Kiini cha Falsafa, dini za Uislamu na Ukristu ni Afrika

Kiini cha Falsafa, dini za Uislamu na Ukristu ni Afrika

Eiyer kuna watu hupaswi kujibizana nao... its a waste...!
Not a waste, kama huna hoja za kumpinga jamaa ni bora ukagonga like tu.

Hoja za jamaa zinaeleweka, there is no one being who is responsible for creation, is to be worshiped na vitu kama hivyo,
Jamaa yuko sawa tu, ukiangalia wakristo mungu wao ni tofauti kabisa na wa waislamu, wahindu ni tofauti na wa wayahudi n.k,

So who is God by the way
 
Not a waste, kama huna hoja za kumpinga jamaa ni bora ukagonga like tu.

Hoja za jamaa zinaeleweka, there is no one being who is responsible for creation, is to be worshiped na vitu kama hivyo,
Una ushahidi kuwa hakuna?
Jamaa yuko sawa tu, ukiangalia wakristo mungu wao ni tofauti kabisa na wa waislamu, wahindu ni tofauti na wa wayahudi n.k,

So who is God by the way
Nni sawa na useme hakuna njia ya kwenda Dar es Salaam kwasababu tu kuna watu 40 na kila mmoja anasema anajua njia na wote wanatofautiana

Hii ni hatari sana!
 
Huu ni ufinyu tu wa fikra kama kigezo cha lugha kinakutoa nje utawezaje kudadavua hoja za kiundani?

Je hicho kinyamwezi chako kinajitosheleza kichwani kwako? Je,hicho kinyamwezi chako kinatosheleza kuelezea dhana za kiimani na kihistoria kutoka katika muktadha wa kiafrika, kiarabu, kigiriki, kiebrania, kimharaki, kilatin na kimisri?

Lugha ya mkopo haiwezi kukutosheleza aidha, hakuna lugha inayoshindwa kuelezea dhana" concept" za lugha nyingine. Na ndio maana utamaduni wa kiafrika au kihindi(mf.Kigujarati) unaweza elezwa kwa kiingereza japo waingereza hawana msamiati kwa kila neno na dhana ya kiafrika au kihindi.

Wewe ulipaswa useme hivi kwa kuwa suala ninaloenda kulijadili ni pana nitalazimika kuchanganya msimbo. Hili ni jambo la kawaida katika lugha, je hivi unajua kwamba % 40 ya maneno ya kiingereza yamekopwa na kutohorewa kutoka kifaransa? Je unajua kwamba maneno ya kisayansi takribani % 80 katika kiingereza yanatokana na kigiriki na kilatini? Ndivyo kwa kijapan, kichina, kirusi nk.

Hivyo basi, ukitumia lugha ya kiswahili kujadili mada yako huku ukitupia maneno ya kirejista na kiistilahi utakuwa unaikuza lugha ya kiswahili.

Heshima yako mkuu, umenena jambo la msingi sana na mwenye macho ametazama, anayetumia pua kuona ndiye atakayepingana na maelezo yako.
 
Huu ni ufinyu tu wa fikra kama kigezo cha lugha kinakutoa nje utawezaje kudadavua hoja za kiundani?

Je hicho kinyamwezi chako kinajitosheleza kichwani kwako? Je,hicho kinyamwezi chako kinatosheleza kuelezea dhana za kiimani na kihistoria kutoka katika muktadha wa kiafrika, kiarabu, kigiriki, kiebrania, kimharaki, kilatin na kimisri?

Lugha ya mkopo haiwezi kukutosheleza aidha, hakuna lugha inayoshindwa kuelezea dhana" concept" za lugha nyingine. Na ndio maana utamaduni wa kiafrika au kihindi(mf.Kigujarati) unaweza elezwa kwa kiingereza japo waingereza hawana msamiati kwa kila neno na dhana ya kiafrika au kihindi.

Wewe ulipaswa useme hivi kwa kuwa suala ninaloenda kulijadili ni pana nitalazimika kuchanganya msimbo. Hili ni jambo la kawaida katika lugha, je hivi unajua kwamba % 40 ya maneno ya kiingereza yamekopwa na kutohorewa kutoka kifaransa? Je unajua kwamba maneno ya kisayansi takribani % 80 katika kiingereza yanatokana na kigiriki na kilatini? Ndivyo kwa kijapan, kichina, kirusi nk.

