Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

NOW I KNOW FOR SURE.... what I have been suspecting all along.

Let me start whistling again........ don't ask me why.
 
GENTLEMEN, IS IT GOD WHO POISONED DK BALALI IN DODOMA??? kwa nini tunamsingizia mungu kwa kazi aliyoifanya binadamu? Was Muungwana realist on this or not. I wonder kama ni kweli huo ni ukweli au ni political talk.
 
Mheshimiwa Raisi wa Tanzania -JK ameshasema kuwa kifo cha Balali ni kazi ya mungu. Je wewe unabishana na Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania?

Amefanya kipi kinachostahili aaminiwe na wananchi? Si alikuwa mstari wa mbele kusema tuhuma za wapinzani dhidi ya BoT zilikuwa ni uzushi tu!!!? ukweli sasa tunaujua. Alikuwa kimya kabisa muda wote huu kuzungumzia ufisadi mkubwa uliotokea BoT sasa mmoja wa wahusika kafariki, jamaa kapata nguvu ya kuongea. Hakuwepo hospitali, hakuona ripoti ya kifo kilisababishwa na nini, hivyo ni bora anyamaze tu awaachie familia ya Ballali wakitaka kuongea wataongea.
 
Huyu Jamaa naona akili yake iko likizo au labda iko UFISA.........................DINI. Naona yeye anaamini binadamu na sio MUNGU. JK akisema .....NDIO MZEE, EL akisema .....NDIO MZEE, CHENGE akisema .......NDIO MZEE. Hii ndio sababu kubwa iliyomfikisha BALALI alipo. Anaishia kuwa mtumwa wa MAFISADI baada ya kumtumia watakavyo kwa matakwa yao binafsi. Dawa ni kuondoa hiki CHAMA CHA MAFIA madarakani au kuweka watu ambao wako competent katika nafasi zao za kazi.

GAVANA wa benki kuu lazima U-QUESTION any move ambayo SERIKALI inachukua haswa maswala ya FEDHA na UCHUMI kwa ujumla. Sio unakurupuka na BILLION 25 kwa wananchi bila kumshiriksha MCHUMI yeyote eti tu upate ujiko wa MABILION YA JK. Matokeo yake ufisadi tu wa kutupwa usiokuwa na kipimo wala utu.

Kwa hiyo serikali isipike watu hapa kupitia tume ya kuchunguza EPA kuziba watu midomo na kuwatangazia UMMA eti BALALI KAFA. Huyo aliyefanya FACE-LIFT lazima amekuwa milionare kwa jasho la wananchi wa Tanzania.
 
Kwa kawaida sisi waTanzania tuna utaratibu wa kusafirisha mwili nyumbani iwapo atafariki nje ya nchi. Michangi huwa inafanyika kwa sababu hii..... Halafu pia hatuna tabia ya kuchoma mwili.......
Sasa maswali yangu kuhusu Ballali ni:
Kwanza: Kwanini waTanzania hatukuelezwa au kushirikishwa katika jambo hili....? (Niko Boston ndio maana nauliza swali hili).
Pili: Kwa nini mwili wake usirudishwe nyumbani....?
Tatu: Kwa nini mwili wake uchomwe....?
Nne: Ballali alikuwa mfanya kazi wa serikali. Kwa nini Serikali ilimtelekeza katika mauti yake....?
Siungi mkono ufisadi alioufanya Ballali....kwahiyo ningependa kuona picha yake kabla ya mazishi ili nihakikishe kama kweli amefariki dunia au walitafuta pacha wake na kumzika.....na Ballali akayesa.
 
Ila nimekubali mafisadi ni soo babake... duuuu! Yaani unaambiwa wamemfanyia plastic sugery Balali na kumshauri abaki Marekani maisha yake yote yaliyobaki , then wakaishauri familia yake zitangaze msiba na waseme watazika kulekule marekani... na hairuhusiwi mtu wa nje ya wanafamilia kuhudhuria kwa kuwa mtashtukia kwamba anayezikwa ni maiti iliyonunuliwa mortuary ya hukohuko majuu na kuvikwa sura ya balali. Then baada ya hapo wabongo mnaletewa picha za mazishi kama vile kafariki kweli..... loooo kama hamjashtukia hilo mmeliwa!!!! Poleni eeeee wabongo wenzangu kwa kulishwa mchanga wa macho!!!!!! MAfisadi Hureeeeeeeee! Mkapa, Chenge, Mgonja, Mramba, Kikwete, Lowasa, na wengine wote naona mna-toast glass za wine tu kushangilia dili kutimia... Mna akili fyetu nyie !!!!
 


