Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

You know the pendullum swings both ways, na kama kuna watu wanafikiria kuna mduara kama huo hapa JF na mimi nachelea kufikiria kuwa akina Yebo Yebo, Kitila Mkumbo, Mtanzania na Kuhani Mkuu nao wako kwenye mduara wa kuendeleza hizi conspiracy theories ili ionekane kuwa Balali aliziiba zile hela na sasa amefake kifo and out of reach na kuwakinga mafisadi halisi ili waendelee kupeta untouched kule bongo.Vipi na ninyi wana JF mmetumiwa na mafisadi, au?

Hili mkuu halina ubishi. Balali yeye ni kinara kabisa wa wizi wetu pale BoT. Swali ni jinsi alivyoshiriki, na hapa kuna scenario mbili ambazo ni: a) yeye alikuwa sehemu ya wale majambazi b) alizidiwa nguvu akawapa funguo na kuwaonyesha majambazi safe la hela zetu yakabeba yeye akibaki ameduwaa na pengine amefungwa kamba.

Hiyo scenario ya pili haina maana tena maana ingekuwa ni hivyo angetuambia baada ya kuondolewa kwenye umateka. Sasa scenario iliyobaki ni hiyo ya kwanza tu. Sasa unless wewe mwenzetu unakataa pia kwamba tuliibiwa hela pale BoT wakati Balali ndiye akiwa mlinzi wetu.

Kwa hiyo kwenye ushiriki wa Balali kuiba zile pesa hakuna conspiracy theory, it is the real thing.
 
Inaonekana kuna kundi limeshaamua kuwa kuna "mduara" wa kudanganya kuhusu ukweli wa kuugua na kufa kwa Balali. Fair enough.

Tunaoamini hivi tunazidi kuongezeka. Huyu hapa mwingine kasema kwenye Rais Mwema. Jina lake ni Padre Karugendo. Hebu naye msome hapa chini.



Kwa hili mimi ni Thomaso

Padri Privatus Karugendo Mei 21, 2008




THOMASO aliishi na Yesu. Yeye kama Mitume wengine alimshuhudia Bwana Yesu akifanya miujiza mbali mbali kama ule wa kugeuza maji kuwa divai, kuponya vipofu na kufufua wafu. Yesu, alipomfufua Lazaro, alikuwa na mitume wake.

Ni wazi Thomaso naye alishuhudia muujiza wa Lazaro. Pamoja na kushuhudia miujiza yote hiyo, iliyoonyesha kwamba Bwana Yesu hakuwa mtu wa kawaida, bado Thomaso hakuamini ufufuko ya Yesu, mpaka pale alipougusa mwili ya Yesu na kushuhudia makovu kwenye mikono na ubavuni.

Wanateolojia, wanasema alikuwa na imani haba. Imani ya kuamini baada ya kuona! Tunaambiwa kwamba ana heri mtu yule anayeamini bila ya kuona! Lakini enzi hizi za sayansi na teknolojia, ni vigumu kabisa mtu kuamini bila ya kuona.

Mimi pia kwa hili la kifo cha Dk.Ballali, nina imani haba! Nilipata habari za kifo cha Dk. Daudi Ballali, nikiwa vijijini Karagwe. Nimeshuhudida jinsi watu wanavyofuatilia kwa karibu kila tukio. Kusema ukweli wana uchungu mkubwa juu ya wizi uliotokea Benki Kuu (BoT).

Maisha yanavyozidi kuwa mgumu, ndivyo wanavyolaumu viongozi wanaopora mali ya Taifa. Sasa hivi mafuta ya taa yamepanda bei, ni machungu kwa kila mtu kule vijijini. Hivyo habari za kifo cha Dk. Ballali, wamezipokea kwa uchungu mkubwa. Walitaka arudi akiwa mzima, asaidie kurudisha fedha zao zilizoporwa. Ingawa kule vijijini watu wameonyesha kukiamini kifo cha Dk. Ballali, mimi nimekuwa Thomaso! Rafiki yangu mmoja nilipomtumia ujumbe juu ya imani yangu haba kwa kifo cha Dk. Ballali alinishauri niachane na Uthomaso.

Anataka niamini kwa kusikia na labda kwa vile Serikali imetoa tamko na kututangazia kifo hicho. Lakini kwa hili kwangu inakuwa vigumu kuuvua Uthomaso. Ni lazima nione, nihakikishe ndipo niamini. Hata wakionyesha picha za Dk. Ballali akiwa kwenye jeneza bado sitaamini kifo hiki, hata nikionyeshwa picha za mazishi yake akiingizwa kaburini kule Marekani sitaamini, mpaka pale nitakapoambiwa kwamba DNA imechukuliwa na kupimwa na kuhakikisha kwamba huo ni mwili wa Dk. Ballali. Katika hali hii, inawezekana wakatengeneza kitu tu na kukipachika picha ya Dk. Ballali, ili tuaamini kwamba amekufa, na maisha yakaendelea kama kawaida.

Watanzania tumejijengea utamaduni wa kushangaza kabisa. Utamaduni wa kutofuatilia kitu hadi mwisho wake. Hata kabla ya kutangaza kifo cha Dk. Ballali, tulikuwa tumeliacha hili na kuanza kufukuzia mengine, ambayo nayo ni wazi tungeyaachia njiani! Sasa nguvu zote zimewekwa kwa Rais mstaafu Benjamin Mkapa na Kura za maoni kule Zanzibar.

Tunafanana na mbwa anayefukuza gari, likisimama zaidi anachoweza kufanya mbwa ni kulikojolea gari na kuendelea na safari zake. Zile hasira anazokuwa nazo mbwa wakati akilifukuza gari, likisimama zinayeyuka. Kuna orodha ndefu ya mambo yasiyokwenda sawa, lakini wakati ukipita, tunasahau kabisa.

Sasa kwa vile tumetangaziwa kifo basi ndiyo tutazika kila kitu kuhusu kashfa ndani ya BoT.

Uwezekano wa yeye kuendelea kuishi ni mkubwa sana. Fedha zinazongumzwa katika wizi wa BoT ni nyingi. Kama alikuwa na fedha nyingi kiasi hicho, ujumbe ni kwamba anaweza kuendelea kuishi popote hata baada ya "kifo" chake. Baada ya Hitler kushindwa vita, wafuasi wake walitangaza kifo chake. Hakuna aliyeiona maiti ya Hitler wala kaburi lake. Kuna walioendelea kuamini kwamba Hitler, alijificha Marekani Kusini na akaendelea kuishi hadi miaka ya karibuni!

