Kikwete Alipata Wapi Madaraka ya Kuanzisha Mchakato wa Kuandika Katiba Mpya ya JMT?

Kikwete Alipata Wapi Madaraka ya Kuanzisha Mchakato wa Kuandika Katiba Mpya ya JMT?

MM
Kwakweli nimecheka sana, swali ni rahisi lakini lina majibu tofauti kabisa. Watu wanafeli mitihani si kwa kutojua bali kwa kutoelewa swali.

Swali ni hivi, ili katiba ibadilishwe kwa kutumia sheria na utaratibu wa bunge unaosemwa ni lazima kuwepo na chanzo cha kufanya hivyo. Sasa hivi tunajua chanzo ni JK kwasababu hakuna mahali CCM au Serikali yake imejadili kuhusu kuandikwa kwa katiba.

Kwa mantiki hiyo hili ni wazo la JK. Swali wazo hili limepataje uhalali hadi liandikiwe katiba?
Kupitia taratibu za bunge ni matokeo ya wazo hilo, uhalali wa wazo umepatikana wapi.

Yupo aliyesema wazo limepitia njia halali, well hata wenye pesa chafu za damu wakiziingiza katika mzunguko zinakuwa na uhalali lakini je chanzo cha pesa hizo ni halali?

Maana ya swali hili ni kuwa kama tutaruhusu mtu aamke asubuhi na kubadili mambo mazito kama haya basi rais X ajaye naye anaweza kuamka asubuhi na kuamua iandikwe katiba nyingine. Kila baada ya maiaka 5 tutaandika tu kwasababu kuna mtu ana wazo hilo.

Mwanzo wazo lililopotolewa tulihoji kama ilikuwa ipo katika ilani ya uchaguzi au ni sera au kuna kukao chochote kilichofikia maamuzi japo kwa uchahce. Jibu ni hakuna. Tunajua ilikuwa hoja ya wananchi kupitia wapinzani.
Hata hivyo kama taifa hatujawahi kukaa na kupanga tunataka taifa la namna gani na tuliandae vipi.

Tukasema mchakato wa katiba wa kutumia wazo la JK si sawa na kuanzisha chuo cha UDOM. Hili ni suala zito linaloweza kuivuruga nchi sana. Tukaambiwa ni mafaataani sasa nadhani ukweli unaonekana.

Huu ni mwanzo tu ninachokiona ni nchi kuingia katika machafuko. Hilo ninaliona kwa mbali.


There ur....100%. What is the main objective for us 'Tanzanian' 2 write a new constitution?baada ya kujibu swali hili uhalali na sio uhalali, mchakato uendeje, na usainiwe au usisainiwe majibu ya haya yote yatapatikana kwa jibu la swali hilo.
 
Debe Tupu Haliachi Kuvuma.

Mwanzilishi wa thread hii ni Debe Tupu, linavuma...
 
Sujui wenzangu labda wamepata hoja flan kupitia huu uzi, ila binafsi huyu muheshimiwa hana hoja zaidi ya kujichekesha mwenyewe.

Mchakato wa katiba uko halali kisheria kwa7bu umepitia kwenye bunge la tanzania na sheria zote zimetoka huko.

Rais hakuanzisha mchakato huu, si hoja yake, ni hoja ya watanzania walio wengi, si hoja ya jana na juzi ni hoja ya miaka nadhan ukirejea nyuma historia utaona hoja nyingi sana ikiwemo ya G55.

Katiba ya Zanzibar kwa sasa imetangaza wazi kwamba Zanzibar ni Nchi! Nenda kwenye dictionary la kiswahili angalia neno "nchi" lina maana gani? Haikuishia hapo imetangaza mipaka yake na vielelezo vyenginevyo. Hili pia limezidisha haja ya katiba mpya ili Tanganyika nayo irud kwakua kisheria katiba ya zanzibar imeamuliwa na wazanzibari wenyewe.

Kuna hoja nyingi sana ila mbali ya yote mazingira nayo yanaruhusu sasa kuandika hii katiba mpya, sisi hatuigi kenya wala wapi ni muda muafaka kufanya haya hasa ikizingatiwa hii ni katiba ya muungano.

Hii si hoja ya kikwete, na maswala ya migongano ni lazima coz tunatengeneza katiba ( sheria mama) kwaiyo kutofahamiana au kuwepo na khitilafu za hapa na pale si hoja ya msingi hapa, ingekuepo hata tungefanya vipi haya ni maswala ya kisheria.

Nawasilisha.


Mwanzilishi wa hii thread ni mtu ambaye anaombe Tanzania iwe nchi ya vurugu. Sasa hivi roho inamuuma sana anapoona mchakato wa katiba unaendelea kwa utulivu.