Hivyo basi, ukitumia lugha ya kiswahili kujadili mada yako huku ukitupia maneno ya kirejista na kiistilahi utakuwa unaikuza lugha ya kiswahili.

Asante kwa kumpa somo la bure huyu jamaa maana hawa watu wamezidi sana kuidharau lugha yao na kuona lugha za wengine ni bora zaidi!
 
weka ushahidi wewe kama kweli yupo!

Hii tabia ya kuuliza swali kabla ya kujibu swali mmeitoa wapi?

Huyo mwenzako kakurupuka huko alikotoka na kuja kudai ana ushahidi pamoja na mtoa mada,nikamuuliza ulipo huo ushahidi,kabla hata hawajajibu wewe nawe unakurupika kutoka huko unakuja kuuliza swali bila kuangalia nani aleyeanza kuuliza swali

Nyie watu mna matatizo sana!
 
Wandungu, kwanza sitaki hii topic ijadili kuwepo au kutokuwepo kwa Mungu. Naomba msiharibu uzi huu. Katika topic hii nataka kuonyesha kuwa kiini cha dini za kiislamu na kikristu ni mawazo ya waafrika wa kale. Baadae nitaingia kwenye falsafa na nitaonyesha kuwa falsafa/ science ya ‘wagiriki' ilitoka Misri kwa kiasi kikubwa kama wagiriki wenyewe walivyosema.

Tuanze na Dini.
Msingi wa uislamu na ukristu na Judaism uko kwenye agano la kale, na agano la kale linasema kwamba Musa, ambaye aliwapa amri kumi za Mungu na kuwatoa wayahudi utumwani Misri aliishi Misri ( Afrika) tangia kuzaliwa mpaka miaka zaidi ya 40. Kama aya hii inavyosema hapa chini,

ACTS 7:20-21
‘At that time Moses was born, and he was no ordinary child.d For three months he was cared for by his family. 21When he was placed outside, Pharaoh's daughter took him and brought him up as her own son. 22Moses was educated in all the wisdom of the Egyptians and was powerful in speech and action.

Sasa hapa tunaona kuwa Moses alizijua mila zote za wamisri , isitoshe alizaliwa misri, na bila shaka mtizamo wake ulikuwa wakimisri ( wa kiafrika) zaidi ya kuwa ' kiisraeli' kuna hata wanazuoni wengine wanaosema kuwa Moses alikuwa ‘mwafrika' lakini that is an argument for another day.

Je wamisri wa kale walikuwa ni watu gani na walifananaje?

Himaya ya wamisri ilianza takriban mwaka 3100BC na kupotea / kufa takriban 500 BC.Kufa kwa himaya ya Wamisri kulitokana na nchi kuvamiwa na wa hykos, wasiria, wagiriki, warumi na mwisho waarabu. Kwa hiyo wamisri wanaoishi sasa hivi misri sio wale waliokuwa wanaishi miaka ya zamani kabla ya 500 BC. Kama vile wamerekani wanaoishi sasa hivi USA sio walewale waliokuwa wanaishi miaka 1000 iliyopita kabla ya Columbus. Wamisri wa zamani kujumuisha mafarao walikuwa ni waafrika weusi na uthibitiso upo kwenye:

1) Lugha

Lugha ya wamisri wa zamani imeshakufa( sasa hivi lugha inayotumika ni kiarabu) lakini maandishi waliyoyaacha yanaweza kusomeka, na mfumo wa lugha yao umeshathibitishwa na wataalamu wa lugha( without exception) kuwa ni lugha ya kiafrika. Lugha hii ina uhusiano wa karibu na lugha zifuatazo za Afrika.
- Hausa ( Nigeria)
- Oromo (Ethiopia)
- Borana (Kenya)
- Iraqw ( Tanzania)
- Gorwaa (Tanzania)
- Kisomali
- Lugha jingi za Chad ( Chadic languages)
- Na nyingine nyingi ambazo sina muda wa kizitaja hapa

Sasa kama wazungumzaji wa hizi lugha ni waafrika weusi basi bila shaka wamisri wa zamani walikuwa weusi kwa ssababu lugha yao ipo kwenye group hilo hilo. Logic hiyohiyo unaweza ukaitumia kwa lugha za kibantu. Tunajua washona wa Zimbabwe ni waafrika kwa sababu wanaongea kibantu, ambacho ni group hihiyo na Kiswahili.