Imani yangu haba juu ya kifo hiki inasababishwa na maswali mengi juu ya kashfa ya BoT ambayo hayana majibu. Huko nyuma tuliambiwa kwamba Serikali, haifahamu kabisa Dk. Ballali amelazwa hospitali gani. Ingawa wakati anaondoka alikuwa Gavana wa BOT, aliaaga na kupewa ruhusa na kuna ushahidi kuonyesha kwamba kabla hajafukuzwa kazi, alikuwa na mawasiliano na ofisi yake.

Tulisikia kwenye vyombo vya habari kwamba alimwandikia Rais Jakaya Kikwete, barua ya kutaka kujiuzulu nafasi yake maana afya yake ilikuwa mbaya. Kama barua hiyo ilimfikia Rais, ni wazi kulikuwa na mawasiliano. Karibuni zaidi Serikali ilisema haimuhitaji, kwamba siku ikimuhitaji kumpata si kazi kubwa. Juzi tu, vyombo vya habari vimetangaza kwamba sasa makachero wa Tanzania, wametumwa kwenda kumtafuta. Hazikupita hata siku tano, tukasikia habari za kifo cha Dk. Ballali na kwamba alikufa Mei 16,2008.

Taarifa ya Serikali ya kifo hicho ilitanguliwa na habari zilizotoka magazetini. Kwa maneno mengine, ni kama Serikali imeshinikizwa na taarifa za magazeti kutangaza kifo cha Dk. Ballali.

Inakuwa vipi mtu kama Dk. Ballali, afe, zipite siku kama nne, bila habari kuvuja? Tuliambiwa alikuwa akitibiwa kwa fedha za Serikali. Hii ina maana hospitali, ilikuwa kiwasiliana na Serikali ya Tanzania. Hivyo kifo chake kingejulikana haraka. Pia sina imani kwamba hospitali hiyo haikuwa na mtu kutoka Tanzania au Afrika. Habari zake zimeandikwa kwenye magazeti mengi ya nje na ziko kwenye mtandao. Picha yake imezagaa kwenye magazeti na kwenye mtandao. Hivyo habari za kufa kwake zisingechukua muda mrefu kujulikana.

Binafsi sikutaka Dk. Ballali afe. Nina imani kwamba Watanzania wenye uchungu na Taifa hawakutaka mtu huyu afe. Tulitaka aje ajibu maswali. Tulitaka kujua jinsi fedha za EPA, zilivyochotwa, tulitaka kufahamu ukweli wa fedha hizi kuingizwa kwenye kampeni ya CCM. Tulitaka kujua mambo mengi yanayohusu BOT, hasa ujenzi wa jengo la BOT, ambao hadi leo hii umeleta utata mkubwa.

Nashawishika kuamini kwamba kuna maelewano ya aina fulani kati ya Serikali na familia ya Dk. Ballali. Wamekubaliana kutangaza kifo, ili Dk. Ballali, aishi kwa amani nje ya nchi bila kusumbuliwa na baadhi ya viongozi wa Serikali walioshiriki kupora fedha za EPA, waishi kwa amani?

Je, wale makachero waliotumwa kumtafuta Dk. Ballali, ndio wamekula njama za kutangaza kifo chake baada ya kukutana naye? Je, Serikali imeamua kufanya mchezo huu mchafu? Hili linawezekana? Ukitafakari kwa undani – unagundua kwamba kama Dk. Ballali, angehojiwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria mambo mengi yangefumuka na kuiweka Serikali kwenye wakati mgumu?

Nimesikia kwenye vyombo vya habari kwamba dada zake wanaomba au wameombewa ulinzi, kwa maana eti wana wosia mzito! Kwamba baadhi ya viongozi wanaohisi kutajwa kwenye wosia huo wanaweza kutishia maisha ya dada hawa.

Sina imani kama kuna wosia mzito kutoka kwa Dk. Ballali. Kama upo, basi huu ni ushahidi kwamba muda wote huo alikuwa na akili timamu, na angeweza kuhojiwa akiwa bado hai. Vinginevyo wosia huo ni mkakati mzima wa familia na Serikali kutaka kutufumba macho.

Mtu anaweza kujiuliza swali ni kwa nini mtuhumiwa aliachiwa kuwa huru wakati wote huo? Kwa nini, hata kama alikuwa hospitalini, hakuwekwa chini ya ulinzi? Kama Rais Kikwete, alifikia hatua ya kutengua uteuzi wake ni kwamba kulikuwa na ushahidi wa kutosha juu ya shutuma zilizokuwa zikitajwa juu yake. Na hii ilitosha kwa Rais kutoa agizo la mtu huyu kukamatwa na kurudishwa nchini kwa mahojiano.

Rais, angeagiza mali zake zote zikamatwe. Kwa kifo chake, mali zote zitaendelea kumilikiwa na ndugu na jamaa zake. Kwa nini mali hizi zilizopatikana kwa kupora, ziendelee kuwa chini ya urithi wa Dk. Ballali? Ni vigumu kumshitaki marehemu. Lakini kama angezikwa hapa Tanzania, nina imani vizazi vijavyo wangeifukua mifupa yake na kuishitaki.

Labda wakati makala hii inatoka, tutakuwa tumeonyeshwa picha za mazishi ya Dk. Ballali, lakini kama nilivyosema hapo juu, mimi ni Thomaso. Bila vipimo vya kuhakikisha kwamba aliyekufa ni Dk. Ballali, sintaamini kifo hiki na bado nitaendelea kuiomba Serikali imkamate na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria!

Mwandishi wa makala hii anapatikana kwa S. L. P. 114 Magu, Mwanza. Simu: 0754 633122


Source ya makala hii ni hii hapa: http://www.raiamwema.co.tz/08/05/28/karugendo.php
 
4. Balali and his wife Anna Muganda, maintain foreign bank accounts, houses
and property along side Vimal Mehta, Jeetu Patel and Don Andy in
Switzerland, London, Dubai, and Mauritius.

Serengeti Breweries Ltd. Factory was bought with stolen tax payers VAT
money from 1994. Currently making claims of investing millions in Tanzania.
Source of funds is Bank of Tanzanias Foreign Debt Service Account

Sanjay Mehta& Ajay Mehta: Capo Bastones. Brothers of Vimal
Mehta who are all managing different businesses which have stolen estimated
funds of USD 285 million from Government of Tanzania since 2002 and USD 25
Million in 1992-1 995 period.
Bank M: Recently licensed by Bank of Tanzania without proper procedure. The
owners of the Bank are Jeetu Patel, Daudi Balali through an
offshore company, Vimal Mehta, Sanjeev Kumar, Bhasker Narayanan, Anna
Muganda. See section on Bank M for detail
JMushi1
Do you believe everything you read on the internet? Do you know who wrote and distributed that e-mail. Do you have any evidence that what is written in the e-mail is true? Do you know an Indian by the name of Ladwa?
Do you know of his relationship/non relationship to Jeetu Patel?
Can you give us the addresses of the houses that the late Balali and his wife maintains in Switzerland, London, Dubai and Mauritius?
 
