Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
NOW I KNOW FOR SURE.... what I have been suspecting all along.
Let me start whistling again........ don't ask me why.
Let me start whistling again........ don't ask me why.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
NOW I KNOW FOR SURE.... what I have been suspecting all along.
Let me start whistling again........ don't ask me why.
NOW I KNOW FOR SURE.... what I have been suspecting all along.
Let me start whistling again........ don't ask me why.
Tell us something mheshimiwa... Wengine ni walinzi wa PPF tower hapa... Tuko kazini, ila tunaibia-ibia computer za kazi...
Mheshimiwa Raisi wa Tanzania -JK ameshasema kuwa kifo cha Balali ni kazi ya mungu. Je wewe unabishana na Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania?
Ila nimekubali mafisadi ni soo babake... duuuu! Yaani unaambiwa wamemfanyia plastic sugery Balali na kumshauri abaki Marekani maisha yake yote yaliyobaki , then wakaishauri familia yake zitangaze msiba na waseme watazika kulekule marekani... na hairuhusiwi mtu wa nje ya wanafamilia kuhudhuria kwa kuwa mtashtukia kwamba anayezikwa ni maiti iliyonunuliwa mortuary ya hukohuko majuu na kuvikwa sura ya balali. Then baada ya hapo wabongo mnaletewa picha za mazishi kama vile kafariki kweli..... loooo kama hamjashtukia hilo mmeliwa!!!! Poleni eeeee wabongo wenzangu kwa kulishwa mchanga wa macho!!!!!! MAfisadi Hureeeeeeeee! Mkapa, Chenge, Mgonja, Mramba, Kikwete, Lowasa, na wengine wote naona mna-toast glass za wine tu kushangilia dili kutimia... Mna akili fyetu nyie !!!!
Ballali alikiona kifo
na Kulwa Karedia na Salehe Mohamed
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
MAELEKEZO ya kuzikwa Washington nchini Marekani kwa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), yalitolewa na yeye mwenyewe, siku kadhaa kabla hajafikwa na mauti, Ijumaa ya wiki iliyopita.
Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka kwa ndugu wa karibu wa Ballali aliyeko katika msiba huo Washington, zinaeleza kuwa, gavana huyo wa zamani wa BoT alifikia uamuzi wakati hali yake kiafya ilipokuwa ikizorota kutokana na kuumwa.
Mmoja wa wanafamilia ya Ballali aliyezungumza na Tanzania Daima jana, kutoka Washington, Marekani uliko msiba huo, alisema Ballali alitangaza uamuzi huo mbele ya jamaa zake, akiwamo mkewe Anna Muganda.
Kwa mujibu wa mwanafamilia huyo ambaye juzi alikuwa mmoja wa watu walioithibitishia Tanzania Daima kuhusu kifo hicho cha Ballali, hata kusababisha kuwa chombo pekee cha habari kilichoandika taarifa hizo jana, Ballali alifikia uamuzi huo kutokana na kufadhaishwa na namna jina lake lilivyokuwa likihusishwa na tuhuma nzito za ufisadi.
Yeye mwenyewe ndiye aliyeamua azikwe huku Washington. Siku zote amekuwa akitueleza namna alivyokuwa akifadhaishwa sana kutokana na kuchafuliwa kwa jina lake, hata baada ya kuitumikia nchi yake kwa juhudi kubwa, moyo mkunjufu na kwa uadilifu wa hali ya juu.
Alitueleza hapa kwamba hajapata kuiibia nchi yake hata senti moja. Hapo ndipo aliposema akifa angetaka azikwe huku huku Washington na si nyumbani, ambako alihusishwa na kila aina ya tuhuma, alisema mwanafamilia huyo ambaye hakupenda kutajwa jina gazetini, akisema yeye hakuwa msemaji.
Mwanafamilia huyo alisema kwamba, katika mazishi yake, Ballali atazikwa bila ya kuwapo mama yake mzazi, aliyepo hapa nchini, ingawa atasindikizwa na dada zake wawili ambao walikwenda kumjulia hali huko Washington hivi karibuni.
Inavyoonekana mama yake hataweza kuwahi mazishi. Hata hivyo dada zake wawili, Elizabeth na Margaret, wote tunao hapa msibani na hao ndio watakaoiwakilisha familia yake katika mazishi, alisema mtoa habari wetu huyo.
