Kikwete aamuru mitambo ya IPTL iwashwe mara moja!

Kikwete aamuru mitambo ya IPTL iwashwe mara moja!

Lakini Ngereja si ndio alikuwa anatakiwa kumweleza Rais kuwa nimeamua kuwasha mitambo ya iptl? Mbona Zitto kaongea na yametekelezwa. Je waziri hana nguvu ya kufanya maamuzi? Naomba kujua Nguvu ya Waziri. Kipi anaweza kutekeleza bila Rais kumwingilia na kukawa na maslahi kwa Taifa?

Labda kutengeneza watoto ndo JK haezi mwingilia kwani atakua anaongeza idadi ya nguvu kazi (watu) ambao ni maslahi kwa taifa kwa upande mwingine.
 
Zzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzzz, wananchi na viongozi wake wote wapo usingizin, Wote kwisha kazi. Bora tubinafsishe uongozi tumlete mtu kama Josie Mourinho au Jerry Lawrings waje kutuongoza. Sisi wenyewe tumeshindwa kazi
 
Ninajiquote nilichosema tarehe 15/10/2009

Ninapendekeza;

  • Serikali ihakikishe mitambo ya IPTL inawashwa mara moja wakati mazungumzo yake na IPTL yakiendelea kwa kuharakishwa (fast tracking). Hali ya nchi ni mbaya, ni sawa na vita, haiwezekani serikali yenye mamlaka ishindwe kuhakikisha IPTL inazalisha umeme wakati mazungumzo yakiendelea. Haiwezekani.Labda kama haina uchungu na maisha ya watu wake.
  • Sikutaka kusema chochote nikiamini kwamba Shirika la TANESCO, Serikali, na kwa upande wa bunge, Kamati ya masuala ya Nishati na Madini, wangeweza kutoa majibu ya tatizo linatukabili. Badala yake, juhudi nyingi zimetumika kutafuta chanzo cha tatizo na kuchelea kutoa suluhuInaumiza sana kuona kuwa tunaendekeza siasa rahisi tunaposhugulikia masuala mazito ya kitaifa kama Nishati. Inasikitisha zaidi pale tunapoona kuwa serikali inashindwa kuchukua hatua mahususi za kuhami uchumi wa Taifa letu. Serikali na Bunge hazitoi suluhisho la hali hii na ni wazi kuna kutupiana mpira wakati nchi inaumia. Serikali imewekwa madarakani ili ifanye maamuzi na tuihukumu kwa maamuzi hayo. Serikali ni lazima sasa iamue.
  • Mazingira magumu kama haya yanahitaji maamuzi magumu (extra ordinary circumstances require extra ordinary decisions). Ninaamini serikali itazingatia ushauri wangu.
Mnisamehe kwa kujiquote!

Ikulu inasema wafanyabiashara ndio wamemwomba Rais. Ni sawa tu........

Si kwamba wamemwomba, si unajua mambo ya "karoti na fimbo!!"
 
Tatizo litaendelea kuwepo ingawa kwa kiwango kidogo (unless mkuzimwa kwa mitambo zaidi kwenye mabwaya maji). Last week tanesco walisema deficit kwenye grid ya taifa imefikia MW150. Iwapo IPT itazalisha at full capacity, tutapata MW 100. Sngas ikianza kufanya kazi kesho kama tulivyoahidiwa, tutapata MW20 nyingine hivyo tutabakiwa na derficit ya MW30
Vipi kuhusu 45 MW za Tegeta? Ile plant ilishakamika toka June this year. Mambo ya siasa bwana mpaka leo hakuna la maana linaloendelea ili kuiunganisha na grid ya Taifa
 
2002 � present day

iptl's local shareholder in tanzania, vip engineering & marketing limited, files a petition at the high court in dar es salaam to wind up iptl. The case has been ordered to be referred to the london court of international arbitration (lcia), which says it has jurisdiction over such claims.
Mechmar''s executive director and group financial controller, loh kiat loon, dismisses the move, saying the court action was nothing more than an attempt by vip engineering to obtain a ''better valuation for their share'' of iptl.

Meanwhile, the government has been forced to pay a staggering $30m (approx. 35bn/-) each year to iptl, whose malaysian owners now say they have no intention of selling the power plant to the government, as previously implied.

The current ministry of energy and minerals is reluctant to answer any queries on the iptl saga, referring queries to the attorney general's chambers.


tanzanian, please read the quoted news.

it is exhaustive and give you knowledge of what is going on in this country. Peole are doing blunders, and we are still tolerating them. Wake up
 
Pamoja na yote matatizo tulokuwa nayo sasa hivi, ningepenbda kuelewa kaa hatua hii itaondoa tatizo la Umeme au kupunguza tatizo kwa kiazsi gani..
Naelewa fika mahitaji yetu zi zaidi ya Mw 100, ni zaidi ya mtambo huu, wa Songos, Dowans na Witsila zote zikifanya kazi kwa wakati mmoja..bado tutakuwa na matatizo ya Umeme kama ilivyo ktk Maji safi..
Je, serikali ina mkakati gani na kwa muda gani kufikia TATIZO kuwa historia maanake hizi hadithi tumeziona toka enzi ya Mkapa.
Mkuu naona sasa suala la kuongeza thermal na wind power plants lipewe msisitizo. Tuna coal nyingi sana Tanzania. Tufike mahali tuamue bila kuangalia huruma za wajomba. Tatizo letu kubwa ni kuwa hatuwezi kuamua kufanya kitu mpaka tuambiwe na world bank na IMF. Hawa jamaa baadhi ya project kama hizi huwa kuzipa go ahead ni ngumu sana. Kwa mfano, Msumbiji walipogomewa na hawa jamaa kujenga reli ili kuziunganisha sehemu nyeti za uchumi, waliamua kufanya wao bila consent yao.
 