Kitila,'
Hiyo ya Karugendo niliisoma juzi. Jibu langu kwake ni sawa na lile kwako. Huyu kasoma JF kapata idea ya kuandika article. Fine! Ongezekeni tu. Hata wale waliomchagua Barabas walikuwa majority.
 
Mkuu Jasusi,

Heshima mbele naomba tu mkuu utuachie hii kitu for now, sidhani kama ninakuomba too much, please tuachie sisi hii mkuu tumeongea ya kutosha sisi ni watu wazima ni wakati sasa wa kupunguza moto,

tutayamaliza haya, yaliyosemwa yametohsa, wewe sasa mkuu tuachie imetosha, ni kawaida kwenye vichwa kama hapa kuwa na malumbano ila binafsi ninajaribu kuelewa the agony, please let it go

Wakuu wengine naomba tu-take a time out kidogo, mkuu Invisible sijui kama kuna ubaya ukiisimamisha hii kwa muda ili tupunguze munhali!

ni ombi tu na ushauri wa bure kwa wote, ahsante wakuu! yote tumeyasikia kila mmoja ni kweli ana hoja nzito, tunkaribia kufarakana hapa kwa sababu ya taifa inakubalika, ninaomba tena wakuu tupumzike kidogo, mimi binafsi nimenawa mikono kwa sasa nitarudi hii topic ikiwa na kichwa kingine lakini sio kifo tena unless kukiwa na news!
 
Kitila Mkumbo,

Mkuu navyofahamu mimi wewe ni mwanasiasa na umesoma yaani una elimu ya darasa, hivyo ni mategemeo yangu utakuwa mbele zaidi ya watu kama hawa kia Karugendo maadam kasema yeye ni Padre hana jipya!..

Kwa lugha fupi mnaturidisha kule kule tulikotoka, na nadhani wanaojenga mduara ni kina nyie hapo ambao kwa kila hoja yenu swala la EPA limekuwa secondary kwenu isipokuwa Balali ambaye toka ameondoka mwaka jana hakuwa muhimu isipokuwa baada ya kifo chake, almost 1 year have passed.
Kwa maelezo kama ya huyu Padre:-
Ni lazima nione, nihakikishe ndipo niamini. Hata wakionyesha picha za Dk. Ballali akiwa kwenye jeneza bado sitaamini kifo hiki, hata nikionyeshwa picha za mazishi yake akiingizwa kaburini kule Marekani sitaamini, mpaka pale nitakapoambiwa kwamba DNA imechukuliwa na kupimwa na kuhakikisha kwamba huo ni mwili wa Dk. Ballali. Katika hali hii, inawezekana wakatengeneza kitu tu na kukipachika picha ya Dk. Ballali, ili tuaamini kwamba amekufa, na maisha yakaendelea kama kawaida

Sasa kama ukweli wenyewe unatakiwa kwa nguvu hizo kweli hii tutafika? Kama hamuamini kafa sasa DNA ya nini ikiwa mtu huyo ni mzima na nani anajua kuisoma hiyo DNA! kamba si bado zitaendelea? Na kuna sheria gani inayowalazimisha familia ya marehemu kutimiza hayo kuridhisha baadhi ya watu ambaop hawataki kuamini...
Hata hivyo ikisha bainika kweli ni yeye mtafanya nini? au akiwa sii yeye mtafanya nini maanake kila kitu ni hatua.. nini hatua yenu baada ya kuthibitisha..Oooh samahani kabla ya yote hayo mnataka nini kifanyike sasa hivi..Kuundwa kwa kamati nyingine ya kuchunguza kifo au sio?... swala la EPA ambalo report yake imetoka inakaribia mwaka sasa liwekwe kando kwanza!
Unajua Kikwete kisha wajulia sana na kawapateni anapotaka... mtaundiwa kamati, majibu yatakuja kwake kwanza na baada ya hapo yatalala kwa miezi sita kwisha yaende bungeni ambako Sitta atakataa kuyazungumzia na kadhalika.
Hivi kwa kuuliza kwenu hamuoni kama mnawajengea CCM kibanda cha kuficha mengine yote!..Na jinsi navyoiona picha hata swala la EPA bungeni limepata nafasi ya kuulizwa wabunge kuwa Balali hayupo sasa hili swala tutalimaliza vipi bila shahidi muhimu kuwepo!..wao wataendelea kudai hawajui aliko wala hawakupata nafasi ya kuona maiti, wakati hao hao walitueleza mwanzo kuwa amekufa nasi hatukukubali. Hivyo interest za wananchi zinatangulia kwanza.
Mkuu jengeni hoja zenu kwenye issue ya EPA kama ilivyo wakilishwa na kama ikibidi muufikishe ujumbe kwa wananchi kuwa serikali imekataa katakata kuwachukulia hatua mafisadi (Wahujumu) basi na iwe kwa maandamano makubwa kila mkoa!...msicheze mchezo wa CCM hata kidogo never intertain that crap!
Bila woga kwa mara ya kwanza watajeni majina wahusika wote... liwe na liwe tuone kama watawafungulia mashtaka mahakamani, hapo mtawaita wakaguzi wa Ernst and Young kutoa ushahidi..Sijui nao watawaficha ama kuwaua...
 
breaking news - - - - - - - - - hillary wins puerto rico ! (ballali ameshatangulia mbele ya haki jamani)
 
Mtanzania,

Heshima mbele mkuu, muache Jasusi, tuendele sisi wengine mkuu sidhani kama it too much to ask, ninajua kuwa wewe ni mstaarabu badala yake nitwange mimi ikiwezekana, leave the man alone please!

Mkuu FMES,

Lengo langu kwenye mjadala huu si kumuudhi mtu yeyote wala sidhani kama kuna mtu hapa JF anaweza kusema nimemshambulia yeye binafsi ukiachia hao Ballali na mkewe ambao naamini ni mafisadi hivyo wanastahili nguvu zote za JF.

Tumejibizana na Jasusi lakini sio kwa lengo la kukashifiana bali kuelemishana.

Hapa JF wote tunaowajadili wana ndugu, wana baba, wana watoto, wana wajomba na wana mashemeji. Maana ya kumkoma nyani geledi, usemi ambo wewe ni mwanzilishi, una maana kubwa zaidi. Tukianza kuangaliana usoni kabla ya kujenga hoja, JF itapoteza mwelekeo.