Hata hivyo, taarifa nyingine kutoka kwa jamaa wa Ballali walio Dar es Salaam zinaeleza kuwa, ingawa dada zake hao wawili walikwenda kumjulia hali kaka yao, waliwasili Washington, Marekani wakiwa wamechelewa na kumkuta ameshafariki dunia.
Mtoa habari wetu kutoka Washington aliieleza Tanzania Daima kwamba, ndugu hao wawili wa Ballali walikuwa wakitarajia kurejea nchini wakati wowote kuanzia Jumatatu ijayo.
Pengine msiniulize mimi hapa maswali mengi. Mpango uliopo hapa ni kwamba hawa dada zake wawili, Eliza na Maggy, wanatarajia kuitisha mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam na kutoa taarifa kamili kuhusu kifo cha kaka yao, alisema ndugu huyo wa Ballali.
Alisema alikuwa na imani kwamba, katika mkutano wao huo na waandishi wa habari, unaotarajiwa kufanyika wakati wowote wiki ijayo, maswali yote kuhusu nini hasa kilimpata Ballali hata kufikwa na mauti hayo kitawekwa hadharani.
Habari nyingine kutoka Boston na Washington zinaeleza kwamba, kulikuwa na taarifa zilizokuwa zikisema kwamba, Ballali alikuwa akisumbuliwa na aina moja ya saratani kwa muda mrefu sasa.
Hata hivyo wakati kukiwa na taarifa hizo, baadhi ya ndugu, marafiki na jamaa zake wamekuwa wakieleza wasiwasi wao kwamba, Ballali alilishwa aina fulani ya sumu isiyojulikana, siku kadhaa kabla hajakimbizwa Marekani kwa matibabu.
Taarifa hizi za kulishwa sumu zimekuwa zikienea kwa haraka katika maeneo tofauti, mbali ya Tanzania Daima pekee kuligusia jambo hilo jana, likimkariri ndugu mmoja wa Ballali aliyekiri kuwapo kwa wasiwasi huo miongoni mwa wanafamilia.
Jamaa mwingine wa Ballali aliyeko huko huko Washington Marekani, aliieleza Tanzania Daima kwamba, familia ilikuwa ikijiandaa kuwasiliana na Balozi wa Tanzania nchini Marekani ili kesho aweze kuhudhuria misa maalumu ya kumuombea marehemu itakayofanyika kabla ya mazishi yake yanayopangwa kufanyika kesho hiyo hiyo.
Ndugu huyo wa Ballali alisema, walikuwa na imani kuwa serikali ilikuwa na taarifa kamili, baada ya wao kuwasilisha Ofisi ya Rais Ikulu na baadaye kwa Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, juzi hiyo jioni.
Wakati Ballali akitarajiwa kuzikwa kesho, uongozi wa BoT jana alasiri ulitoa taarifa rasmi ya kukiri kupokea taarifa hizo za kifo cha Ballali na kusema unaungana na familia yake katika kipindi hiki kigumu.
Akitoa taarifa hiyo ya maandishi kwa waandishi wa habari jana, Ofisa Mwandamizi wa Kitengo cha Habari cha BoT, Emmanuel Mwero, alisema ofisi ya Gavana (Ndulu) ilipokea habari hizo kwa masikitiko makubwa.
Ofisi ya Gavana imepokea habari za kusikitisha jana usiku (Jumanne) kuwa gavana wa zamani wa BoT, Daudi Ballali, amefarikia Ijumaa Mei 16, mwaka 2008 huko Boston, Marekani, ilisema taarifa hiyo wakati ukweli ni kwamba Ballali alikuwa amefia Washington.
Katika taarifa hiyo, Ballali anaelezwa kuwa alijiunga na BoT kama gavana Julai 14, 1998, nafasi aliyodumu nayo hadi Januari 8 mwaka huu, uteuzi wake ulipotenguliwa na Rais Kikwete, baada ya kupokea taarifa za ukaguzi wa EPA, uliofanywa na Kampuni ya ukaguzi wa hesabu ya Enrst & Young.
Hata hivyo, si BoT wala serikali, ambayo ilikuwa mwajiri wa Ballali, iliyotoa taarifa ya ufafanuzi kuhusiana na mazishi ya Ballali, ambaye ni mmoja wa watu waliopata kushika nafasi nyeti za uongozi nchini.
