SoC01 Kifo cha mtu uliyemzoea mtihani mgumu sana kufaulu

SoC01 Kifo cha mtu uliyemzoea mtihani mgumu sana kufaulu

Stories of Change - 2021 Competition

Deejay nasmile

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2011
Posts
5,794
Reaction score
5,352
KIFO NI KIBAYA SANA..NI BORA UFE WEWE KULIKO ATANGULIE YULE ULIMPENDA NA KUMZOEA.

Habari wakuu,poleni na majukumu

Najua kila mtu ameshawahi kusikia neno KIFO..ndio ni neno fupi lenye herufi chache tu,Herufi nne yaani K I F O.

Nadhani tukiongelea katika maneno ambayo yanaogopwa na hayapendwi na kiumbe yeyote,neno KIFO linaweza kuwa namba moja.

KIFO hakipendwi, KIFO kinaogopwa,KIFO kinachefua.Haijailishi ni KIFO cha kitu gani,KIFO cha kiumbe hai mfano Binadamu/mnyama au KIFO cha Kitu kingine mfano Biashara,kazi,uhusiano n.k

Hili neno lipo miaka na miaka, nadhani tangu kuumbwa kwa ulimwengu tumekuwa tunalisikia Au kuona kifo cha watu,mimea,wanyama na hata kifo cha biashara,kazi..Japo leo mada kuu ya leo ni kuhusu KIFO cha binadamu.

KIFO NI NINI??
Kifo ni fumbo kubwa sana ambapo hakuna mtu hata mmoja aliye hai anajua fumbo hili,ni fumbo ambalo Mungu amewafumbia wanadamu,viumbe hai,na utajua fumbo hili pindi utakapo kufa.

Japokuwa kuna baadhi ya watu kutokana na imani/akili au mawazo yao wamejaribu kusema maana tofauti tofauti kuhusu KIFO.Wengine wanasema ni KIFO ni Usingizi,ndoto N.k

Lakini maana iliyo kuu au maalumu ni kwamba KIFO ni hali ya kufarakana au kutengana kwa vitu au hali zinazofanya UHAI kuwepo.Ndio Ni tendo la KUKOSA au kutokuwa na UHAI.

Kwanini Kuna KIFO?
Hili swali nalo lina majibu mengi sana kutokana na imani au elimu zetu za duniani.
Kutokana na imani yangu naamini tunakufa ili Kurudi kule kwa MUUMBA WETU.Ndio huwezi kumuona muumba wako kama hujafa,lakini tu kama utatimiza kazi ile uliyotumwa na muumba wako ipasavyo .

KIFO hakina muda maalum ni wakati wowote kifo kinaweza kukumba,haijalishi u mzima au mgonjwa au umejificha mahali gani.

TURUDI KWENYE MADA

Mwaka huu 2021 kwa upande wangu ndio mwaka ambao nimejua uzito,maumivu na ubaya wa KIFO. Nilimpoteza Mtu muhimu. Mtu niliyezoea kumuona kwa miaka yote 30s niliyonayo.Mtu ambaye sikuwahi wala kuweza kuishi naye mbali kwa muda wa miezi mitatu bila kuonana nae.. Hata wakati nikiwa chuo kila mwisho wa semister lazima tu nitaenda kuhakikisha naonana nae,naongea nae,nacheka nae..kisha ndio naendelea na ratiba zingine.

Mtu ambaye hata nikifanya ukorofi,ujinga wowote alikuwa achoki kunitetea. Mtu ambaye nikiwa na huzuni analiwaza na kunipa ushauri HAKIKA nilijiona nina bahati mimi. Sikuwaza kumpoteza Mtu huyu.

Sio kwamba sikuwahi kusikia KIFO,au kuwahi kufiwa kabla.. HAPANA!!..Nilifiwa na Baba yangu mzazi,Bibi na Babu zangu,Mashangazi,Walimu,Marafiki N.k lakini sikuumia sana..

Najua utajiuliza KWANINI?
Je, nilikua siwapendi? HAPANA!
Nilikuwa nawapenda sana,lakini shida kubwa hapa ni ...