Kwenye hili lengo ni Ballali kwahiyo kama kuna ndugu hapa inabidi waelewe kwamba hatutaacha kumjadili Ballali ambaye sisi wengine tunaamini ni jambazi ambaye amepora mali ya Watanzania kwa kushirikiana na majambazi wenzake. Kama mambo ni too hot basi watupishe jikoni kwa muda.

Nimesikia ushauri wako na mashambuli yangu yote yataelekezwa kwa the fugitive "Ballali" pamoja na mafisadi wenzake. Jasusi, samahani kama maandishi yangu yoyote yamekuudhi, tuko kazini mzee wangu, kutetea nchi yetu Tanzania.
 
Kitila Mkumbo,

Mkuu navyofahamu mimi wewe ni mwanasiasa na umesoma yaani una elimu ya darasa, hivyo ni mategemeo yangu utakuwa mbele zaidi ya watu kama hawa kia Karugendo maadam kasema yeye ni Padre hana jipya!..

Kwa lugha fupi mnaturidisha kule kule tulikotoka, na nadhani wanaojenga mduara ni kina nyie hapo ambao kwa kila hoja yenu swala la EPA limekuwa secondary kwenu isipokuwa Balali ambaye toka ameondoka mwaka jana hakuwa muhimu isipokuwa baada ya kifo chake, almost 1 year have passed.
Kwa maelezo kama ya huyu Padre:-

Sasa kama ukweli wenyewe unatakiwa kwa nguvu hizo kweli hii tutafika? Kama hamuamini kafa sasa DNA ya nini ikiwa mtu huyo ni mzima na nani anajua kuisoma hiyo DNA! kamba si bado zitaendelea? Na kuna sheria gani inayowalazimisha familia ya marehemu kutimiza hayo kuridhisha baadhi ya watu ambaop hawataki kuamini...
Hata hivyo ikisha bainika kweli ni yeye mtafanya nini? au akiwa sii yeye mtafanya nini maanake kila kitu ni hatua.. nini hatua yenu baada ya kuthibitisha..Oooh samahani kabla ya yote hayo mnataka nini kifanyike sasa hivi..Kuundwa kwa kamati nyingine ya kuchunguza kifo au sio?... swala la EPA ambalo report yake imetoka inakaribia mwaka sasa liwekwe kando kwanza!
Unajua Kikwete kisha wajulia sana na kawapateni anapotaka... mtaundiwa kamati, majibu yatakuja kwake kwanza na baada ya hapo yatalala kwa miezi sita kwisha yaende bungeni ambako Sitta atakataa kuyazungumzia na kadhalika.
Hivi kwa kuuliza kwenu hamuoni kama mnawajengea CCM kibanda cha kuficha mengine yote!..Na jinsi navyoiona picha hata swala la EPA bungeni limepata nafasi ya kuulizwa wabunge kuwa Balali hayupo sasa hili swala tutalimaliza vipi bila shahidi muhimu kuwepo!..wao wataendelea kudai hawajui aliko wala hawakupata nafasi ya kuona maiti, wakati hao hao walitueleza mwanzo kuwa amekufa nasi hatukukubali. Hivyo interest za wananchi zinatangulia kwanza.
Mkuu jengeni hoja zenu kwenye issue ya EPA kama ilivyo wakilishwa na kama ikibidi muufikishe ujumbe kwa wananchi kuwa serikali imekataa katakata kuwachukulia hatua mafisadi (Wahujumu) basi na iwe kwa maandamano makubwa kila mkoa!...msicheze mchezo wa CCM hata kidogo never intertain that crap!
Bila woga kwa mara ya kwanza watajeni majina wahusika wote... liwe na liwe tuone kama watawafungulia mashtaka mahakamani, hapo mtawaita wakaguzi wa Ernst and Young kutoa ushahidi..Sijui nao watawaficha ama kuwaua...

Hata USA walijua watu hawataamini waliokufa ni watoto wa Saddam, wakaprove kwa DNA.

Palipo na utata njia pekee ya kuondoa utata ni kupenyeza facts.

Katika maisha yangu yote nimegundua palipo na usiri panaongozana na udanganyifu. Kama mtu hutaki kudanganya usiri wa nini?

Hata wanasiasa wanapoona wataongea ukweli hujitahidi hata ku encourage waandishi kuuliza maswali, lakini wanapoficha mambo utaona majibu yao yalivyo mafupi na ya kujiuma uma.

Uwezo wa kuwafungulia mashitaka watuhumiwa ni wa serikali, wajibu wetu sisi kama raia ni kupiga kelele na kuwaadhibu hao wanasiasa watakaoshindwa kutimiza wajibu wao hapo 2010.

Mimi naamini kwa kuuliza kwetu, tunafunua njama za Ballali na hao CCM za kutaka yaishe, eti amekufa basi yaishe. Ukiiba vya wananchi jua tutakuandama mpaka huko makaburini.

Hapa anayekubaliana na CCM ni wewe, ndio uko kundi moja na Kada Mpinzani kusema yaishe, tumwache Ballali apumzike. Angalia list ya unaokubaliana nao kwenye hili, ni JK, Pinda, Warioba, Mama Simba, Rostam nk. Sasa niambie kwenye mjadala huu nani anatetea maslahi ya CCM?
 
Mkandara,

Nakusikia. Hii issue imezidi kiwango cha kawaida cha usomi na uanasiasa. Maana kama ni usomi ndo huko kujenga scenario, research na kutengeneza jumuisho. Sasa scenario zote na tafiti zilizofanyika, ikiwemo waliokwenda kuaga mwili, hazitupeleki kuthibitisha kwamba Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania Dk Balali kweli amefariki. Kwa hiyo kilichobaki pekee hapa cha kutumia katika kukubaliana kuwa Balali yu hai au kafariki ni imani, na hapa ndipo akina Karugendo wanapoingia. Panapokuwa hakuna ushahidi wa kuthibitisha au kukanusha jambo usomi huwa hauwezi tena kutumika maana usomi na imani haviendani!

Hakuna hata siku moja ambapo relevance ya Balali katika EPA imewahi kuwa underestimated. Balali was and remains a key player kwenye hii saga ya EPA na ndio maana wakubwa walikuwa wanahangaika kumtafuta na kutumana huko US usiku na mchana.

