Kijana aliyeuawa na watu wanaojiita Sungu sungu Mburahati, Rais Samia ingilia kati

Kijana aliyeuawa na watu wanaojiita Sungu sungu Mburahati, Rais Samia ingilia kati

Mheshimiwa raisi, Mama Samia Suluhu Hassan, sisi wanawake tuna Imani sana na wewe, tutakupa kura zetu zote za urais mwaka 2025 ila kuna mambo machafu sana yanayofanyika katika serikali yako.

Sisi wanawake wa Tanzania tumesikitishwa sana na mauaji ya kijana mdogo mkazi wa kata ya Mabibo kitongoji cha Soweto yaliyofanywa na watu wanaojiita Sungu sungu.

Kijana huyo anaitwa Jumanne Jongo.Ameuawa kikatili sana kwa kukatwa miguu na mikono.

Cha ajabu wauaji wa kijana huyu wanajulikana na hawajakamatwa hata mmoja.Taarifa nilizokuwa nazo bado wameahidi kuua vijana wengine wanaowahisi vibaka.

Genge hili la mauaji ya vijana linaongozwa na watu wanaojiita Sungu sungu kutoka kata ya Jitegemee ,Mabibo wilaya ya Ubungo.

Haya sio mauaji ya mara ya kwanza,huko nyuma sungu sungu hao wa Jitegemee wameshawahi kuua vijana wengi kwa kisingizio kuwa vijana hao ni vibaka.Hata kama ni vibaka kwa nini wasiwakamate na kuwapeleka Polisi?

Kwa nini sungu sungu wanajichukulia sheria mkononi?

Mh.Rais nchi yako ni nchi inayofata utawala wa sheria, iweje wapumbavu wachache watie doa uongozi wako?

Taarifa nilizokuwa nazo mauaji hayo yanapata baraka kutoka katika uongozi wa serikali ya mtaa wa Jitegemee chini ya mwenyekiti Kilema.

Hivi OCD wa Kinondoni hana taarifa ya tukio hili? Mpaka sasa hivi amechukua hatua gani? Anapata kigugumizi kipi cha kuwakamata wauaji hao wakiongozwa na mpumbavu mmoja anayeitwa Samwel?

Kwa taarifa yako mh.rais sisi wanawake wa Mburahati na Jitegemee tumeguswa sana na kifo cha huyu kijana, tunatafakari mara mbili mbili kuwa wanachama wa CCM.

Embu ukiwa kama rais tumia mamlaka yako kushughulikia suala hili.Maana sisi wanawake wenzako tuna wasiwasi sana kuhusu maisha ya watoto wetu wanaouawa kila kukicha na hawa watu walio juu ya sheria wanaojiita Sungu sungu.

Kuna hoja kwamba huyu kijana alikuwa kibaka,lakini sheria inasemaje? Kwani hukumu ya kibaka mauaji?

Chonde chonde mh.Rais fanyia kazi suala hili ikibidi mwajibishe kamanda wa Polisi wa Kinondoni kwa kushindwa kuwakamata hao wauaji wa huyu kijana.

Inaonyesha wewe hujawahi kukumbana na hao vibaka au wewe una hisa nao. Kwa taarifa yako sio binaadamu kabisa wakukuta katika anga zao za ukabaji, hawana huruma wala utu, sio wa kuhurumiwa kabisa, by the way kama ni mwanao pole , ila kumbuka methali 2 za wahenga:
1.Mchelea mwana kulia, hulia yeye.
2.Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu.
 
Halaf hao kibaka ni hatari watoto wakike wamebakwa sana kinguvu na wengne kulawitiwa kabsa tena kinguvu na wanamchezo hao panya road wanaweza mvutia dem mmoja baadae wanampiga mtungo kilazima.
 
USSR nionenye kifungu Cha sheria kinachosema adhabu ya kibaka kuuawa
Kwani vibaka wao kuna vifungu vya sheria vinawaruhusu kuua?

Mbona wanaua watu na hamsemi na kuuliza maswali ya hivi?

Ninadhani kikubwa hapa kama mzazi ni jukumu lako kuchunga tabia na mwenendo wa kijana wako ili aishi kimaadili katika jamii.

Hili la kutetea vibaka kwamba watendewe haki wakati wao wakipora haki za wengine ni kupigia mbuzi gitaa ili acheze.
 