2)
Tamaduni za kutahiri au jando

Sasa turudi kwa Musa. Bila shaka kutahiri ni tamaduni za kiafrika na si za kiyahudi au kiislamu kama wengi wanavyofikiri. Vilevile, kutahiri ni mojawapo ya uthibitisho unaoonyesha kwamba Wamisri walikuwa waafrika na Musa alijifunzia kutahiri Misri na kuwapa utamaduni huu wayahudi . Waislamu walijifunza kutoka kwa wayahudi. Proof ni hii hapa.
Miili ( Mummies) ya wamisri wa kale inaonyesha kutahiriwa, na hata kuna picha kwenye mapiramidi zinazoonyesha kutahiri. Wamisri walitahiri kabla hata ‘Musa' kuzaliwa. Afrika kuna makabila mengi sana yanatahiri kuanzia wazulu ( ambao sio waislamu) kuja kwa wamasai bila hata kutaja makabila lukuku Afrika ya magharibi. Rituals ( tamaduni) za kutahiri Afrika hazihusiani kabisa na uislamu au uyahudi. Wataalamu wa anthropology wanasema kwamba ukitaka kujua chanzo cha kitu chochote angalia diversity au mkusanyiko mkubwa wa hicho kitu uko wapi.

Ukiangalia dunia nzima, afrika ndio yenye tamaduni nyingi za kutahiri zaidi ya sehemu nyingine duniani . Kwa hiyo hakuna shaka kuwa Musa alijifunza kutahiri kwa waafrika alipokuwa Misri na kuwafundisha wayahudi. Hii ni proof tosha ya commonality au uwiano wa tamaduni za wamisri na waafrika wengine, na inaonyesha kuwa wamisri walikuwa waafrika.
Vilevile, , Herodotus (490-425 BC) mwanahistoria mahiri wa kigiriki ambaye wanahistoria wanasema ndiye baba wa historia ya ulaya, anathibitisha hayo yote niliyoyasema:

"For the people of Colchis are evidently Egyptian, and this I perceived for myself before I heard it from others. So when I had come to consider the matter I asked them both; and the Colchians had remembrance of the Egyptians more than the Egyptians of the Colchians; but the Egyptians said they believed that the Colchians were a portion of the army of Sesostris. That this was so I conjectured myself not only because they are dark-skinned and have curly hair (this of itself amounts to nothing, for there are other races which are so), but also still more because the Colchians, Egyptians, and Ethiopians alone of all the races of men have practised circumcision from the first. The Phenicians and the Syrians who dwell in Palestine confess themselves that they have learnt it from the Egyptians, and the Syrians about the river Thermodon and the river Parthenios, and the Macronians, who are their neighbours, say that they have learnt it lately from the Colchians. These are the only races of men who practise circumcision, and these evidently practise it in the same manner as the Egyptians. Of the Egyptians themselves however and the Ethiopians, I am not able to say which learnt from the other, for undoubtedly it is a most ancient custom; but that the other nations learnt it by intercourse with the Egyptians, this among others is to me a strong proof."

Kwa kifupi nimeonyesha kuwa:
1) Moses alichukua tamaduni za Afrika ( mojawapo ikiwa kutahiri) ambayo ni msingi mmojawapo wa uislamu na uyahudi.
2) Kwamba Wamisri wa kale walikuwa ni waafrika weusi na nimeprove kwa kuonyesha uwiano katika lugha. Kuna proofs nyingi za uafrika wa wamisri lakini nitaziongeza baadae kama kuna mashaka.
Nitakaribisha maswali halafu nitaendelea na mambo mengine ambayo dini za uislamu na ukristu zimegeza kutoka Afrika.

Nakaribisha maswali
 
God is still a delusion, whether it originates from Afrika or Middle-East or Europe.

Yes, I would have preferred a black god, but he/she does not exist, anyway. Nevertheless, this could be a nice disccussion on the history of Ibrahimic religions and their relation to Afrikan belief systems.

Samahani wandugu nimeingiza Kinyamwezi, hii topic kwangu ngumu kwa kutumia kinyumbani (yaani Kiswahili).

Mista Yo yoo mnyamwezi wa mamtoni tushushie vitu kwa kiswahili bana acha mbwembwe. mbona Monstgala alishusha manondo ya mabig bang na magalaksi tukamsoma vizuri?