UPENDO NA MAZOEA
Wakati baba anafariki nilikuwa na miaka 4..kwa hiyo hapo utaona kuwa kwanza sikuwa na kitu HISIA na kujua nini kimetokea kutokana na umri wangu..Pia sikumzoea sana kutokana na kuishi nae muda mchache (4yrs)

Nilifiwa na marafiki,jamaa na ndugu wengine wengi. Hao wote niliumia lakini naweza kusema sio sana...au niseme maumivu/majonzi yaliwahi kuisha/kusahaulika mapema.

KWANINI?
Ni kwa sababu niliwapenda ila SIKUWAZOEA!!

Mwalimu ilikuwa ni mpaka nimuone shuleni/darasani tu,
Shangazi au Rafiki ni mpaka tukutane kwenye miadi,kikao,michezo au kwa shughuli flani.
Hivyo tukiachana hapo kila mtu anawaza yake anaendelea na mambo yake. Je? Hujawahi kuona unapata taarifa tu kuwa rafiki yako yule siku hizi Mbunge! Alafu ukawa hujui aliingia lini kwenye siasa,chama gani wala jimbo gani..??
Au shangazi yako amefariki !!! ukawa hujui ameumwa lini,au alipatwa na nini.

NDIO MAANA NAONA NI BORA NINGETANGULIA MIMI (MUNGU ANISAMEHE KAMA NAKOSOA KAZI YAKE)KULIKO YULE NILIYEMPENDA NA KUMZOEA!!!

MAMA! MAMA YANGU

Umeniachia pigo kubwa sana katika maisha yangu, sidhani kama nitakuja kuamini kuwa sitakuona tena..MAMA nilikupenda,ninakupenda na nitakupenda daima...SIO TU NILIKUPENDA LAKINI PIA NILIKUZOEA SANA.

Kuna muda natamani hata nisikanyage hapa nyumbani pale tu ninapokumbuka kuwa HAUPO tena humu ndani...NILIZOEA nikitoka huko mtaani nakuja nakusimulia story zote zinazoendelea huko mtaani,nikifanya jambo baya unaniita kwa upole,unanikalisha na kunifundisha namna nzuri ya kuishi.

Juzi timu yetu pendwa imepatwa na matokeo mabaya najua Tungeliwazana wenyewe.Lakini nasikitika hata hukupata nafasi ya kutazama timu yako pendwa japo uliipania sana Ile mechi..Na sio hayo tu kuna mambo mengi tulipanga but hayajakamilika bado na UMENIACHA mpendwa wangu.najua hata nikikamilisha peke yangu sitakuwa na fuaraha sana kama vile na wewe ungeona kile tulichopanga kimekamilika..sitakuwa na thamani nacho kama wewe HAUPO..

MAMA ni mtu ambaye kwangu mimi alikuwa ni kila kitu..Ilifika mahali nilisahau kabisa kama kuna KIFO..Na hata mara chache nilipokuwa nikikumbuka kuhusu KIFO nilijua ni mimi nitakufa,yule atakufa,wale watakufa ila sio yeye MAMA.sikawahi kujua watu wanapitia uchungu wa namna hii..Nilidhani wanajiliza tu kujifanyisha,niliwaona ni wajinga sio majasiri,lakini HATIMAYE pamoja na ujasiri wangu hatimaye NIMELIA MIMI, NIMELIA MBELE ZA WATU...MBELE YA WATOTO WADOGO.....Mtu NILIYEMPENDA NA KUMZOEA HAYUPO TENA..SITAMUONA TENA DAH!!!


HEBU FIKILIA YULE UNAYEMPENDA NA ULIYEMZOEA

1:ANAKUFA!

Yaan hana pumzi,haongei unamuuliza hakujibu,unatamani umpe kile chakula akipendacho lakini hawezi kula.Unaiona namba yake ya simu kwenye simu yako unatamani kumpigia lakini unakumbuka kuwa HATAPOKEA,Hatajibu sms...unawaza vipi niifute? HAPANA!! HAPANA!! Huko aliko ananiona nafuta namba yake...anasikitika kuwa namtenga ..SIWEZI kuifuta namba yake na sitaisahau Daima..

