Kijana aliyeuawa na watu wanaojiita Sungu sungu Mburahati, Rais Samia ingilia kati

Kijana aliyeuawa na watu wanaojiita Sungu sungu Mburahati, Rais Samia ingilia kati

Lady Mwali

Senior Member
Joined
Nov 15, 2018
Posts
147
Reaction score
333
Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, sisi wanawake tuna imani sana na wewe, tutakupa kura zetu zote za urais mwaka 2025 ila kuna mambo machafu sana yanayofanyika katika serikali yako.

Sisi wanawake wa Tanzania tumesikitishwa sana na mauaji ya kijana mdogo mkazi wa kata ya Mabibo kitongoji cha Soweto yaliyofanywa na watu wanaojiita Sungu sungu.

Kijana huyo anaitwa Jumanne Jongo. Ameuawa kikatili sana kwa kukatwa miguu na mikono.

Cha ajabu wauaji wa kijana huyu wanajulikana na hawajakamatwa hata mmoja.Taarifa nilizokuwa nazo bado wameahidi kuua vijana wengine wanaowahisi vibaka.

Genge hili la mauaji ya vijana linaongozwa na watu wanaojiita Sungu sungu kutoka kata ya Jitegemee ,Mabibo wilaya ya Ubungo.

Haya sio mauaji ya mara ya kwanza, huko nyuma sungu sungu hao wa Jitegemee wameshawahi kuua vijana wengi kwa kisingizio kuwa vijana hao ni vibaka.Hata kama ni vibaka kwanini wasiwakamate na kuwapeleka Polisi?

Kwanini sungu sungu wanajichukulia sheria mkononi?

Mh.Rais nchi yako ni nchi inayofata utawala wa sheria, iweje wapumbavu wachache watie doa uongozi wako?

Taarifa nilizokuwa nazo mauaji hayo yanapata baraka kutoka katika uongozi wa serikali ya mtaa wa Jitegemee chini ya mwenyekiti Kilema.

Hivi OCD wa Kinondoni hana taarifa ya tukio hili? Mpaka sasa hivi amechukua hatua gani? Anapata kigugumizi kipi cha kuwakamata wauaji hao wakiongozwa na mpumbavu mmoja anayeitwa Samwel?

Kwa taarifa yako mh.Rais sisi wanawake wa Mburahati na Jitegemee tumeguswa sana na kifo cha huyu kijana, tunatafakari mara mbili mbili kuwa wanachama wa CCM.

Embu ukiwa kama Rais tumia mamlaka yako kushughulikia suala hili.Maana sisi wanawake wenzako tuna wasiwasi sana kuhusu maisha ya watoto wetu wanaouawa kila kukicha na hawa watu walio juu ya sheria wanaojiita Sungu sungu.

Kuna hoja kwamba huyu kijana alikuwa kibaka,lakini sheria inasemaje? Kwani hukumu ya kibaka mauaji?

Chonde chonde mh.Rais fanyia kazi suala hili ikibidi mwajibishe kamanda wa Polisi wa Kinondoni kwa kushindwa kuwakamata hao wauaji wa huyu kijana.

FB_IMG_16327404840931609.jpg

 
Wanatusumbua sana hao,,, wanakaba wazi wazi kabisa alafu mama zao wanawatetea,,, mi nikajua labda huyo dogo anakaa mbezi, kumbe mabibo,, huyo kibaka tu,, maeneo kama mabibo,mburahati,kigogo, manzese, tandale, mwananyamala, Argentina na kagera mikoroshini haya ni maeneo korofi kwa tabia hizo za wizi vijana wadogo kabisa,,, na ndio maana raia wamechoka na kujichukulia maamuzi kwa kuwa hata wakipelekwa vituoni wazazi wao wanawawatetea,, sasa tutafanya kama tulivyofanya kipindi cha komando yosso,, msako nyumba hadi nyumba.
 
Mheshimiwa raisi, Mama Samia Suluhu Hassan, sisi wanawake tuna Imani sana na wewe, tutakupa kura zetu zote za urais mwaka 2025 ila kuna mambo machafu sana yanayofanyika katika serikali yako.

Sisi wanawake wa Tanzania tumesikitishwa sana na mauaji ya kijana mdogo mkazi wa kata ya Mabibo kitongoji cha Soweto yaliyofanywa na watu wanaojiita Sungu sungu.

Kijana huyo anaitwa Jumanne Jongo.Ameuawa kikatili sana kwa kukatwa miguu na mikono.

Cha ajabu wauaji wa kijana huyu wanajulikana na hawajakamatwa hata mmoja.Taarifa nilizokuwa nazo bado wameahidi kuua vijana wengine wanaowahisi vibaka.

Genge hili la mauaji ya vijana linaongozwa na watu wanaojiita Sungu sungu kutoka kata ya Jitegemee ,Mabibo wilaya ya Ubungo.

Haya sio mauaji ya mara ya kwanza,huko nyuma sungu sungu hao wa Jitegemee wameshawahi kuua vijana wengi kwa kisingizio kuwa vijana hao ni vibaka.Hata kama ni vibaka kwa nini wasiwakamate na kuwapeleka Polisi?

Kwa nini sungu sungu wanajichukulia sheria mkononi?

Mh.Rais nchi yako ni nchi inayofata utawala wa sheria, iweje wapumbavu wachache watie doa uongozi wako?

Taarifa nilizokuwa nazo mauaji hayo yanapata baraka kutoka katika uongozi wa serikali ya mtaa wa Jitegemee chini ya mwenyekiti Kilema.

Hivi OCD wa Kinondoni hana taarifa ya tukio hili? Mpaka sasa hivi amechukua hatua gani? Anapata kigugumizi kipi cha kuwakamata wauaji hao wakiongozwa na mpumbavu mmoja anayeitwa Samwel?

