanahitaji umeme na maji'' utadhani katiba mpya itazuia watu kupata umeme na maji.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Tofautisha watu wanaonufaika binafsi na hali iliyopo. Usisahau hao nao wamo humu JF.
 
Back
Top Bottom