Ni ujinga na upungufu wa akili kuua Binadamu wenzetu kwa kigezo eti ni Kibaka. Uhai wa mtu uulinganishe na kitu?
Hata Kama Mtu kaiba kiasi gani bado kuna sehemu maalum za kumpeleka au kumshitaki na akawajibishwa.
Eti mtu kaibiwa sijui taa ya gari tu au kuku, basi akimkamata huyo mwizi ni kuua huo ni upumbavu na roho ya kimaskini tu.
Vitu vinatafutwa Lakini uhai hautafutwi. Tuache kuhalalisha mambo ya kipumbavu kwa sababu za kimaskini tulizonazo
Vipi kuhusu uhai wako wewe au unaweza kutafuta mwingine?

Ukipigwa kisu mpaka kufa na mmoja kati ya hao mafala utaenda kununua uhai mwingine wapi?
 
Hance nioneshe sheria inayoruhusu sungu sungu waue?

Kijana huyu aliuawa barabarani baada ya kupigiwa simu
kuna wakazi wangapi eneo hilo mpaka wampigie simu yeye tu, inaonekana kwa vyovyote anahusika na hawa si wakuhurumia wanarudisha nyuma maendeleo watupishe mitano tena kazi iendelee
 
Daa, kweli vibaka ni tatizo, lakini walau wasiwaue kikatili namna hiyo, atandikwe bakora za kutosha then apelkwe kituo cha polisi, maana kule kituoni huwa wanaachiwa tu, so watandikwe kwanza bakora, ila sio kuwaua kikatili na namna hiyo
 
Kumbe ni kibaka mzoefu na amepata halali yake sasa huyu mama anamsumbua nini rais wakati Ana mambo ya msingi ya kufanya.
Jamani, tukubali tukatae, halali ya kila mwenye kosa ni kupelekwa kwwnye vyombo vya sheria, ila kwakua vibaka wanakera na polisi huwa wanawaachia, basi wapewe kichapo tu kama bakora za kutosha kisa wapelekwe polisi, ila kukatana mikono na miguu kisha kumuua nashani si ubinadamu
 
Naunga mkono hoja yako Brazaj kwamba jeshi la polisi liko kudhibiti vya vya siasa vya upinzani
Na wewe kama ni kibaka au umezaa kibaka na anakuletea mali za wizi nyumbani basi jiandae kuuawa ni siku tu haijasoma kwenye saa. Ndipo ulalamike kabisaa kuwa unamuomba Rais aingilie kati kwa wewe kuuawa na wananchi. Endelea na huu ujinga wako.
 
Mleta mada unajua ni damu ngapi zimemwaga na hao vibaka? Unajua wangapi wamepoteza Maisha sababu za hao vibaka?
Watu wamepoteza mali kiasi gani kwa kukabwa na hao vibaka?

Vibaka si watu wa kuwatetea hata kidogo dawa yao ni kuwamalizia mbali.
Wa kuwalaumu ni wafanyabiashara wa madawa ya kulevya, maana mali na fedha zinazoibwa zote huishia kwao.
 
Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, sisi wanawake tuna imani sana na wewe, tutakupa kura zetu zote za urais mwaka 2025 ila kuna mambo machafu sana yanayofanyika katika serikali yako.

Sisi wanawake wa Tanzania tumesikitishwa sana na mauaji ya kijana mdogo mkazi wa kata ya Mabibo kitongoji cha Soweto yaliyofanywa na watu wanaojiita Sungu sungu.

Kijana huyo anaitwa Jumanne Jongo. Ameuawa kikatili sana kwa kukatwa miguu na mikono.

Cha ajabu wauaji wa kijana huyu wanajulikana na hawajakamatwa hata mmoja.Taarifa nilizokuwa nazo bado wameahidi kuua vijana wengine wanaowahisi vibaka.

Genge hili la mauaji ya vijana linaongozwa na watu wanaojiita Sungu sungu kutoka kata ya Jitegemee ,Mabibo wilaya ya Ubungo.

Haya sio mauaji ya mara ya kwanza, huko nyuma sungu sungu hao wa Jitegemee wameshawahi kuua vijana wengi kwa kisingizio kuwa vijana hao ni vibaka.Hata kama ni vibaka kwanini wasiwakamate na kuwapeleka Polisi?