Yote yanawezekana unayosema pia yawezekana ila jamaa alikuwa dhaifu kitambo kwa mujibu wa vipimo vya macho yangu some kind of progressive disease.

Katika yote yaliongelewa ktk maada zote kuhusu kifo chake kuwa ni fake au halisi nimeona hakuna pande inayoweza kusema kuwa kinyume cha wanavyoamini ni uwongo (and the vice verse is the truth).
Kwa kuwa mtu ana haki za kusimamia kuwa jamaa hajafa kama bado unamuona by your naked eyes kuwa yu mzima vinginevyo usibishe kuwa kafa ila labda uombe kudhibitishiwa kifo chake kwa njia ambayo ww utaamini.

Na pia mtu ana haki ya kusimamia kuwa it is the death fake kama ameona hilo likifanyika kwa macho yake vinginevyo asibishe akiambiwa kweli kafa kihalisi.
Mtu ana haki ya kusimamia kuwa kweli jamaa kafa kama na kama tu kaona hatua ya kufa ya anayesemwa kuwa kafa,mwili halisi wa mfu anayesemWa kufa.

Logic by connecting some facts its depents on what is fact to you and its reliability.Basi si matumizi ya faida na sanifu ya nishati ktk kongamano juu ya hili.
 
Kuhusu kulipua mabomu mbona mwanzisha maada naona kaweka kiulizo mimi sioni la wao kusema likawa kwenye mfumo wa bomu litakalo tikisa.
 

Mwe maswali ya wadanganyika atajibu nani kama balaaa hili limeshachukuliwa na mwenyezi mungu lakini bora mungu kamchukua maana wabongo wangeweza kujichukulia sheria mkononi wakamchoma moto kama kibaka wa tandale bila hata kumsikiliza. eee baba muweke mahala pema peponi balaa hili!

na mjimwema,KIGOMA
 
Kama ni kweli Balali alihuzunishwa na kitendo cha kudhalilishwa hapa nchini akiwa bado mzima kwa nini hakusema lolote. Kama hakuiba hata senti tano kwa nini alikaa kimya? Ndugu zake wakaribu watueleze.
 
Kuna mtu amefikiria kwamba Balali labda kafa ukimwi maana ndiyo ugonjwa bila tiba. kama alipewa sumu basi alichomwa damu ya ukimwi.
 
Ansbert Ngurumo



NILIWAHI kudokeza mambo mawili kwenye safu hii kuhusu aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), hayati Daudi Ballali.

Kwanza nilihoji kama ugonjwa wake ulitokana na kulishwa sumu. Sikujibiwa. Pili, nilisema kwamba taarifa za watu wanaojua mambo yanayoendelea serikalini zilieleza kuwa Ballali asingerejea Tanzania.

Yote mawili yamekuwa. Ballali hakurejea. Sasa taarifa mpya zinasema kwamba kabla hajafa alimtaja mtu aliyemlisha sumu iliyosababisha ‘ugonjwa' wake, hadi akakimbizwa nje ya nchi kutibiwa.

Watu wake wa karibu wamemnukuu hayati Ballali akimtaja mtu aliyemlisha sumu. Yawezekana hii ni kauli mojawapo ambayo wanafamilia walitaka kuiweka hadharani katika mkutano na wanahabari. Tuwape muda.

Kwa sababu zinazoeleweka, hatutamtaja ‘muuaji' huyo hapa kwa sasa. Lakini kadiri siku zinavyokwenda, iwapo na sisi hatutalishwa sumu, kama hatajitaja, tutamtaja siku moja, katika kuweka vema historia ya mapambano dhidi ya ufisadi.

Siku mambo yote yatakapokuwa yamewekwa vizuri, Watanzania watakaokuwa hai wakati huo watapata fursa ya kutambua jinsi ufisadi ulivyowahi kuwa sehemu nyeti ya utawala wa nchi hii.

Kitu kimoja hakitawashangaza. Nacho ni sura na majina yanayozungumzwa na kuhusishwa na ufisadi katika serikali za awamu ya tatu na ya nne.

Hata katika hili la sasa, mtu yule yule aliyetajwa na hayati Ballali, kwamba ‘ndiye alinilisha sumu,' ni kigogo yule yule ambaye amekuwa anahusishwa katika mazingira na matukio mengi ya ufisadi wa kupindukia.

