Kiengereza kitumike shule za umma tokea msingi mpaka chuo

Kiengereza kitumike shule za umma tokea msingi mpaka chuo

Korea Lugha yao wameanza nayo 1444, japan wana lugha yao toka zamani sanaaa, China vivyo hivyo,
Sisi kiswahili kimeingia mwaka 1950+
Huko ndani ndani hadi leo watu hawajui kiswahili vizuri, 😂 huyo mtu bado unampa kazi ya kujifunza English then Physics iliyo katika English, utakuta tu mtu hajui
Uko sahihi kabisa,hata mimi natamani tuchague lugha moja tu ya kufundishia kuanzia awali hadi chuo kikuu,kuliko huu mchanganyo wa sasa.
 
Mataifa yasiyotumia kingereza kama lugha ya kufundishia na yamefanikiwa kielimu yamewezaje????

Kingereza sio suruhisho la elimu bora, ile ni lugha tu.

Kwetu hii lugha ni changamoto, yani tunajifunza kitu tusichokijua (physics) kwa lugha tusiyoijua ( Yani vyote viwili hatuvijui) unategemea tuwe na elimu bora.

Tutumie lugha tunayoijua tujifunze hayo tusiyoyajua.
Ongezea pia kwamba walimu wengi wanaofundisha nao hawajui wanachofundisha.

Shule nyingi za serikali, failures ndio walimu wa wanafunzi. Sasa hapo tutegemee nini?

Hapo pia tusiwasahau waongoza wizara, maafisa elimu, waratibu, nk. Hali ni tete kwa kweli.

Elimu ni muhimu sana, lakini serikali inaweka kipaumbele (tena nacho kidogo tu) kwenye majengo, wanasahau kuboresha nyenzo, hali na taaluma ya walimu na wadau wengine wa elimu.
 
 
Engine ya gari inavyofanya kazi wanaoelezea kitalaamu zaidi na wanaongea English,Sasa mtt akaishia la Saba ama la 11 anataka kujifunza ujuzi wa namna ya engine ya gari ulivyo anaweza akala lecture huko YouTube akapata ufahamu zaidi akichanganya aliyoelezewa aanakuwa very deep in know why/how
Kumbe sio shida lugha, shida mnashindwa kupakia videos ambazo hazipo kwenye lugha yenu, ndio muone mlivyo wazito sasa, mbona kwenye lugha zingine wanazipata.

Kama shida ni lugha hao waliosoma English medium mbona wapo mtaani humu, kama taifa wamelisaidia nini ?

Nchi ngapi hapa Africa wanatumia English kama official language na wamefikia wapi ? [emoji849]
 
Kumbe sio shida lugha, shida mnashindwa kupakia videos ambazo hazipo kwenye lugha yenu, ndio muone mlivyo wazito sasa, mbona kwenye lugha zingine wanazipata.

Kama shida ni lugha hao waliosoma English medium mbona wapo mtaani humu, kama taifa wamelisaidia nini ?

Nchi ngapi hapa Africa wanatumia English kama official language na wamefikia wapi ? [emoji849]
Watuambie Malawi hawa hapo tu.
 
Kiswahili tu tujitenge na dunia,
English tu tuue lugha yetu,
Kiswahili then English (kama ilivyo sasa)cha moto tunakiona.
 
Habari zenu.

Nimekaa hapa nimewaza Ni kwa Nini elimu yetu kingereza kisitumike kuanzia chekechea mpaka elimu ya juu.

Shida Ni Nini yaani Kuna watu wamekaa huko wakaona kuwa maarifa mengi yamevumbuliwa na waswahili ama Ni Nini.

Maarifa mengi mno yapo kwa lugha ya KIENGEREZA.

Mtoto akifika sekondari anaanza KIENGEREZA sio kumtesa hapa Ni Nini Mana anabakia kuumia kwa kukariri. Nawaza Hawa jamaa Wana shule zao hivyo wakiweka English watakosa watoto huko Ni mawazo yangu.

Yaani wakiwa huko kwa Sera na mipango ya elimu wao wanawaza Nini juu ya hili kuwa Kuna changamoto gani mtoto ataipata.