Kwangu mimi sasa hivi hapa ni kutoa hasira tu. Najua kabisa sasa kwamba madamu Balali kafariki au kapotezwa, kamwe hatuwezi kujua ukweli kuhusu majambazi walioiba zile pesa pale BoT na wala issue ya EPA haiwezi kuwa na maana tena. Kwa maana ingine kufariki au kupotezwa kwa Balali ilikuwa ni silaha ya mwisho ya mafisadi ambayo sasa wameipata na huko waliko wanacheza na kusherehekea kwa kutumia sehemu ya fungu waliloiba. Ni kwa sababu hii ninalazimika kuwasuta wanaotaka kutudanganya kwamba ukweli utaanikwa hivi karibuni. Madamu walishindwa kutupa ukweli Balali akiwepo hakuna ukweli tena. Haya ndiyo maneno waliyoyasema baada ya dada yetu Amina kufariki ili kutupoza, lakini tunajua kwamba hiyo ndiyo imeshatoka hiyo. I hope unaweza kuelewa kwa nini katika hili jambo hasira zimetawala kuliko kitu kingine chochote.
 
Mkandara,

Unajua kwamba kwenye haya ya Ballali, Jaji Warioba ni katika wale ambao wangeumbuliwa kwenye Meremeta? Ana kila haki ya kusema tumwache apumike salama. Wako wengi kwenye hilo kundi.

Mtanzania,

Angalia habari vizuri....Jaji Warioba hahusiki, hajawahi kuhusika wala kuhusishwa na Meremeta....naamini amejisemea kama private citizen na sio kama mtu mwe masilahi binafsi na kifo cha marehemu Balali!
 
Mtanzania,

Angalia habari vizuri....Jaji Warioba hahusiki, hajawahi kuhusika wala kuhusishwa na Meremeta....naamini amejisemea kama private citizen na sio kama mtu mwe masilahi binafsi na kifo cha marehemu Balali!

Kigoma,

Fuatilia hili na unaweza kutafuta hata hapa JF maana tulishajadili hili jambo.

Jaji Warioba ni katika wahusika wa Meremeta & Mwananchi, ndio maana wengine tungetaka uchunguzi huu uwe mkubwa zaidi na uchunguze pesa zote zilizochotwa BOT na kupewa wanasiasa. Wapo wengi kwenye kundi.

Nakushauri fuatilia, ukishindwa nijulishe, nitakusaidia.

Soma hii link: http://www.klhnews.com/index2.php?option=com_docman&task=doc_view&gid=10&Itemid=85

http://www.thisday.co.tz/News/403.html

JF ni jungu kuu, ukiona watu tunaandika jua kuna ushahidi.
 
Mmoja wa wanasiasa wakongwe nchini, Jaji Joseph Warioba akizungumzia kifo hicho cha Dk. Ballali wiki hii, ameiambia Raia Mwema kwamba anaona unafiki wa hali ya juu katika matamshi na matendo ya wanasiasa.
“Huu ni unafiki mkubwa. Muacheni Ballali apumzike kwa amani. Kwanza walimwita ni fisadi, sasa wanasema shahidi muhimu amekufa. Katoka kuwa fisadi wakati wa uhai kuwa shahidi katika mauti,” alisema Warioba katika mahojiano ya simu mwanzoni mwa wiki hii.
Aliongeza Warioba: “Amekuwa kafara. Taarifa ya Serikali kuhusu fedha za EPA ilionyesha wazi Ballali amechukuliwa hatua katika utaratibu wa kawaida wa kuwajibika. Haikumtuhumu kwamba alikuwa ameiba fedha. Fedha zile bilioni 133 ni jumla ya fedha zote zilizochukuliwa na kampuni 22 zilizotajwa katika taarifa ya Serikali.
“Ballali hakutajwa katika orodha ya kampuni hizo. Hilo Serikali inajua, viongozi wa siasa wanajua na vyombo vya habari vinajua. Lakini wote hao, kwa kipindi chote alichokuwa hai walimhukumu kama mtu aliyekuwa ameiba fedha. Lakini waliochukua fedha zile wanafahamika.
“Kwa muda wa miezi mitano Kamati (ya uchunguzi wa kashafa ya EPA) imekuwa ikiwaambia wananchi inakusanya fedha hizo kutoka kwa watu wanaoitwa. Ilipoulizwa kuhusu Ballali ilisema haimuhitaji. Maana yake hakuwamo katika orodha ya waliochukua fedha zile. Lakini sasa amefariki wimbo umebadilika. Wanasiasa na vyombo vya habari vinamwita si fisadi tena, bali shahidi muhimu wa wizi wa EPA.
“Huu ni unafiki mkubwa. Kuna visingizio kwamba ugonjwa wa Ballali haujulikani, lakini Serikali inajua kwani alikuwa analipiwa matibabu na Benki Kuu. Alikuwa Boston, Marekani, ile nchi iko wazi mtu angetaka kujua angejua. Lakini sasa wanasiasa na vyombo vya habari vinalalamika kwamba ugonjwa wake ulifanywa siri. Kumbe ni uzembe wao.
“ Sasa tumeanza kutafuta mchawi huku. Na hapa ikisha kutamkwa neno fisadi tu, basi hata kama mtu hana ushahidi unakuwa fisadi. Lakini yote haya hakuna anayekuambia Ballali aliiba kiasi gani. Wamuache apumzike kwa amani, siku moja ukweli utafahamika.”


Mheshimiwa Warioba, sikiliza Mzee!

Marekani ni nchi ya wazi, ni kweli, lakini mtu baki yeyote huwezi kuambiwa habari zozote za mgonjwa. Ndo maana hakuna aliyejua afya ya mgombea John McCain mpaka wiki iliyopita alipotoa health report yake. Vinginevyo daktari hawezi kusimama jukwaani akasema 'mgonjwa wangu Ballali ana Ukimwi ...amelazwa hospitalini kwangu chumba namba tisa!" Hapo umechemsha!

Pili, unasema hela za EPA zote zililipwa kwa makampuni ambayo siyo ya Ballali, na kwa mtaji huo, Ballali hakuwa fisadi. Wewe ulikuwa Mwanasheria wetu mkuu, na leo ni Jaji wa Kimataifa, utajifanye hujui kitu kinachoitwa "kickback"? Ballali analipa fedha za EPA kwa kampuni X, inayomilikiwa na ndugu Y, halafu Y anakuja kumpoza Ballali pembeni bila kuacha fingerprints kwenye makaratasi. Mzee Warioba hiyo concept huijui, au unataka kufanya wenzio wajinga kwa sababu umepata bullhorn ya Raia Mwema unakozungumza bila kuswalishwa?

Tatu, unasema Ballali aachwe apumzike kwa amani, halafu hapo hapo unasema siku moja ukweli utajulikana. Ukweli utashuka wenyewe kama mvua za masika kutoka mbinguni? Si ndo maana watu wanachunguza? Na kuna ubaya gani unapofanya uchunguzi ukamhusisha aliyekuwa anatunza ufunguo sehemu ujambazi ulipotokea bila kufuli kuvunjwa? Ndio hivyo ulivyo kuwa unaendesha Wizara ya Sheria? Warioba hata wewe unachemsha hivi?