2:Mnamuweka kwenye JENEZA.
Marafiki zako,ndugu zako wanaenda kuchagua jeneza,huku wakisema HILI ZURI!! dah kuna JENEZA zuri??? unatamani uwatukane,unaona kama wanafanya ukatili..lakini BASI SASA!! Ndio utaratibu huo.


3:MNAMFUKIA chini ya ardhi..
Unawaza Vipi
Labda pengine Alilala tu na ameamka na kuzinduka kisha anatuita tumfukue lakini hatusikii na tunaondoka tu,
Mnamuacha peke ake makaburini,anakata tamaa..anajiuliza mpaka wewe kipenzi chake unamtenga?? humsikii??
Usiku vile unavotisha lakini unamuacha kule peke ake??...Lakini wewe umelala ndani,umejifunika shuka! umewasha taa! na umefunga milango..INAUMA SANA !!!

Ni MTIHANI MGUMU SANA KUMPOTEZA MTU ULIYEMZOEA...KUNA MUDA NAJIULIZA KWANINI NISINGEANZA MIMI AKABAKI YEYE...PUMZIKA MAMA YANGU

HITIMISHO:
NAJUA KILA MTU ANA MTU WAKE ANAYEMPENDA NA ALIYEMZOEA AMBAYE HAKUPENDA/HATAPENDA AFIKWE NA UMAUTI.LAKINI AMINI KIFO KIPO JAPO HATUKIPENDI,MIMI NIMEAMINI JAMANI KIFO KIPO.

MIMI KIFO CHA MAMA NI KIFO KINACHONIPA MTIHANI MKUBWA SANA WA KUSAHAU..SIDHANI KAMA NITAFAULU,WAPO WANAOMPENDA NA WALIOMZOEA
BABA YAO
MAMA YAO
DADA YAO
KAKA YAO
MKE WAKO
MUME WAKO
MTOTO/WATOTO WAKO
N.K
JE UTAFAULU MTIHANI WA UCHUNGU UTAKAOPITIA SIKU WAKITUTOKA?? SIKU KIKIWAKUMBA????


TUZIDI KUWAOMBEA KWA MWENYEZI MUNGU KILA SIKU.SARA NI MUHIMU..
INAUMA SANA KUFIWA NA UNAYEMPENDA NA ULIYEMZOEA.

LAKINI PIA TUKUMBUKE KUWA SIO KILA KIFO NI KIBAYA KUTOKANA NA TULIVYOJIANDA SISI WENYEWE KWA MUUMBA WETU.

Tunapitia kipindi kigumu sana..

Ewe Mola, nisamehe dhambi zangu, dhambi za baba yangu, mama yangu, mke/mume wangu na wanangu na jamaa zangu na marafiki.
Ewe Mwenyezi Mungu , usiuchukue uhai wangu ila pale nitakapo kuwa tayari kukutana nawe.AMEENI


By nasmiletz
july 2021
nasmiletz@gmail.com
 
Upvote 23
Neno la Mungu linasema jinsi Mwanadamu alivyoumbwa kwanza.
#Mwanzo 2:7 BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
#NOTE: Kumbe Mwanadamu aliumbwa kwa Mavumbi au Udongo. Na baada ya kuumbwa kwa Mavumbi huyu Mwanadamu hakuwa na uhai, Ndipo Mungu akampulizia Mwanadamu pumzi ya uhai puani.
#note: Ili Mwanadamu aweze kuwa kiumbe hai ilibidi Apuliziwe pumzi ya Mungu, na sio aliwekewa.
Hivo kuna siku binadam atakufa...Hapo najifunza kuwa kufa ni lazima lakini kinauma sana hasa kwa mtu unayempenda na kumzoea..
 
Ukweli ni kwamba ili shindano linaanza kukosa maana.

Uwezi kuandika article ya ushauri on first person, na ili tatizo lipo kwa watu ambao mpaka wanajiita professionals.

Hii topic sijui kwa kiswahili inaitwaje lakini kwa watu waliosoma ‘health and social work management’ ulaya hii topic inaitwa ‘siginificant life events’.

