Kiengereza kitumike shule za umma tokea msingi mpaka chuo

Kiengereza kitumike shule za umma tokea msingi mpaka chuo

Wachina hawahangaiki kujifunza kiingereza tu, mchina anajifunza lugha ya sehemu anayotarget kwenda kama ni ujeruman atajifunza lugha yao kama ni Italy au ufaransa ni hivyo hivyo

Kwa nchi yetu tunahitaji sana kuwa na ujuzi wa lugha zote mbili
Mkuu, una kitu, naishauri serikali ikusikilize na ikupe ulinzi.
 
Kiingereza hakiwezi kutumika vyema kama lugha ya kufundishia kama kiswahili. Sababu ni kuwa siyo lugha ya kila siku ya mtanzania.
Lengo la elimu ni kupenyeza maarifa na ujuzi wa maana akilini ili kuleta tija kwa wanufaika.

Kwa nini Kiswahili & Inglishi visitumike kama sasa, ukaongezwa tu msisitizo na uboreshaji kwenye suala zima la ufundishaji?

Kwa nini visiendelee kutiliwa mkazo katika nyanja zote za elimu tangu awali?

Kwa nini mwalimu asifafanue maana ya atomu au mlango-bahari au nguzo za demokrasia au kazi za ubongo wa mbele au hata athari za biashara ya utumwa, kwa kutumia lugha zote mbili?

Kiswahili kina manufaa mengi sana kitaifa na kimataifa. Inglishi vilevile ina manufaa mengi kitaifa na kimataifa.
 
Kiswahili ni lugha finyu sana. Lugha ya kitumwa na inafifisha akili za watu.
Kiswahili ni lugha pana sema kuna wajinga fulani wamekihusisha na Uislam.

Ukisikia Mswahili, elewa kuwa ni Muislam.
 
Utumwa na ukoloni haujakutoka kichwani, ujerumani wanatumia kiingereza!?..hawana maarifa!?.. kiingereza kiwe somo Kama masomo mengine,boresha walimu wa English,mtu asome mpaka form four,kwisha
Nyie waswahili mmegundua nini Cha kuelezea kwa lugha yenu kwa kiswahili. Usiongee kwa hisia
 
Yaani mtu analipa hela kubwa ishu kubwa Ni English Ila knowledge Ni Ile Ile. So why wasifanye English itumike kwa watoto wetu from chekechea mpaka chuo kikuuu. Hii inawapa hata wepesi wa kuwasiliana fasta na watu wa mataifa mengine,hata Ajira nje Ni rahisi mno mtu kuitafuta ama akiipata lugha sio kikwazo. Kuna wakenya kadhaa manesi wamekosa kazi uk kisa Cha lugha hivi majuzi
 
Kisaikolojia, ni rahisi mtoto mdogo kujifunza lugha yoyote.

Watu wanazidharau hizi English medium za bei nafuu, lakini watoto wanafahamu Kiingereza cha Kitanzania ambacho kinawasaidia wakifika sekondari.

Kamwe, Kiingereza hakiwezi kufafana dunia nzima kwa sababu mbalimbali mojawapo ni kuathiriwa na lugha za wazawa ndio maana kuna East African English, lakini mimi nasema kuna Tanzanian English.

Pamoja na utofauti huu, lakini wanaozungumza Kiingereza kutoka nchi tofauti tofauti wataelewana hivyo hivyo kibishi tofauti na yule ambaye hajui kabisa.
 
Back
Top Bottom