Ndugu waandishi habari hii imejitosheleza, hivyo tunawaomba mkaitumie na kama kutakuwa na jambo lolote, Gavana Beno Ndullu atawaita, alisema Mwero.
Taarifa kutoka ndani ya benki hiyo zinasema kuwa, jana asubuhi wafanyakazi wote walisambaziwa kupitia anuani zao za e-maili, wakijulishwa kuhusu msiba huo.
Tanzania Daima ilipofika katika nyumba aliyokuwa akiishi wakati akiwa gavana, iliyoko Masaki Plot 387, jijini Dar es Salaam, hali ilikuwa ya utulivu, ingawa walikutwa walinzi wa Kampuni ya Ultimate Security.
Ni kweli hapa ni nyumbani kwa Gavana, lakini tangu Ballali alipoondolewa, nyumba imebaki wazi, tupo sisi na mfanyakazi wa ndani tu, alisema mmoja wa walinzi hao.
Naye Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, jijini Dar es Salaam, Salvatory Rweyemamu, alipoulizwa kuhusu taarifa hizo za msiba alisema yeye hakuwa msemaji na akamwita Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo) Kassim Mpenda aliyekuwapo hapo.
Mpenda kwa upande wake alisema serikali imepanga utaratibu juu ya taarifa hizo na kwamba msemaji mkuu ni Gavana wa BoT, Ndullu.
Ni kweli hata miye nimesikia kwamba Ballali amefariki dunia, sasa mimi siyo msemaji, kumbukeni serikali inafanya kazi kwa utaratibu, hivyo imemteua Dk. Ndullu kuwa msemaji mkuu wa suala hili, nawaomba mtafuteni, alisema Mpenda.
Kabla ya kuteuliwa kushika wadhifa huo, Ballali aliwahi kuwa mchumi wa BoT mwaka 1967-1976, kabla ya kufanya kazi katika Shirika la Fedha Duniani (IMF).
Ndugu wa karibu wa Ballali alisema wanatarajia kufanya misa ya mazishi ya Ballali na kumualika Balozi wa Tanzania nchini Marekani, katika shughuli za mazishi zitakazofanyika kesho jijini Washington, Marekani.
Maoni ya Wasomaji
Maoni yanayotolewa na wasomaji wa safu hii ni ya kwao na sio maoni ya kampuni ya Freemedia Ltd. Aidha sio maoni ya mtunzi au mwandishi wa habari au makala husika hapo juu. Maoni haya hayajahakikiwa wala kuafikiwa na kampuni ya Freemedia Ltd.
Maoni 22 yameshatolewa. (Nawe toa maoni yako!)
ningependa maiti ya huyu mheshimiwa iletwe nchini ili tuwe na uhakika kuwa ni kweli amefariki kwa sababu naona kuna zengwe, angalia namna viongozi wetu wanavyolikwepa na kutupiana mzigo juu ya taarifa hiyo.
na juma magogo - 22.05.08 @ 08:18 | #12509
Wanadamu mwisho wao mavumbi,fedha na mali ni za Mungu;Mafisadi jifunzeni kuwa mambo haya yana mwisho,ingawa hatuna hakika kuwa balali alikuwa fisadi,chenye uhakika ni kwamba alisaidia kufilisi nchi na kusaidia wengine kula nchi;Fisadi tunaye humu nchini "Mzee wa Vijisent"aukumbuke mwisho wa Balali arudishe fedha zetu Akamrudie Mungu.
na kibeberu, tanzania, - 22.05.08 @ 08:19 | #12510
Yaani hapa naona ni changa la macho BOT wanasema amefia BOSTON ila ndugu zake wanadai amefia Washington kweli kuna ukweli hapa mm naona yupo visiwa vya Malta anakula maisha taratibu huku ss tukipigwa changa la macho wadanganyika wenzangu.
na Mkula, Namanga, - 22.05.08 @ 08:27 | #12512
kama ni ukeli Dk.Ballali kafariki, Mungu amlaze mahali pema peponi.Kifo, kwa wakati wowote sio jambo la kushabikia hata kama mtu aliye aga dunia alikuwa muovy kiasi gani.Japo Dk.Ballali alishtumiwa kwa visanga vingi vya ufisadi si vyema kuaanza kusheherekea kifo chake.La msingi ni serikali ifanye mpango wa kuusafirisha mwili mpaka tanzania na kufanya mipango ya mazishi ili kuwahakikishia watanzania wote ni kweli amefariki.
na deco, kenya, - 22.05.08 @ 08:45 | #12517
Jamani tusianze kumkumu marehemu.