Wengine nadhani mtaongezea na kutoa maoni yenu.

Mie ninavyojua Kama mtoto anajua English anaweza anajifunza na kusoma kitu chochote mtandaoni akajifunza na akakimasta kabisa.

Afrika afrika afrika afrika Tanzania Tanzania Tanzania
Hapana haiwezekani, nchi inahitaji wapagazi kwenye bandari zao, sasa wote tukifunga tai na suti nani atajulikana kuwa si mtoto wa waziri, shukuru na ujivunie lugha yako.
 
Hili naunga mkono 100% .

Cha kujiuluza, hao walimu wa kuwafundusha Kingereza masomo yote , wako wapi?

Labda ndiyi twebde hivyohuvyi bora lenders au na Walimu nao wainguzwe darasani kula wiki siju mija kufundishwa Kingereza jwa somo wanalo fundisha.


Mpangi mwengune nzuri ni u OK e aliokwisha uanzisha Kikwete, Mkonga utumije kufikisha mawasiliano shuke zote, wawe wanasomeshwa kwenye screen jutoka kwa Mwalim mmoja competent kwenye fani yake, walimu mashuleb I n j azu yai itakuwa ni supervision na facilitation.


...naunga mjono hoja
Napendekeza lugha hii ndiyo itumike nchini kote na huyu apate nishani kwa kubuni lugha hii.
 
Habari zenu.

Nimekaa hapa nimewaza Ni kwa Nini elimu yetu kingereza kisitumike kuanzia chekechea mpaka elimu ya juu.

Shida Ni Nini yaani Kuna watu wamekaa huko wakaona kuwa maarifa mengi yamevumbuliwa na waswahili ama Ni Nini.

Maarifa mengi mno yapo kwa lugha ya KIENGEREZA.

Mtoto akifika sekondari anaanza KIENGEREZA sio kumtesa hapa Ni Nini Mana anabakia kuumia kwa kukariri. Nawaza Hawa jamaa Wana shule zao hivyo wakiweka English watakosa watoto huko Ni mawazo yangu.

Yaani wakiwa huko kwa Sera na mipango ya elimu wao wanawaza Nini juu ya hili kuwa Kuna changamoto gani mtoto ataipata.

Wengine nadhani mtaongezea na kutoa maoni yenu.

Mie ninavyojua Kama mtoto anajua English anaweza anajifunza na kusoma kitu chochote mtandaoni akajifunza na akakimasta kabisa.

Afrika afrika afrika afrika Tanzania Tanzania Tanzania
Wazo zuri, ila je walimu hao wa kufundisha kimombo tangu shule ya msingi wapo ?! Walimu wenyewe wa msingi ze... ze... ok... nyingi wazo lako litatimia ?
 
Mbona zipo shule za kiingereza za Serikali nyingi tu ? Mfano kwa Ilala pekeyake kuna shule 9 za kiingereza
 
Nchi ngapi za Afrika zinatumia kingereza lakini bado zipo hoi ?

Afu kule Asia nchi kibao hazitumii kingereza lakini zipo mbali, hata uko ulaya nchi nyingi tu hazitumii kingereza na bado zipo mbali.
Wajuaji Kama nyinyi ndo mmeifikisha hii nchi hapa

Wachina wahindi mpaka leo wanajitahid wakijue kiingereza pamoja na kwamba wameendelea kiiteknolojia,sembuse tz kajamba nani hatuña teknolojia yeyote eti tunajifanya kiingereza sio lazima
 
Wajuaji Kama nyinyi ndo mmeifikisha hii nchi hapa

Wachina wahindi mpaka leo wanajitahid wakijue kiingereza pamoja na kwamba wameendelea kiiteknolojia,sembuse tz kajamba nani hatuña teknolojia yeyote eti tunajifanya kiingereza sio lazima
Mimi nimesema wapi tusijue kingereza ?

Mimi point yangu ni kwenye masomo yawe ya kiswahili na English libakie kama somo.
 
Back
Top Bottom