Tumeshamzoe na harakati zake za kuchochea vurugu na chuki. Watu wameshaanza kumshtukia, ndio maana mgomo wake wa simu ulifeli.
 
Kama huu mchakato ni haramu, kwa ushauri wako ni kuendelea na katiba tuliyonayo?

Chombo halali ni kipi?
Mkuu,

Usiumize kichwa chako bure.

Wapo watu ambao katika kila jambo lazima watafute jinsi ya kuchafua hali ya hewa. Mchakato uko hatua za mwisho, anatoke mtu kuuliza kama mchakato una uhalali wa kuanzishwa!!!

Kwa vile mleta thread anajulikana historia yake ya kuchochea vurugu baina ya watanzania, basi msipate shida kushughulisha vichwa vyenu kwa hoja zake mfu...
 
Nina mashaka na hoja kama hizi iwapo wanaozishupalia hajabeba ajenda ya makundi ya mafisadi ambao tunasikia wasingependa katiba mpya ipite kwa vile itawakwamisha malengo yao ya 2015. Tafakari.

Aliyeleta mada haitakii mema Tanzania. Ni mtu ambaye kila siku yuko mstari wa mbele kuchochea vurugu na kupinga harakati za maendeleo ya watanzania. Mtu wa namna hiyo hawezi kutoa ushauri mzuri kwa ajili ya taifa la Tanzania.
 
MM
Kwakweli nimecheka sana, swali ni rahisi lakini lina majibu tofauti kabisa. Watu wanafeli mitihani si kwa kutojua bali kwa kutoelewa swali.

Swali ni hivi, ili katiba ibadilishwe kwa kutumia sheria na utaratibu wa bunge unaosemwa ni lazima kuwepo na chanzo cha kufanya hivyo. Sasa hivi tunajua chanzo ni JK kwasababu hakuna mahali CCM au Serikali yake imejadili kuhusu kuandikwa kwa katiba.

Kwa mantiki hiyo hili ni wazo la JK. Swali wazo hili limepataje uhalali hadi liandikiwe katiba?
Kupitia taratibu za bunge ni matokeo ya wazo hilo, uhalali wa wazo umepatikana wapi?

Yupo aliyesema wazo limepitia njia halali, well hata wenye pesa chafu za damu wakiziingiza katika mzunguko zinakuwa na uhalali lakini je chanzo cha pesa hizo ni halali?

Maana ya swali hili ni kuwa kama tutaruhusu mtu aamke asubuhi na kubadili mambo mazito kama haya basi rais X ajaye naye anaweza kuamka asubuhi na kuamua iandikwe katiba nyingine. Kila baada ya maiaka 5 tutaandika tu kwasababu kuna mtu ana wazo hilo.

Wazo lililopoletw tulihoji kama ilikuwa ipo katika ilani ya uchaguzi au ni sera au kuna kikao chochote kilichofikia maamuzi japo kwa uchahce. Jibu ni hakuna.
Tunajua ilikuwa hoja ya wananchi kupitia wapinzani.Hata hivyo kama taifa hatujawahi kukaa na kupanga tunataka taifa la namna gani na tuliandae vipi.

Tukasema mchakato wa katiba wa kutumia wazo la JK si sawa na kuanzisha chuo cha UDOM.
Hili ni suala zito linaloweza kuivuruga nchi sana. Tulihitaji mjadala wa kitaifa na siyo 'suprise suprise ya hotuba za mwezi' tena ikipigiwa vigelegele na viongozi wa upinzani!!!
Tukaambiwa ni fataani sasa nadhani ukweli unaonekana.

Huu ni mwanzo tu ninachokiona ni nchi kuingia katika machafuko. Hilo ninaliona kwa mbali.
Tunaingia huko kutokana na ukiukwaji wa misingi ya kuandika katiba ya wananchi. Sasa hivi katiba ya CCM inaandikwa halafu itaitwa ya Tanzania. Nchi inachafuka wenye macho wanaona! wabishi wasubiri utaratibu wa sheria halali.

Nguruvi3

Wewe ukiwa miongoni mwa wanaoipigania agenda ya serikali tatu inabidi uanzekujiuliza kwa kina ni nani mwenye mamlaka ya kusimamia mchakato wa kuandika katiba ya Tanganyika? This is what people should be discussing now because unlike Tanzania, Tanganyika has no organ at all. Mambo ya Tanzania yanaweza kusimamiwa na Bunge la Tanzania, je ya Tanganyika?

Haya maswali ya kitoto ya mwanakijiji amnbayo yanawachanganya zaidi watu badala ya kuonyesha way forward at this time mngeyapuuza tu. Watu wafikirie mbele badala ya kukaa chini na kuzogoana!!!
 
