#COVID19 Kihongosi: Polepole uwe na nidhamu na adabu kama ulivyokuwa Awamu ya Tano

#COVID19 Kihongosi: Polepole uwe na nidhamu na adabu kama ulivyokuwa Awamu ya Tano

Ipo shida kwa Safu ya CCM, mwenezi nae! Bora Wamshukuru Kamanda Ssiro kwa support.
 
"Chama cha Mapinduzi (CCM) sio chama cha harakati bali ni chama kilichojijenga katika misingi ya kutii na kuheshimu viongozi, hivyo jambo lolote la kupingana au kuendeleza mijadala ambayo Mwenyekiti wa CCM Taifa ameshalitolea maelekezo ni utovu wa nidhamu" hayo yamesemwa leo tarehe08.08.2021 na Ndugu Kenani Kihongosi ambaye ni katibu wa umoja wa vijana ccm taifa

"Maendeleo hayana vyama lakini tuheshimu uhuru wa maoni yoyote ya kila mwananchi kutoa maoni yake siyo dhambi wala siyo kupinga kila mtu anamitazamo yake"
 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Ndugu Kenani Kihongosi amemtaka Mbunge wa kuteuliwa wa CCM na aliyewahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Ndugu Humphrey Polepole kuwa na nidhamu na adabu kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya 6 iliyo chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kama aliyokuwa nayo kipindi cha awamu...
Humphrey Polepole ni mpuuzi na mnafiki sana! Hayati Rais Magufuli aliondoka kipindi ambacho hawakutegemea!

Hata hivyo Rais Magufuli alishamshtukia kwa upigaji, walipiga sana pesa kwenye kupitisha wagombea Ubunge wa CCM 2020!
Katibu Mkuu UVCCM mwambie kabisa Polepole kuwa wao ni CCM maslahi ambao hubadilika kulingana na upepo!

Wakati wa Magufuli akina Polepole walijifanya mazezeta wa kujichekeshachekesha hadi aibu! Walimjua Rais Magufuli kuwa ni mpenda sifa na kwa kweli walijitahidi kumsifia na kum- win Magufuli!

Wao walijua Rais Magufuli alikuwa ni Mungu na kumbuka hata Prof.Palamagamba Kabudi alifikia kuropoka na kumwita Magufuli, Mheshimiwa Mungu!

Aggrey Mwanri yeye akataka Mwenyezi Mungu amshukuru Magufuli! Tunajua vijembe vyote anavyotoa kuhusu COVID 19 ni kumpinga Rais Samia Suluhu Hassan kwani kawapiga chini!

Bila uteuzi Polepole anaweza kushinda nini ndani ya CCM?

Tunajua mipango yao yote dhidi ya Rais Samia na hawatakaa wafanikiwe hata saa moja!

Polepole ni panya tu anayetumwa kupima upepo!
 
CCM inasemewa na Stephen Nyerere.!? Maskini Tanzania ndio tulipofikia hapa. Uhiari wa chanjo unafungwa na Rais kuchanja? Kwa nini waliochanja wawe na haki ya kuhimiza wasio chanja kuchanja. Wasio chanja wasiwe na haki ya kuhimiza watu waikatae chanjo yenye walakini mwingi.

Kwa nini Mh Polepole na sio Mh Askofu Gwajima? Ubunge wa Polepole alipewa na JPM hili nalo UV-CCM hawalijui? Heshima hailazimishiwi itakuja yenyewe kutokana na matendo yako kwa jamii.
 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi - UVCCM, Kenani Kihongosi amesema, wanasikitishwa na matendo yanayofanywa na mbunge Humphrey Polepole kuhusu suala la ya Covid-19, kwani Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameshasema kwamba chanjo ni hiyari na maamuzi yake lazima yaheshimiwe.

"Tunapenda kumwambia mbunge Humphrey Polepole kwamba awe na nidhamu na adabu kama aliyokuwa nayo wakati wa Utawala wa Awamu ya Tano. Nidhamu ile ile aiendeleze pia katika utawala huu wa awamu ya Sita Inayoongozwa na Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan " Kenani Kihongosi, Katibu Mkuu wa UVCCM.