Kwanza ailikuwa hajahojiwa ili apate kutoa utetezi wake, bahati mbaya kifo imemkuta.
Kwa kuwa suala la EPA lina watu wengi, na Balali alikuwa na wasaidizi wengi , kwa mawazo yangu naona bado mengi yatafahamika hata bila kuwepo huyu mzee.
Mungu amlaze pema peponi- ndiyo maisha yana mwanzo na mwisho.
na john, mwanza, - 22.05.08 @ 08:46 | #12518
Nimepokea kwa maskitiko makubwa taarifa ya kifo cha Dr Daudi Balali,kwa sababu kuu mbili kama sio tatu 1 amefariki wakati ambao taifa linamhitaji kuliko wakati uwao wote 2 Balali amekufa wakati ambao watanzania walikuwa wanamsubili kwa hamu kubwa iliaweze kuwajibia maswali mengi yanyo husu pesa zao 3 ni dhahili kuwa mheshimiwa Raisi sasa atapumua vizuri sasa pamoja na wale wote wanao husika na upotevu wa pesa zetu katika account ya madeni ya nje [epa] Ndio watapumua kwa sababu Balali ndiye aliye kuwa anajua nani amechukua nini na kupeleka wapi na tarehe gani,kwa upande mwingine ni kwamba Balali ndiye aliye kuwa ameshikilia hatima ya pesa za watanzania na kuweza kuwafichua wote walio husika ktk wizi wa pesa zetu.Sasa kwa kifo hiki tutegemee nini kipya juu ya Taifa hili iliyo baki ni kuendelea kumwomba Mungu atuhurumie juu ya Viongozi wetu wasio na huruma na watu wengine.
na Mch:Ibrahim Mwandandila, Mbeya/Tanzania, - 22.05.08 @ 08:49 | #12520
Mjomba kaa chonjo mchanga sasa wanamwaga kwa kutumia malori machoni , iweje tu gazeti la tanzania daima ndio liseme la kwanza haya magazeti mengine yalipata kigugumizi gani kusema au makampuni mengine yako karibu na mafisadi , au serikali imeona atasema mengi ikaamua kukata umeme kwenye gridi ?
na msemakweli, Dar -Tanzania , - 22.05.08 @ 08:56 | #12522
MIMI NAULIZA SWALI NI KWELI KWAMBA SERIKALI HAIKUONA UMUHIMU WA KUMLETA MAREHEMU NYUMBANI TANZANIA?NA FAMILIA YAKE MNAFIKIRI INAJISIKIAJE KUMZIKA MPENDWA WAO HUKO WASHNGTON MAREKANI?ANY WAY MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI AMEN.
na HILDER MMBANDO, TANZANIA, - 22.05.08 @ 08:57 | #12524
Balali anazikwa Washington!!!!!! Je Serikali imelipokeaje hilo? (Huyu mtu alikuwa na siri kubwa sana na Serikali). Hata kama atazikwa huko au Tanzania,Naomba angalizo juu ya ugonjwa wake na tuhuma dhidi yake (ufisadi). Je inawezekana alipoona anakabiliwa na tuhuma aliamua kunywa sumu yeye mwenyewe? Je ni kwanini alikimbilia huko? Je Tayari alikuwa na himaya yake huko tangu akiwa gavana na ndio maana ameweza kupata hata kibali cha kuzikwa nje ya nchi yake mtu mwenye wadhifa na uwezo wa kurudishwa nyumbani kutunza heshima ya familia na serikali?
na Mamboleo - 22.05.08 @ 09:07 | #12527
HIVI KUMBE SIKU HIZI ZOTE ILIKUWA INAJULIKANA WAPI BALALI YUPO!! DU AMA KWELI MFICHA MARADHI KIFO HUMUUMBUA! LEO HATA NYUMBA YAKE INAJULIKANA ILIKUWA WASHINGTON NA HATA DADA ZAKE JUZI WALIONDOKA KWENDA MJULIA HALI! WALIPITA VIPI HAPA US EMBASSY? KUNA MCHEZO UNACHEZWA HAPA, KAENI CHONJO, HUYO HAJAFA, ILA LIMEULIWA JINA TU, ILI APATIWE JINA JIPYA NA URAIA MPYA AWE MWINGINE KABISA! KALAGABAHO!!