Kwanini sungu sungu wanajichukulia sheria mkononi?

Mh.Rais nchi yako ni nchi inayofata utawala wa sheria, iweje wapumbavu wachache watie doa uongozi wako?

Taarifa nilizokuwa nazo mauaji hayo yanapata baraka kutoka katika uongozi wa serikali ya mtaa wa Jitegemee chini ya mwenyekiti Kilema.

Hivi OCD wa Kinondoni hana taarifa ya tukio hili? Mpaka sasa hivi amechukua hatua gani? Anapata kigugumizi kipi cha kuwakamata wauaji hao wakiongozwa na mpumbavu mmoja anayeitwa Samwel?

Kwa taarifa yako mh.Rais sisi wanawake wa Mburahati na Jitegemee tumeguswa sana na kifo cha huyu kijana, tunatafakari mara mbili mbili kuwa wanachama wa CCM.

Embu ukiwa kama Rais tumia mamlaka yako kushughulikia suala hili.Maana sisi wanawake wenzako tuna wasiwasi sana kuhusu maisha ya watoto wetu wanaouawa kila kukicha na hawa watu walio juu ya sheria wanaojiita Sungu sungu.

Kuna hoja kwamba huyu kijana alikuwa kibaka,lakini sheria inasemaje? Kwani hukumu ya kibaka mauaji?

Chonde chonde mh.Rais fanyia kazi suala hili ikibidi mwajibishe kamanda wa Polisi wa Kinondoni kwa kushindwa kuwakamata hao wauaji wa huyu kijana.


Kuua Ni vibaya Sana
 
USSR nionenye kifungu Cha sheria kinachosema adhabu ya kibaka kuuawa
Kikubwa mama ni kuishi kwa nidhamu katika jamii inayotuzunguka ili uheshimike na kuishi kwa amani.

Unajua kwa nini raia wanajichukulia sheria mkononi?

Ni kwamba kesi za vibaka mahakamani ni nyepesi sana kuliko uzito wa matukio na madhara wanayofanya, maana kuunganisha ushahidi usiotia shaka hadi kuwatia hatiani ni mgumu jinsi ya kupata vielelezo vya kutosha kutokana na mazingira ya namna wanavyofanya uhalifu.

Pia shata shata ya mahakamani kufuatilia kitu kisichokuletea manufaa ni kupoteza wakati na watu hudharau kufuatilia.

Kwa hiyo kesi zinapuuzwa na waliodhuriwa kushindwa kupata haki zao.

Sakata aina hii wa kwanza kulaumiwa hapa ambao ni chanzo, ni sisi wazazi tunavyodili na watoto zetu majumbani kwa kutofatilia nyendo zao ama kubariki matendo yao kwa kupokea na kufurahia vitu vya wizi wanavyopora na kuvileta nyumbani.

Kwa kuwa kila mtu anaelewa uchungu wa mwana uumizavyo akiuawa, hivyo mfiwa utaendelea kupewa pole za kebehi, lakini pembeni watu wakiendelea kuunga mkono kuuawa kwa kibaka husika.

Tuwalee watoto zetu kwa kuwafundisha maadili mema.
 
Muwe mnawapa malezi bora watoto wenu, na sio kutetea vibaka kisa ni watoto wenu.
Kazi nzuri sana wanafanya hao sungu sungu.
 
Hiyo ni sheria ya jamii au kwa kifupi ni sheria ya wananchi wenye hasira kali
Kwa mujibu wa sheria kuua kibaka ni kosa ila kwa mujibu wa haki siyo kosa
*Mwizi au jambazi anavunja SHERIA dhidi ya HAKI
* Je Mtu akivunja SHERIA kwa ajili ya HAKI kafanya kosa gani?
 
Bokilo,hiyo sheria ya nchi gani ya kuua vibaka? Jibu
Kwa mujibu wa sheria kuua kibaka ni kosa ila kwa mujibu wa haki siyo kosa
*Mwizi au jambazi anavunja SHERIA dhidi ya HAKI
* Je Mtu akivunja SHERIA kwa ajili ya HAKI kafanya kosa gani?
 
Afu mtoa mada anatetea upumbavu
JamiiForums621852611.jpg
 
Back
Top Bottom