"Mijadala yake (Humphrey Polepole) kuhusu chanjo ni bora akakaa kimya kama hahitaji kuchanja lakini sio kujificha katika kivuli cha chanjo kuipinga serikali." Kenani Kihongosi, Katibu Mkuu wa UVCCM.

"Tunamuonya na tunamtaka Humphrey Polepole aache mara moja mijadala yake kuhusu chanjo kwani hatutakubali kiongozi yoyote avunje heshima ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan au kupinga yale aliyoyaelekeza" Ndugu Kenani Kihongosi, Katibu Mkuu wa UVCCM.

"Hatutovumilia utovu wowote wa nidhamu kwa Rais. Humphrey Polepole kuendelea kutengeneza maneno ya kejeli, dhihaka na mengine ya aina hiyo yanabeba mazingira yanayotia shaka dhamira yake aliyonayo kwa Mwenyekiti wetu na Rais wetu, hivyo tunamtaka aache mara moja" Kenani Kihongosi.

"Chama cha Mapinduzi (CCM) siyo chama cha harakati bali ni chama kilichojijenga katika misingi ya kutii na kuheshimu viongozi, hivyo jambo lolote la kupingana au kuendeleza mijadala ambayo Mwenyekiti wa CCM Taifa ameshalitolea maelekezo ni utovu wa nidhamu"

Ndugu. Kenani Kihongosi
Katibu Mkuu wa UVCCM.


E8SZYC3XMAU-vNH.jpg


E8SZYSXWEAIubt3.jpg
 
CCM inasemewa na Stephen Nyerere.!? Maskini Tanzania ndio tulipofikia hapa. Uhiari wa chanjo unafungwa na Rais kuchanja? Kwa nini waliochanja wawe na haki ya kuhimiza wasio chanja kuchanja. Wasio chanja wasiwe na haki ya kuhimiza watu waikatae chanjo nyenye walakini mwingi.

Kwa nini Mh Polepole na sio Mh Askofu Gwajima? Ubunge wa Polepole alipewa na JPM hili nalo UV-CCM hawalijui? Heshima hailazimishiwi itakuja yenyewe kutokana na matendo yako kwa jamii.
Pole pole na Gwajima ni wanafiki.
Pole pole na Gwajima ni CCM maslah.
Pole pole na Gwajima Wana chuki na roho mbaya sana ya wivu.
Pole pole na Gwajima ni benders data upepo, hawana msimamo.
Pole pole mlafi wa madaraka. Alitaka awe mwenezi wa milele CCM?? Muasisi wa chama mwalimu aling'atuka, yeye nani mpaka awe against na chama kimadharau? Pole pole tulia, kinda heshma yako.
Gwajima galiba ya Joseph Kibwetere.
Gwajima Ana hofu ya biashara yake ya sadaka kuathiriwa na hii vita dhidi ya corona, Ile ni biashara pale hemani anafanya. Hivi watanzania wenzangu tunasahau Mara hii huyu alilaghai hua anafufua wafu?? Tumesahau Ile video yenye sura yake ya utupu kweli [emoji24][emoji24][emoji24]

SERIKALI isipokua makini na huyu Gwajima atasababisha maafa.
 
CCM is dead. Kuna vitoto vitoto tu ambavyo vinasaka ajira tu maskini. Huyo ni kiongozi ndani ya secretariat. Hata ukimuuliza mahitaji ya umeme ya Tanzania mwaka 2035 hata hajui. Halafu ni vizuri hawa vijana wafahamu how systems work. Hii ni nchi.
 
"Chama cha Mapinduzi (CCM) sio chama cha harakati bali ni chama kilichojijenga katika misingi ya kutii na kuheshimu viongozi, hivyo jambo lolote la kupingana au kuendeleza mijadala ambayo Mwenyekiti wa CCM Taifa ameshalitolea maelekezo ni utovu wa nidhamu" hayo yamesemwa leo tarehe08.08.2021 na Ndugu Kenani Kihongosi ambaye ni katibu wa umoja wa vijana ccm taifa

"Maendeleo hayana vyama lakini tuheshimu uhuru wa maoni yoyote ya kila mwananchi kutoa maoni yake siyo dhambi wala siyo kupinga kila mtu anamitazamo yake"
Mwenyekiti aliyepita alitoa Maelekezo gani?