Kuidadavua lazima uzungumzie psychology ya mazoea kwanza using existing academic literature kuelezea kwanini inakuwa shida ku cope na hayo mabadiliko.

Then explain changamoto zako by analysing literature in third or second person.

Hivi vyuo vyetu vinashida hamjui kuandika academically 90% ya watu mlioanzisha mada and about 95% ya proposal advice are written in first person without appropriate literature review nor subject matter.

Our education system needs an overhaul, nyie watu amjatatarishwa vizuri hamjui kuandika.
Asante.kwa ushauri na darasa
 
KIFO NI KIBAYA SANA..NI BORA UFE WEWE KULIKO ATANGULIE YULE ULIMPENDA NA KUMZOEA
Hii ni kauli ya dependant. Mfano mama wa nyumbani kufiwa na mume aliyekuwa anamtegemea kwa kila kitu. Unless, hata afe nani, unaweza ku move on ndani ya mwezi mmoja as long as ulikuwa humtegemei kiuchumi.
 
Hii ni kauli ya dependant. Mfano mama wa nyumbani kufiwa na mume aliyekuwa anamtegemea kwa kila kitu. Unless, hata afe nani, unaweza ku move on ndani ya mwezi mmoja as long as ulikuwa humtegemei kiuchumi.
Ndani ya mwez mmoja haiwezekan mkuu..labda kama hamkuzoeana....
 
Hii ni kauli ya dependant. Mfano mama wa nyumbani kufiwa na mume aliyekuwa anamtegemea kwa kila kitu. Unless, hata afe nani, unaweza ku move on ndani ya mwezi mmoja as long as ulikuwa humtegemei kiuchumi.
Mkuu kupitia hali kama hii ni ngum sana...ndio maana baadhi wanahama kabisa makaz yao,au wanauza vitu vyote ili tu kupunguza mawazi hasa wanapoviona vitu ambavyo vinamkumbusha mpendwa wake
 
Death is Inevitable....

“I learned that everyone dies alone. But if you meant something to someone, if you helped someone, or loved someone. If even a single person remembers you, then maybe you never really die.” Person of Interest
 
kuna baadhi ya mambo au vt vinatokea/unaviona vinakurudisha nyuma enzi za lifestyle ile uliyoish na marehem..mfano muziki,maeneo mliyozoea kutembelea,vyakula,marafiki/kampan n.k
 
Pole sana mkuu. Tuseme nini sasa kama sio Bwana kuteta nasi katika vipindi vigumu vya majonzi
 
kuna baadhi ya mambo au vt vinatokea/unaviona vinakurudisha nyuma enzi za lifestyle ile uliyoish na marehem..mfano muziki,maeneo mliyozoea kutembelea,vyakula,marafiki/kampan n.k
kuna baadhi ya mambo au vt vinatokea/unaviona vinakurudisha nyuma enzi za lifestyle ile uliyoish na marehem..mfano muziki,maeneo mliyozoea kutembelea,vyakula,marafiki/kampan n.k
 
Ndani ya mwez mmoja haiwezekan mkuu..labda kama hamkuzoeana....
kuna watoto wa kiume huwa wanadekezwa sana na mama zao...kuna wanaume wanaoa na wanakuwa wategemezi sana (siyo kifedha, ila ni huduma za mke) kwa wake zao ...hawa watu wakiondokewaga huwa wanaona maisha yamefika mwisho! Mi nashukuru nilioaga mwanamke ambaye alikuwa hanihudumii chochote kama mume zaidi ya kunipa tendo la ndoa..hivyo baada ya yeye kuondoka duniani , ikawa rahisi kwangu ku adapt sababu hakuna nilichokuwa na kimiss kwake zaidi ya mazoea na mastress kibao, na tendo la ndoa linapatikana popote
 
Mwamba utasahau tu mzeee wote tulijua itakuwa ivoo
yaani utasahau afu inakuwa story ya kaiwaida tu, sema utofauti ni kwamba utaishi kwa kuthamini mchango wao katika maisha yako nk
you have my vote
 
Back
Top Bottom