Hapa hata mkuu wa nchi kutoa uamuzi huo jana, amechelewa kimtindo..mgawo ulishaanza kitambo saana kimya kimya..baadae sana tanesco ndo wakajibeba beba kuja kutoa taarifa wakati tiari mishipa ya shingo ishatuuma saana kwa kulalamika. mi nafikiri tangia wakati huo hii mitambo ilikuwa inaonekana, sio kua ilikuwa imefukiwa ardhini. Kingine..hamna mtu yoyote huko tanesco aliyewahi kulifikiria hilo wazo kama la J.K na kulitanguliza mbele???
 
Laiti kama Zitto angekuwa anapitia CHADEMA na mawazo kama haya halafu anapewa nafasi kutoa matamko haya kwa niaba ya chama chake. Bwana mdogo yuko busy kujijenga yeye kama taasisi. Tutaiondoa CCM madarakani kweli kwa UMIMI wa kiwango hiki cha Zitto?

Hivi mtu haruhusiwi kuwa na maoni yake binafsi, natumai chama chenu(CHADEMA) kina amini katika misingi ya kidemokrasia na uhuru kuwa na maoni binafsi, ndio maana mwanzo kabisa wa sakata hili Mheshimiwa Zitto na katibu wake mkuu Mheshimiwa Slaa walikuwa na msimamo tofauti juu ya jinsi ya kutatua tatizo la umeme. Nadhani kuna wakati tunahiataji kutenganisha masuala ya siasa za kivyama na masuala ya maslahi ya nchi la sivyo tutaendelea kupiga jaramba kwa kurudi nyuma.
 
Zitto ameanza kujikwoti hapo juu kuwa yeye ndiye alitoa hili wazo la IPTL. Je alilitoa kama nani? umejiuliza hilo swali?

Ametoa kama MTANZANIA mwenye uzalendo na nchi hii na anayekerwa na kuwepo kwa mgao wa umeme
 
Nataraji issue isiwe kupunguza makali ya mgao,ila iwe ni kujizatiti kupata umeme wa kutosha hata km tukiwauzia majirani,nchi hii haina matumizi makubwa ya umeme( load ), hii inathibitishwa na hali iliyopo sasa, just mW100 zinawatoa jasho watu 40million? we are not serious hata magenerator tu yanatosha,huu ni uvivu wa mawazo, na haya yanatokana na kupeana nafasi za maamuzi ya juu bila kuwa na sifa, wenye sifa wanafanya kazi za kuamrishwa wasio nazo ndo wanaamua, tena ndo wenye hela, haututafika namna hii ndugu zangu!!
 
Kikwete is now facing a Truman moment.


I wish he knew that. It would have been a great idea if he had a chance to read the Truman dossier on the "Weapon" to show Stalin what America is! But JK has and will never be in a Truman line of handling tough issues.
 
Ndo hapo mtakapo gundua mgao wa umeme unahusishwa na mambo ya kisiasa alafu ndani yake ni dili la wanene waliopo juu wanao faidi cake ya nchi.
 
Hivi mtu haruhusiwi kuwa na maoni yake binafsi, natumai chama chenu(CHADEMA) kina amini katika misingi ya kidemokrasia na uhuru kuwa na maoni binafsi, ndio maana mwanzo kabisa wa sakata hili Mheshimiwa Zitto na katibu wake mkuu Mheshimiwa Slaa walikuwa na msimamo tofauti juu ya jinsi ya kutatua tatizo la umeme. Nadhani kuna wakati tunahiataji kutenganisha masuala ya siasa za kivyama na masuala ya maslahi ya nchi la sivyo tutaendelea kupiga jaramba kwa kurudi nyuma.
Burn,
Kinachotakiwa ni kujenga taasisi zenye nguvu sio mtu. CCM ina nguvu sana, tulitarajia baada ya NCCR kufulia kwa sababu ya kutukuza watu wenye nguvu CHADEMA italiepuka hilo. Zitto anaweza kuijenga CHADEMA kwa michango mizito ya mawazo kama haya ya IPTL, badala yake anajinadi yeye mwenyewe ingawa ni CHADEMA iloomfikisha hapo alipo sasa. Hatutafika na CCM itatawala milele.
 
Ni tatizo kwa vyombo vinavyotegemea ruzuku kujiendesha. Tatizo linazidi pale siasa inapoingia wakati menejiment ikitaka kufanya kazi yake. Hakuna cha hongera jk wala zitto. Utility is necessity. Tukiwaona hawa watu wa maana kipindi hiki tunaonekana majuha
 
I hate this kind of man/woman to be my president. He is always in deep sleep until he is shouted at!
 
Back
Top Bottom