na Mtanzania, Tz, - 22.05.08 @ 09:08 | #12528
muda huu hatutakiwi kuserehekea kifo cha balali kwa sababu kila mmoja atakufa,lakini nadhani hawa ndugu zake wahajaribu kumtetea tu,ukwli ni kwamba kamati ilioundwa kuchunguza kashfa ya epz imebakisha mwezi mmoja tu kuweka kila kitu hadharani,na hii huenda ikawa sababu iliomfanya balali afariki,maaana hata ndugu ake wanasema alisema azikwe huko huko,inamaana alikuwa na wasiwasi mkubwa na alijuwa mwisho wake,mimi bado naimani kuwa itakapotoka taarifa ya epz kutafichuka ma´*** mengine mengi tu,hivi muheshimiwa mkapa yuko wapi,balali alikuwa mtu wake wa karibu sana,kikazi na kifamilia,kwa nini ananyamaza kimya,huu si uungwana,na kama andhani akinyamaza kimya ndo watu watamsahau anajidanganya,hii serikali ya sasa inamvumilia kwa ajili inataka iingie tena madarakani 2010,na inahitaji watu wa mkapa wawape kura,lakini baada ya 2010 watamdhalilisha mkapa,msishangae akipandishwa mahakani,ni bora ajitokeze atueleze watanzania serikali yake ilivyofanya madudu kama hakuhusika.
na john mzalendo - 22.05.08 @ 09:08 | #12529
Kifo cha ndg balali kinatukumbusha wajibu wetu kwa Muumba.mambo yote ya duniani ni ya muda mfupi na yakupita.Ni vema watu tuliokabidhiwa dhamana kuwa waadilifu.Kifo hutukumbusha na kutuasa kuwa wongofu katika maisha yetu.Kila mtu ni lazima kijihukumu mwenyewe kabla ya kuwahukumu wengine.Ufisadi si kwa viongozi tu,bali hata kwa watu wa kawaida.Hatuwezi jua haki ya balali machoni pa Bwana.Tumuombee mwenzetu alietangulia mbele za haki kwani siku ya mwisho kila mmoja wetu anawezajikuta nae yufisadi.Mungu amsamehe na kumrehemu mpendwa wetu Balali.amen
na PETER B KADILIKANSIMBA, TANZANIA/mbeya, - 22.05.08 @ 09:09 | #12530
Hapa nazidi pata wasiwasi juu yakifo cha mheshimiwa huyu.kwan taarifa za kifo chake zinachanganya,Wengine boston(serikali)wengine washington(wanafamilia).Muda wa siku tatu.Kweli serikali ilishindwa kupata taharifa sahihi na kwa haraka!utandawazi kama huu?LAKINI IPO SIKU AMBAYO UKWELI UTAJITENGA NA UONGO.
na alfredy fabian, tanzania, - 22.05.08 @ 09:16 | #12533
Kwanza natoa pole sana kwa ndugu na jamaa wa marehemu Dr. Daud Balali pili naomba serikali ishiriki kikamilifu katika mazishi ya marehemu maana aliifanyia kazi kwa muda mrefu, na baadaye waendelee na uchunguzi wa upotevu wa fedha zetu. Hili linawezekana maana kama gavana ni lazima wasaidizi wake wanajua kilichokuwa kinaendelea kuhusu akaunti ya epa. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi
na amos, Arusha, - 22.05.08 @ 09:18 | #12536
itakuwa vyema zaidi kama Balali atazikwa nchini Tanzania ambako ndiko alikozaliwa, na kulitumikia taifa hili. kwani kwa yote yaliyotokea ni mengi na watanzania tumsamehe, tumuombee kwa Mola apate kupumzika vema peponi. pia mafisadi wengine jifunzeni sana kuhusu nchi hii
na Mrs Kissia, Kahama, - 22.05.08 @ 09:21 | #12537
Balali huko ulikoenda kaa chonjo kujibu tuhuma ulizofanya kuhusiana na nchi hii. binadamu ni mavumbi na mavumbini umerudi hela zote umeziacha wapi?