Yumo katika orodha ya mafisadi 11 walioanikwa hadharani na Dk. Willibrod Slaa, Septemba 15, 2007 katika mkutano wa hadhara wa Temeke Mwembe Yanga, Dar es Salaam.

Yumo miongoni mwa waasisi wa kaulimbiu ya ‘Maisha bora kwa kila Mtanzania.' Ni mmoja wa watu ambao kwa sasa wanaangaliwa kwa macho ya chuki, kwa kuwasababishia Watanzania maisha duni.

Ni mmoja wa vinara waliofadhili na kutangaza kwa nguvu zote dhana ya ‘Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya' ambayo imekuwa ikifupishwa kwa kuitwa ANGUKA; na kuwa kiini cha anguko la Tanzania.

Ni muasisi wa dhana iliyoangusha uchumi wa nchi na kudunisha maisha ya Watanzania, huku akiasisi dhana nyingine ya kimya kimya ya ‘Maisha bora kwa kila fisadi.' Mtu huyu huyu aliyetajwa na hayati Ballali kwamba ndiye alimlisha sumu, yumo miongoni mwa vigogo wanaotuhumiwa kulihujumu taifa kwa kuunda mitego ya uchotaji wa pesa za wananchi kutoka Akaunti ya Madeni ya Nje ya Benki Kuu (EPA).

Ndiye anayetajwa kuwa mmoja wa vigogo walionufaika na pesa za Richmond; mtu ambaye inasemekana alikula njama kuchomoa mafaili ya Richmond katika kumbukumbu za msajili wa makampuni ili ‘kuiingiza mjini' Kamati ya Bunge iliyokuwa inachunguza tuhuma dhidi ya kampuni hiyo.

Ni kigogo huyo huyo ambaye kwa wakati fulani alidhaniwa kuwa na hisa katika urais wa Jakaya Kikwete, hata ikawalazimu wanahabari kumhoji rais moja kwa moja kuhusu suala hilo.

Ni mtu huyo huyo ambaye miezi michache iliyopita, kabla ya masuala ya ufisadi kupamba moto, alikuwa akidhaniwa kuwa mfadhili na mkombozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM); na ambaye baadhi ya watu wanaojua jinsi awamu hii inavyofanya kazi, waliwahi kudokeza kwamba ‘ndiye rais' wa Tanzania asiyeishi Ikulu, anayeendesha nchi atakavyo kupitia kwa rais aliyechaguliwa, anayeishi Ikulu.

Lakini kikubwa kinachomgusa na kumfadhaisha kigogo huyu ni taarifa kwamba ndiye ameshiriki kwa kiasi kikubwa kuchota mabilioni ya EPA kutoka BoT na kuyazungusha kwenye miradi yake, huku akiingiza mengine kwenye kazi za CCM, zikiwamo harakati za kampeni za uchaguzi mkuu.

Kutokana na ukaribu wake na walio madarakani, serikali imeshindwa hata kuchukua hatua madhubuti dhidi ya walioiba pesa za EPA; ikasema haiwajui, lakini ikakiri kwamba wanarudisha pesa taratibu! Serikali hii hii ikashindwa kuiweka hadharani ripoti kamili ya uchunguzi wa wizi wa EPA kama ilivyoandaliwa na wataalamu wa Ernst & Young.

Serikali ikamficha mtu wake kwa jinsi ile ile ilivyokuwa inaficha ugonjwa wa Ballali, nchi aliko na hospitali alikolazwa, huku baadhi ya maofisa wa serikali wakisemekana kumtembelea mgonjwa wao kushuhudia kama bado yuko hai.

Usiri wa serikali katika suala la Ballali umeiaibisha yenyewe, na umeondoa kabisa imani ya wananchi kwa serikali hii. Umeonyesha unyonge na udhaifu mkubwa wa watawala wa sasa, na kudhihirisha wasiwasi ambao tumekuwa nao siku zote, kwamba nchi hii sasa inaendeshwa na mafisadi.

Lakini huu umekuwa usiri uliokithiri, kiasi cha serikali kudiriki kuficha hata kifo chake, hadi gazeti hili lilipoibua taarifa hizo, na kulazimisha serikali kukiri.

Nawaonea huruma watumishi wa serikali hii wasio mafisadi, lakini wanaofunzwa kutunza siri za mafisadi.

Tabia hii ya serikali ndiyo imewafanya wananchi wengine kudhani kwamba hata Ballali mwenyewe hajafa; kwamba ni njama za mafisadi kumficha kabisa ili kuua ushahidi katika suala la EPA.