Mbona hamuyafuati
 
TATIZO NI KWAMBA UONGOZI WA CCM UMEKUA NA MANENO MENGI BILA MATENDO. KUNA AKINA GWAJIMA WAMEKUFURU NA MNAWANYAMAZIA TU.
 
Katibu Mkuu wa UVCCM ,Camarada El Comandante mtunduizi mh.Kenani Kihongosi amemtaka mh.mbunge kamarada Humphrey Polepole atambue kuwa CCM si chama Cha kiharakati (vilivyo vya upinzani) bali chama kilichoaminiwa vyema na watanzania kusimamia maslahi yao kuntu.

Ameendelea kumkumbusha kaka yetu ndugu H.Polepole kuwa CCM imesimikwa juu ya nidhamu kuu kwa mwenyekiti wetu na viongozi wengine.

Hii ni ada na kawaida ya CCM inayosisitiziwa sana katika MADARASA YA ITIKADI.

Kamarada Kenani Kihongosi amemkumbusha ndg.Kamarada Polepole ya kwamba AENDELEE KUIHESHIMU SERIKALI NA VIONGOZI WAKE KAMA ALIVYOFANYA NA KUONEKANA AKIENENDA VYEMA WAKATI WA UTAWALA WA AWAMU YA 5.

Ndg.Polepole anakumbushwa kuwa CHANJO NI HIYARI NA SI LAZIMA....ila kuipinga kwa hoja kinzani ni kumpinga mwenyekiti wake wa CCM mh.Rais SSH na SERIKALI YAKE.


SIEMPRE CCM
HASTA LA VICTORIA CCM

#SiempreSSH
#TujitokezeniKuchanjwa
#KaziIendelee
 
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Ndugu Kenani Kihongosi amemtaka Mbunge wa kuteuliwa wa CCM na aliyewahi kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Ndugu Humphrey Polepole kuwa na nidhamu na adabu kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya 6 iliyo chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kama aliyokuwa nayo kipindi cha awamu ya 5 iliyokuwa inaongozwa na Hayati Rais Magufuli na kumuonya kuwa kama Vijana hawatakubali na kuvumilia mtu yeyote ndani ya Chama hicho kuvunja heshima au kupinga maelekezo ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniah Mhe Samia Suluhu Hassan.

Ndugu Kihongosi amesema hawatavumilia maneno ya kejeli, dhihaka na mengine ya aina hiyo ambayo yanabeba dhamira ya kutia doa dhamira njema ya Rais Samia kwa nchi hii na kumtaka Ndugu Polepole kuacha mara moja mijadala yake kuhusu chanjo ambayo amekuwa akiibua siku za hivi karibuni.

Kihongosi ameenda mbali zaidi kwa kusema wanasikitika sana na matendo ya upotoshaji ya Polepole kuhusu suala la chanjo na kumtaka kukaa kimya kama hahitaji kuchanja lakini sio kujificha kwenye suala la chanjo kuipinga Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan ambayo imeonyesha nia njema ya kuwalinda Watanzania.

Mwisho na tena kwa kukazia Ndugu Kihongosi akamtaka Polepole kuelewa kwamba CCM sio Chama cha kiharakati bali ni Chama kilichojijenga katika misingi ya kutii na kuheshimu viongozi hivyo jambo la kupingana na kuendeleza mijadala ambayo Mwenyekiti wa CCM ameshaitolea maelekezo ni utovu wa nidhamu.

Maneno hayo ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kenani Kihongosi ya kusikitishwa kwake na mienendo ya Mbunge Polepole yanakuja baada ya kushuhudia siku za hivi karibuni Ndugu Polepole akishiriki mijadala ya kwenda kinyume na maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Mhe Samia Suluhu Hassan, maelekezo ya Chama na Serikali kuhusu chanjo ya Uviko-19.

#MtumishiWaWote
#KaziIendelee

CCM angalieni msije mkawa mfano mbaya kwa CHADEMA. Kuraruana kwenu kwa style hii kunaweza kuwahamasisha BAVICHA kuwawinda kwa shoka na mapanga wote wanaowaona kuwa ni waasi dhidi ya Ayatollah Freeman Mbowe, ambaye wanasadiki ni msafi kuliko wasafi wote wa nchi hii!
 
Back
Top Bottom