na Meryciana Joram, Kahama, - 22.05.08 @ 09:24 | #12538
hapo hakuna kifo wanataka macavel style .huyo balali aliogopa nini hata kuzikwa hapa bongo wakati yeye ni safi?hivyo huyo mtu alipanga kutokanyaga tz milele mpaka akatae pia kuzikwa hap?watu kama hawa wanpewaje nyazifa nyeti wakati si wazalendo?pia kumbe waweza kuwa kibuli kwa gvnmt.sas ukweli ni kwamba yupo la azikwe hapa ili kuwe na udhibitisho,na ikishindikana twende watnzania wakutosha kudhibitisha hilo na si ndugu wanatuzingua
na big mo, tanzania, - 22.05.08 @ 09:32 | #12539
Nakumbuka serikali ilisema haimuhitaji Balali kwa sasa,sijui inatuambia nini kwani ndiye mtuhumiwa namba moja katika uwizi wa fedha za EPA.
na robi, arusha, - 22.05.08 @ 09:38 | #12543
Kifo sio kitu kizuri kwa yeyote;tusikitike pamoja na wafiwa.Historia itasema kama Balali alikuwa mkosa au la; lakini Mungu ndiye hakimu wa HAKI.
na john, Tanzania-Dsm, - 22.05.08 @ 09:43 | #12546
Waafrika kukubali kifo cha kawaida huwa si rahisi. Ndio maana hata mzee mwingine akifa akiwa na miaka 80 baadhi ya makabila ya Afrika huenda kupiga bao kujua kwa nini amekufa.
Bahati nzuri Balali amefia kwenye hospitali zenye uwezo mkubwa kiteknolojia. Badala ya waandishi wa hapa bongoland kupepeta pumba eti kapewa sumu wapate ukweli huu kutoka kwa waganga waliomshughulikia huko Marekani.
na Maarufu - 22.05.08 @ 09:43 | #12547
maswaiba wawekwe kiti moto hapo kuna kitu.che brother tunakuomba mwenyewe utoe mali zako na unifuate kabla ya kuukumiwa na wanadam hapa dunian.sas jamaa anakwenda maakama kuu huko hakuna wakili mguu wala kidole kwani haki ya watz haiwezi kwenda bila kuwjibishwa na kufilisiwa mali..kama atzikwa huko basi aliyempa kibarua aliyajua hayo kama si kummaliza ushaidi usiwe na ukweli wa kutosha.sas hakuna kuogopa K KAZA BUTI 2010 tunakupa wewe hao wanopanga kugombea hata maoni hawavuki na wakati huo watakuwa watuhumiwa hawagombei tena
.mwisho mauti yanawakuta na tuhuma nzaito ujafaidi visent zaidi ya posho zetu tu.
na mwenyenia, tanganyika, - 22.05.08 @ 09:47 | #12552
MH, UMAFIA UNA MAMBO. HAPA HUYU KAFA ILI WAANZILISHI WA DILI HILI WAWEZE KUFANIKISHA UONGO WAO. Bila shaka MR. Clean atashanglia sana maana huyu jamaa angekuja kumropokea siku moja. Hongera waliofanikisha kifo chake maana mwosha huoshwa. Lakinio, bado JK ana kazi: Balali alimfukuza.. je mwanzilishi wa dili hili atatajwa?
MJOMBA, BADO MIAKA MIWILI UNATAKIWA UTWAMBIE ULICHOTUAHIDI MWAKA 2005 WAKATI WA KAMPENI KIMEFIKIA WAPI. Maana mpaka sasa naona kama umeduwaa , hujui wapi tunatoka na kuelekea.....hizo ni salamu tu
na nyumbu, Arusha, - 22.05.08 @ 10:08 | #12557
Damn it! Why not mention him we dare talk openly.
Damn it! Why not mention him we dare talk openly.
Siamini kama kufa kwa Balali ndio kufutika kwa ushahidi wote kuhusu EPA. Siamini kama Balali alikuwa akifanya mambo yote haya ndani ya BOT bila kumhusisha mtu mwingine. Ukweli ni kwamba Balali alikuwa ni shahidi mkuu, lakini naamini wapo watu wengine wengi ndani ya BOT, ndani ya Wizara ya Fedha na ndani ya serikali kwa ujumla wenye ushahidi kuhusu ufisadi wa EPA. Cha msingi ni kuwalinda wasinyweshwe "sumu" kama ilivyotokea kwa Balali.