Kwa taarifa yako mh.rais sisi wanawake wa Mburahati na Jitegemee tumeguswa sana na kifo cha huyu kijana, tunatafakari mara mbili mbili kuwa wanachama wa CCM.

Embu ukiwa kama rais tumia mamlaka yako kushughulikia suala hili.Maana sisi wanawake wenzako tuna wasiwasi sana kuhusu maisha ya watoto wetu wanaouawa kila kukicha na hawa watu walio juu ya sheria wanaojiita Sungu sungu.

Kuna hoja kwamba huyu kijana alikuwa kibaka,lakini sheria inasemaje? Kwani hukumu ya kibaka mauaji?

Chonde chonde mh.Rais fanyia kazi suala hili ikibidi mwajibishe kamanda wa Polisi wa Kinondoni kwa kushindwa kuwakamata hao wauaji wa huyu kijana.

Loh poleni sana.
Vipi matukio ya uhalifu huko kwenu yapoje?

Marehemu alikutwa kwenye tukio au walimsaka kimya kimya na kumpangusa kimya kimya?

Tuelimishane kutochukua sheria mkononi
 
Kuna Jamaa yetu aliuawa maeneo ya Mburahati GINE..alikatwa mfupa wa nyuma wa kisigino na hao hao Sungu Sungu..Nawachukia Sn Hao Wange.S.e.
 
Wewe subiria mahakamani ila waliowahi kukabwa au kuchomwa visu au kuibiwa na huyo kibaka hukufanya jitihada kuwasaidia kumkamata huyo mhalifu au kuwasaidia kumfikisha mahakamani.

Kwa tuliowahi kukabwa, kujeruhiwa na kuibiwa na vibaka tunajua uchungu wake. Siku ukifanyiwa hayo usisite kutupa mrejesho hapa.
 


Genge hili la mauaji ya vijana linaongozwa na watu wanaojiita Sungu sungu kutoka kata ya Jitegemee ,Mabibo wilaya ya Ubungo."

Poleni sana.

Wilaya ya Ubungo haina Kata inaitwa Jitegemee, ila ina Mtaa wa Jitegemee, uliopo Kata ya Mabibo.

Halafu muwape wanenu malezi mema. Kuna uvunjifu mkubwa sana wa maadili mitaa hiyo ya Kata za Mburahati na Mabibo. Kuna vibaka sana. Kabla ya kufikia kuuwawa, vijana wenu wakanyeni na muwafuatilie mjue nyendo zao.
 
Ndugu msanii: hawajamkuta eneo la tukio.Walimpigia simu ,wakamwita,wakamuua
 
Mheshimiwa raisi, Mama Samia Suluhu Hassan, sisi wanawake tuna Imani sana na wewe, tutakupa kura zetu zote za urais mwaka 2025 ila kuna mambo machafu sana yanayofanyika katika serikali yako.

Sisi wanawake wa Tanzania tumesikitishwa sana na mauaji ya kijana mdogo mkazi wa kata ya Mabibo kitongoji cha Soweto yaliyofanywa na watu wanaojiita Sungu sungu.

Kijana huyo anaitwa Jumanne Jongo.Ameuawa kikatili sana kwa kukatwa miguu na mikono.

Cha ajabu wauaji wa kijana huyu wanajulikana na hawajakamatwa hata mmoja.Taarifa nilizokuwa nazo bado wameahidi kuua vijana wengine wanaowahisi vibaka.

Genge hili la mauaji ya vijana linaongozwa na watu wanaojiita Sungu sungu kutoka kata ya Jitegemee ,Mabibo wilaya ya Ubungo.

Haya sio mauaji ya mara ya kwanza,huko nyuma sungu sungu hao wa Jitegemee wameshawahi kuua vijana wengi kwa kisingizio kuwa vijana hao ni vibaka.Hata kama ni vibaka kwa nini wasiwakamate na kuwapeleka Polisi?

Kwa nini sungu sungu wanajichukulia sheria mkononi?

Mh.Rais nchi yako ni nchi inayofata utawala wa sheria, iweje wapumbavu wachache watie doa uongozi wako?

Taarifa nilizokuwa nazo mauaji hayo yanapata baraka kutoka katika uongozi wa serikali ya mtaa wa Jitegemee chini ya mwenyekiti Kilema.

Hivi OCD wa Kinondoni hana taarifa ya tukio hili? Mpaka sasa hivi amechukua hatua gani? Anapata kigugumizi kipi cha kuwakamata wauaji hao wakiongozwa na mpumbavu mmoja anayeitwa Samwel?

Kwa taarifa yako mh.rais sisi wanawake wa Mburahati na Jitegemee tumeguswa sana na kifo cha huyu kijana, tunatafakari mara mbili mbili kuwa wanachama wa CCM.

Embu ukiwa kama rais tumia mamlaka yako kushughulikia suala hili.Maana sisi wanawake wenzako tuna wasiwasi sana kuhusu maisha ya watoto wetu wanaouawa kila kukicha na hawa watu walio juu ya sheria wanaojiita Sungu sungu.

Kuna hoja kwamba huyu kijana alikuwa kibaka,lakini sheria inasemaje? Kwani hukumu ya kibaka mauaji?

Chonde chonde mh.Rais fanyia kazi suala hili ikibidi mwajibishe kamanda wa Polisi wa Kinondoni kwa kushindwa kuwakamata hao wauaji wa huyu kijana.

Kama hakua kibaka haki ipatikane kama alikua kibaka haki imetendeka. Quran inasema wakatwe mikono.
 
Back
Top Bottom