Kijana unayejitafuta kimaisha, katika utafutaji wako Zanzibar iweke namba moja

Kijana unayejitafuta kimaisha, katika utafutaji wako Zanzibar iweke namba moja

Thats opportunity machupa mengi mnoo ya plastiki. Napambania niweze kupata mashine ya kusaga unga hizi. Huku chupa zenye thaman ni zile ndogo mana wamama wanazitumia kuwekea juisi za matunda. Naweka picha muda mfupi ujao
Biashara ya kununua machupa na. Kuya leta dar haifanyiki huko ? Kalaga Baho Nongwa
 
Wanawakenwa bara wa nn mkuu? Mm nimepata mshangazi mmoja Michamvi una trako la kwenda. Siku ya kwanza nilokutana nao ulinipitia karibu unanukia al-Udi nkadinda masaa 3.. kuna mimama inajipenda wazee sio poa
Umeanza kuniumiza mbavu zangu 😹😹

Shem utaibuka na jini unakoendea..!!
 
Binafsi nilishaamua long time lazima nije Zanzibar kupiga vibarua vya ujenzi Ili nipate nauli ya kwenda Ukraine kwenye ujenzi baada ya vita kuisha.
* Ukitaka utafute maisha, usikae nchi yoyote au sehemu ambapo wanatumia dini yao kama sehemu ya serikali*
Nchi yoyote au sehemu ambapo dini ndiyo kipaumbele, siwezi kukaa maana tutakwaruzana.
Wewe umefunga, mimi nisile sehemu ya wazi kisa wewe umefunga. Huo ni ujinga mkubwa sana
 
Mafunzo hutolewa bure kabisa, inshu hapo ni kupata connection tu ya kuingia kwenye hoteli husika. Pia utapata chakula na usafiri bure, na mwisho wa mwezi unapewa pesa ya kujikimu. Hoteli niliyo kuwepo walikuwa wanatoa 100k kwa trainee, ukimaliza trainee unaanza kulipwa mshahara husika kutokana na sekta uliyopo.
Mafunzo miezi 4 bure? Mnapenda sana kuacha magepu
 
Shukrani kwa ufafanuzi mzuri zaidi.
Huu ni ukweli mtupu, miaka ya nyuma mimi binafsi niliamua kujichanganya Zanzibar kwa jamaa yangu alie kuwa ana sukuma kazi za ujenzi. Akaniunganisha tukawa tunapiga pamoja, ila ile kazi nilifanya kwa muda mchache nikatafuta connection ya hotelini. Nikapata hoteli moja iko Nungwi pale nikaingia kama mwanafunzi (trainee) na nilikuwa kitengo cha Muhudumu awali nilienda kwa lengo la kuwa Bar Man ila nilikuta nafasi zimejaa, hivyo nikaona kuliko kukosa ngoja nikomae hapo hapo.

Nikapiga trainee miezi 4, faida niliyo pata hapa nilivyo maliza na msimu wa high season ndio ulikuwa unaingia. Hoteli hiyo hiyo ikanipa ajira na mshahara ulikuwa 350k kwa mwezi, usafiri kwenda na kurudi pamoja na chakula ukiwa kazini hoteli inatoa vyote bure kabisa. Na uzuri zaidi kwa kitengo nilicho kuwepo nilikuwa napata sana tip kutoka kwa wageni, kwa mwezi tu nilikuwa sikosi angalau 200k hiyo nje ya mshahara. Hiyo hela ilikuwa inapiga tafu kwenye masuala ya kulipia chumba maana staff wengi walikuwa wanakaa mjini ndio maana hoteli ilikuwa inatoa usafiri.

Kwa namna hiyo nilikuwa na uwezo wa kuto gusa mshahara wangu, maana kula ilikuwa tunakula pale pale hotelini mara moja moja sana nilikuwa napika geto. Kwa hiyo huyu jamaa anacho sema ni sahihi kabisa, huenda tu jamaa hajafunguka zaidi ili watu waelewe vizuri. Nimetoa huo mfano wangu ili kila mmoja aelewe mambo yanavyo enda. Chukulia huo mfano kwa kijana unae jitafuta uamue ku focus na maisha kweli na uwe na malengo, ukiamua kutunza hiyo 350k ndani ya miaka mitatu utakuwa umetengeneza pesa nzuri sana. Pesa ambayo unaweza toka na kuamua kujiajiri wewe mwenyewe.

Mwezi wa sita kazi za hoteli huwa nyingi sana kwa hiyo mnaweza jichanganya. Kingine nacho weza kusema Zanzibar ukiwa mzuri kwenye kuongea na kuandika kwa ufasaha angalau lugha ya Kiingereza ni bingo sana. Kupata kazi ni rahisi sana hasa receptionist, utapiga trainee yako baada ya hapo unapata ajira unaanza kula mshahara wa 600k. Sasa kuliko kukaa tu unaweza tafuta mwalimu mzuri akufunze hiyo lugha, jipe muda wa kujifunza kisha zama Zanzibar.
 
Back
Top Bottom