Nne, unadai Serikali inajua ugonjwa kwa sababu walilipia gharama. Hilo tunalijua, ni Kisukari tuliambiwa. Mbona husemi kuhusu Hospitali? Au Ballali alipewa hela taslimu akaambiwa kajitibie kokote, zitakazobaki turudishie chenji? Na zikipungua tuma ki-memo tukuongezee? Hospitali haitumi bili? Si ndio ufisadi huo tunaoungelea. Na wewe si hivi karibuni umekuwa ukikemea ufisadi, sasa tukueleweje we Mzee unapoongea kutoka pande zote mbili za mdomo wako? Ni hospitali gani hiyo waliyo ilipa lakini hawaijui, kama sio ya Profesa Maji Marefu?

Credentials za huyu Mzee Warioba ni za Mwanasheria Mkuu, na Jaji wa Kimataifa, na Waziri Mkuu, na Waziri wa Sheria, na Makamu wa Rais wa Jamhuri. Na bado anachemsha hivi. Unadhani kuna matumaini Tanzania?
 
Kitila Mkumbo,

Mkuu navyofahamu mimi wewe ni mwanasiasa na umesoma yaani una elimu ya darasa, hivyo ni mategemeo yangu utakuwa mbele zaidi ya watu kama hawa kia Karugendo maadam kasema yeye ni Padre hana jipya!..

Kwa lugha fupi mnaturidisha kule kule tulikotoka, na nadhani wanaojenga mduara ni kina nyie hapo ambao kwa kila hoja yenu swala la EPA limekuwa secondary kwenu isipokuwa Balali ambaye toka ameondoka mwaka jana hakuwa muhimu isipokuwa baada ya kifo chake, almost 1 year have passed.
Kwa maelezo kama ya huyu Padre:-

Sasa kama ukweli wenyewe unatakiwa kwa nguvu hizo kweli hii tutafika? Kama hamuamini kafa sasa DNA ya nini ikiwa mtu huyo ni mzima na nani anajua kuisoma hiyo DNA! kamba si bado zitaendelea? Na kuna sheria gani inayowalazimisha familia ya marehemu kutimiza hayo kuridhisha baadhi ya watu ambaop hawataki kuamini...
Hata hivyo ikisha bainika kweli ni yeye mtafanya nini? au akiwa sii yeye mtafanya nini maanake kila kitu ni hatua.. nini hatua yenu baada ya kuthibitisha..Oooh samahani kabla ya yote hayo mnataka nini kifanyike sasa hivi..Kuundwa kwa kamati nyingine ya kuchunguza kifo au sio?... swala la EPA ambalo report yake imetoka inakaribia mwaka sasa liwekwe kando kwanza!
Unajua Kikwete kisha wajulia sana na kawapateni anapotaka... mtaundiwa kamati, majibu yatakuja kwake kwanza na baada ya hapo yatalala kwa miezi sita kwisha yaende bungeni ambako Sitta atakataa kuyazungumzia na kadhalika.
Hivi kwa kuuliza kwenu hamuoni kama mnawajengea CCM kibanda cha kuficha mengine yote!..Na jinsi navyoiona picha hata swala la EPA bungeni limepata nafasi ya kuulizwa wabunge kuwa Balali hayupo sasa hili swala tutalimaliza vipi bila shahidi muhimu kuwepo!..wao wataendelea kudai hawajui aliko wala hawakupata nafasi ya kuona maiti, wakati hao hao walitueleza mwanzo kuwa amekufa nasi hatukukubali. Hivyo interest za wananchi zinatangulia kwanza.
Mkuu jengeni hoja zenu kwenye issue ya EPA kama ilivyo wakilishwa na kama ikibidi muufikishe ujumbe kwa wananchi kuwa serikali imekataa katakata kuwachukulia hatua mafisadi (Wahujumu) basi na iwe kwa maandamano makubwa kila mkoa!...msicheze mchezo wa CCM hata kidogo never intertain that crap!
Bila woga kwa mara ya kwanza watajeni majina wahusika wote... liwe na liwe tuone kama watawafungulia mashtaka mahakamani, hapo mtawaita wakaguzi wa Ernst and Young kutoa ushahidi..Sijui nao watawaficha ama kuwaua...

Mkandara,

Huu msisimko wa kutaka kujua Ukweli kama Ballali amekufa au yuko hai, kunatufanya tuonekane mabwege.

Ubwege wetu ulikuwa ni pale tulipoanza kutoa tuhuma, tukadai tuna ushahidi, kisha baada ya kelele nyingi tukatoa mkataba kwa wakaguzi wa mahesabu E&Y wafanye uchunguzi, wakatoa hitimisho na taarifa ambazo tulipewa nusu nusu, kisha Ikulu wakaunda kamati ya Raisi kuchunguza kile kile kilichofanywa na Deloitte Touche na E&Y na wafanye mchakato wa kuchukua hatua za kisheria.

Laiti kama tungeishupalia Serikali itoe ripoti ya Deloitte Touche na E&Y hadharani kama tunavyoshupalia Serikali na familia ya Ballali itoe ukweli kuhusu mahali alipo/alipokuwa, kufa au kuwa hai basi tusingepoteza muda na kugundua baada ya kuambiwa Ballali amekufa tunajikanganya kwa udhaifu wetu wa kikatiba na kisheria kuachia suala zima la EPA, na hata Meremeta na Tangold yaonekane kama kichekesho.

Kosa tulilolifanya na mapungufu ya kuamini tutalisawazisha kwa kupata Ukweli tukijua Ballali alipo (hai au mfu),ni kushindwa kuiwajibisha Serikali ambaye ni mdhibiti mkuu wa fedha za Taifa.

As far as I am concerned, Ballali alifukuzwa kazi kwa Uzembe, ndio maana hata barua yake ya kujiuzulu ilikataliwa. Sasa wakumfuata na kumkaba koo si Ballali tena bali ni Serikali ambayo ilionelea ni vema kumfukuza kazi na hata kutomtafuta au kutoa hati ya kutaka akamatwe kwa tuhuma za uzembe, ubadhirifu na hata uhujumu.

Let say Ballali hakuiba na alishinikizwa kuruhusu malipo ambayo ni kinyume cha taratibu, je huko aliko akituambia alilojua ambalo aliwaambia wabunge na Takukuru tutapata majibu ya kuridhisha?

