Kifo cha Sokoine: Watoto wake wataka mwili uchunguzwe kubaini kama alikufa kwa ajali au la!

Kifo cha Sokoine: Watoto wake wataka mwili uchunguzwe kubaini kama alikufa kwa ajali au la!

Watazame mambo mengine ya kufanya kwa kuwa kifochake kilitokana na ajali ya gari labda wamtafute mkimbizi Dube wa afrika kusini maana hata uchunguzi ukifanywa watakuta mifupa imevunjika kitu ambacho nikweli kwa sababu ya ajali this is too late jombaa!
 
Hata kifo cha nyerere kichunguzwe bana kuna vitu mi sivielewi kabisa
 
hapa utakuta kuna gamba moja kishaenda kupandikiza chuki ndani ya family.yetu macho na masikio
 
Hii habari inanichanganya. Nakiri kwamba sikuwahi kusikia kabisa habari za mazishi ya pili ya Ndugu Edward Moringe Sokoine hapo mwaka jana (sijui ni tarehe zip za mwezi upi?). N'nachokumbuka tu ni kwamba Moringe tulimzika katikati ya zizi la ng'ombe kijijini kwao Monduli na zizi likaendelea kutumika kusetiri ng'ombe kama ilivyo desturi yetu. Nakumbuka mengi yalisemwa baada ya kifo cha Moringe; ya kishirikina na ya kimafya kinyume kabisa na "post mortem report" ya madaktari. Leo ninapopata habari kama hii najiuliza maswali yafuatayo:

  1. tangu Sokoine afariki tarehe 12 Aprili 1984 hao watoto wake walikuwa wapi?
  2. Post mortem investigation hufainyika ili kubaini sababu za kifo cha marehemu si kwa malengo ya maelezo na kumbu kumbu tu bali pia ili kuchukua hatua kama kuna ushaidi wa kutosha kwamba kifo kimesababishwa na uzembe au makusudi ya mtu yeyote. uchunguzi huu ukifanyika sasa na ikagundulika kuna mazingira ya kuwa kifo kilisababishwa na makusudi au uzembe wa yeyote itasaida nini iwapo wasabishaji walishakufa miaka mingi?
  3. Mazingira mazuri zaidi ya kufanya post mortem investigation ni wakatimwili bado mbichi kikemikali. Kwa hali ya kifo hiki cha takribani miaka 29 tangu kitokee na mazingira aliyozikwa (na kuzikwa tena baada ya tetemeko) huo uchunguzi utatumia sayansi ipi?
  4. Uchunguzi huu unachochewa na nini sasa hivi na una maslahi gani kwa taifa na familia (kwa hao watoto wa marehemu?)
watoto wamekuwa sasa na bila shaka wameelimika
 
kwani vipi mbona mashaka miongoni mwetu,naomba tukaombe serikali ya marekani mwili wa BALALI maana hapo kuna tija kwa watanzania wengi.
Kazi ya Lowasa hiyo.

Natamani wangefanya vile wakati Marehemu Mzee Kawawa na Cleopa Msuya wote wakiwepo.
 
kwani vipi mbona mashaka miongoni mwetu kila tukionana nami ,naomba tukaombe serikali ya marekani mwili wa BALALI uchunguzwe maana hapo kuna tija kwa watanzania wengi.
Kazi ya Lowasa hiyo.

Natamani wangefanya vile wakati Marehemu Mzee Kawawa na Cleopa Msuya wote wakiwepo.
 
kwani vipi? mbona mashaka miongoni mwetu kila tukio nami ,naomba tukaombe serikali ya marekani mwili wa BALALI uchunguzwe maana hapo kuna tija kwa watanzania wengi.
Kazi ya Lowasa hiyo.

Natamani wangefanya vile wakati Marehemu Mzee Kawawa na Cleopa Msuya wote wakiwepo.
 
inawezekana kuna viashiria ambavyo watoto waliviona wakati wa kuhamisha mwili wa baba yao na kuuzika mara ya pili
tumeona fuvu la farao mahali fulani humu humu jf ambaye alikufa na kuzikwa zamani,
sembuse sokoine wa majuzi tu, acha watoto wachunguze mwili wa baba yao ili wajiridhishe wenyewe.
 
Itawasaidia nini hata kama wakijua aliuawawa na si kufa kwa ajali ya gari?
 
kwani vipi? mbona mashaka miongoni mwetu kila tukio nami ,naomba tukaombe serikali ya marekani mwili wa BALALI uchunguzwe maana hapo kuna tija kwa watanzania wengi.
Ngoswe, la BALALI umenena. Mimi hata nikiambiwa nitoe mchango kufanikisha zoezi hilo nilikuwa tayari ila tu serikali ikubali kuwajibisha kila aliyehusika na tukio la kiaina hilo. Wewe uliona wapi msibani watu wanaingia kwa card tena tkatika tamaduni zetu hapa. Umewahi kusikia tena baada ya msiba huo kuna mweingine umetokea wa namna hiyo? LA SOKOINE NDUGU YANGU KAMA HUJUI, CHAMA KILISHIKA HATAMU!NATAMANI WAFANYE KWA GHARAMA ZA FAMILIA ILA NA DR ALIYEKUWA ZAMU MOROGORO SIKU HIYO ATUSAIDIE KUELEZA SOKOINE ALIFARIKI AKIWA WAPI?
 
Siri kubwa kuhusiana na kifo cha Sokoine anayo Lowassa, kwa hili hata JKN alikuwa anamgwaya sana Edo! Mnakumbuka jinsi ambvyo edo alimtaka JKN aende Monduli kumsafisha baada ya kumtuhumu kuwa alimchafulia jina kwa kauli zake? Captain Lowassa ana mambo mengi ambayo akiamua kuyaweka hadharani watu wengi sana watabadilika kimitazamo!

Sijui kwanini ameamua kukaa kimya hata pale ambapo huwa anaonewa wazi kabisa! kuna watu ambao hofu haziwaishi kwa kuogopa kuwa ipo siku atalipiza kisasi kwa wanayomtendea hivyo kuzidisha kasi ya kuendelea kumchafua.

...Moringe aliuawa na hili halina pingamizi! kuna watu walikuwa hawako radhi kumuona mtu anambishia JKN...walikuwa wanauwezo wa kukupoteza faster then wanaenda kumpa taarifa! wakati mwingine JKN alikuwa anaishia kusikitika tu maana hakuwa na uwezo wa kurejesha uhai!
 
Binti yake marehemu kapewa zawadi ya special seat mp! Atakubali hayo?? Hata dr aliyemfanyia postmortem mbona alikufa kwa mazingira ya kutatanisha? Chezea ccm weye?
 
Ikisha bainika hakufa kwa ajali itasaidia nini sasa ambapo ni muda mrefu tangu kifo kitokee? Hao watoto nao! Badala ya kumuombea baba yao apumzike kwa amani wao wanataka kuanza kuhangaika na mambo ya uchunguzi. R.I.P Moringe.
 
Back
Top Bottom