Si CCM kama chama wala viongozi wake wakuu walikuwa tayari kuanzisha mchakato wa kuandika katiba mpya!

Hata hivyo JK alisukumwa kuanzisha mchakato huu ili kupunguza upinzani dhidi ya serikali yake na hasa kutoka vyama vya upinzani na wanaharakati! Kwa kuanzisha mchakato huu JK amepata nafuu sana katika kuongoza nchi hii kwa kuwa wengi wa wapinzani wake wameelekeza nguvu kubwa katika kujadili katiba badala ya utendaji wake wa kazi!

Upinzani tu usingekuwa sababu ya kufanya kitu kikubwa na nyeti hivi. Kumbuka alishinda na kuapa kulinda na kuhifadhi Katiba anayotaka kuibadilisha. Nafikiri factor ya Zanzibar ilikuwa msingi mkubwa wa mchakato huu. Zanzibar kwa Katiba yao walishakinzana na Katiba ya Muungano. Hakuna njia ingine isipokuwa kutengeneza Katiba mpya ili kuondoa msigano huu.
 
Kaka heshima kwako,

Nakubaliana kwa kiasi flani na hoja yako, kidogo natofautiana na wewe pengine wawezakunielewesha zaidi maana binadamu tunatofautiana kimtizamo. Kifupi nadhani mchakato wa katiba una-uhalali maana umeanzishwa kupitia bunge na sheria kutungwa kwa kutumia katiba ya sasa.

Labda niweke wazi pia nakubaliana na wewe kwamba hatuna objective tunayoilenga kwenye katiba mpya ndio maana vurugu hazitaisha kama unavyosema mkuu. Kumbuka "wenzetu wanafanya hivi na sisi tusifanye hivi kwann" hapo ndipo kuna tatizo.

Ila ushauri wako kuwa mchakato uvunjwe kwakua ni haramu mie sikubaliani kaka. Umesema mwenyewe kuwa pesa nyingi zimetumika na sio pesa tu hata muda na human resource hivyo kaka fikiria au tufikirie uhalali tutauweka vipi kwenye mchakato wa sasa. Asante

Tanzania kazi yetu ni kuiga nini Kenya wamefanya na sisi tufanye. Kwenye vyama vingi mambo yalikuwa hivi hivi. CCM wanajaribu kufanya kitu wasichokita...........hivyo hakufanikiwa mpaka pale wananchi watakapoamua kwa dhati kuwa kweli wanaitaka katiba mpya.
 
MM
Kwakweli nimecheka sana, swali ni rahisi lakini lina majibu tofauti kabisa. Watu wanafeli mitihani si kwa kutojua bali kwa kutoelewa swali.

Swali ni hivi, ili katiba ibadilishwe kwa kutumia sheria na utaratibu wa bunge unaosemwa ni lazima kuwepo na chanzo cha kufanya hivyo. Sasa hivi tunajua chanzo ni JK kwasababu hakuna mahali CCM au Serikali yake imejadili kuhusu kuandikwa kwa katiba.

Kwa mantiki hiyo hili ni wazo la JK. Swali wazo hili limepataje uhalali hadi liandikiwe katiba?
Kupitia taratibu za bunge ni matokeo ya wazo hilo, uhalali wa wazo umepatikana wapi?

Yupo aliyesema wazo limepitia njia halali, well hata wenye pesa chafu za damu wakiziingiza katika mzunguko zinakuwa na uhalali lakini je chanzo cha pesa hizo ni halali?

Maana ya swali hili ni kuwa kama tutaruhusu mtu aamke asubuhi na kubadili mambo mazito kama haya basi rais X ajaye naye anaweza kuamka asubuhi na kuamua iandikwe katiba nyingine. Kila baada ya maiaka 5 tutaandika tu kwasababu kuna mtu ana wazo hilo.

Wazo lililopoletw tulihoji kama ilikuwa ipo katika ilani ya uchaguzi au ni sera au kuna kikao chochote kilichofikia maamuzi japo kwa uchahce. Jibu ni hakuna.
Tunajua ilikuwa hoja ya wananchi kupitia wapinzani.Hata hivyo kama taifa hatujawahi kukaa na kupanga tunataka taifa la namna gani na tuliandae vipi.

Tukasema mchakato wa katiba wa kutumia wazo la JK si sawa na kuanzisha chuo cha UDOM.
Hili ni suala zito linaloweza kuivuruga nchi sana. Tulihitaji mjadala wa kitaifa na siyo 'suprise suprise ya hotuba za mwezi' tena ikipigiwa vigelegele na viongozi wa upinzani!!!
Tukaambiwa ni fataani sasa nadhani ukweli unaonekana.