Hapa jukwaani kina Kiranga, eiyer na mamemba wengine wanashusha vitu kwa lugha ya mama na wanasomeka vizuri tu. sasa wewe posti mbili tatu unashindwaje kuzishusha kwa kiswahili lugha tamu tunayoipenda.

Aaah babu acha masihara.
 
Last edited by a moderator:
Ukijadiliana na mtu akachepukia kwenye bing bang na evolution theories achana nae. Nakushauri hata huyo achana nae,utapoteza muda.

Hii ndio attitude ambayo inaturudisha nyuma sana. Yani unaona ni bora watu waachane na mambo ya kisayansi na kiteknolojia ili mradi uendelee kuamini miujiza? Badala ya kujifunza jinsi ya kuyatawala mazingira yako, wewe unataka wenzako wazibe masikio na kufunga macho ili mradi mzidi kuendeleza imani za maombi, dua, kutoa mapepo, na kikombe cha babu Loliondo!

Kweli tuna kazi kubwa...
 
Mzee2000 endelea, binafsi nakupata vizuri coz

1. Hoja za msingi kama umisri wa zamani umeidadavua vizuri

2. Unaendana na fikra zangu pevu fulani hivi though sikusoma sehemu yoyote. Na jana tu nilikuwa namuambia mtu jambo hilo. Sipendi kuliweka hapa coz sitaki liiivuruge mada yako tamu.

Pse continue, hilo pozi la 2hrs linatosha.
 
Last edited by a moderator:
Mzee2000 kwanza hongera kwa mada nzuri inayo fikirisha na kupanua akili!

Swali langu kwako ni;je unatambua ya kuwa utaratibu wa kutahiri haukuanza kwa moses bali kawa ibrahim kwa upande wa kimaandiko,hii ikijumuisha wayahudi(maana ibrahim ni babu wa moses,kwamba yeye ni way back before moses?.HOJA YANGU ni je hapa unaweza vp kutrace utaratibu huu kama ni asili ya Misri kwa kupitia moses ili hali kabla yake yeye ibrahim alisha ongozwa kufanya tena eneo tofauti na misri?

Hongera kwa mada nzuri!.Nawasilisha!
 
Last edited by a moderator:
Mzee2000 kwanza hongera kwa mada nzuri inayo fikirisha na kupanua akili!

Swali langu kwako ni;je unatambua ya kuwa utaratibu wa kutahiri haukuanza kwa moses bali kawa ibrahim kwa upande wa kimaandiko,hii ikijumuisha wayahudi(maana ibrahim ni babu wa moses,kwamba yeye ni way back before moses?.HOJA YANGU ni je hapa unaweza vp kutrace utaratibu huu kama ni asili ya Misri kwa kupitia moses ili hali kabla yake yeye ibrahim alisha ongozwa kufanya tena eneo tofauti na misri?

Hongera kwa mada nzuri!.Nawasilisha!

Ahsante kwa swali lako, ni kweli kabla ya Moses waisraeli walitahiri kuanzia enzi za Ambraham, lakini ukiangalia amri kumi za Mungu na taifa la Israel chanzo kikuu cha sheria zao ni Moses, na huyu ni nabii muhimu wa Judaism, na alikulia Misri.Vilevile Abraham anasemwa kwamba aliishi Misri wakati kuna njaa Canaan, kwa hiyo alikuwa esposed na mila za wamisri.Vilevile wakati Abraham anaishi ( hapa tuna-assume alikuwa real historical character) wamisri/ waafrika walikuwa washaanza kutahiri. Kwa kufafanua:

1) Wataalamu wa timeline ya biblia, wanakubaliana kuwa historia ya agano la kale sanasana kuhusu Abraham iliandikwa takriban 500BC. Kwa kupiga mahesabu nyuma vizazi/matukio vilivyoandikwa kwenye bible,( wanasayansi kwa kulinganisha na sayansi ya archeology na rekodi nyingine) hayaendi zaidi ya 2000BC ( at the latest). Wayahudi hawakuwa literate( hawakuweza kuandika) kabla ya huo mwaka (500BC) kwa hiyo yaliyoandikwa ni ‘oral traditions' za zamani za wayahudi. Sasa wamisri wa kale walikuwa ‘literate' miaka mingi sana nyuma, yaani walianza kuandika historia yao kuanzia 3100BC ( kumbuka alfabeti tunayoitumia sasa hivi chanzo chake Misri).Na Katika historia yao iliyoko kwenye maandishi( na miili yao ) inaonyesha kuwa walifanya circumcision kabla hata ya Abraham yaani kabla 2000BC. Kwa kifupi, wamisri walikuwa ni ‘wazee' zaidi ya nabii yoyote yule wa waisraeli.