Lengo letu kumtafuta Ballali na kumtaka aongee ni ili tumfunge kitanzi au kuwapata wale waliompa amri?

Kama ni wale waliompa amri, kwa nini hatuwafuati sasa hivi na kuwahoji ilikuwaje nao wakazembea kukagua vitabu vya mahesabu ya BOT na kugundua kuna mmomonyoko wa maadili ya kimahesabu na uhasibu na kuwa Ballali kaidhinisha hujuma?

Je serikali mpya ilipokuja madarakani 2006 wakagundua kuna walalakini katika mambo ya fedha kama Mama Meghji alivyotamka kuwa mambo ni dole na baadaye kutamka alidanganywa na Ballali, kwa nini Serikali haikumchukulia Ballali hatua za kinidhamu na hata sheria ilipobainika kuwa kuna uhujumu?

Hivi tukifukua maiti ya Ballali na kufanya DNA na kujua ni kweli ni Ballali na tukagundua kuwa alikufa kwa sumu mfano ile Pollonium 210, what will be our next step? obvious itakuwa ni kutafuta aliyemuua, at the same time uchunguzi wa EPA, Meremeta na Tangold unawekwa kando, focus inakuwa ni Ballali!

Does this make any sense? Je if Ballali is alive and was involved or he is dead and was never involved, why are we wasting time to find out about his wherebouts while we have other people to prosecute at our expense?

Why delay to prosecute those who participated in the scheme itself?

Kitila kasema Ballali tulimpa dhamana kulinda kitita cha Taifa, je ni sisi wananchi tulimchagua Ballali awe Gavana au ni Raisi na Serikali ambazo zimepewa dhamana na Wananchi zilimpa Ballali dhamana hiyo?

Kwa nini tunakuwa wagumu kuikalia kooni Serikali na wale wote wa awamu ya tatu ambao kwa njia moja au nyingine walihusika na sakata hili kama Ballali mwenyewe?

Why aren't we demanding explanation from the government not about Ballali but how did the government fell asleep for 5 years to catch Ballali or schemers of Tangold, Meremeta and later EPA? Why there is such delay in full investigation and criminal case using Economic sabotage laws of 1984?

We are barking at a wrong tree, Ballali may be a component on the whole saga, but it is the Government which we need to hold at its throat and not anyone else.

Once we have Government at its knees and demand full accountability and esponsibility, then we will be able to figure out how Ballali "outsmarted" everyone or how Ballali was a simple victim of his job and kiapo cha utii kwa Serikali na Raisi!

Otherwise if we can not demand this to our current Governement, we may as well wait until Opposition is the majority in the Parliament and also controls Ikulu!
 
Kitila Mkumbo,
Mkuu sikubaliani nawe hata kidogo kwenye hili.. Elimu yako ni zaidi ya haya kwa sababu moja muhimu sana. Balali alikuwa muhimu akiwa hai na tetezi zilizotoka toka mwaka jana ni kwamba amelishwa sumu na yuko hospital Marekani.. Hapo mkuu ndipo maswali haya yote yangejengwa akiwa hai, utata wote huu wa kifo cha Balali umezungukwa na issue ya EPA, ambayo ingewezekana tu akiwa hai. Viongozi wa CCM kwa jeuri zao siku zote wamekuwa wakitufunga kamba nasi tukakubali kufungwa.. Dr. Slaa alipiga makelele weee hakuna mtu aliyemwona na akili kama alivyokuwa Mwanakijiji ktk kesi ya Chifupa...
Leo tumesikia kafa sasa swala limekuwa kafa kweli?...I mean hii inatusaidia nini zaidi ya kutujengea ukuta zaidi na kuwapa CCM point zaidi.
Unajua Mwaka 1972 kule Nyamagana ktk fainali za ligi Kuu kati ya Simba na Yanga, kulikuwa na uhakika Simba anachukua ushindi ule na tegemeo lao kubwa lilikuwa mchezaji Saad Ally, lakini dakika tano kama sio kumi toka mpira kuanza huyo Saad Ally alipata concussion ikabidi atolewe kwa machela... Simba wote waliona ushindi ujmeondoka wakashikwa na butaa... Hapo hapo nilijua Mpira umekwisha Yanga aliondoka mshindi kwa magoli 2-1..
Kwa hiyo hapa mnaweza shinda goli moja la Balali lakini ktk issue nzima ya EPA mkuu mtawaangusha wananchi vibaya sana kwa hayo magoli yanayohusiana na EPA. Elimu yenu ni pamoja na kuyaona haya madogo yaliyojificha ambayo kina yakhe sisi tufuate kwa nguvu moja..Hata Castro alipokuwa akipigania Uhuru wa Cuba alikutana na mengi ikiwa ni pamoja na kumpoteza Che lakini mkuu mapambano yaliendela kama vile hakuwepo...
Huu ndio usia wangu kwenu, haya maneno ya Mtanzania kuhusu Usiri, usiri upo kwenye EPA yenyewe na Balali ni kafara tu ya usiri huo.. Tukiweza kufungua EPA basi Balali hana nguvu na pengine kuna uwezekano akajitokeza maana kesi ya BoT zitakuwa zimekwisha.. Mkapa and Co ndani ya Segerea..

Kuhani Mkuu,
Warioba kasema hivi:-"Huu ni unafiki mkubwa. Kuna visingizio kwamba ugonjwa wa Ballali haujulikani, lakini Serikali inajua kwani alikuwa analipiwa matibabu na Benki Kuu. Alikuwa Boston, Marekani..

Ni kweli ukitaka kuijua mgonjwa kalazwa hapo hospitalini hakuna tatizo kabisa isipokuwa kama unataka kufahamu maradhi ya mtu huyo kupitia daktari wake. Kisha Warioba ameonyesha mshangao ikiwa Benki kuu walikuwa wakilipia gharama za matibabu.. Nadhani yupo ktk msitari swafi!

Rev Kishoka,
Mkuu umemaliza yoteee yaliyokuwa rohoni mwangu Shukran nyingi sana na nadhani mimi nimefikia mahala pa kusema BASI TENA... sina mjadala zaidi kuhusiana na Balali.
 
Mheshimiwa Warioba, sikiliza Mzee!

Marekani ni nchi ya wazi, ni kweli, lakini mtu baki yeyote huwezi kuambiwa habari zozote za mgonjwa. Ndo maana hakuna aliyejua afya ya mgombea John McCain mpaka wiki iliyopita alipotoa health report yake. Vinginevyo daktari hawezi kusimama jukwaani akasema 'mgonjwa wangu Ballali ana Ukimwi ...amelazwa hospitalini kwangu chumba namba tisa!" Hapo umechemsha!