Lakini hata wale wanaoamini kwamba amefariki dunia, wanajenga hoja hiyo hiyo; kwamba wamemuua ili kuficha siri yao.

Kwa kifo cha Ballali lipo jambo ambalo hatutalijua kamwe kuhusu wizi wa EPA. Maana kabla hajafa, Ballali mwenyewe alisema hakula hela za EPA, bali anawajua waliozichota, na kwamba asingekufa peke yake.

Sasa wamemtanguliza wakidhani atakufa peke yake. Lakini sisi wengine tunasema kwamba hao hao waliomtanguliza, watamfuata.

Hatuwezi kujua mapenzi ya Mungu, na si vema kumsingizia Mungu. Lakini akili timamu inatueleza kuwa kama tungekuwa na serikali makini, kifo cha Ballali kingeahirishwa.

Huyu ndiye alipaswa kulindwa na serikali ili aweze kutoa ushahidi ambao ungeiwezesha serikali kuchukua hatua za kujisafisha, na kudhibiti ufisadi mwingine.

Lakini kwa kuwa si serikali makini, na kwa kuwa haina nia ya kujisafisha; na kwa kuwa inawajua na kuwalinda waliohusika na wizi wa EPA; na kwa kuwa wanaohusishwa na kifo cha Ballali ni wale wale walioshiriki kuiumba serikali hii; Watanzania hawatakuwa na makosa wakiibeza na hata kuituhumu kwa kumuua Ballali.

Ndiyo maana, ingawa kwenye misiba hatutarajii watu wamkejeli marehemu, Watanzania wameshindwa kuzuia hisia zao. Kwa kujitahidi sana, wamezielekeza zaidi kwa serikali badala ya marehemu.

Mojawapo ya kauli zilizozagaa mitaani sasa ni kwamba ‘kafa Ballali, bado wengine kumi.' Hawa wanaosema hivi wanarejea orodha ya ‘mafisadi' iliyotajwa na Dk. Slaa, ambayo huko nyuma niliwahi kuiita ‘JK Eleven.' Lakini kikubwa ni kwamba huyo anayesemekana kumlisha sumu Ballali ni mmojawapo wa hao kumi waliobaki.

Hili linakomaza dhana nyingine kwamba watu hawa sasa wameamua kumalizana wakigombea maisha bora walioyowanyima wananchi.

Tunachojua tulio wengi ni kwamba Ballali si wa kwanza. Na hawezi kuwa wa mwisho. Lakini mwisho wao wote ni mmoja.

Yawezekana bado kumi au zaidi ya kumi. Lakini ukweli ni kwamba Ballali ametangulia, ushahidi wa EPA umekufa, na imani ya watu kwa serikali imekufa!

+447853850425
ansbertn@yahoo.com
www.ngurumo.blogspot.com

source: http://www.freemedia.co.tz/daima/2008/5/25/makala2.php

Kama RA vile
 
Damn it! Why not mention him we dare talk openly.
 
Siamini kama kufa kwa Balali ndio kufutika kwa ushahidi wote kuhusu EPA. Siamini kama Balali alikuwa akifanya mambo yote haya ndani ya BOT bila kumhusisha mtu mwingine. Ukweli ni kwamba Balali alikuwa ni shahidi mkuu, lakini naamini wapo watu wengine wengi ndani ya BOT, ndani ya Wizara ya Fedha na ndani ya serikali kwa ujumla wenye ushahidi kuhusu ufisadi wa EPA. Cha msingi ni kuwalinda wasinyweshwe "sumu" kama ilivyotokea kwa Balali.
 
Damn it! Why not mention him we dare talk openly.

No hatuwezi kumtaja kwa kuunganisha hisia za mtu kwani hitaharibu kijiwe chetu, kumbukeni wanatafuta sababu ya msingi kuakikisha hiki kijiwe kinafungwa huu ndo wakati wa kuwa makini zaidi ili tuendelee kumkoma nyani gradi, kama kuna ushaidi wa kutosha tafadhari mtaje kama unaushaidi wa mazingira then please do not do that.
 

Itakuwa vipi kamati ya EPA itakapoleta taarifa ambayo kila jambo anatakiwa athibitishe Ballali kama vile nani alimwndikia vimemo vya akasaini.
Au walete taarifa kuwa yale ni makampuni ya Ballali na Ditto na kwa sababu wameshakufa no Mo MONEY
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…