2) Waisraeli/ watu wa mashariki ya kati( middle east) walikuwa na mawasiliano mara nyingi na wamisri, wengine waliishi huko kama wafanyakazi/wavamizi. Kumbuka Misri ya kale ilikuwa empire kubwa sana yenye utajiri mwingi na kuna wakati ilitawala karibu maeneo yote ya Middle east, hata mpaka ugiriki, kwahiyo inawezekana walisambazo mila za kutahiri kama jinsi Herodotus alivyoandika kwenye post yangu hapo juu.

3) Angalia vilevile na sababu zinayotolewa na makabila ya Kiafrika kuhalalisha Kutahiri. Ukiangalia argument ya waafrika inaenda sana kiundani zaidi ya waisrel ambao wanasema tu ‘Mungu ametuambia'. Circumcission ya kiafrika inafanywa kwa sababu nyingi zikiwemo, kumfanya kijana kuingia kwenye uanaume. Zaidi, katika Afrika yako makabila yanayotahiri hata wanawake, na hii kitu huwezi kuona middle east. Kwa hiyo kutahiri Afrika kuko very DIVERSE/ DEEPER kimaumbile na kisababu ( justification) kuliko middle east na hu ni uthibitisho tosha kuwa waisraeli walijifunza hii mila kutoka kwa wamisri/ waafrika.


Kama hakuna maswali mengine nitaendelea na mada.
 
mkuu big up, tiririka na hii elmu uwaache na ma question mark hawa wanojifanya dinifanatics, babu zenu walikamatwa na kuteswa na walosambaza hizi dini za kilowezi, nyinyi bado ni maslaves mkae mkijua, brain slaves, mna uhuru wa kusoma na kufanya kila kitu ila kiimani y'all are still slaves, watu ndugu same race bado mnatukanana mnauana kisa ukristo uislamu etc afu mnajiona wajaanja,eti mpo kwenye njia nyembamba sahihi, my feet.

me sikuwaga na convincing proofs kama hizi nondo unazoshusha hapa, let em read and learn,
tena wengine mgoogle ethiopian jews ndio mjifunze source ya jewry was in ethiopia not the other way.
 
3) Angalia vilevile na sababu zinayotolewa na makabila ya Kiafrika kuhalalisha Kutahiri. Ukiangalia argument ya waafrika inaenda sana kiundani zaidi ya waisrel ambao wanasema tu ‘Mungu ametuambia'. Circumcission ya kiafrika inafanywa kwa sababu nyingi zikiwemo, kumfanya kijana kuingia kwenye uanaume. Zaidi, katika Afrika yako makabila yanayotahiri hata wanawake, na hii kitu huwezi kuona middle east. Kwa hiyo kutahiri Afrika kuko very DIVERSE/ DEEPER kimaumbile na kisababu ( justification) kuliko middle east na hu ni uthibitisho tosha kuwa waisraeli walijifunza hii mila kutoka kwa wamisri/ waafrika.

Vp, lakini pia yapo makabira mengi mno yasiyotahiri hapa afrika kwa uchache tu wasangu, wamalila, wasafwa tz, wabemba na nyamwanga zambia, shona sioni hoja
 
jitazame,

Ndio, sio makabila yote Afrika yanatahiri, yapo mengi sana tu ambayo hayatahiri. Lakini tukiangalia jinsi tamaduni za kutahiri( ambazo hazina justification ya dini) zilivyosambaa Afrika, tunaona bila ubishi kuwa waafrika ndio walianzisha utamaduni huu ambao uligezwa na kurudishwa afrika kwa sababu za dini.
 
Last edited by a moderator:
Nimeanza kufunguliwa hizi minyororo za imani za ki "dogma" "godma" zisizo na majibu zaidi ya vitisho.
Mwl. Endelea na somo tupo wanafunzi wengi.
 