Huu ni mwanzo tu ninachokiona ni nchi kuingia katika machafuko. Hilo ninaliona kwa mbali.
Tunaingia huko kutokana na ukiukwaji wa misingi ya kuandika katiba ya wananchi. Sasa hivi katiba ya CCM inaandikwa halafu itaitwa ya Tanzania. Nchi inachafuka wenye macho wanaona! wabishi wasubiri utaratibu wa sheria halali.

wewe ndio ume nielewesha....huyu jamaa sijaelewa alicho kua anaongea.
 
"Chombo halali" kitapatikanaje?Kuuliza si ujinga...

chombo halali kinapatikana kwa njia halali. Chukulia kwa mfano; Rais Kikwete akiamua kesho kuwa anaanzisha Mahakama ya Wanawake - je itakuwa ni halali kwa yeye kufanya hivyo kwa sababu tu anaamini kesi zinazohusiana na wanawake zinahitaji mahakama maalum; na wakatokea wanawake wengi wakamuunga mkono... sisi wengine tutapinga kwa sababu hana madaraka ya kuanzisha mahakama!
 
Haya maswali ya kitoto ya mwanakijiji amnbayo yanawachanganya zaidi watu badala ya kuonyesha way forward at this time mngeyapuuza tu. Watu wafikirie mbele badala ya kukaa chini na kuzogoana!!!

Tuchukulie kuwa ni swali la kitoto lijibu basi; maana hata mtoto akiuliza swali anapewa jibu. Ukiona mtu mzima anashindwa kujibu swali la mtoto ni kwa sababu mtoto kauliza swali gumu. Wewe unaamini Kikwete (Rais wa Tanzania) ana madaraka ya kuanzisha mchakato wa Katiba Mpya.
 
wewe ndio ume nielewesha....huyu jamaa sijaelewa alicho kua anaongea.

Usipoelewa ni vizuri ukauliza usichoelewa; kwani kila mtu ana uelewa wake. Wakati mwingine ni matatizo ya mwelewa au ya mweleweshaji. Ningejaribu kukufafanulia; lakin ikwa vile wengine wanaelewa vizuri - kama alivyofanya Nguruvi basi ni vizuri kuwasoma wengine uone wameelewa vipi na wao wakakuelewesha.
 
mwanakijiji tulipaswa tufuate njia ipi!?

Incredible and very intelligent question:

a. Kwanza na zaidi kabisa walitakiwa kuangalia Katiba ya sasa inasemaje kuhusiana na kuandika Katiba Mpya.
b. Kwa vile Katiba ya sasa hairuhusu kuandika Katiba Mpya (chini ya Ibara ya 98) basi walitakiwa kufanyia marekebisho Katiba ya sasa (hasa kwa watu wanaosema wanafuata utawala wa Katiba na Sheria)
c. Katika mabadiliko hayo ya Katiba walitakiwa kuweka utaratibu wa kuandika Katiba Mpya kama ulivyo utaratibu wa kufanyia marekebisho Katiba ya sasa.

Kutoka hayo matatu ndio tungezungumzia kuandika Katiba Mpya.

Sasa hivi wote hawa wanaweza kuitwa wahaini tu!
 
Nadhani alifanya hiyo sababu ya uwoga wa Vyama vya upinzani.Kwa sababu hata kwenye ilani ya CCM mchakato wa katiba haukuwepo.Pili labda baada ya kuona wenzetu Kenya wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuandika katiba mpya,ila hakufahamu kuwa wakenya walikuwa na nia ya dhati ya kuandika katiba.
 
kwahiyo mnasemaje wadau , tuuchinjie baharini au ? Maana uwezo tunao !
 
Hili ni swali ambalo jibu lake liko wazi; kuwa Rais Kikwete hakuwa na madaraka hayo. Hata hivyo, wapo wanaoamini kuwa kwa vile Rais kaamua kufanya kitu basi kitu hicho ni halali.

Mimi na baadhi yetu tumekataa kuutambua mchakato huu wa Katiba Mpya kwa sababu ni haramu; haukuanzishwa na chommbo halali na hata hivi sasa matatito tunayoyaona na yatakayotokea mbeleni (kwenye Bunge la Katiba na Kura ya Maoni) itakuwa ni mwendelezo tu wa kosa hili kubwa.

HUU NI MCHAKATO HARAMU. Sikiliza HOJA MARIDHAWA

[JFMP3]https://www.jamiiforums.com/attachment.php?attachmentid=115504&stc=1&d=1381127129[/JFMP3]
WE mzee umefulia huna jipya uwe unanyamaza kama huna ya kusema
 
Back
Top Bottom