Pili, unasema hela za EPA zote zililipwa kwa makampuni ambayo siyo ya Ballali, na kwa mtaji huo, Ballali hakuwa fisadi. Wewe ulikuwa Mwanasheria wetu mkuu, na leo ni Jaji wa Kimataifa, utajifanye hujui kitu kinachoitwa "kickback"? Ballali analipa fedha za EPA kwa kampuni X, inayomilikiwa na ndugu Y, halafu Y anakuja kumpoza Ballali pembeni bila kuacha fingerprints kwenye makaratasi. Mzee Warioba hiyo concept huijui, au unataka kufanya wenzio wajinga kwa sababu umepata bullhorn ya Raia Mwema unakozungumza bila kuswalishwa?

Tatu, unasema Ballali aachwe apumzike kwa amani, halafu hapo hapo unasema siku moja ukweli utajulikana. Ukweli utashuka wenyewe kama mvua za masika kutoka mbinguni? Si ndo maana watu wanachunguza? Na kuna ubaya gani unapofanya uchunguzi ukamhusisha aliyekuwa anatunza ufunguo sehemu ujambazi ulipotokea bila kufuli kuvunjwa? Ndio hivyo ulivyo kuwa unaendesha Wizara ya Sheria? Warioba hata wewe unachemsha hivi?

Nne, unadai Serikali inajua ugonjwa kwa sababu walilipia gharama. Hilo tunalijua, ni Kisukari tuliambiwa. Mbona husemi kuhusu Hospitali? Au Ballali alipewa hela taslimu akaambiwa kajitibie kokote, zitakazobaki turudishie chenji? Na zikipungua tuma ki-memo tukuongezee? Hospitali haitumi bili? Si ndio ufisadi huo tunaoungelea. Na wewe si hivi karibuni umekuwa ukikemea ufisadi, sasa tukueleweje we Mzee unapoongea kutoka pande zote mbili za mdomo wako? Ni hospitali gani hiyo waliyo ilipa lakini hawaijui, kama sio ya Profesa Maji Marefu?

Credentials za huyu Mzee Warioba ni za Mwanasheria Mkuu, na Jaji wa Kimataifa, na Waziri Mkuu, na Waziri wa Sheria, na Makamu wa Rais wa Jamhuri. Na bado anachemsha hivi. Unadhani kuna matumaini Tanzania?

KM,

Tatizo ni maslahi, jaji Warioba hapo anatetea pesa ambazo na yeye amefaidi kule Mwananchi Gold.

Si umeona hata Mzindakaya naye katusaliti baada ya kupewa bilioni tisa kule kwenye kiwanda fake cha nyma?

Warioba anamlaumu Mkapa, huku na yeye ameruhusu mafisadi kumchangia kwenye kampuni yake? Mkapa na yeye angemkatia kidogo kama alivyofanya Ballali, leo hii angelikuwa anamtetea.

Tanzania tumejaza mafisadi kila sehemu.
 
Kigoma,

Fuatilia hili na unaweza kutafuta hata hapa JF maana tulishajadili hili jambo.

Jaji Warioba ni katika wahusika wa Meremeta, ndio maana wengine tungetaka uchunguzi huu uwe mkubwa zaidi na uchunguze pesa zote zilizochotwa BOT na kupewa wanasiasa. Wapo wengi kwenye kundi.

Nakushauri fuatilia, ukishindwa nijulishe, nitakusaidia.

Soma hii link: http://www.klhnews.com/index2.php?option=com_docman&task=doc_view&gid=10&Itemid=85

Meremeta na Mwananchi.....ni kampuni tofauti......
Mwananchi Gold....ni kampuni ya kusafisha dhahabu na kuiongezea thamani....kabla haijauzwa....Jaji Warioba ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi....usijaribu kuwapotosha wana JF...

http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2005/12/02/55188.html

http://www.bot-tz.org/Publications/FinancialReports/FinancialStatements/2004/NOTES.pdf

'The government owns 35 per cent of the 80 per cent owned by Tanzanians, while the rest belongs to a consortium of Tanzanian companies under the umbrella of Mwananchi Trust'


Unaweza kumhukumu Jaji Warioba kwa kukubali...kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa hii kampuni....LAKINI sio kwa yeye binafsi kujihusisha na ufisadi...huyu jamaa sio fisadi, hajawahi kuwa fisadi na sidhani kama ataanza leo wala kesho!
 
'The government owns 35 per cent of the 80 per cent owned by Tanzanians, while the rest belongs to a consortium of Tanzanian companies under the umbrella of Mwananchi Trust'
Wait a minute, Utamlaumu vipi ikiwa kuna HISA kubwa ya serikali?
 
Meremeta na Mwananchi.....ni kampuni tofauti......
Mwananchi Gold....ni kampuni ya kusafisha dhahabu na kuiongezea thamani....kabla haijauzwa....Jaji Warioba ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi....usijaribu kuwapotosha wana JF...

http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2005/12/02/55188.html

http://www.bot-tz.org/Publications/FinancialReports/FinancialStatements/2004/NOTES.pdf

'The government owns 35 per cent of the 80 per cent owned by Tanzanians, while the rest belongs to a consortium of Tanzanian companies under the umbrella of Mwananchi Trust'


Unaweza kumhukumu Jaji Warioba kwa kukubali...kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa hii kampuni....LAKINI sio kwa yeye binafsi kujihusisha na ufisadi...huyu jamaa sio fisadi, hajawahi kuwa fisadi na sidhani kama ataanza leo wala kesho!

Mkuu Kigoma,

Hapa JF tukisema EPA, Meremeta, Mwananchi, Tangold na makampuni mengine tunaongelea deals fake za BOT na baadhi ya makampuni.

Mwananchi Gold ni moja kati ya makampuni hayo ambayo yalitumiwa kifisadi kuchota pesa za wananchi.

Huwezi kutofautisha kati ya Meremeta na Mwananchi au Meremeta na Tangold, wote wametumia njia zile zile kutuibia.

Ukisema hivyo basi hata Mzindakaya sio fisadi kwenye kiwanda chake cha nyama, maana na yeye ni kampuni yake binafsi. Kachotewa bilioni tisa, unategemea mtu kama huyo amshambulie Billali?

Jaji Warioba ni mhusika kwenye haya mambo ya BOT na ndio maana hamlaumu Ballali, kuna conflict of interest na hicho ndio nilitaka kukuambia.

Kama nimechanganya majina ya Meremeta na Mwananchi sio hoja, issue hapa ni deals fake kati ya makampuni ya watu binafsi na BOT. Wanajifanya hizo ni kampuni za serikali kumbe walizitumia tu katika kutuibia Watanzania.
 
Back
Top Bottom