Baada ya kuonyesha jinsi waisraeli walivyochukua mila za kutahiri kutoka kwa waaAfrika( yaani misri ya zamani) Sasa nitaangalia Amri kumi za Mungu ambazo Moses alipewa na Mungu kwenye mlima wa sinai kama biblia inavyosema.

Wamisri wa kale walikuwa wana sheria zao ambazo zilikuwa very complex ambazo mpaka leo zinaweza kuonekana kwenye mahekalu yao pamoja na majeneza ya wafu wao. Ukiangalia mfumo wa amri hizo zinafanana sana na Amri kumi za Mungu alizopewa Moses na wataalamu wengi wanauhakika kuwa hizo za Moses zilichukuliwa kutoka misri ingawa zilibadilishwa kidogo na waisraeli.

Amri za wamisri wa zamani ziliandikwa kwenye kitabu chao kinachoitwa ' kitabu cha wafu' hayo ni maneno ambayo mtu akifa anapaswa ayaseme mbele ya jaji ( Mungu wao Osiris ambaye atatoa hukumu kufuata principles za Maat(haki).Maandishi ya Amri hizi za wamisri ni ya zamani sana mifano iliyopo sasa kwenye maandishi inaenda mpaka kabla ya 2000BC hii ni kabla hata nabii hata mmoja wa waisraeli hajazaliwa.

Hebu tuoe jinsi amri za Mungu za waisraeli zanavyofanana na za Wamisri, Hizi kwanza ni amri za wamisri:
1. I have not done iniquity
2. I have not committed robbery. ( usiibe ya waisraeli)
3. I have not stolen with violence.
4. I have not committed theft.
5. I have not killed men. ( Usiue waisraeli)
6. I have not made light the bushel of corn.
7. I have not acted deceitfully. ( usiseme uongo- waisraeli)
8., I have not robbed the property of god.
9. I have not uttered falsehood. ( usiseme uongo- waisraeli)
10. I have not stolen food.
11. I have not cursed.
12. I have not attacked any man.
13. I have not slain the cattle of god.
14. I have not used deceit
15. I have not stolen grain.
16. I have not acted the part of the spy (eavesdropper).
17. I have not slandered.
18. I have not been angry without cause.
19. I have not lain with another man's wife. (usizini ya waisreli)
20. I have not abused myself.
21. Ihave made no man to be afraid.
22. I have attacked no man.
23. I have no been a man of wrath.
24. I have not been deaf to the words of truth.
25. I have not stirred up strife.
26. I have made no one weep.
27. I have neither acted impurely, nor lain with men. ( hapa wanakataza ushoga)
28. I have not eaten my heart.
29. I have not cursed any man.
30. I have not done deeds of violence.
31. I have not acted hastily.
32. I have not ... my skin, I have not ... the god.
33. I have not made loud my voice in speaking.
34. I have not acted deceitfully, I have not acted wickedly.
35. I have not cursed the king.
36., I have not fouled water.
37. I have not made my voice loud.
38. I have not cursed the god. ( usilitaje bure jina la Mungu wako)
39. I have not acted insolently.
40. I have not worked for honors.
41. I have not increased my possessions except through my own goods.
42. I have not treated with contempt the god of my city


Hizi amri kumi za Mungu za waisraeli:
1. You shall have no other gods before Me.
2. You shall not make idols.
3. You shall not take the name of the LORD your God in vain.
4. Remember the Sabbath day, to keep it holy.
5. Honor your father and your mother.
6. You shall not murder.
7. You shall not commit adultery.
8. You shall not steal.
9. You shall not bear false witness against your neighbor.
10. You shall not covet.

Sasa ukiangalia hizo amri za wamisri na ukilinganisha na za waisraeli unaona kuwa za wamisri ni nyingi sana na zimejaa zaidi na unaona amri za waisraeli ni kama kifupisho cha amri za wamisri ingawa za waisraeli zimebadilishwa kidogo lakini unaona wametumia ‘principles' za wamisri. Kama waisrael walikuwa utumwani misri na walikaa muda mrefu huko bila shaka walichukua tamaduni za wamisri, walichukua ‘template' ya wamisri walibadilisha kidogo ili iwiane na tamaduni zao, hakuna ubishi hapa.

Nakaribisha maswali na hoja kabla ya kuendelea.
 
Back
Top Bottom